Thursday, April 3, 2025

KIONGOZI MBIO ZA MWENGE ASIFU MRADI WA MAEGESHO YA MALORI YA MIZIGO

MBIO za Mwenge zimekagua eneo la mradi wa maegesho ya magari makubwa ambao utakapokamilika utaiingizia Halmashauri ya Mji Kibaha kiasi cha shilingi bilioni 3.3 kwa mwaka.

Akikagua na kupata taarifa kwenye mradi huo uliopo Kata ya Misugusugu kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ussi amesema kuwa hicho ni chanzo kizuri cha mapato kwa Halmashauri hiyo.

Ussi amesema kuwa mradi huo wa maegesho hayo ambayo yatakuwa ya kisasa yataifanya Halmashauri kuongeza mapato yake hivyo kuendelea kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.

"Jambo ambalo ni zuri ni kulipa fidia na maendelezo kiasi kikichotengwa ni bilioni 1.8 kwa watu 23 ambapo kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kimelipwa kwa watu 21 hii inaonyesha kuwa wananchi wanalipwa haki zao na hakuna mtu atakaye kosa haki yake,"amesema Ussi.

Kwa upande wake Mthamini wa Halmashsuri ya Mji Kibaha Patrick Kibwana amesema kuwa mradi huo utakuwa wa shilingi bilioni 23 ikiwa ni mapato ya ndani.

Amesema kuwa hadi sasa kiasi cha shilingi milioni 317.8 bado hakijalipwa huku watu wawili wakiendelea na taratibu za kibenki.

Kibwana kuwa mradi utakuwa na nyumba za kulala wageni sehemu ya kuoshea magari kituo cha zimamoto mama lishe hoteli sehemu ya kutengeneza magari mifumo ya miundombinu ya gesi vyoo na mabafu kituo cha mafuta kituo cha polisi fremu za biashara huduma za afya ghala za kuhifadhia mizigo na mizani ya kupimia uzito.

Amesema kuwa mradi amesema kuwa mradi huo utatoa ajira kwa vijana 1,000 ambapo eneo hilo lina ukubwa wa hekari 18 na utaondoa msongamano wa malori kutoka Jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John amesema kuwa maegesho hayo yamejengwa jirani na eneo la viwanda la Zegereni hivyo huduma hiyo inahitajika sana.

John amesema kuwa mradi huo utakuwa ni sehemu ya kuzalisha ajira kwa wananchi hususani vijana kwenye Wilaya hiyo na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano.

 



Wednesday, April 2, 2025

KIONGOZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA AFURAHISHWA MRADI MAEGESHO YA HALMASHAURI YA MJI KIBAHA


MBIO za Mwenge zimekagua eneo la mradi wa maegesho ya magari makubwa ambao utakapokamilika utaiingizia Halmashauri ya Mji Kibaha kiasi cha shilingi bilioni 3.3 kwa mwaka.

Akikagua na kupata taarifa kwenye mradi huo uliopo Kata ya Misugusugu kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ussi amesema kuwa hicho ni chanzo kizuri cha mapato kwa Halmashauri hiyo.

Ussi amesema kuwa mradi huo wa maegesho hayo ambayo yatakuwa ya kisasa yataifanya Halmashauri kuongeza mapato yake hivyo kuendelea kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.

"Jambo ambalo ni zuri ni kulipa fidia na maendelezo kiasi kikichotengwa ni bilioni 1.8 kwa watu 23 ambapo kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kimelipwa kwa watu 21 hii inaonyesha kuwa wananchi wanalipwa haki zao na hakuna mtu atakaye kosa haki yake,"amesema Ussi.

Kwa upande wake Mthamini wa Halmashsuri ya Mji Kibaha Patrick Kibwana amesema kuwa mradi huo utakuwa wa shilingi bilioni 23 ikiwa ni mapato ya ndani.

