WAKALA wa Vipimo Nchini (WMA) imetaka vipimo vya ujazo urefu na uzito wakati wa kupima bidhaa au kuhudumia wananchi lazima vihakikiwe kila baada ya miezi 12.
Friday, June 6, 2025
WAKALA WA VIPIMO (WMA) YATAKA VIPIMO VIHAKIKIWE KILA MWAKA
Thursday, May 29, 2025
MWANASHERIA MATATANI AKITUHUMIWA KUGHUSHI AKAUNTI YA KIJIJI NA KUJIPATIA FEDHA

Saturday, May 24, 2025
DIWANI MTAMBO AWASILISHA TAARIFA UTEKELEZAJI WA ILANI YA MIAKA 5
GRACE JUNGULU AONGOZA KIKAO UTEKELEZAJI ILANI KATA YA PICHA YA NDEGE
Wednesday, May 21, 2025
ATAKA SIMBA IUNGWE MKONO KUCHUKUA KOMBE LA SHIRIKISHO DHIDI YA BERKANE
WACHEZAJI viongozi na benchi la ufundi la timu ya Simba wametakiwa kupambana kuhakikisha wanatwaa kombe la Shirikisho.
Aidha washabiki na wapenzi wa soka nchini wametakiwa kuwa na mshikamano na kuacha tofauti zao za ushabiki na kuungana ili kuisadia timu ya Simba kwenye mchezo wao wa fainali dhidi ya Berkane mchezo utakaochezwa uwanja wa Amani Zanzibar.
Akizungumza na Brailo Media aliyewahi kuwa mlezi wa Tawi la Simba Tishio Kibaha Fahim Lardhi amesema kuwa Watanzania wanapaswa kuungana kwenye mchezo huo kwani ni wa heshima kwa nchi.
Lardhi amesema kuwa licha ya Simba kufungwa kwenye hatua ya kwanza kwa magoli 2-0 lakini wanaimani kuwa Simba itapindua matokeo na kuwa mabingwa.
"Tuenzi maneno ya Rais Hayati Dk John Magufuli aliyoitoa kwenye uwanja wa Mkapa wa kutaka Simba au timu nyingine ya Tanzania kuleta kombe la Afrika,"amesema Lardhi.
Amesema kuwa itakuwa ni fedhaha kwa Simba kuchukua kombe hilo ambalo litakuwa kwenye ardhi ya Tanzania ambapo mwaka 1993 walifungwa kwenye fainali na Stella Abidjan ya Ivory Coast.
"Mwaka huu kwa uzalendo wetu tuhakikishe tunalipigania Taifa letu kama kila mtu atatimiza wajibu wake kuanzia wachezaji hadi kwa mashabiki,"amesema Lardhi.
Amewaomba Watanzania kuwa na mshikamano kwa wakati wa maandalizi na wakati wa mchezo kwa kuungana na kuacha tofauti kwani hiyo ni mechi ya heshima kwa nchi.
Monday, May 19, 2025
WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA WARIPOTI HABARI ZA UCHAGUZI KWA UMAKINI
VYOMBO vya Habari nchini vimetakiwa kutoa taarifa za vyama vyote vya siasa kwenye kampeni wakati wa uchaguzi wa mwaka huu ili wananchi waweze kujua sera za vyama na kuchagua viongozi bora.