Sunday, June 15, 2025

RIDHIWANI KIKWETE AKISHIRIKI MAADHIMISHO UELEWA KUHUSU ALBINO

Nimeshiriki shughuli za kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Uelewa Kuhusu Albino.

Shughuli hii iliongozwa na Mh. Kassim Majaliwa Majaliwa , Waziri Mkuu wa JMT , zilizofanyika katika viwanja wa Mwanga Mkoani Kigoma tarehe 13 Juni 2025.

Maadhimisho haya yamekuwa yakifanyika kila mwaka na utumika kukumbushana umuhimu wa kushirikisha wenye Ualbino, Haki zao, umuhimu wa serikali kuendelea kuangalia maslahi na ulinzi wao.  

Katika Shughuli ya Mwaka huu mtandao maalum wa kusajiri watu wenye Ulemavu unaowezesha usajiri kwa njia ya Elektronik hata kwenye maeneo yaliyo nje ya mtandao nao ulizinduliwa. 

Mfumo huo unawezesha taarifa za watu wenye ulemavu kuchukuliwa na kuchambuliwa ambapo zitaiwezesha serikali kupata taarifa za kina zitakazowezesha kupanga mipango ya maendeleo ikiwemo kuwashirikisha wenye Ulemavu.  


Waziri Mkuu wa JMT alitumia nafasi hiyo pia kutoa maagizo mahsusi kwa wakuu wa Mikoa na wadau waliokuwapo kuhusu matumizi sahihi ya mtandao huo na kuwashirikisha watu wenye Ulemavu kwa jumla katika shughuli mbalimbali ikiwemo Uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadae Mwezi Oktoba mwaka huu uku akiwahamasisha watu wenye Ualbino nao kujitokeza kushiriki uchaguzi huo.

Friday, June 13, 2025

SUBIRA MGALU ATOA GARI KWA (UWT) BAGAMOYO

MBUNGE wa Mkoa wa Pwani Subira Mgalu ameupatia gari uongozi wa Jumuiya ya Wanawake CCM kupitia Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani.

Akizungumza wakati wa kukabidhi gari hilo aina ya Noah Mgalu amesema kuwa moja ya nadhiri aliyojiwekea kipindi cha nyuma ilikuwa ni kuhakikisha anainunulia chombo cha usafiri Jumuiya hiyo ili kurahisisha utendaji kazi.

Mgalu amesema kuwa ni vyema gari hilo likatumika kutafuta kura za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan huko kwenye matawi kwa kuwakumbusha wananchi kile kilichofanyika kwenye maeneo yao.

"Gari hili likatumiwe na Jumuiya zote za chama ikiwemo Wazazi na Vijana ili ziweze kufanikisha malengo ya chama chetu,"amesema Mgalu.

Akikabidhi gari hilo kwa Katibu wa  Wilaya ya Bagamoyo Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mery Chatanda amempongeza  Mbunge huyo kwa jinsi ambavyo amekuwa akijitoa kwa Jumuiya hiyo.

Chatanda amewataka viongozi wa Bagamoyo kuhakikisha wanaitumia gari hiyo kwa makusudio yaliyokusudiwa ili kurahisisha shughuli za utendaji wa Jumuiya

Friday, June 6, 2025

CHOKALA AISHUKURU SERIKALI KUTOA BILIONI 4.2 ZA MAENDELEO KATA YA TUMBI

DIWANI wa Kata ya Tumbi Halmashauri ya Mji Kibaha Raymond Chokala amesema fedha zilizotolewa na serikali kiasi cha shilingi bilioni 4.2 kwa kipindi cha miaka mitano zimeleta maendeleo makubwa kwenye Kata hiyo.

Akizungumza kwenye Mkutano wa kuwasilisha taarifa ya utekelezaji ilani kwa kipindi cha miaka mitano 2020-2025 kwa wanachama wa CCM na wananchi wa Mitaa ya Mwanalugali A na B Chokala amesema Kata hiyo imepiga hatua kubwa ya kimaendeleo.

Chokala amesema fedha hizo zimetumika vizuri kwenye sekta za elimu, afya, vikundi vya kiuchumi kupitia asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri, barabara, maji, umeme, kilimo na mifugo.

"Tunaishukuru serikali kwa kutupatia fedha hizo ambazo matokeo yake yameonekana kwani huduma zimeboreka licha ya changamoto chache ambazo zimeendelea kutatuliwa kulingana na bajeti inayopatikana,"amesema Chokala.

