Friday, May 9, 2014

VIJANA KUSAIDIWA NA RED CROSS

Na John Gagarini, Kibaha
ASASI isiyo ya Kiserikali ya Amani Development Organization (ADEO) la Kibaha mkoani Pwani limetenga kiasi cha shilingi milioni 10 kwa ajili ya kuwakopesha wasichana waliokuwa wakifanyabiashara ya ngono na matumizi ya dawa za kulevya zaidi ya 20.
Mbali ya kuwakopesha fedha hizo pia shirika hilo linawapatia elimu ya kuepukana na mambo hayo ambayo yamekuwa chanzo cha maambukizi ya magonjwa ukiwemo UKIMWI.
Akizungumza jana mjini Kibaha kwenye mkutano shirikishi wa utekelezaji wa programu ya vijana kupambana na UKIMWI inayofadhiliwa na Sat Tanzania, mratibu wa shirika hilo Jane Apollo alisema kuwa lengo la kuwakopesha fedha hizo ni kuwapatia njia mbadala ili wajiepushe na vitendo hivyo.
Apollo alisema kuwa kupitia mpango huo umeweza kuwafikia vijana wa ndani na nje ya shule 3,817 ambapo kati yao wasichana wanaofanya biashara ya ngono 41 wanaume 11 wanaofanya mapenzi ya jinsia moja, vijana 63 wanaotumia dawa za kulevya na machimbo sita ya mchanga.
"Lengo ni kuwafanya vijana kuachana na vitendo vya matumizi ya dawa za kulevya na biashara ya ngono na kuwafundisha shughuli za ujasiriamali ili kuinua kipato chao na kupunguza umaskini katika maisha yao," alisema Apollo.
Moja ya waischana waliokuwa wakifanya biashaya ya ngono (Subira Hatibu) Jasmini siyo jina halisi alisema kuwa alikuwa akiishi Jijini Dar es Salaam na kujiuza kwa wanaume ambapo kwa siku alikuwa akitembea na wanaume watatu au wanne.
"Nilikuwa nikifanya biashara ya kujiuza kuanzia shilingi 50,000 hadi 30,000 kwa mtu mmoja ambapo nilifanya biashara hii kwa muda mrefu lakini sikuona faida yake zaidi ya kupata matatizo," alisema Jasmini.
Naye kijana aliyejitambulisha kwa jina la Omary Mkumba alisema kuwa alikuwa akijihusisha na uvutaji wa bangi pamoja na dawa za kulevya ambazo zilimsababisha kupata ugonjwa wa kifua kikuu lakini baada ya kupatiwa elimu aliamua kuachana na matumizi hayo.
Shirika hilo lilianzishwa mwaka 2010 na linajihusisha na mapambano dhidi ya dawa za kulevya, UKIMWI, biashara ya ngono, mimba za utotoni, ndoa kwenye umri mdogo na afya ya uzazi.
mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA cha Msalaba Mwekundu mkoani Pwani kimtoa misaada ya viatu na vifaa vya shule kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Nyumbu na vituo vya kulelea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu.
Chama hicho kilitoa misaada hiyo kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi hao waweze kusoma kwa kuwa na mahitaji muhimu ili kufanikisha masomo yao.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mara baada ya sherehe ya siku ya chama hicho inayoadhimishwa kila mwaka ambapo bkitaifa ilifanyika mkoani Mbeya, katibu msaidizi wa msalaba mwekundu mkoani humo, Felisiana Mmasi alisema kuwa waliamua kuadhimisha siku hiyo kwa kuwasaidia wanafunzi.
Mmasi alisema kuwa lengo la chama hicho ni kuwasaidia watu wenye matatizo mbalimbali kwenye jamii ikiwa ni pamoja na kutoa msaada kwenye majanga na maafa yanoyojitokeza ikiwa ni pamoja na ajali, mafuriko na kwenye vita.
"Mbali ya kutoa viatu pia tumetoa madaftari na kalamu ambapo vituo vya watoto waishio kwenye mazingira magumu vya THADEI na Buloma wamenufaika na misaada hiyo," alisema Mmasi.
Naye mratibu wa mradi wa Life kupitia chama hicho Kibaha Mjini Agnes Lubogo alisema kuwa mbali ya kusaidia kutoa misaada mbalimbali pia wanasaidia kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI walio majumbani.
Lubogo alisema kuwa wanahudumia wagonjwa ambao watoro ambao hawapati huduma mahospitalini hivyo kuwafuata huko waliko ambapo wana wahudumu wa nyumbani wapatao 73.
Aliwataka watu kujiunga na chama hicho ili waweze kuisaidia jamii ambayo inahitaji misaada mbalimbali ya kiutu ikiwa ni pamoja na kujitolea damu kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa.
mwisho. 

