SERIKALI Kuu imeupatia Mkoa wa Pwani kiasi cha shilingi trilioni 1.1 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo imeainishwa kwenye ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Wednesday, November 22, 2023
PWANI YAMSHUKURU RAIS KWA KUIPATIA FEDHA ZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO.
Monday, November 20, 2023
MAOFISA TARAFA NA WATENDAJI KATA PWANI WATAKIWA KUWA WABUNIFU KULETA MAENDELEO KWA WANANCHI
Friday, November 17, 2023
TAASISI YA KUMBUKUMBU YA NYERERE YAADHIMISHA SIKU YA WATOTO NJITI DUNIANI YATOA MISAADA
KATIKA kuadhimisha siku ya watoto waliozaliwa kabla ya muda (Watoto Njiti) Duniani Tasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na baadhi ya wadau imetoa misaada kwa watoto njiti kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Mloganzila.
Monday, November 13, 2023
KAMATI YA BUNGE YA UWEKEZAJI WA MITAJI YA UMMA YARIDHISHWA MRADI WA MAJI WAMI AWAMU YA TATU.
KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma imetembelea mradi wa Maji wa Wami awamu ya tatu kwenye chanzo Mto Wami na kufurahishwa na jitihada za Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kuhakikisha huduma ya upatikanaji maji inakuwa ya uhakika.
Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa kamati hiyo Deus Sangu wakati wa ziara iliyofanywa kutembelea mradi huo kuangalia maendeleo ya mradi huo ambao kwa awamu zote umegharimu kiasi cha shilingi bilioni 160.
Sangu amesema kuwa wameridhishwa na jitihada za Dawasa na kuahidi kuendelea kuipambania ili iweze kukabili changamoto za upungufu wa maji na kupitia Bunge kati ya maazimio 14 mawili ni ya kuisaidia mamlaka hiyo.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa upatikanaji wa maji kwa mkoa huo ni asilimia 86 ambapo aliomba miradi itekelezwe vizuri ikizingatiwa ni mkoa wa uwekezaji wa viwanda na mahitaji ya maji kwa sasa ni makubwa kwani kuna ongezeko la watu na uwekezaji mkubwa ambapo bila ya maji hakuna uwekezaji.
Naye Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete ameishukuru kamati hiyo kwa kupambani Chalinze kupata maji kwani kwenye mikutano yake hakuna jambo ambalo lilikuwa kero kwa wananchi kuhitaji maji ambapo kwa sasa changamoto ya maji imepungua kwa kiasi kikubwa.
Awali akiwasilisha taarifa ya mradi huo wa awamu ya tatu Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa Kiula Kingu amesema kuwa maji yatazalishwa kutoka lita milioni saba hadi lita milioni 21 ambapo mabomba yatatandazwa kwa kilometa 124 na matenki 18 na kutakuwa na vituo vikubwa vya maji Miono, Msoga na Mboga.
Mwisho.
Monday, November 6, 2023
WAFANYABIASHARA WATAKIWA KULIPA KODI KWA HIYARI
WAFANYABIASHARA nchini wametakiwa kulipa kodi kwa hiyari ili wawe huru kufanyabiashara na kuchangia mapato ya serikali ili iweze kutoa huduma bora kwa wananchi.
Friday, November 3, 2023
MAGONJWA YAONGEZEKA MWINGILIANO WA BINADAMU WANYAMA NA MAZINGIRA
DODOMA.
SHUGHULI za kijamii na kiuchumi, mwenendo na mifumo ya maisha na mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi kumekuwa na ongezeko la magonjwa yanayoibuka kutokana na mwingiliano uliopo baina ya binadamu, wanyama na mazingira.
Hayo yamebainishwa leo jijini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu ( Sera, Bunge na Uratibu) Mhe.Jenista Mhagama , wakati akifungua kongamano la kitaifa la Afya Moja ambapo amesema kuwa duniani kote takriban visa bilioni 1 vya ugonjwa na mamilioni ya vifo hutokea kila mwaka kutokana na magonjwa yanayotoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu.
Aidha amezisihi Wizara za Kisekta kuwa na mipango ya kutekeleza na kuimarisha ushirikiano wa kisekta kwa kutumia mbinu ya Afya Moja na kila sekta kushiriki kikamilifu katika tafiti kuhusu magonjwa yanayoweza kuambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu, utunzaji wa mazingira, usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa, usalama wa chakula na lishe na magonjwa yasiyo ya kuambukiza.
Nao baadhi ya washiriki wa kongamano hilo wamesema kuwa dhana ya Afya moja faida yake ni njia inayowaleta pamoja na sekta mbalimbali ambapo ni afya, mifugo na wanyamapori ili kukabiliana na changamoto zinazohusiana na afya.
Kila ifikapo Novemba 3 ya kila mwaka wadau mbalimbali huadhimisha siku ya Afya Moja kwa lengo la kuimarisha uratibu na utendaji uliopo baina ya sekta katika kuzuia na kupunguza madhara pamoja na kujiandaa kukabiliana na majanga ya milipuko ya magonjwa ya binadamu, wanyama na mimea ambapo kauli mbiu mwaka huu inasema “Afya Moja: Mbinu ya Pamoja kuboresha afya ya binadamu, wanyama, mimea na mfumo wa ikolojia kwa ustahimilivu wa maafa.
SHUGHULI ZA KIJAMII NA KIUCHUMI ZACHANGIA ONGEZEKO LA MAGONJWA
DODOMA.
IMEELEZWA kuwa shughuli za kijamii na kiuchumi, mwenendo na mifumo ya maisha na mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi kumekuwa na ongezeko la magonjwa yanayoibuka kutokana na mwingiliano uliopo baina ya binadamu, wanyama na mazingira.
Hayo yamebainishwa leo jijini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu ( Sera, Bunge na Uratibu) Mhe.Jenista Mhagama , wakati akifungua kongamano la kitaifa la Afya Moja ambapo amesema kuwa duniani kote takriban visa bilioni 1 vya ugonjwa na mamilioni ya vifo hutokea kila mwaka kutokana na magonjwa yanayotoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu.
Aidha amezisihi Wizara za Kisekta kuwa na mipango ya kutekeleza na kuimarisha ushirikiano wa kisekta kwa kutumia mbinu ya Afya Moja na kila sekta kushiriki kikamilifu katika tafiti kuhusu magonjwa yanayoweza kuambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu, utunzaji wa mazingira, usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa, usalama wa chakula na lishe na magonjwa yasiyo ya kuambukiza.
Nao baadhi ya washiriki wa kongamano hilo wamesema kuwa dhana ya Afya moja faida yake ni njia inayowaleta pamoja na sekta mbalimbali ambapo ni afya, mifugo na wanyamapori ili kukabiliana na changamoto zinazohusiana na afya.
Kila ifikapo Novemba 3 ya kila mwaka wadau mbalimbali huadhimisha siku ya Afya Moja kwa lengo la kuimarisha uratibu na utendaji uliopo baina ya sekta katika kuzuia na kupunguza madhara pamoja na kujiandaa kukabiliana na majanga ya milipuko ya magonjwa ya binadamu, wanyama na mimea ambapo kauli mbiu mwaka huu inasema “Afya Moja: Mbinu ya Pamoja kuboresha afya ya binadamu, wanyama, mimea na mfumo wa ikolojia kwa ustahimilivu wa maafa.