Wednesday, October 14, 2015

RIDHIWANI AMWAGIA SIFA DK MAGUFULI

Na John Gagarini, Chalinze
MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk John Magufuli amepongezwa kwa kuuachia mkoa wa Pwani hususani wilaya ya Bagamoyo miradi mikubwa ambayo itakapokamilika itasaidia kuinua kipato cha wakazi wa mkoa huo.
Miradi hiyo ambayo inatoka kwenye Wizara Ujenzi na Miundombinu aliyokuwa akioongoza Dk Magufuli kabla ya kuteuliwa na chama chake kuwa mgombea Urais kwenye kinyanganyiro kitakachofanyika Oktoba 25 mwaka huu.
Pongezi hizo zimetolewa na mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze kupitia chama hicho Ridhiwani Kikwete, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye Kijiji cha Miono wilayani Bagamoyo na kusema kuwa mgombea huyo kila mkoa ameupatia miradi ambayo itachochea maendeleo.
Ridhiwani alisema kuwa Dk Magufuli ni kiongozi ambaye anastahili kuongoza nchi hii kwani wakati akiwa waziri alihakikisha kila mkoa unatumia rasilimali zake viuzuri ili kujiletea maendeleo hali ambayo imesababisha nchi kupiga hatua.
“Sisi wakazi wa wilaya ya Bagamoyo tunamshukuru kwani ametuachia miradi mikubwa ikiwa ni pamoja na ule wa Barabara ya Afrika Mashariki itakayoanzia Bagamoyo,  Makuruge,  Saadani hadi mkoa wa Tanga hadi Mombasa nchini Kenya,” alisema Ridhiwani.
Alisema kuwa mradi mwingine ni ule wa Bandari ambayo itakuwa ni kubwa ambao utaanza wakati wowote kuanzia sasa kwani mipango tayari imekamilika huku mradi wa barabara tatu zitakazoanzia Jijini Dar es Salaam hadi mkoani Morogoro pia mzaini wa kisasa uliopo Vigwaza ambao tayari unafanya kazi.
“Mradi mwingine ni ule wa upanuzi wa Daraja la Mto Wami ili kupunguza ajali zinazotokea kwenye daraja hilo ambapo kwa sasa magari hayawezi kupishana, hakika miradi hii ni mikubwa na itafungua fursa za maendeleo kwa kukuza uchumi wao kutumia fursa zilizopo na zitakazokuwepo kwenye miradi hiyo,” alisema Ridhiwani.
Aidha alisema Dk Magufuli ni kiongozi ambaye hana kashfa yoyote na ameonyesha kuwa anafaa kuliongoza Taifa la Tanzania kutokana na uchapa kazi wake pamoja na uadilifu aliokuwa nao ukilinganisha na viongozi wengine wanaowania nafasi hiyo.
Aliwataka watanzania kumchagua kwa kumpiga kura nyingi za kishindo ili awe Rais wa awamu ya tano na anaamini kuwa uwezo wa kuongoza nchi anao akiwa chini ya CCM ambao kwa wakati huu imechagua viongozi wenye sifa na wanaopendwa na wananchi.

Mwisho.
 Meneja kampeni wa Jimbo la Chalinze Alhaj Amiri Mkangata kushoto akimtambulisha mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Ridhiwani Kikwete kwenye Kijiji cha Kikwazu wilayani Bagamoyo

Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze kupitia CCM Ridhiwani Kikwete akizindua  huku akiwa amekaa kwenye kigoda tawi la vijana wa Boda boda kwenye Kijiji cha Pongwemnazi 


Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze kupitia CCM Ridhiwani Kikwete akizindua tawi kwa kupandisha bendera kwenye moja ya matawi wakati wa kampeni kuwania kiti hicho.

 Mgombea Udiwani kata ya Kimange kwa tiketi ya CCM Husein Hadingoka akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Kikwazu wakati wa mkutano wa kampeni

 Mama Mwenye ulemavu ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja akiwa kwenye mkutano wa kampeni wa Mgombea wa CCM Ridhiwani Kikwete kwenye Kijiji cha Pongwemnazi kata ya Kimange.

Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea wa CCM Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kwenye kijiji cha pongwekiona kata kimange wilayani bagamoyo 

 wananchi wa kijiji cha pongwekiona wakiwa wanamsikiliza mgombea ubunge jimbo la chalinze ridhiwani kikwete hayupo pichani wakati wa mkutano wa kampeni

 Mwigizaji aitwaye Puto akitoa burudani kwa wananchi waliohudhuria mkutano wa kampeni kwenye kijiji cha Pongwemnazi kata ya Kimange wilayani Bagamoyo

 Mwimbaji Sam wa Ukweli akiimba na moja ya wananchi kwenye mkutano wa kampeni wa CCM kwenye kijiji cha Pongwemnazi 

 Wagombea Ridhiwani Kikwete kushoto akicheza na mgombea Udiwani kata ya Kimange Hussein Hadingoka wakati wa uzinduzi wa kampeni za udiwani kwenye kijiji cha Pongwekiona

 Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Ridhiwani Kikwete kushoto akimkabidhi ilani mgombea udiwani wa kata ya Kimange Hussein Hadingoka wakati wa uzinduzi wa kampeni za udiwani kwenye Kijiji cha Pongwekiona

 Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kupitia CCM akimkabidhi ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015-2020, diwani wa Viti maalumu Nuru Mpwimbwi wakati wa uzinduzi wa kampeni za udiwani kata ya kimange kwenye Kijiji cha Pongwekiona 

 Mgombea Ubunge wa CCM Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akimkabidhi moja ya wanachama wapya kwenye Kijiji cha Pongwekiona

Friday, October 9, 2015

DK MAGUFULI AFUNIKA BAGAMOYO

 Baadhi ya wakazi wa wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani wakimskiliza mgomea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM John Magufuli kwenye uwanja wa shule ya msingi Majengo Bagamyo.

 Mkuu wa mkoa wa Tanga mwenye miwani Mwantumu Mahiza akielekeza jambo wakati wa kumsubiri mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dk John Magufuli kwenye kijiji cha Mbwewe wilayani Bagamoyo

 Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze  wilayani Bagamoyo Ridhiwani Kikwete akifurahia jambo na wananchi wa Kijiji cha Mbwewe wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wakati wa kumsubiria mgombea Urais kwa Tiketi ya CCM Dk John Magufuli

 Baadhi ya wananchi wakiwa na mabango

 Mgombe urais wa CCM Dk John Magufuli kulia akitete jambo na Waziri wa Elimu na Mafunzo ambaye pia ni mgombe Ubunge Jimbo la Bagamoyo Dk Shukuru Kawambwa 
Aliyekuwa mgombea Ubunge kura za maoni wa CCM Jimbo la Bagamoyo Abdul Sharif kulia akiwa amepozi kushoto ni Dk zainab Gama katibu mwenezi wa CCM mkoa wa Pwani

 Abdala Bulembo mjumbe wa kampeni wa CCM Taifa akionyesha mfano wa fomu ya kupigia kura

 Mgombea Urais wa CCM Dk John Mgafuli akiongea na wananchi wa Bagamoyo waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa shule ya msingi Majengo

 Wananchi wakiinua mikono juu kumuunga mkono mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dk John Magufuli

 Wananchi wakimshangilia mgombea Urais Dk John Magufuli

 Mgombea Urasi CCM Dk John Magufuli katikati akisisistiza jambo kushoto ni Waziri wa Elimu na Mafunzo na mgombea Ubunge Jimbo la Bagamoyo mkoani Pwani Dk Shukuru Kawambwa kushoto na Ridhiwani Kikwete Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze


 Mgombea Urasi Dk John Magufuli kushoto akimnadi mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika bagamoyo

 Dk John Magafuli kulia mgombea Urais CCM akimtambulisha mgombea Ubunge Jimbo la Bagamoyo Dk Shukuru Kawambwa

 Baadhi ya madiwani wa wilaya ya Bagamoyo

 Mgombea Ubunge kupitia Umoja wa Wanawake UWT mkoa wa Pwani Subira Mgalu kulia akitambulishw ana mgombea Urais CCM Dk John Magufuli wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika Bagamoyo.