   
Na John Gagarini, Kibaha
ASASI isiyo ya Kiserikali ya Amani Development Organization (ADEO) la Kibaha mkoani Pwani limetenga kiasi cha shilingi milioni 10 kwa ajili ya kuwakopesha wasichana waliokuwa wakifanyabiashara ya ngono na matumizi ya dawa za kulevya zaidi ya 20.
Mbali ya kuwakopesha fedha hizo pia shirika hilo linawapatia elimu ya kuepukana na mambo hayo ambayo yamekuwa chanzo cha maambukizi ya magonjwa ukiwemo UKIMWI.
Akizungumza jana mjini Kibaha kwenye mkutano shirikishi wa utekelezaji wa programu ya vijana kupambana na UKIMWI inayofadhiliwa na Sat Tanzania, mratibu wa shirika hilo Jane Apollo alisema kuwa lengo la kuwakopesha fedha hizo ni kuwapatia njia mbadala ili wajiepushe na vitendo hivyo.
Apollo alisema kuwa kupitia mpango huo umeweza kuwafikia vijana wa ndani na nje ya shule 3,817 ambapo kati yao wasichana wanaofanya biashara ya ngono 41 wanaume 11 wanaofanya mapenzi ya jinsia moja, vijana 63 wanaotumia dawa za kulevya na machimbo sita ya mchanga.
"Lengo ni kuwafanya vijana kuachana na vitendo vya matumizi ya dawa za kulevya na biashara ya ngono na kuwafundisha shughuli za ujasiriamali ili kuinua kipato chao na kupunguza umaskini katika maisha yao," alisema Apollo.
Moja ya waischana waliokuwa wakifanya biashaya ya ngono (Subira Hatibu) Jasmini siyo jina halisi alisema kuwa alikuwa akiishi Jijini Dar es Salaam na kujiuza kwa wanaume ambapo kwa siku alikuwa akitembea na wanaume watatu au wanne.
"Nilikuwa nikifanya biashara ya kujiuza kuanzia shilingi 50,000 hadi 30,000 kwa mtu mmoja ambapo nilifanya biashara hii kwa muda mrefu lakini sikuona faida yake zaidi ya kupata matatizo," alisema Jasmini.
Naye kijana aliyejitambulisha kwa jina la Omary Mkumba alisema kuwa alikuwa akijihusisha na uvutaji wa bangi pamoja na dawa za kulevya ambazo zilimsababisha kupata ugonjwa wa kifua kikuu lakini baada ya kupatiwa elimu aliamua kuachana na matumizi hayo.
Shirika hilo lilianzishwa mwaka 2010 na linajihusisha na mapambano dhidi ya dawa za kulevya, UKIMWI, biashara ya ngono, mimba za utotoni, ndoa kwenye umri mdogo na afya ya uzazi.
mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA cha Msalaba Mwekundu mkoani Pwani kimtoa misaada ya viatu na vifaa vya shule kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Nyumbu na vituo vya kulelea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu.
Chama hicho kilitoa misaada hiyo kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi hao waweze kusoma kwa kuwa na mahitaji muhimu ili kufanikisha masomo yao.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mara baada ya sherehe ya siku ya chama hicho inayoadhimishwa kila mwaka ambapo bkitaifa ilifanyika mkoani Mbeya, katibu msaidizi wa msalaba mwekundu mkoani humo, Felisiana Mmasi alisema kuwa waliamua kuadhimisha siku hiyo kwa kuwasaidia wanafunzi.
Mmasi alisema kuwa lengo la chama hicho ni kuwasaidia watu wenye matatizo mbalimbali kwenye jamii ikiwa ni pamoja na kutoa msaada kwenye majanga na maafa yanoyojitokeza ikiwa ni pamoja na ajali, mafuriko na kwenye vita.
"Mbali ya kutoa viatu pia tumetoa madaftari na kalamu ambapo vituo vya watoto waishio kwenye mazingira magumu vya THADEI na Buloma wamenufaika na misaada hiyo," alisema Mmasi.
Naye mratibu wa mradi wa Life kupitia chama hicho Kibaha Mjini Agnes Lubogo alisema kuwa mbali ya kusaidia kutoa misaada mbalimbali pia wanasaidia kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI walio majumbani.
Lubogo alisema kuwa wanahudumia wagonjwa ambao watoro ambao hawapati huduma mahospitalini hivyo kuwafuata huko waliko ambapo wana wahudumu wa nyumbani wapatao 73.
Aliwataka watu kujiunga na chama hicho ili waweze kuisaidia jamii ambayo inahitaji misaada mbalimbali ya kiutu ikiwa ni pamoja na kujitolea damu kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa.
mwisho. 