Amesema mafanikio hayo yametokana ushirikiano mkubwa ulioonyeshwa baina ya Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka, wananchi, viongozi na watendaji wa serikali bila kusahau chama tawala CCM ambao ndiyo wasimamizi wa ilani.

WAKALA WA VIPIMO (WMA) YATAKA VIPIMO VIHAKIKIWE KILA MWAKA






WAKALA wa Vipimo Nchini (WMA) imetaka vipimo vya ujazo urefu na uzito wakati wa kupima bidhaa au kuhudumia wananchi lazima vihakikiwe kila baada ya miezi 12.

Hayo yamesemwa na Meneja wa Kituo cha (WMA) kilichopo Misugusugu Wilayani Kibaha Mkoani Pwani Charles Mavunde alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.

Mavunde amesema kuwa uhakiki huo ni takwa la kisheria ya vipimo sura 340 namba 19 ya mwaka 2002 inataka vipimo vinavyotumika kupima katika biashara au huduma nyingine za kijamii lazima vihakikiwe ndani ya muda huo.

Amesema kuwa sheria inatoa adhabu kwa mtu ambaye hata hakiki vifaa vinavyotumika katika kubebea au kupimia ambapo faini ni kati ya shilingi 100,000 hadi milioni 20 au kifungo jela miaka miwili.

"Kipimo chochote  kinachopima kuhudumia wananchi kinatakiwa  kufanyiwa uhakiki kila baada ya miezi 12 pia tunawapongeza wananchi kwa kuwa  na mwamko   kwenye uhakiki wa dira za maji kwani ni mkubwa," amesema Mavunde.

Amesema wanatarajia kuhakiki mita za maji  zaidi ya 87,000 kufikia mwishoni wa mwezi Juni 2025 ili kutambua usahihi wake kabla ya kwenda kufungwa kwa wateja na wamefanya zoezi la  uhakiki wa mita za umeme zaidi ya 5,500 za umeme mkubwa wa viwanda vya Mkoa wa Dar  es Salaam na mikoa mingine ili kuona kama zipo sahihi kulingana na matumizi viwandani. 

"Kwa upande wa dira za maji katika kipindi cha Julai  hadi Mei mwaka huu tayari wamehakiki dira  57,997 huku wakiwa na uwezo wa kuhakiki dira 100,000 kwa mwaka

Naye Ofisa  Vipimo  Mkuu Gaudence Gaspery amesema kuwa hivi sasa wanahakiki dira za  maji kwa kutumia mtambo wa kisasa wenye uwezo wa kuhakiki dira 10 kwa wakati mmoja.

Gaspery amesema kuwa baada ya kuhakikiwa na kuonekana zinafaa kwa matumizi huwekewa rakili yenye rangi ya chungwa  na ambazo zitagundulika zinahitaji kufanyiwa marekebisho hurekebishwa huku zile ambazo zitagundulika kwamba hazifai huteketezwa.

 

Thursday, May 29, 2025

MWANASHERIA MATATANI AKITUHUMIWA KUGHUSHI AKAUNTI YA KIJIJI NA KUJIPATIA FEDHA

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Pwani imefanikiwa kuokoa kiasi cha shilingi zaidi ya milioni 385 fedha za mauzo ya ardhi ambazo ziliwekwa kwenye akaunti ya kughushi ya mtu binafsi badala ya akaunti ya Kijiji cha Msufini Kidete Wilaya ya Mkuranga.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Pwani Domina Mukama akitoa taarifa ya Januari hadi Machi alisema kuwa fedha hizo zilikuwa ni asilimia 10 ya malipo baada ya Kijiji kuuza ardhi.

Mukama alisema kuwa mtu anayetuhumiwa kughushi akaunti hiyo ya Kijiji na kuingia kwenye akaunti yake binafsi ni mwanasheria wa kampuni ya Briliant Sanitary Ware Company Limited ambayo ilinunua eneo hilo.

"Fedha hizo ni asilimia 10 ya mapato kwa ajili ya Kijiji baada ya mauzo ambapo zilipoingia mtu huyo alizitumia kwa matumizi binafsi lakini Takukuru walifanikiwa kuzirejesha fedha hizo ambapo kwa sasa kesi yake iko hatua ya uchunguzi,"alisema Mukama.