Wednesday, October 7, 2015

WAOMBA KUONDOLEWA 100,000 KWA AJILI YA GARI LA WAGONJWA

Na John Gagarini, Chalinze
WAKAZI wa Kijiji cha Kwaruhombo Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo wametoa kilio chao kwa kuomba viongozi watakaochaguliwa kwenye uchaguzi mkuu kuwaondolea changamoto ya kutozwa kiasi cha shilingi 100,000 kwa ajili ya mafuta ya kuweka kwenye gari la wagonjwa wanaopata rufaa toka kwenye kituo cha afya cha Kwaruhombo.
Akizungumza Kijijini hapo mara baada ya mkutano wa kampeni wa mgombea ubunge jimbo hilo Ridhiwani Kikwete, Ally Rashid alisema kuwa hali hiyo inawapa wakati mgumu kutokana na hali halisi ya kipato chao kidogo.
Rashid alisema kuwa changamoto hiyo ni kubwa kwani wao kupata fedha hizo mzigo mkubwa ikizingatiwa maisha ya Kijijini ni magumu na hawana vyanzo vikubwa vya mapato zaidi ya kilimo ambacho nacho kimekuwa si cha uhakika kutokana na mvua kutokuwa za uhakika.
“Tunaomba viongozi watakaochaguliwa wahakikishe wanashughulikia kero hii kwani kwa sasa ni muda mrefu na tumekuwa tukilalamika lakini hakuna hatua zinazochukuliwa pia tunaomba Halmashauri itenge bajeti kwa ajili ya mafuta ya gari hilo la wagonjwa,” alisema Rashid.
Naye mgombea Udiwani wa kata ya Kwaruhombo ramadhan mahamba alisema kuwa kero hiyo ni kubwa kwa wanakijiji na kumwomba mgombea huyo wa ubunge kuhakikisha nawasemea huko halmashauri ili gari hilo liwe na bajeti ya mafuta.
Mahamba alisema kuwa mbali ya kero hiyo ya wananchi kutakiwa kutoa kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya kuwekea mafuta ya kuwasafirisha wagonjwa wanapopata rufaa kwenda hospitali kubwa pia kuna tatizo la upungufu wa wahuduma wa afya.
Kwa upande wake Ridhiwani Kikwete alisema kuwa kero hiyo ameisikia na mara atakapochaguliwa atahakikisha anashinikiza kutenga fedha za mafuta kwa ajili ya vituo vya afya ili kuwaondolea mzigo wananchi.
Ridhiwani alisema kuwa utaratibu umewekwa na Halmashauri wa bajeti ya mafuta ya magari hayo hivyo akichaguliwa hiyo ni moja ya vitu atakavyovifuatilia kwa karibu ili kuhakikisha mafuta yanapatikana kwenye gari hilo.
Mwisho.
NA John Gagarini, Chalinze
KIJIJI ch Kwaruhombo Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo kinakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji hali inayowafanya wakazi wake kuchota maji ya visima vya kienyeji ambavyo viko chini ya ardhi huku vingine vikiwa na urefu wa futi 12.
Mbali ya visima hivyo kuwa na urefu mkubwa ambapo huwabidi wachotaji wengi wao wakiwa ni wakinamama kushuka kwa kutumia ngazi pia kumekuwa na foleni kubw ahali ambayo inawafanya wakeshe wakisubiri maji ambayo yamekauka kutokana na hali ya kiangazi.
Moja ya wanakijiji aliyejitambulisha kwa jina la Hadija Yusufu alisema kuwa maji ni changamoto kubwa kwao kwani wamekuwa wakitumia muda mrefu wa kusubiria maji hasa kipindi hichi cha kiangazi pia ni hatari kwa maisha yao kutokana na urefu wa visima hivyo.
“Tunaiomba serikali kutusaidia kupatikana maji ili kutuondolea adha hii kwani tumeletewa maji ambapo kuna vioski kwa ajili ya kuchota maji lakini havitoi maji hatujui kuna tatizo gani linalosababisha maji yasitoke hivyo tumebaki tunategemea maji ya visima hivyo vya kienyeji ambavyo navyo ni hatari kweteu,” alisema Yusufu.
Kwa upande wake mgombea udiwani kwa tiketi ya CCM Ramadhan Mahamba alisema kuwa endapo atachaguliwa atahakikisha anafuatilia suala hilo ili maji yaweze kupatikana kwa kutatua changamoto iliyopo ili maji yapatikane na kuwaondolea kero wananchi.
Naye mgombe ubunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete alisema kuwa tatizo la ukosefu wa maji ni kutokana na miundombinu iliyowekwa kuwa ya zamani hivyo kushindwa kuhimili kasi ya maji na kupasuka.
Ridhiwani alisema kuwa endapo atachaguliwa atahakikisha miundombinu mipya ambayo ni mabomba inapatikana ili kuondoa kero hiyo inayowanyima usingizi wananchi hao ambao hicho ni kilio chao kikubwa.
Mwisho.