   

Tuesday, May 6, 2014

WASAIDIZI WA SHERIA WATAKA KUTAMBULIWA

Na John Gagarini, Kibaha
KITUO cha Msaada wa Kisheria wilayani Kibaha mkoani Pwani kimeiomba serikali kuwatambua wasaidizi wa kisheria ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi.
Kutokana na changamoto nyingi za kisheria kuikabili jamii na watu wengi kukosa haki zao kwa kushindwa kujua sheria ambazo ndo msingi wa haki za binadamu wasaidizi hao.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mafunzo kwa wasaidizi wa kisheria wa wilaya ya Kibaha ambayo yalitolewa na kituo cha msaada wa kisheria kwa wanawake (WLAC), mwenyekiti wa kituo hicho Israel Sazia alisema kuwa wasaidizi hao bado hawajatambuliwa rasmi na serikali.
Sazia alisema kuwa endapo wasimamizi wa msaada wa kisheria watatambuliwa wataweza kuisaidia jamii kutambua sheria mbalimbali ambazo zitawafanya wapate haki zao mara inapotokea migogoro kwenye jamii.
"Endapo watatambuliwa itasaidia hata kuwapatiwa misaada na fursa mbalimbali kutoka serikalini kupitia kwenye halmashauri kwa ajili ya kuiwezesha jamii katika masuala yanayohusu sheria," alisema Sazia.
Alisema kuwa wananchi wengi hawajui taratibu za kutafuta haki ikiwa ni pamoja na wanawake kwenye masuala mbalimbali endapo watashindwa kuendelea kuishi na mume wake pamoja hivyo kudai talaka.
"Kumekuwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na masuala ya mirathi, haki za watoto, migogoro ya ardhi na masuala ya ndoa ambazo zimekuwa zikileta migogoro mingi kwenye jamii," alisema Sazia.
Aidha alisema kuwa kituo chao kilichoanzishwa mwaka 2001 kimekuwa na changamoto kubwa ya wasaidizi hao kulegalega katika utendaji kazi kutokana na wengi wao kushindwa kujitolea hivyo kushindwa kufanya kazi kikamilifu.
Aliwataka wasaidizi hao wa kisheria kufanya kazi kwa kuzingatia weledi wa kazi zao ili kuweza kuisaidia jamii ambayo ina mahitaji makubwa ya kujua sheria mbalimbali katika maeneo yao ili waweze kupata haki zao za msingi.
Baadhi ya masomo waliyofundishwa ni pamoja na uelewa kuhusu dhana ya ya msaidizi wa kisheria, misingi na vyanzo vya sheria, sheria ya ndoa, sheria ya mirathi na taratibu za ufunguaji wa mirathi, sheria ya ardhi sura namba 113, sheria ya utatuzi wa migogoro ya ardhi ya mwaka 2002, haki ya mtoto ya mwaka 1999 na ukusanyaji na utunzaji wa taarifa za wateja na uandishi wa ripoti ya mwezi. Mafunzo hayo yaliwahusisha wasaidizi zaidi ya 30.
mwisho. 
 