Aidha alisema kuwa fedha hizo baada ya kuzirejesha fedha hizo kwenye akaunti ya Kijiji hicho zimepangiwa matumizi ya kujenga madarasa mawili ya Shule ya Sekondari Mbezi Gogoni na madarasa mawili Shule ya Msingi Msufini.

"Katika hatua nyingine Takukuru imefuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo 338 yenye thamani ya zaidi ya Bilioni 18 na utekelezaji wake unaridhisha,"alisema Mukama.

Alibainisha kuwa wamewafikia wananchi wa makundi mbalimbali ili waweze kuiunga Serikali mkono katika kuzuia vitendo ya rushwa kwa kupitia semina 67, mikutano ya hadhara 72, vipindi vya redio 5, uimarishaji klabu za wapinga rushwa 130.

"Tumejipanga Kuzuia na Kupambana na vitendo vya Rushwa katika uchaguzi Mkuu kwa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu madhara ya rushwa katika uchaguzi kwa kuwafikia wadau wote,"alisema Mukama.

Aliongeza kuwa wanatoa elimu kwa wadau ambao ni vyama vya siasa, wasimamizi wa uchaguzi, wanahabari, wananchi na jamii nzima kwa ujumla ambapo anawaasa wananchi kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa ili kuwa salama na kuepuka migogoro yenye kuleta viashiria vyenye rushwa.

"Katika kipindi tajwa Ofisi ilifanya chambuzi za mifumo 14 ikiwa ni pamoja na eneo la makadirio ya ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri ya
Mji Kibaha, Mafia, kituo cha Utalii Kazimzumbwi katika chambuzi wa mfumo wa usambazaji maji uliofanyika kuna mapungufu yalibainika na hatua zilichukuliwa.

Saturday, May 24, 2025

DIWANI MTAMBO AWASILISHA TAARIFA UTEKELEZAJI WA ILANI YA MIAKA 5

KATA ya Picha ya Ndege Halmashauri ya Mji Kibaha umeishukuru serikali kwa kutoa fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye kata hiyo.

Hayo yamesemwa na Diwani wa Kata hiyo Karim Mtambo alipokuwa akiwasilisha utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kipindi cha miaka mitano 2020-2025.

Mtambo amesema kuwa anaishukuru serikali kwani imegusa sekta zote za kiamendeleo hivyo kufanya kero nyingi kupungua na wananchi kupata huduma kwa urahisi.

"Mfano hospitali ya Wilaya ya Lulanzi kwa sasa haina changamoto ya maji ikilinganishwa na kipindi cha nyuma na wananchi nao wanapata huduma ya maji kwa asilimia 95, ujenzi wa ofisi ya Kata ambapo iko hatua ya ukamilishaji",amesema Mtambo.

Amesema kuwa huduma za afya nazo zimetengewa fedha nyingi, miundombinu ya barabara nayo imeboreshwa, soko bado lina changamoto na kituo cha polisi nacho bado.

"Sekta ya elimu nayo imepatiwa fedha nyingi ambapo kwenye shule zetu za msingi miundombinu imeboreshwa na ufaulu umeongezeka ikilinganishwa na zamani,"amesema Mtambo.

 

GRACE JUNGULU AONGOZA KIKAO UTEKELEZAJI ILANI KATA YA PICHA YA NDEGE

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Grace Jungulu amewataka viongozi wanaotokana na chama kutoa majibu ya changamoto za wananchi baada ya vikao vya chama na siyo kubaki nayo ndani kwani wao ndiyo wanayoisimamia serikali.

Jungulu ameyasema hayo wakati akiongoza kikao cha uwasilishwaji wa utekelezaji wa ilani ya CCM ya miaka mitano iliyowasilishwa na diwani wa kata hiyo Karim Mtambo.

Amesema kuwa viongozi wamekuwa wakitoa majibu juu ya changamoto mbalimbali kwenye vikao vya chama hivyo kajibu hayo wayapatie na wananchi. 

"Twendeni na kwa wananchi kupitia mikutano ya kila baada ya miezi mitatu tuwajibu wananchi maswali yao kwa kupokea kero zao na kuzitafutia ufumbuzi,"amesema Jungulu.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Picha ya Ndege Karim Mtambo amesema kuwa anaishukuru serikali kwa kutoa fedha ambazo zimetekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Mtambo amesema sekta zote zimeguswa na miradi hiyo na kufanya changamoto za wananchi kupungua huku serikali ikiendelea kutatua kero zilizopo.