Tuesday, October 6, 2015

DIWANIA AHIDI KUNUA GARI LA WAGONJWA

Na John Gagarini, Chalinze
MGOMBEA Udiwani kata ya Vigwaza Jimbo la Chalinze kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Muhsin Bharwan amesema kuwa endapo atafanikiwa kuchaguliwa atanunua gari la kubeba wagonjwandani ya kipindi cha miezi sita kwa ajili ya kuwapeleka wagonjwa wanaopata rufaa kwenda hospitali kubwa.
Aliyasema hayo kwenya mkutano wa kampeni ya kumnadi mgombea Ubunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete kwenye Kijiji cha Buyuni kwenye kata hiyo na kusema kuwa gari hilo litatumika kwenye vijiji vya kata hiyo ya Vigwaza.
Bharwan alisema kuwa kutokana na kata hiyo kutokuwa na gari la wagonjwa wakazi  hao wamekuwa wakipata taabu kuwapeleka wagonjwa wao wanaopata rufaa kwenda kwenye hospitali kubwa kama vile Tumbi au Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
“Endapo nitafanikiwa kuchaguliwa kwenye nafasi hii ya Udiwani ndani ya miezi sita nitahakikisha nimenunua gari la kubeba wagonjwa, tutamwomba mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo kupata msamaha wa kodi toka serikalini ili kufanikisha kupatikana gari hilo,” alisema Bharwan.
Alisema kuwa kwa kushirikiana na Wanakijiji hao atahakikisha ujenzi wa zahanati unakamilika ili waanze kupata huduma za afya kijijini hapo badala ya kupata huduma hiyo mbali kwani kwa sasa hakuna huduma hiyo kutokana na kukosa zahanati.
“Sera inasema kila Kijiji lazima kiwe na zahanati na kata inakuwa na kituo cha afya hivyo tutahakikisha tunatimiza hilo ili kusogeza huduma za afya kwa wananchi,” alisema Bharwan.
Kwa upande wake Ridhiwani Kikwete alisema kuwa moja ya vipaumbele vyake ni pmaoja na upatikanaji wa huduma za afya ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wahudumu wa afya wanapatikana.
Ridhiwani alisema kuwa pia upatikanaji wa madawa, vifaatiba, pamoja na ujenzi wa nyumba za wahudumu wa afya ili waishi kwenye vituo vyao vya kazi kwa lengo la kutoa huduma kwa urahisi.
Naye mkazi wa Kijiji hicho Pamilasi Sambana alisema kuwa huduma hizo za kiafya zikipatikana itawasaidia kukabiliana na matatizo yanayotokana na umbali wa upatikanaji wa huduma hizo.
Sambana alisema kuwa huduma za afya ni moja ya vilio vya wananchi na mara anapotokea mgonjwa inakuwa ni taabu sana hivyo wanawaomba wagombea hao kutimiza ahadi zao ili kuwapunguzia adha ya kupata huduma hizo.
Mwisho.