Amesema kuwa hadi sasa kiasi cha shilingi milioni 317.8 bado hakijalipwa huku watu wawili wakiendelea na taratibu za kibenki.

Kibwana kuwa mradi utakuwa na nyumba za kulala wageni sehemu ya kuoshea magari kituo cha zimamoto mama lishe hoteli sehemu ya kutengeneza magari mifumo ya miundombinu ya gesi vyoo na mabafu kituo cha mafuta kituo cha polisi fremu za biashara huduma za afya ghala za kuhifadhia mizigo na mizani ya kupimia uzito.

Amesema kuwa mradi amesema kuwa mradi huo utatoa ajira kwa vijana 1,000 ambapo eneo hilo lina ukubwa wa hekari 18 na utaondoa msongamano wa malori kutoka Jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John amesema kuwa maegesho hayo yamejengwa jirani na eneo la viwanda la Zegereni hivyo huduma hiyo inahitajika sana.

John amesema kuwa mradi huo utakuwa ni sehemu ya kuzalisha ajira kwa wananchi hususani vijana kwenye Wilaya hiyo na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano.

 

Tuesday, April 1, 2025

TAASISI YA BEGA KWA BEGA NA TANZANIA PWANI YACHANGIA DAMU CHUPA 19

TAASISI ya Bega kwa Bega na Tanzania Mkoani Pwani imechangia damu chupa 19 kwenye benki ya damu ajili ya wagonjwa wanaohudumiwa kwenye hospitali Wilayani Kibaha. 

Kiasi hicho cha damu kilipatikana wakati wa bonanza la kuhamasisha wananchi kujitokeza kushiriki kwenye uzinduzi wa mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa Mkoani Pwani 2025 lililofanyika kwenye uwanja wa Bwawani Kibaha.

Mratibu wa taasisi hiyo kitaifa Ruth Mateleka bonanza hilo limefanywa ili kuhamasisha wananchi kushiriki uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru zitakazofanyika leo kwenye uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha.

"Kazi yetu kubwa ni kuhamasisha wananchi kushiriki shughuli za kimaendeleo na kutaja kazi zilizofanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan na tunashukuru watu kujitolea damu ili kusaidia wagonjwa,"amesema Mateleka.

Kwa upande wake Zuhura Sekelela ambaye ni mratibu wa taasisi hiyo Mkoa wa Pwani alisema kuwa upatikanaji wa damu hiyo kutasaidia benki ya damu kuwa na damu ili kusaidia wagonjwa.

Sekelela alisema kuwa shughuli nyingine ambazo wanazifanya ni kupanda miti, kufanya usafi kwenye taasisi za umma ikiwa ni pamoja na shuleni, hoapitali na maeneo mbalimbali pamoja na kusaidia watoto waishio kwenye mazingira magumu.

Naye Mchungaji Josephine Mwalusama amesema kuwa yeye kama Mchungaji anamshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuhimiza wanawake kushika nafasi za uongozi.

Mwalusama amesema kuwa Rais amefanya kazi kubwa na zinaonekana na ameshukuru Mwenge kuwashiwa Mkoani Pwani kwani utautangaza Mkoa na wajasiriamali watanufaika kwa kuwashwa mwenge huo wa uhuru.

Naye Mwenyekiti wa Vijana kutoka taasisi hiyo ya Bega kwa Bega na Tanzania Mkoa wa Pwani Athuman Lusambi  amesema kuwa wanawahamasisha vijana kushiriki kwenye Mwenge ili wawe wazalendo na nchi yao.

Monday, March 31, 2025

NMB KUTUMIA ZAIDI YA BILIONI 6 MIRADI YA MAENDELEO

BENKI ya inatarajia kutumia kiasi cha shilingi bilioni 6.4 kwa ajili ya kuchangia shughuli za maendeleo kwa mwaka wa 2025.

