MBIO za Mwenge zimekagua eneo la mradi wa maegesho ya magari makubwa ambao utakapokamilika utaiingizia Halmashauri ya Mji Kibaha kiasi cha shilingi bilioni 3.3 kwa mwaka.
Thursday, April 3, 2025
KIONGOZI MBIO ZA MWENGE ASIFU MRADI WA MAEGESHO YA MALORI YA MIZIGO
Wednesday, April 2, 2025
KIONGOZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA AFURAHISHWA MRADI MAEGESHO YA HALMASHAURI YA MJI KIBAHA
Tuesday, April 1, 2025
TAASISI YA BEGA KWA BEGA NA TANZANIA PWANI YACHANGIA DAMU CHUPA 19
Monday, March 31, 2025
NMB KUTUMIA ZAIDI YA BILIONI 6 MIRADI YA MAENDELEO
BENKI ya inatarajia kutumia kiasi cha shilingi bilioni 6.4 kwa ajili ya kuchangia shughuli za maendeleo kwa mwaka wa 2025.
Sunday, March 30, 2025
WAZIRI MKUU MAJALIWA AUPIGIA DEBE UWANJA WA SHIRIKA LA ELIMU KIBAHA KUTUMIWA NA TIMU ZA CHAN NA AFCON
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameupigia debe uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha kutumiwa na Timu za Taifa zitakazokuwa zinajiaandaa na michuano ya CHAN na AFCON kwa ajili ya mazoezi.
WAZIRI MKUU MAJALIWA ARIDHISHWA MAANDALIZI UZINDUZI WA MWENGE WA UHURU PWANI 2025
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ametembelea kuangalia maandalizi ya uwanja utakaotumika kuzindua mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2025 mkoani Pwani.
Majaliwa alitembelea uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha kuangalia maandalizi ya uzinduzi huo na kuridhishwa na maandalizi hayo na kutaka wakamilishe sehemu ambazo bado hazijakamilika.
Alisema kuwa ameridhishwa na maandalizi hayo ambapo pia alitumia muda huo kutembelea watoto wa halaiki na kusema amefurahishwa na jinsi walivyokuwa na hamasa ya uzinduzi huo.
"Nawapongeza kwa maandalizi mnayoendelea nayo nimeridhishwa kamilisheni sehemu zilizosalia ili kukamilisha mapema,"alisema Majaliwa.
Alisema kuwa amefurahishwa kuona viongozi wakiwemo mawaziri na makatibu wakuu wakiwa mstari wa mbele kuhakikisha maandalizi yanakuwa mazuri.
"Alikeni hata mikoa ya jirani Dar es Salaam, Morogoro na Tanga na watu mbalimbali kwani hili ni jambo la kitaifa shirikisheni wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ili hamasa iwe kubwa,"alisema Majaliwa
Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Watu Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete maandalizi yako vizuri ila baadhi ya maeneo ikiwemo katikati ya uwanja ndiyo kunahitaji marekebisho kidogo.
Kikwete alisema kuwa mialiko kwa wageni mbalimbali imetolewa ikiwa ni pamoja na wakuu wa mikoa, wakurugenzi na watu wengine ili kushiriki uzinduzi huo.
Friday, March 28, 2025
VIJANA WAFUNDISHWE UMUHIMU WA MBIO ZA MWENGE
