Saturday, February 3, 2024

TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE YATEMBELEA BUNGENI




Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani yatembelea Bungeni Tarehe 2.2.2024 Kwa Mwaliko wa Mhe Subira Mgalu Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Pwani Kwa lengo la Kujifunza Shughuli za Bungeni.

Katibu wa Taasisi hiyo Mkoa wa Pwani Ndugu Omary Punzi Kwa niaba ya Taasisi alitoa Shukrani Kwa Mbunge Subira Mgalu Kwa namna alivyoipokea Taasisi na kuheshimu sambamba na hilo alipongeza Juhudi za Serikalini ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Daktari Samia Suluhu Hassani namna Bunge lilivyokuwa linafanya kazi Vizuri Kwa uchangamfu sana na Kujibu hoja vizuri

Thursday, February 1, 2024

AMEND TANZANIA LATOA MAFUNZO KWA MAOFISA USAFIRISHAJI.



Shirika la AMEND Tanzania ambalo linajihusisha na masuala ya kutoa elimu kwa wananchi kuhusu usalama barabarani limeweza kutoa elimu na mafunzo kwa maafisa wasafirishaji wa vituo tofauti katika jiji la Dodoma.

Shirika hilo ambalo lipo chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Uswisi nchini Tanzania limeweza kutoa elimu na mafunzo kwa maafisa wasafirishaji maarufu kwa jina la bodaboda kwa malengo ya kudhibiti wigo ajali barabarani pamoja na kuwapa mafunzo mbali mbali pamoja na utumiaji wa alama za barabarani ambazo zimekuwa zikipuuzwa na maafisa wasafirishaji hao.

Nuhu Toyi ambaye ni balozi wa mafunzo na afisa msafirishaji kutoka kituo cha UDOM  jijini Dodoma amesema alibaatika kupata mafunzo ambayo yametolewa na shirika la AMEND Tanzania na kupitia mafunzo hayo yameweza kumsaidia kuendesha chombo chake kwa kujihamini bila kusababisha ajali.

“Pongezi za dhati ziende kwa Ubalozi wa Uswisi nchini Tanzania hususan kitengo cha afya kinachofadhiliwa na miss Vivian kwa kutambua umuhimu wa kundi hili la vijana wa bodaboda wengi ni vijana ambao tupo kati ya umri wa miaka 25. Kazi hii wengi tumekuwa tukiifanya kwa mazoea na hatuna elimu kwaio wengi tumekuwa ni wahanga wa kusababisha au kusababishiwa ajari kwasababu ya kukosa elimu barabarani lakini Ubalozi wa Uswisi nchini Tanzania umeona itakuwa ni vyema kama vijana hawa ambao ni taifa la kesho na nguvu kazi ya taifa wasiweze kudhuulika na ajali” alisema Toyi.

Kwa upande wake afisa usafirishaji, Laurenti Mayowa amesema alikuwa haelewi alama za barabarani lakini kupitia mafunzo hayo wamepokea kutoka shirika la AMEND Tanzania kwani limekuja kitofauti katika kutoa mafunzo yao kwani wamefundishwa kwa nadharia pamoja na vitendo.

“Tulipata mafunzo mazuri sana kwenye swala la uendeshaji wa pikipiki lakini pia tumeweza kufundishwa namna ya kutumia barabara lakini pia namba ya kutumi vyombo vyetu, kwa kweli mafunzo yalikuwa mazuri nimejifunza mambo mengi na mazuri na kabla ya mafunzo nilikuwa sielewi kwamba barabarani nilikuwa naendesha hovyo hovyo tu na baada ya mafunzo nashukuru mpaka sasaivi nime elewa na tulikuwa wengi sana tukifundishwa awamu kwa awamu nafikiri bodaboda takriban 230 au 250 kwa Dodoma hapa na sasahivi wame elimika”, alisema Mayowa.

Alisema alama za barabarani ilikuwa ni changamoto kwa madereva wengi , walikuwa wanaziona lakini wanashindwa kuzitumia kama ipasavyo na walidhani ni michoro tu lakini baada ya mafunzo waliweza kuelewa aina za michoro na alama zinazotumiwa barabarani.