Na John Gagarini, Chalinze
UTUNGWAJI wa sheria ndogondogo kwenye Kijiji cha Malivundo kata ya Pera kwenye Jimbo la Chalinze kumesaidia kupunguza migogoro baina ya wakulima na wafugaji ambayo ilikuwa imekithiri katika Kijiji hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari moja ya wanakamati ya maridhiano baina ya wakulima na wafugaji ya Kijiji hicho Charles Antony alisema kuwa tangu kuundwa kamati hiyo miezi minne iliyopita migogoro imepungua kwa kiasi kikubwa.
Antony alisema kuwa mkutano wa Kijiji ulipitisha sheria ya kumtoza mfugaji gunia nane za mahindi kwa hekari moja  endapo ataingiza mifugo kwenye shamba la mkulima ambalo lina mazao na kwa shamba ambalo limeandaliwa halina mazao atatozwa kiasi cha shilingi 50,000 kwa hekari moja  na 40,000 kwa shamba ambalo limevunwa mazao.
“Sheria hii iliridhiwa na wakulima na wafugaji licha ya kuwa tatizo kubwa lipo kwa wafugaji ambao wamekuwa wakilisha mifugo kwenye mashamba ya wakulima hali ambayo ilikuwa inasababisha migogoro ya mara kwa mara lakini toka sheria hii imepitishwa na Kijiji matatizo hayo yamepungua,” alisema Antony.
Alisema kuwa endapo mlalamikiwa anakataa kutekeleza agizo la kamati suala hilo linapelekwa ngazi ya kata ambako nao husisitiza mlalamikiwa kulipa faini hiyo mara baada ya kamati kupita kwenye eneo ambalo limefanyiwa uharibifu.
“Kamati hii inaundwa na watu 10 wakulima watano na wafugaji watano ambao huangalia ukubwa wa tatizo kisha hutoa maamuzi juu ya uharibifu uliofanywa lakini pia pande mbili zinazohusika nazo huruhusiwa kukaa na kuangalia namna ya kutatua tatizo hilo,” alisema Antony.
Ashura Ramadhan alisema kuwa kwa sasa angalau mazao yao yanaweza kukua bila ya tatizo lolote tofauti na ilivyokuwa awali ilikuwa ni ugomvi mkubwa kati ya wakulima na wafugaji lakini kwa sasa angalau amani inapatikana kutokana na sheria hizo.
Kwa upande wake mgombea udiwani  kata ya Pera kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM)Lekope Laini alisema kuwa endapo atachaguliwa atahakikisha anatumia taaluma yake ya sheria kukabili migogoro ya wakulima na wafugaji pia kuwaunganisha ili waishi kama ndugu.
Naye mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze kupitia CCM Ridhiwani Kikwete alisema kuwa endapo atachaguliwa atahakikisha mpango wa matumizi bora ya ardhi unawekewa mkazo ili kuwe na maeneo ya wakulima na wafugaji kupunguza migogoro hiyo.
Mwisho.
Na John Gagarini, Chalinze
WAKINAMAMA wa Jamii ya wafugaji kwenye Kijiji cha Wafugaji cha Chamakweza wameiomba serikali kuwapatia matenki makubw aya kuhifadhia maziwa pamoja na soko la uhakika la kuuza maziwa yao.
Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ridhiwani Kikwete Anastazia Masaka alisema kuwa maziwa wanayozalisha ni mengi lakini hawana sehemu ya kuhifadhia pamoja na soko la uhakika.
Masaka alisema kuwa wanaiomba serikali kuwapatia matenki hayo ili waweze kuhifadhi maziwa yao ili yasiweze kuharibika wakati yakisubiri kusafirishwa au kuwasubiri wanunuzi wa maziwa hayo ambayo yanapatikana kwa wingi kwenye kijiji chao ambacho ni cha wafugaji.
“Maziwa ni mengi lakini tunataabika na soko pamoja na sehemu ya kuhifadhia hivyo tunaiomba serikali kupitia mgombea Ubunge kutusaidia kupata matenki ya kuhifadhia pamoja na soko la uhakika kwani soko likiwa kubwa vijana wetu watapata ajira kupitia maziwa,” alisema Masaka.
Alisema kuwa wakipata ufumbuzi wa masuala hayo basi itakuwa ni ufumbuzi wa changamoto wa namna ya kuhifadhi pamoja na soko la kuuza bidha hiyo ambayo inapendwa na watu kutokana na umuhimu wake kiafya.
Kwa upande wake Ridhiwani Kikwete alisema kuwa endapo atafanikiwa kuchaguliwa kwenye nafasi hiyo atahakikisha soko pamoja na matenki hayo vinapatikana ili kuwaondolea adha ya kuhifadhi maziwa yao pamoja na soko.
Ridhiwani alisema kuwa kwa kupitia umoja wao wa wauzaji maziwa atahakikisha anawaletea wanunuzi wa maziwa pia wanawezeshwa kuptia fedha ambazo zitatolewa kwa kila Kijiji kiasi cha shilingi milioni 50.
Naye mgombea Udiwani Lekope Laini alisema kuwa endapo atachaguliwa atahakikisha anakabiliana na changamoto za akinamama wa kifugaji ili nao waweze kujikwamua kiuchumi kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya kufanya shughuli zao.
Mwisho.

Na John Gagarini, Bagamoyo

KATIKA kuhakikisha kurahisisha utendaji kazi hasa katika kipindi hichi cha uchaguzi CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani kimetoa pikipiki 12 kwa makatibu kata kwenye Jimbo la Bagamoyo ili kuwaondolea tatizo la usafiri wakati wakutimiza majukumu yao.


 Akikabidhi pikipiki hizo mwenyekiti wa CCM wilayani hapo Maskuzi alisema walikuwa wakikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa usafiri kwa makatibu hao hivyo kushindwa kutekeleza kikamilifu shughuli za chama.

Maskuzi alisema kuwa lengo lingine ni kuwawezesha makatibu kata hao kuweza kusimamia majukumu yao kikamilifu pamoja na uhai wa chama na kurahisisha shughuli hasa katika kipindi hichi cha uchaguzi.

“Utoaji wa pikipiki hizi zenye thamani ya  shilingi milioni 24 kwa makatibu wa kata ni muendelezo  ambapo awali kwenye awamu ya kwanza tulitoa pikipiki 15 katika Jimbo la Chalinze na sasa kumalizia na jimbo la Bagamoyo,” alisema Maskuzi.

Alisema kuwa kwasasa anaamini watendaji hao watafanya kazi zao pasipo usumbufu kwani tatizo kubwa lilikuwa ni ukosefu wa usafiri wa uhakika wakutembelea maeneo mbalimbali ya kazi.

