MITI 6,379 itapandwa Mkoani Pwani katika kuadhimisha siku ya kumbukizi ya kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan.
Monday, January 26, 2026
MITI 6,379 KUPANDWA PWANI KUMBUKIZI KUZALIWA DK SAMIA SULUHU HASSAN
HALMASHAURI YAKABIDHI MADAWATI 4,000
HALMASHAURI ya Manispaa ya Kibaha imetoa madawati viti na meza 4,000 kwa Shule za Msingi na Sekondari vikiwa na thamani ya shilingi milioni 400.
Akikabidhi madawati viti na meza Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John alisema kuwa Halmashauri imefanya jambo zuri la kukabili changamoto ya wanafunzi kukaa chini.
Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Kibaha Dk Nicas Mawazo alisema kuwa idadi ya wanafunzi inaongezeka kutokana na wazazi kuhamia Kibaha.
Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa alisema kuwa walitenga kiasi cha shilingi milioni 400 kwa ajili ya kutengeneza madawati viti na meza 4,000 ikiwa kwa Shule za Msingi madawati 2,000 na Sekondari viti na meza 2,000.
Sunday, January 25, 2026
VIJANA WATUNZE AMANI
MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) NEC Taifa kupitia Jumuiya ya Wazazi Hamoud Jumaa ameitaka Jumuiya hiyo kuwapa vijana malezi mazuri ili watunze amani.
Saturday, January 24, 2026
VIJANA WAPEWE MALEZI BORA KULINDA AMANI
Jumaa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini ameyasema hayo Mjini Kibaha wakati akifungua kikao cha Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Pwani.
Amesema kazi ya Jumuiya hiyo ni kuhakikisha jamii hususani vijana wanakuwa na malezi bora ili kutojiingiza kwenye makundi ambayo hayana maadili mema.
"Tuwape elimu na malezi mazuri vijana wetu na tuzungumze nao juu ya amani kwani amani pia huleta afya njema na amani ndiyo kila jambo hivyo tuhubiri amani,"amesema Jumaa.
Aidha amesema vijana nchini wanapaswa kudumisha amani na kutokubali kurubuniwa ili wasivunje amani iliyopo kwani bila amani hatutaweza kufanya mambo ya maendeleo.
"Vijana wanapaswa kulinda amani kwani ndiyo msingi wa Taifa la Tanzania na wasukubali kushawishiwa na watu kuharibu amani iliyopo kwani ikipotea ni gharama kuirudisha,"amesema Jumaa.
Amewataka viongozi wa Jumuiya hiyo kuanza maandalizi ya uchaguzi wa Jumuiya utakaofanyika mwakani kwani uchaguzi ndani ya chama ni mgumu kuliko uchaguzi wa vyama.
"Muanze maandalizi na kama kuna kiongozi anaona anauwezo ajiandae kugombea kwenye chama wakati ukifika kwani Jumuiya hii ndiyo inayobeba jumuiya zote za chama,"amesema Jumaa.
Aliongeza kuwa viongozi wanapaswa kuacha alama kwa kuwa na miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kununua ardhi pamoja na ofisi za makatibu wa jumuiya kwa kila wilaya.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Pwani Josiah Jackson amesema kuwa uchaguzi umekwisha kilichobaki ni kujenga jumuiya na chama.
Jackson amesema kuwa wanachama waache makandokando kwa kuwaacha waliochaguliwa wafanye kazi zao na kuwaunga mkono ambapo kwa mkoa walipata madiwani 17 kutoka jumuiya.
Naye katibu wa CCM Mkoa wa Pwani Kitte Mfilinge amesema kuwa anaipongeza jumuiya kwa kufanya vizuri kwenye uchaguzi mkuu kwani mkoa umeshika nafasi tatu za juu hapa nchini.
Mfilinge amesema kuwa Jumuiya hiyo iko vizuri kwani ina mshikamano na imetulia hivyo kwa sasa wajiandae na uchaguzi wa jumuiya mwakani lengo ni kujenga chama ili kiwe imara.
Friday, January 23, 2026
AJIPATIA KIPATO KUPITIA PANYA WEUPE
Wednesday, January 21, 2026
FIDIA LAMI MAILI MOJA SHELI-MUHEZA ZAIVA
Diwani wa Kata ya Maili Moja Ramadhan Lutambi amesema kuwa zoezi hilo ni muhimu kabla ya kuanza kutekelezwa kwa mradi huo Uboreshaji Miundombinu ya Miji Tanzania (TACTIC) kwa Manispaa ya Kibaha.