“Tulifundishwa kuna alama za onyo, alama za amri, kuna alama za maelekezo kwaio hayo yote tumefundishwa lakini pia nimefundishwa alama nyengine ambazo nilikuwa sizielewi vizuri kama alama za michoro juu ya sakafu ya barabara hizo nazo nilikuwa sizielewi nilikuwa naona tu michoro na sielewi maana yake lakini baada ya elimu nimevielewa vizuri” alisema Mayowa

Aidha alisisitiza kwa maafisa usafirishaji kubadilika  na kuwa na mahudhurio mazuri ya mafunzo yanayotolewa na shirika la AMEND Tanzania kwasababu yanafundishwa kwa vitendo pamoja na kutii sheria za barabarani.

“Tumefundishwa dereva kujihami kwaio wale ambao hawajapata mafunzo hawezi kuelewa na kutii sheria akiwa yupo barabarani na anaweza kusababisha ajali kwasababu anakuwa hana uelewa wowote na vigumu kujilinda anapotumia chombo chake”,Mayowa.

Naye afisa usafirishaji kutoka kituo cha Ndasha,Bw. Ally Rashid Ally alisema kuwa bodaboda ni ajira kama zilivyo ajira nyengine na imeteka soko kubwa la ajira kwa vijana kwenye upataji wa kipato na awali haikupewa thamani kama zilivyo biashara nyengine.

Amesema wamekuwa na madereva usafirishaji wengi lakini baadhi yao kwenye kundi hilo hawana elimu ya kutosha ya barabarani na kutambua alama zilizomo.

Aidha Bw. Ally amesema elimu iliyotewa ni msaada mkubwa kwa maafisa usafirishaji mkoani Dodoma kwani wengi wao wamekuwa na nidhamu iwapo wanatumia vyombo vyao barabarani na changamoto za ajali na vifo vimeweza kuepukika kutokana na maarifa waliopokea kutoka kwa wakufunzi kupitia shirika la AMEND Tanzania.

WIZARA YA KATIBA NA SHERIA KUENDELEA KUWEKA MIUNDOMBINU YA TEHAMA

Wizara ya katiba na Sheria imeendelea kusimamia uwekaji wa mifumo na miundombinu ya TEHAMA thabiti ili kuhakikisha wananchi wote wanafanikiwa na huduma za kisheria na wanafikiwa vizuri ikiwemo kupata elimu ya masuala ya sheria.

Hayo yameelezwa leo Januari 30,2024 jijini Dodoma na Waziri wa Katiba na Sheria Balozi Dkt.Pindi Chana wakati akikabidhi vifaa vya TEHAMA kwa taasisi za haki jinai.

"Masuala ya sheria ni vizuri wananchi nao wakayajua, uendeshaji wa kesi,upatikanaji wa nyaraka za kesi na ushahidi hukumu na maamuzi ya kesi na uwepo wa vyombo vya utoaji haki katika ngazi za jamii"Amesema 

Aidha amesema serikali imejidhatiti katika kuimarisha masuala ya utoaji na upatikanaji wa haki nchini

"Kama alivosema katibu Mkuu unapochelewesha haki ni kama mtu ananyimwa haki,nisingependa tuwe wacheleweshaji wa haki hizo"

Hata hivyo ameongeza kuwa taasisi za haki jinai zimejenga mifumo mizuri ya TEHAMA ambayo inarahisisha upatikanaji wa taarifa na huduma za kisheria kwa wananchi,kwa Wakati bila urasimu na kuepusha rushwa.

"Uwepo wa mifumo ya TEHAMA na matumizi ya teknologia utawapunguzia wananchi muda na gharama za kushughulikia masuala ya kisheria na badala yake watajikita zaidi katika shughuli za Kiuchumi na maendeleo"

Awali akimkaribisha Waziri wa Katiba na Sheria Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bi.Mary Makondo ameeleza Kuwa mradi huu umelenga kuimarisha matumizi na fursa za TEHAMA nchini ili kurahisisha upatikanaji wa haki

Pia kuimarika kwa matumizi ya TEHAMA kunawezesha kuziunganisha taasisi za haki jinai katika mfumo mmoja wa kielectronic katika kuwasiliana kiutendaji na hivyo kuimarisha ubora na upatikanaji wa huduma za kisheria zinazotolewa na taasisi hizi 

"Tangu kuanziashwa kwa mfumo huu Kazi zifuatazo zimetekelezwa ikiwa ni pamoja na upembuzi yakinifu wa mahitaji ya sekta ya sheria pamoja na haki jinai kuelekea haki mtandao,vile vile ujenzi wa miundombinu ya TEHAMA kwenye jengo la Wizara"Amesema

Aidha ameeleza Kuwa Wizara inaendelea kutumia fursa ya TEHAMA kwa kushirikiana na taasisi za serikali pamoja na wadau katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na kwa wakati.