Wednesday, April 30, 2014

AJINYONGA KWA RAFIKI YAKE KWA KUTUMIA KANGA

Na John Gagarini, Kibaha
KIJANA Victor Wilfred (29) mkazi wa  Keko amekatisha uhai wake kwa kujinyonga kwa kutumia kanga aliyoifunga kwenye dirisha la chumba cha rafiki yake.
Marehemu kabla ya kujinyonga aliacha ujumbe usemao kuwa anaomba samahani ndugu zake kwa kufanya kitendo hicho cha kujitoa uhai hata hivyo hakuweza kuweka wazi kwamba aliamua kujiua kwa sababu gani.
Tukio hilo lilitokea Aprili 30 mwaka huu majira ya asubuhi eneo la Maili Moja Shuleni wilayani Kibaha mkoani Pwani ambapo umati wa watu ulikuwa umejazana kushuhudia tukio hilo la kusikitisha.
Akithibitisha kutokea tukio hilo kamanda wa Polisi mkoani Pwani Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Ulrich Matei alisema kuwa tukio hilo ambalo lilitokea kwenye sebule ya chumba cha Emanuel Lawrance mkazi wa Keko Jijini Dar es Salaam ambaye amepangisha nyumba kwa Emanuel Msengi marehemu alikuwa mgeni kwenye nyumba hiyo na alifika kwa lengo la kutafuta kazi.
"Marehemu aliachwa na rafiki yake ambaye alikuwa amekwenda kazini na kwa kuwa rafiki yake alimuahidi kumtafutia kazi na aliporudi alikuta marehemu kajinyonga kwa kutumia kanga kwenye dirisha la chumba hicho," alisema Kamanda Matei
Hata hivyo marehemu aliacha ujumbe kwenye karatasi lililokutwa pembeni ya mwili wake kuwa kutokanana na kifo chake ana omba samahani na asisumbuliwe mtu yoyote kwani kaamua kujiua yeye mwenyewe.
mwisho.

