Akizungumza na waandishi wa habari Mjini Kibaha ofisa masoko wa soko hilo la kisasa Sabrina Kikoti amesema kuwa soko hilo limejengwa kwa fedha kutoka Serikali Kuu na Halmashauri ya Mji Kibaha.
Kikoti amesema kuwa huduma zote zitapatikana ambaapo bidhaa zitauzwa kwa bei ya jumla na rejareja litafungua fursa kwa wananchi wa Kibaha na litatoa ajira na kufufua uchumi wa Kibaha.
“Mgeni rasmi kwenye ufunguzi huo anatarajiwa kuwa ni Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John ambapo wananchi wa Kibaha wtaanufaika kwani walikuwa wakifuata bidhaa Jijini Dar es Salaam huku wengine watapata ajira kupitia biashara,”amesema Kikoti.
Naye ofisa mapato wa Halmashauri ya Mji Kibaha Luna Kakuru amesema kuwa jengo hilo la kibiashara lina maduka 74 ya biashara ambapo bidhaa zitauzwa kwa bei ya jumla na rejareja.
Kakuru amesema kuwa maratajio yao ni kukusanya kiasi cha shilingi milioni 660 kwa mwaka ambapo mapato yataendelea kuongezeka kutokana na kodi mbalimbali zitakazokuwa zikitozwa hapo ambapo wanapangisha mita za mraba kiasi cha shilingi 15,000.
Nao baadhi ya wafanyabiashara Charles Chandika amesema kuwa ametumi fursa kupangisha hapo ili aweze kufanyabiashara ambapo pia litachangamsha Mji wa Kibaha ambapo lengo ni kuhakikisha wanatoa huduma bora na za kisasa na kuwafikia wananchi.
Chandika amesema kuwa bei watakayouza ni rafiki na hawatakuwa na sababu ya kwenda mbali kuzifuata Jijini Dar es Salaam kwani wataokoa muda na gharama za nauli kufuata bidhaa mbali.
Naye Lydia Vicent ambaye amenufaika kwa kuchangamkia fursa ambapo alikosa sehemu ya kufanyia biashara na wanampongeza Rais kwa kuwapatia fursa wafanyabiashara ambapo fedha zilizotolewa na serikali zimefanikisha kujenga soko hilo.
Vicent amesema kuwa soko hilo litafungua fursa za kibiashara kwa wananchi wengi ambapo ni sehemu ya kukuza uchumi kwa mwananchi mmoja mmoja na Watanzania kwa ujumla.