“Pikipiki hizi tunazitoa sio kwa shughuli nyingine ila ni kwa ajili ya kutekeleza shughuli za kichama kwa kutembelea matawi,kusimamia uhai wa chama na kutekeleza majukumu yatakayotakiwa kufuatilia wakati huu wa kuelekea kwenye uchaguzi mkuu”alisema Masukuzi.

Kata zilizopatiwa pikipiki hizo ni pamoja na Mapinga, Kerege, Zinga, Kilomo, Yombo, Dunda, Magomeni, Kisutu na Nianjema, Makurunge na Fukayosi na pikipiki moja itakuwa kwa ajili ya mtendaji mkuu CCM wilayani hapo.
                            
Kwa upande wake katibu wa CCM kata ya Kisutu Buruhani Setebe alisema amepokea pikipiki na amekishukuru chama kwa kutambua changamoto yao hivyo atahakikisha anaitunza pikipiki hiyo.

Naye katibu wa CCM kata ya Mapinga ,Muhdin Mipango alisema awali walikuwa wakipata shida katika utendaji wa kazi zao ikiwa ni pamoja na kutembelea kwa miguu ama kukodi pikipiki ili kwenda kutembelea matawi.

                                          Mwisho.




Sunday, October 4, 2015

MCH MTIKILA AFARIKI AJALINI

Na John Gagarini, Chalinze
 
MWANASIASA Mkongwe hapa nchini ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama ChaDemocratic Party (DP) Mchungaji Christopher Mtikila (62) amefariki dunia na watu wengine watatu kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuacha njia na kupinduka.
 
Kwa mujibu wa kamanda wa Polisi mkoani Pwani Jafary Mohamed alisema kuwa tukio hilo lilitokea huko Msolwa Barabara Kuu ya Dar es Salaam Morogoro wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.
 
Kamanda Mohamed alisema kuwa ajali hiyo ilitokea saa 11:45 Alfajiri wakitokea mkoani Njombe wakiwa na gari aina ya Toyota Corola lenye namba za usajili T189 AGM lililokuwa likiendeshwa na dereva aitwaye George Steven (31) maarufu Ponera mkazi wa Mbezi Jijini Dar es Salaam.
 
"Gari hilo likiwa na abiria watatuakiwemo marehemu mkazi wa Mikocheni B, lilikuwa kwenye mwendo wa kasi liliacha njia na kuserereka pembeni mwa barabara kasha kupinduka ambapo marehemu alirushwa nje ya gari na kupoteza maisha papo hapo,"alisema Kamanda Mohamed.
 
Aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni pamoja na dereva wa gari hio, Mchungaji Patrick Mgaya (57) na Ally Mohamed (42) wote wakazi wa Jijini Dar es Salaam ambao wote walikimbizwa kweye hospitali ya Rufaa ya mkoa ya Tumbi pamoja na kuhifadhi mwili wa marehemu.
 
"Chanzo caha ajali hiyo ni mwendo wa kasi wa dereva huyo ambao ulisababisha ashindwe kulimudu gari hilo na kuserereka pembeni ya barabara kasha kupinduka na kupelekea kifo hico cha kusikitisha cha mwanasiasa huyo," alisema Kamanda Mohamed.
 
Hata hivyo taarifa kutoka eneo la tukio zilisemakuwa mara baada ya ajali hiyo wahanga hao hawakuweza kupata msaada kwani eneo hilo halina makazi ya watu.
 
mwisho. 
 
 