Kwa upande wake Mkurugenzi mkuu wa Mashitaka nchini(DPP) Sylvester Mwakitalu akitoa salaam fupi za ofisi yake amesema ofisi ya Mashitaka imefarijika kupokea vifaa hivyo na vitawasaidia katika kuboresha utendaji wao wa kazi na katika kuwahudumia watanzania 


Aidha tunaamini vifaa hivi vitatusaidia katika kuhakikisha kwamba haki za wananchi tunaowahudumia zinapatikana kwa wakati

 

Naye Mkuu wa Gereza la Msalato SSP Flavian Justine ameeleza Kuwa vifaa hivyo kwao ni muhimu kwa kuhifadhi taarifa za wahalifu,lakini pia kwa kurahisisha taarifa za mawasiliano kati ya magereza na mahakama na kuipunguzia serikali gharama za kusafirisha wahalifu kuhudhuria mahakamani.

WANANCHI WAJITOLEA KUJENGA OFISI YA MTAA ZEGERENI





WAKAZI wa Mtaa wa Zegereni Wilayani Kibaha Mkoani Pwani wamejitolea kujenga ofisi ya kisasa ya Mtaa ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye eneo la ujenzi Mwenyekiti wa Mtaa huo Rashid Likunja amesema ofisi iliyopo ni ya zamani ambapo imejengwa miaka 20 iliyopita.

Naye Mtendaji wa Mtaa huo Femida Ayubu amesema kuwa wameweka utaratibu wa kila kaya kuchangia ujenzi huo ambao hufanywa kila Jumatano.

Kwa upande wake moja ya wananchi Leah Chambo amesema kuwa wanashirikiana na mtaa kwa kujitolea shughuli mbalimbali za maendeleo kwenye mtaa wao ili huduma ziwe bora.

Wednesday, January 31, 2024

DAWASA YATAKIWA KUPELEKA MAJI HOSP YA WILAYA LULANZI

HALMASHAURI ya Mji Kibaha imeitaka Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) Kibaha kufanya utaratibu wa kupeleka maji kwenye Hospitali ya Wilaya ya Lulanzi ambapo ni miezi mitatu imepita tangu kutolewa hela kiasi cha milioni 60.

Akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani Mwenyekiti wa Halmashauri Mussa Ndomba amesema kuwa fedha hizo zipo lakini wameshindwa kuzichukua.

Mussa amesema kuwa adha ya maji kwenye Hospitali ni kubwa sana kwa matumizi mbalimbali kwa wagonjwa wakiwemo mama wajawazito hali ni mbaya sana.

Akijibu hoja hiyo Meneja wa DAWASA Kibaha Alfa Ambokile amesema kuwa mradi huo tayari amesha andikia makao makuu juu ya fedha hizo kuchukuliwa.


Wednesday, January 17, 2024

WATUHUMIWA KUKUTWA NA NOTI BANDIA NA MASHINE YA KUZITENGENEZEA

WATU wanne wakazi wa Jijini Dar es Salaam wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Pwani kwa tuhuma za kukutwa na noti bandia zenye thamani ya shilingi milioni 1.5.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Kamanda wa Polisi Mkoani humo ACP Pius Lutumo alisema kuwa watuhumiwa hao pia walikutwa na mtambo wa kutengeneza fedha hizo.

Lutumo alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya mchana huko Kijiji cha Msata Wilaya ya Kipolisi Chalinze 

Alisema kuwa chanzo cha fedha hizo kukamatwa ni taarifa iliyotolewa na raia mwema ambaye alitilia mashaka noti ya shilingi 10,000 aliyoipokea kwa ajili ya malipo kwa huduma ya kulala nyumba ya wageni.