SIMBA YANGA ZAPEWA SOMO

Na John Gagarini, Kibaha
TIMU za soka za Simba na Yanga zimetakiwa kujipanga ili ziweze kupata mafanikio kama ilivyo klabu ya Azam ambayo imepongezwa na Shirikisho la Soka la Miguu la Dunia (FIFA) kwa kuweza kuwa klabu ambayo imepata mafanikio kwa kipindi kifupi tangu kuanzishwa kwake.
Wito huo umetolewa na mdau wa soka wilayani Kibaha mkoani Pwani, Fahim Lardhi alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi na kusema kuwa Azam imeweza kuzipiku Simba na Yanga kwa mafanikio licha ya timu hizo kuanzishwa miaka zaidi ya 50 iliyopita.
Lardhi alisema kuwa Azam imeanzishwa miaka 9 iliyopita lakini imepata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kuwa na uwanja wa kisasa ambao una kidhi haja ya kuwa uwanja ambao unaweza kutumia na timu kubwa kama ilivyo kwa timu za Ulaya.
“Timu za Simba na Yanga zimebaki kuwa timu za malumbano tu badala ya kufikiria masuala ya kimaendeleo kama ilivyo kwa timu ya Azam ambayo ni timu changa katika ramani ya soka hapa nchini na hata barani Afrika,” alisema Lardhi.
Aidha alisema kuwa ili kuleta mafanikio kwenye timu lazima timu hizo zibadili mifumo ya wanachama ili wazichangie timu zao badala ya wao kutaka timu hizo ziwanufaishe hali ambayo inasababisha zishindwe kupata mafanikio.
“Inashangaza kuona timu hizo zinakosa viwanja jambo ambalo linatia aibu ambapo zimebaki kusema tu kuwa zitajenga viwanja matokeo yake yamebaki maneno tu ya kujenga viwanja vyao vya kisasa,” alisema Lardhi.
Alivitaka vilabu hivyo kuwa na mifumo kama ya ulaya ili viweze kupata maendeleo na kuachana na mifumo ambayo haina tija zaidi ya kuleta malumbano na kuzitaka zijifunze kupitia timu ya Azam ambayo inaendeshwa kitaalamu.
Na John Gagarini, Kibaha
MASHINDANO ya kutafuta timu ya wilaya ya Kibaha mkoani Pwani kwa Umoja wa Shule za Sekondari na Sanaa Tanzania (UMISSETA) yanatarajiwa kuanza kutimua vumbi Mei 3 mwaka huu.
Timu hiyo ambayo itaundwa na wachezaji 125 wa michezo mbalimbali inatarajiwa kuchuana kwenye uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha Tumbi ambapo kwa sasa timu hizo zinacheza ngazi ya Kanda ili kupata timu moja ya wilaya.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jana mjini Kibaha mratibu wa mashindano hayo Rajab Kauta alisema kuwa kwa sasa mashindano hayo ya kanda ndogo yanaendelea kwenye vituo vinne ambavyo ni Kibaha Sekondari, Kongowe, Tanita na Kilangalanga.
“Mashindano haya ya kanda ndogo yanshirikisha jumla ya 43 kutoka halmashauri ya Mji wa Kibaha na Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ambapo kila kituo kina wachezaji 125 na baada ya hapo watakutana kupata timu moja ya wilaya,” alisema Kauta
Kauta alisema kuwa michezo hiyo inachezwa kila Jumamosi ili kutoathiri masomo na mara bada ya kumalizika mashindano ya kanda ndogo ndipo wataunda timu moja ili kupata timu ya wilaya hiyo.
“Mashindano ya mkoa yatafanyika Bagamoyo kuanzia Mei 27 na tunaamini tutapata timu nzuri licha ya changamoto zilizojitokeza ikiwa ni pamoja na shule nyingi kutokuwa na viwanja vya michezo, viwanja vingi kujaa maji kutokana na mvua kubwa kunyesha, upungufu wa vifaa vya michezo ,” alisema Kauta.
Aliwaomba wadau kushirikiana na shule ili kusaidia kuboresha viwanja kwenye mashule pmaoja na upatikanaji wa vifaa ili kuweza kupata vijana wenye uwezo.
Mwisho.    