Friday, October 2, 2015

ADHA YA MAJI KIJIJI CHA GONGO KATA YA MKANGE JIMBO LA CHALINZE WILAYA YA BAGAMOYO PWANI





Na John Gagarini, Mkange
WANANCHI wa Kijiji cha Gongo kata ya Mkange wilayani Bagamoyo wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji ambapo huweka foleni ya kuchota maji kwenye kisima kilichopo kijijini hapo baada ya wiki mbili.
Kutokana na usosefu huo wa maji wananchi hao wamekuwa wakinunua maji ya bomba ndoo ya lita 20 kati ya shilingi 1,000 na shilingi 1,500 maji ambayo huuzwa kwenye magari au pikipiki hivyo kuwafanya wajikute hawapati maendeleo kutokana na gharama kubwa kuzitumia kununulia maji.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mkutano wa kampeni wa mgombea Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ridhiwani Kikwete, kwenye kata ya Mkange mwananchi wa Kijiji hicho Hungilo Nyoka alisema kuwa maji yamewafanya washindwe kupata maendeleo.
Nyoka alisema kila kaya inatakiwa ichote madumu manne ili angalau kila mmoja apate baada ya hapo maji hukatika ambapo inatakiwa mtu asubirie tena na mzunguko huo hufanya foleni ya mtu mmoja kufikiwa tena baada ya wiki mbili kwani hapa kuna wananchi 1,690.
Alisema changamoto kubwa kwao ni maji ambayo yamekuwa yakiwafanya washindwe kufanya shughuli za maendeleo ipasavyo kwani hata wakipata fedha kutokana na shughuli zao fedha zote huishia kununulia maji.
“Tunawaomba wahusika kutuangalia kwa jicho la huruma maji kwetu ni kikwazo cha kupata maendeleo kwani hata ukipata fedha kiasi gani zote zinaishia kwenye maji hivyo tunaomba tuchimbiwe kisima kwani kilichopo maji ni kidogo sana yanatoka kila baada ya saa moja yanakatika,” alisema Nyoka.
Aidha alisema kuwa maji wanayokunywa ni ya bomba lakini yanatoka vijiji jirani vya Matipwili ambako kuna umbali wa kilomita 11 na kijiji cha Mkange kilomita tisa na alisema kuwa chanzo cha maji ya kisima kutotoka ipasavyo ni kwamba waliochimba kisima hawakuchimba hadi kuuukuta mwamba ambapo chini ya mwamba ndiyo kuna maji mengi.
“Tunaomba wadau wa masula ya maendeleo kutusaidia kuweza kupata maji kwani tunashindwa hata kujiletea maendeleo kutokana ukosefu wa maji na wkati mwingine watoto hushindwa kwenda shule endapo maji yanakuwa ya shida kwani hawawezi kwenda wachafua kwani mimi kwa siku hutumia madumu matatu hadi matano kwa siku,” alisema Nyoka.
Kwa upande wake mgombea udiwani kupitia CCM Injinia Juma Mgweno alisema kuwa tatizo hilo ni kubwa sana lakini atahakikisha maji yanapatikana kwa kuita wadau mbalimbali ili waweze kuwachimbia kisima.
Naye mgombea wa Ubunge kupitia CCM Ridhiwani Kikwete alisema kuwa visima viwili vilivypo kijiji hapo havitoi maji ambapo kimoja kinahitaji pampu ambayo imeharibika atahakikisha inapatikana mpya ili kuwaondolea kero wananchi wa kijiji hicho.
Ridhiwani alisema kuwa mbali ya kuhakikisha pampu mpya inapatikana pia kuna mradi mwingine wa mjai toka Matipwili na ule wa Wami Chalinze atahakikisha maji yanafika kwani mradi huo utavifikia vijiji na vitongoji ambavyo havikupata maji katika awamu mbili zilizopita vitafikiwa na awamu hii.
Mwisho.