"Katika upelelezi baada ya tukio hilo Polisi walifanikiwa kukamata mtambo wa kutengenezea fedha hizo bandia na zana nyingine kama kompyuta, kemikali mbalimbali za kutengenezea fedha bandia,"alisema Lutumo.

Aidha alisema kuwa mtambo huo ulikamatwa kwa moja ya watuhumiwa huko Goba Jijini Dar es Salaam na watuhumiwa walikutwa na noti za shilingi elfu 10,000 noti 155.

"Baada ya mtuhumiwa wa kwanza kukamatwa na noti hiyo bandia ya shilingi 10,000 aliwataja watuhumiwa wengine watatu wakiwa na bandia milioni 1.2 zikiwa noti za shilingi elfu tano na elfu mbili,"alisema Lutumo.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Mbaraka Miraji (48), Zena Naringa (42) wakazi wa Buza, Masumbuko Kiyogoma mkazi wa Goba na Elias Wandiba (50) mkazi wa Kimara Suka Jijini Dar es Salaam.

Saturday, January 13, 2024

KATA YA MISUGUSUGU YAOMBA WADAU UKAMILISHWAJI JENGO LA WAZAZI

KATA ya Misugusugu Wilayani Kibaha Mkoani Pwani imeomba wadau mbalimbali kuwachangia kiasi cha shilingi milioni 39 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa jengo la mama na mtoto ili kuwaepusha wajawazito kujifungulia majumbani.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Diwani wa Kata hiyo Upendo Ngonyani kuwa wajawazito wengi wanajifungulia majumbani jambo ambalo ni la hatari kiafya.

Alisema kuwa Zahanati iliyopo haina huduma ya kujifungua licha ya kuwa na huduma nyingine za kitabibu isipokuwa za uzazi kutokana na kutokuwa na jengo la wazazi.

"Baada ya kuona changamoto ni kubwa ya akinamama kunifungua tulianzisha ujenzi kwa nguvu za wananchi kupitia wadau mbalimbali tumeweza kujenga jengo hilo la wazazi limeishia kwenye boma,"alisema Ngonyani.

Alisema kwa sasa wanaomba wadau ikiwemo Halmashauri kuwasaidia hatua iliyobaki ili jengo likamilike na kutoa huduma ambapo litanufaisha wananchi wa mitaa minne ya Vitendo, Karabaka, Misugusugu na Miomboni.

"Baadhi ya wajawazito hujifungulia nyumbani kutokana na kutokuwa na kipato wakihofia kwenda Hospitali kuwa gharama ni kubwa hivyo hujifungua kienyeji na wengine hukaa hadi siku ya mwisho ya kujifungua ndipo wanakwenda Hospitali,"alisema Ngonyani.

Aidha alisema wanapopata ujauzito huwa wanakwenda kliniki kwenye Zahanati ya Kata lakini inapofika muda wa kujifungua kwa wale wasio na uwezo hujifungulia nyumbani na kupeleka watoto kliniki kwa ajili ya chanjo mbalimbali.

"Kwa wale wenye uwezo inapofika muda wa kujifungua kwenye vituo vya afya Mkoani, Lulanzi au Mlandizi ambako ni mbali sana na hutumia gharama kubwa kwa usafiri ndiyo tukaona tujenge jengo hilo ili kuondoa changamoto hiyo,"alisema Ngonyani.

Alibainisha kuwa kuna madhara makubwa kwa wajawazito kujifungulia nyumbani kwani ni hatari ambapo mazazi au mtoto au wote wanaweza kupoteza maisha kwa kukosa huduma bora wakati wa kunifungua.

"Tunawapa elimu juu ya umuhimu wa kujifungulia Hospitali lakini wakati mwingine inakuwa vigumu kutokana na baadhi kuwa na kipato kidogo hivyo kushindwa kumudu gharama,"alisema Ngonyani.

Alizishukuru taasisi, wadau mbalimbali na wananchi kwa kujitolea hadi jengo hilo kufikia hapo na kuendelea kuwaomba waendelee kujitolea hadi litakapokamilika ili kunusuru maisha ya akinamama na watoto.

Mitaa hiyo minne ina jumla ya wakazi 8,000 na gharama za mwanzo za ujenzi wa jengi hilo la mama na mtoto limetumia zaidi ya shilingi milioni 20.