Hayo yalisemwa na Meneja wa benki hiyo Kanda ya Dar es Salaam ambaye aliwakilishwa na meneja wa tawi la Mlandizi Wilayani Kibaha William Marwa wakati wa Kongamano la Vijana juu ya umuhimu wa kushiriki mbio za mwenge mkoa wa Pwani 2025.

Alisema vijana wanapaswa kujua historia ya mbio za mwenge wa uhuru na fursa zilizopo kupitia mwenge ambao ni alama ya mshikamano wa kuleta maendeleo ya nchi.

"Tangu mwenge umeanza mbio zake kwa sasa ni miaka 61 na pia tunakumbuka kifo cha mwasisi wa Taifa letu miaka 26 iliyopita lazima tumjue kwani aliifanyia nchi hii mambo makubwa,"alisema Marwa. 

Akizungumzia benki hiyo ambayo ni kubwa kuliko zote nchini imekuwa ikichangia maendeleo na ni chachu kwa kuchangia kwenye sekta ya afya, elimu na kutoa mkono wa pole kwa wananchi wanaopata majanga.

"Benki imekuwa ikirudisha sehemu ya faida kwa kuchangia suala la maendeleo kupitia sekta mbalimbali kwani wao ni sehemu ya wateja kwani ina matawi wilaya zote nchini,"alisema Marwa.

Alisema kuwa benki hiyo ina matawi 241 Atm 720 mawakala 50,000 na wateja milioni 8.7 kote nchini na bado inaendelea kuboresha huduma zake kimtandao.

Sunday, March 30, 2025

WAZIRI MKUU MAJALIWA AUPIGIA DEBE UWANJA WA SHIRIKA LA ELIMU KIBAHA KUTUMIWA NA TIMU ZA CHAN NA AFCON

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameupigia debe uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha kutumiwa na Timu za Taifa zitakazokuwa zinajiaandaa na michuano ya  CHAN na AFCON kwa ajili ya mazoezi.

Majaliwa aliyasema hayo alipotembelea kuukagua uwanja huo ambao utatumika kwenye usinduzi wa mbio za mwenge 2025.

Majaliwa alisema kuwa jana alifanya ukaguzi wa viwanja vitatu viyakavyotumika kwa ajili hiyo ambavyo ni vichache.

"Tanzania tumepata uenyeji wa mashindano hayo mawili ambayo ni makubwa hivyo lazima tuwe na viwanja vingi kwa ajili ya mazoezi na hichi kikiboreshwa kinaweza kutumika,"alisema Majaliwa.

Alisema kuwa wataangalia uwezekano wa uwanja huo kutumiwa kwa ajili ya mazoezi na tutaongea na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kama watakikubali itabidi kitumike.

"Kiwanja hichi kikiimarishwa vizuri kinaweza kutumika kwa ajili hata ya ligi kuu ni uwanja mzuri unahitaji maboresho kidogo tu kwani hata taa zipo kwa kweli hapa ni pazuri,"alisema Majaliwa.

Aidha alisema hayo ni matunda ya uwekezaji kwenye sekta ya michezo ambapo Rais Dk Samia Suluhu Hassan ameamua kuwekeza kwenye michezo.

"Kwa vijana wa Halaiki msiishie hapa endeleeni na mazoezi hii iwe ni sehemu ya kuanzia kwa wale watakaocheza mpira wa miguu, pete, riadha na michezo mingine ili muendeleze vipaji vyenu isiwe hapa ndiyo mwisho,"alisema Majaliwa.



WAZIRI MKUU MAJALIWA ARIDHISHWA MAANDALIZI UZINDUZI WA MWENGE WA UHURU PWANI 2025

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ametembelea kuangalia maandalizi ya uwanja utakaotumika kuzindua mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2025 mkoani Pwani.

Majaliwa alitembelea uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha kuangalia maandalizi ya uzinduzi huo na kuridhishwa na maandalizi hayo na kutaka wakamilishe sehemu ambazo bado hazijakamilika.

