Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la la polisi mkoani Pwani linawashikilia
walinzi wawili wa jengo la ofisi ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) mkoa baada
ya watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi kuvunja na kuiba fedha kiasi ambacho
bado hakijajulikana na computer za ofisi hizo.
Akizungumzia na waandishi wa habari mjini Kibaha kuhusiana
na tukio hilo katibu wa (CWT) Nehemiah Joseph amesema kuwa tukio limetokea
usiku wa octoba mosi kuamkia octoba 2 mwaka huu.
Joseph amewataja walinzi hao kutoka kampuni ya
Noble security Tanzania Ltd ya Kibaha kuwa ni Hamad Kisoki (32) mkazi wa Maili Moja
na Said Mohammed (39) mkazi wa Mwanalugali.
Amesema siku ya tukio walinzi waliotakiwa kuingia
zamu walikuwa ni wawili lakini Said Mohammed pekee ndiye aliyefika kazini na
mwenzake Hamad Kisoki haikuweza kufahamika mara moja ni kwa sababu gani
hakuingia kazini.
Aidha amesema kuwa Said Mohamed alipokuwa kwenye
lindo lake anadaiwa kupatiwa chips na juisi vinavyosemekana kuwa na madawa ya
kulevya kutoka kwa mwanamke asiyefahamika.
Katibu huyo wa CWT mkoa wa Pwani ameeleza kuwa baada
ya kupatiwa chakula hicho mlinzi alipoteza fahamu na hivyo kutoa mwanya kwa
watu hao kuvunja milango ya ofisi hizo na kuingia na kuiba vitu hivyo ambavyo
thamani yake bado haijafahamika.
Ametaja ofisi zilizopo kwenye jengo hilo ambazo
zimeibiwa ni pamoja na CWT mkoa ,CWT wilaya,beem financial services (BFS)
,Chodawu,Tuico na TCCIA ambapo kwasasa wameshafikisha taarifa hizo polisi kwa
hatua zaidi na ofisi ya chama hicho imeshakaa na taasisi zote zilizopanga jengo
hilo kufanya tathmini.
hata hivyo amesikitishwa sana kutokea kwa wizi huo na
kushangazwa na mlinzi huyo kula ama kununua vyakula kwa watu wasiowajua kwani
kwa kufanya hivyo kumesababisha kuwapa wahalifu urahisi kutekeleza tukio hilo
ambalo limesababisha hasara kwa wamiliki wa ofisi hizo.
Kwa upande wake kamanda wa polisi mkoani Pwani,Bonaventure
Mushongi ,amekiri kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema taarifa ya tukio hilo
ilitolewa saa 5 asubuhi kutoka kwa
Elizabeth Thomas ambae ni katibu wa chama CWT wilaya ya Kibaha huko mkoani A
,kata ya Tumbi.
Mushongi amesema kuwa baada ya kufanya wizi huo
watu hao walitokomea kusikojulikana na jeshi hilo bado linawatafuta,huku
akiomba ushirikiano kwa wananchi kuwafichua watu wanaowadhania kuhusika na wizi
huo na kwasasa wanawashikilia walinzi hao kwa ajili ya uchunguzi juu ya tukio
hilo.
Mwisho
No comments:
Post a Comment