Monday, April 28, 2014

AFA KWA MPENZI AKIJARIBU KUTOA MIMBA

Na John Gagarini, Kibaha
MWANAFUNZI wa Chuo cha Eden Hill (EDHICO) kilichopo mtaa wa KwaMfipa
wilayani Kibaha mkoani Pwani Attu Gabriel anayekadiriwa kuwa na umri
kati ya miaka (18) na (19)  amekutwa amekufa kwenye nyumba ya mpenzi
wake kwa kile kinachodaiwa kutaka kutoa mimba.
Awali mwanafunzi huyo aliomba ruhusa kwenye uongozi wa chuo hicho
Jumanne ya wiki hii kuwa anakwenda kumuuguza ndugu yake ambaye alikuwa
amelazwa kwenye hospitali ya Amana Jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa mjumbe wa serikali ya mtaa wa Kwamfipa, Emanuel Kilasa
alisema kuwa tukio hilo limetokea jana majira kati ya saa 9 au 10
alfajiri nyumbani kwa mpenzi wake Hafidh Mohamed (22) ambaye alikimbia
mara baada ya tukio hilo.
Kilasa alisema kuwa marehemu alikutwa na mauti ambapo tangu alipoomba
ruhusa hiyo alikuwa kwa mpenzi wake jirani na chuo hicho na kujaribu
kutoa mimba lakini hakufanikiwa.
"Tulipoingia kwenye chumba cha mpenzi wake tulikuta kuna vitu kadhaa
zikiwemo vidonge, chipsi, sukari na inasadikiwa kuwa alikuwa akijaribu
kutoa mimba," alisema Kilasa.
Alisema kuwa mpenzi wa marehemu siku ya tukio alikwenda kwa mama yake
mzazi  aitwaye Zaina Said na kumwambia kuwa alilala na mpenzi wake
lakini haamki.
"Mama yake alipofika alimwambia kuwa marehemu ameshakufa hivyo aende
akamwambie mwenyekiti wa serikali ya mtaa ndipo alipokimbia kutokana
na tukio hilo," alisema Kilasa.
Aidha alisem akuwa baada ya tukio hilo walitoa taarifa polisi ambapo
walifika na kuuchukua mwili wa marehemu ambaye alikuwa akiishi hosteli
nyumbani kwao ikiwa ni Makambako mkoani Iringa.
Naye baba mdogo wa kijana ambaye ni mpenzi wa marehemu Lukanda Omary
alisema kuwa yeye alipata taarifa majira ya saa 3 asubuhi lakini awali
kijana huyo alisemekana kabla ya kifo hicho alisikika akiongea na
daktari ambaye bado hajafahamika akimwambia ampe marehemu chai.
"Inasemekana marehemu alikuwa akijaribu kutoa mimba lakini hali ikawa
mbaya na kujaribu kuwasiliana na daktari juu ya nini cha kufanya hivyo
inavyoonekana binti huyo alikuwa kwenye zoezi la utoaji mimba,"
alisema Omary.
Kwa upande wake Kamanda wa polisi mkoani Pwani Kamishna Msaidizi wa
Polisi (SACP) Ulrich Matei alithibitisha kutokea tukio hilo na kusema
kuwa bado yuko hospitali ili kufanya uchunguzi kujua chanzo cha kifo
chake.
mwisho.

AFA KWA KUVUTWA SEHEMU ZA SIRI NA MKEWE

Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la Polisi mkoani Pwani linamshikilia Husna Iddi (16) mkazi wa
Tarafa ya Vikindu kata ya Kisemvule wilaya ya mkuranga mkoani Pwani ka
tuhuma za kusababisha mauaji ya mumewe baada ya kudaiwa kumvuta sehemu
zake za  siri.
Inadaiwa kuwa wanandoa hao walikuwa na ugomvi wa kimapenzi hali
iliyosababisha ugomvi kati yao hali iliyosababisha kutokea kwa tukio
hilo la kusikitisha.
Kwa mujibu wa kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msaidizi
Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ulrich Matei alithibitisha kutokea kwa
tukio hilo na alimtaja marehemu kuwa ni Jumanne Mwarami (21).
Kamanda Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Aprili 24 mwaka huu
majira ya saa 2:00 usiku ambapo wakiwa nyumbani na mke wake
kulijitokeza ugomvi kati yao kwa marehemu kumtuhumu mke wake huyo kuwa
siyo mwaminifu katika ndoa yao na ana mahusiano na wanaume wengine
nje.
"Baada ya kutokuwepo kwa maelewano kati yao na ugomvi huo kuwa mkubwa
ndipo mke wake huyo alimshambulia na kumvuta mume wake sehemu zake za
siri hali iliyopelekea kupoteza maisha wakati akipatiwa matibabu
kwenye Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga," alisema Kamanda Matei.
Katika hatua nyingine,Jeshi la Polisi linawashikilia watu watatu kwa
kosa la kukutwa na bangi nusu kilo huko kitongoji cha Mwandege Wilaya
ya Mkuranga.
Watuhumiwa hao ni Seleman Sahdi Ngota (35), KasimuOmari Mlumbita (25)
na Salumu Yusufu Athumani ambao watafikishwa mahakamani mara upelelezi
utakapokamilika.
Mwisho.