Alisema kuwa ameridhishwa na maandalizi hayo ambapo pia alitumia muda huo kutembelea watoto wa halaiki na kusema amefurahishwa na jinsi walivyokuwa na hamasa ya uzinduzi huo.

"Nawapongeza kwa maandalizi mnayoendelea nayo nimeridhishwa kamilisheni sehemu zilizosalia ili kukamilisha mapema,"alisema Majaliwa.

Alisema kuwa amefurahishwa kuona viongozi wakiwemo mawaziri na makatibu wakuu wakiwa mstari wa mbele kuhakikisha maandalizi yanakuwa mazuri.

"Alikeni hata mikoa ya jirani Dar es Salaam, Morogoro na Tanga na watu mbalimbali kwani hili ni jambo la kitaifa shirikisheni wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ili hamasa iwe kubwa,"alisema Majaliwa 

Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Watu Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete maandalizi yako vizuri ila baadhi ya maeneo ikiwemo katikati ya uwanja ndiyo kunahitaji marekebisho kidogo.

Kikwete alisema kuwa mialiko kwa wageni mbalimbali imetolewa ikiwa ni pamoja na wakuu wa mikoa, wakurugenzi na watu wengine ili kushiriki uzinduzi huo.


Friday, March 28, 2025

VIJANA WAFUNDISHWE UMUHIMU WA MBIO ZA MWENGE

TAASISI mbalimbali nchini zimetakiwa kuwajengea uwezo vijana juu ya umuhimu wa mbio za Mwenge wa Uhuru katika kujenga uzalendo na uwajibikaji katika usimamizi wa shughuli za maendeleo na kutambua fursa za kiuchumi.

Hayo yamesemwa na Skauti Mkuu Nchini na Katibu Tawala (RAS) Mkoa wa Pwani Rashid Mchatta wakati Kongamano la Vijana juu ya umuhimu wa kushiriki Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025.

Mchatta amesema kuwa vijana wanapaswa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa namna ambavyo mtaelekezwa na viongozi katika maeneo wanayoishi.

"Tukifanya hivyo tutaupata ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa ufasaha ili muweze kushuhudia kwa vitendo yale yote mtakayojifunza katika Kongamano hili,"amesema Mchatta.

Amesema kuwa Serikali inatambua umuhimu wa kundi la vijana katika kuleta mageuzi ya Kijamii na Kiuchumi kutokana na ari, nguvu na ubunifu walionao. 

"Kwa kutambua hilo serikali kwa kushirikiana na wadau imekuwa ikitoa kipaumbele kwa vijana kupata elimu na makuzi bora kuwapa fursa ya kupata mikopo ya asilimia 10 kupitia Halmashauri na Programu ya Jenga Kesho iliyo Bora (Build Better Tomorrow – BBT) 

Amesema kuwa Mwenge wa Uhuru Mwaka 2025 utazinduliwa mkoa wa Pwani kitendo ambacho kinaonesha nia njema ya Dk Samia Suluhu Hassani Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuendeleza na kuenzi kwa vitendo yale yote aliyoturithisha Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Rais wa Kwanza wa Tanzania. 

Kwa upande wake mratibu wa Kongamano hilo Omary Punzi amesema kuwa ili vijana waweze kufikia mafanikio ya kimaendeleo lazima wazingatie falsafa za Mwalimu Nyerere alizotumia wakati wa kuwashwa Mwenge wa Uhuru.

Punzi amesema moja ya falsafa za Mwenge wa Uhuru ni kuwafanya watu wawe na uzalendo kwa kujitoa kwa ajili ya nchi yao na kutokomeza maadui watatu ujinga umaskini na maradhi. 

Mbio za Mwenge wa Uhuru zitazinduliwa katika viwanja vya Shirika  la Elimu Kibaha Mkoani Pwani na Mgeni rasmi atakuwa Dk Philip Isdor Mpango Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

mwisho.