Monday, October 3, 2016

MWANAMKE ATUMIKA WIZI CWT WALINZI WAWILI WASHIKILIWA

Na John Gagarini, Kibaha

JESHI la la polisi mkoani Pwani linawashikilia walinzi wawili wa jengo la ofisi ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) mkoa baada ya watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi kuvunja na kuiba fedha kiasi ambacho bado hakijajulikana na computer za ofisi hizo.

Akizungumzia na waandishi wa habari mjini Kibaha kuhusiana na tukio hilo katibu wa (CWT) Nehemiah Joseph amesema kuwa tukio limetokea usiku wa octoba mosi kuamkia octoba 2 mwaka huu.

Joseph amewataja walinzi hao kutoka kampuni ya Noble security Tanzania Ltd ya Kibaha kuwa ni Hamad Kisoki (32) mkazi wa Maili Moja na Said Mohammed (39) mkazi wa Mwanalugali.

Amesema siku ya tukio walinzi waliotakiwa kuingia zamu walikuwa ni wawili lakini Said Mohammed pekee ndiye aliyefika kazini na mwenzake Hamad Kisoki haikuweza kufahamika mara moja ni kwa sababu gani hakuingia kazini.

Aidha amesema kuwa Said Mohamed alipokuwa kwenye lindo lake anadaiwa kupatiwa chips na juisi vinavyosemekana kuwa na madawa ya kulevya kutoka kwa mwanamke asiyefahamika.

Katibu huyo wa CWT mkoa wa Pwani ameeleza kuwa baada ya kupatiwa chakula hicho mlinzi alipoteza fahamu na hivyo kutoa mwanya kwa watu hao kuvunja milango ya ofisi hizo na kuingia na kuiba vitu hivyo ambavyo thamani yake bado haijafahamika.

Ametaja ofisi zilizopo kwenye jengo hilo ambazo zimeibiwa ni pamoja na CWT mkoa ,CWT wilaya,beem financial services (BFS) ,Chodawu,Tuico na TCCIA ambapo kwasasa wameshafikisha taarifa hizo polisi kwa hatua zaidi na ofisi ya chama hicho imeshakaa na taasisi zote zilizopanga jengo hilo kufanya tathmini.

hata hivyo amesikitishwa sana kutokea kwa wizi huo na kushangazwa na mlinzi huyo kula ama kununua vyakula kwa watu wasiowajua kwani kwa kufanya hivyo kumesababisha kuwapa wahalifu urahisi kutekeleza tukio hilo ambalo limesababisha hasara kwa wamiliki wa ofisi hizo.

Kwa upande wake kamanda wa polisi mkoani Pwani,Bonaventure Mushongi ,amekiri kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema taarifa ya tukio hilo ilitolewa  saa 5 asubuhi kutoka kwa Elizabeth Thomas ambae ni katibu wa chama CWT wilaya ya Kibaha huko mkoani A ,kata ya Tumbi.

Mushongi amesema kuwa baada ya kufanya wizi huo watu hao walitokomea kusikojulikana na jeshi hilo bado linawatafuta,huku akiomba ushirikiano kwa wananchi kuwafichua watu wanaowadhania kuhusika na wizi huo na kwasasa wanawashikilia walinzi hao kwa ajili ya uchunguzi juu ya tukio hilo.

Mwisho













      

No comments:

Post a Comment