MGOMBEA UDIWANI AHAIDI KUTOA ASILIMIA 50 YA POSHO KUCHANGIA SHUGHULI ZA MAENDELEO

Na Mwandishi Wetu, Kibaha
MGOMBEA Udiwani wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kata ya Kawawa Jimbo la Kibaha Vijijini Otto Kanyonyi amesema kuwa endapo atafanikiwa kuchaguliwa kwenye nafasi hiyo atatoa asilimia 50 ya posho zake atakazokuwa anapata kwenye vikao vya madiwani  kwa ajili ya kuchangia shughuli za maendeleo kwenye kata hiyo.
Kanyonyi aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari huko Mlandizi Kibaha juu ya mikakati yake ya kuwaletea maendeleo wakazi wa kata hiyo endapo atashinda kwenye nafasi ya udiwani kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 25 mwaka huu.
Alisema kuwa moja ya mkakati wake ambao ataupa kipaumbele ni ujenzi wa zahanati katika kata hiyo ili kuwapatia huduma wananchi badala ya kupata huduma hizo kwenye kata za jirani.
“Endapo nitafanikiwa kuwa diwnai wa kata yetu ya Kawawa nitahakikisha natoa asilimia 50 ya posho nitakayokuwa npata naitoa kwa ajili ya shughuli za maendeleo hasa zile huduma za jamii ikiwa ni pamoja na afya, elimu na maji,” alisema Kanyonyi.
Aidha alisema kuwa ameamua kujitolea posho hizo kutokana na kuwa na uchungu wa maendeleo na kuona kuwa moja ya njia za kuleta maendeleo ni kuchagia kwa hali na mali.
“Fedha hizo nataka zilete maendeleo katika kata yangu kwani ili kufanikisha mambo kiongozi lazima uonyeshe njia kwa wale unaowangoza hivyo na mimi nataka niwe kiongozi wa mfano ili niache kumbukumbu kuwa nilihamasisha maendeleo,” alisema Kanyonyi.
Alibainisha kuwa wananchi wanakabiliwa na changamoto nyingi hivyo moja ya njia za kuwahamasisha kujiletea maendeleo ni pamoja na kuchangia shughuli za maendeleo.
Mwisho.
Na John Gagarini, Chalinze
UMOJA wa Wanawake Tanzania (UWT) wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani umetoa salamu za rambirambi kufuatia kifo cha mwenyekiti wa tawi la Ubena Zomozi Kido Antoni (65) kufariki dunia wakati wa mkutano wa kampeni wa diwani wa kata ya Ubena Jimbo la Chalinze.
Mwenyekiti huyo wa tawi alifariki Septemba 30 majira ya saa 7 mchana wakati wakiwa kwenye shamrashamra ya kuwahamasisha wananchi kujiandaa kwa kucheza huku wakimsubiri mgombea udiwani wa kata hiyo kupitia CCM Nicholaus Muyuwa kwa ajili ya mkutano wa kampeni.
Akitoa salamu za pole katibu wa UWT wilaya ya Bagamoyo Mwatabu Hussein alisema kuwa wameupokea msiba huo kwa masikitiko makubwa kwani marehemu alikuwa kwenye harakati za kukipigania chama wakati huu wa kampeni kuelekea uchaguzi mkuu.
Hussein alisema kuwa familia pamoja na chama vimepata pigo kubwa la kuondokewa na kiongozi wao na kumwomba Mungu aipe nguvu katika kipindi hichi bkigumu cha majonzi.
“Tunawapa pole familia pamoja na chama kwa kuondokewa na mpendwa wao kwani alikuwa kwenye harakati za kuhakikisha chama kinapata ushindi kwenye uchaaguzi wa wagombea wa chama kuanzia Rais, Mbunge na Diwani,” alisema Hussein.
Kwa upande wake mgombea huyo wa udiwani Muyuwa alisema kuwa kifo amekipokea kwa masikitiko makubwa kwani marehemu alikuwa mtu muhimu sana ndani ya chama na amekufa wakati akipambana kuhakikisha ushindi unapatikana.
Muyuwa alisema kuwa marehemu alikuwa mzima kabisa na alikuwa kifurahi na wenzake na kutoa hamasa kwa wananchama  na wasio wanachama juu ya kukipigia kura ili kiweze kushinda kwenye uchaguzi m kuu ujao.
Alisema kuwa marehemu alianguka ghafla wakati wakimsubiri yeye aweze kufika kwa ajili ya kuhutubia kwenye mkutano wa kampeni na baada ya kuanguka walimpeleka kwenye zahanati ya Ubena Estate na alifariki wakatia kipatiwa matibabu.
Naye mgombea Ubunge kwenye Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alifika nyumbani kwa marehemu na kutoa salamu za pole kwani wakati tukio hilo linatokea mgombea huyo alikuwa kwenye mkutano wa kampeni katika kata hiyo kwenye Kijiji cha Mdaula.
Taarifa toka kwa daktari mfawidhi wa zahanati hiyo zilisema kuwa alikufa kutokana na presha na upungufu wa damu, marehemu alizikwa juzi kwenye makaburi ya Ubena na ameacha watoto watano.
Mwisho.
Na John Gagarini, Bagamoyo
MGOMBEA ubunge jimbo la Bagamoyo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM),Dk Shukuru Kawambwa, amesema endapo atachaguliwa kuongoza Jimbo hilo atahakikisha zahanati ya Yombo inapandishwa hadhi na kuwa kituo cha afya ili kupanua huduma za kiafya.
Sambamba na kupandishwa hadhi kwa zahanati hiyo pia Dk Kawambwa  atahakikisha kunakuwa na gari la kubeba wagonjwa wanaopata rufaa kwenda hospitali kubwa  tofauti na ilivyo sasa.
Dk Kawambwa aliyasema hayo kwenye Kijiji cha Yombo wakati wa mkutano wa kampeni na kusema kuwa vipaumbele vyake ni kuhakikisha huduma muhimu za jamii zinapatikana kwa uhakika.
“Mara zahanati hii ikipandishwa hadhi na kuwa kituo cha afya huduma zitaboreka ikiwa ni pamoja na kuwa na wataalamu wa kutosha na huduma nyingi zitatolewa hapa hivyo itapunguza kutumia muda mwingi kufuata huduma mbali,” alisema Dk Kawambwa.
Aidha alisema kuwa pia kipaumbele kingine ni kuhakikisha anasimamia utekelezaji wa ujenzi wa barabara kutoka Makofia-Yombo hadi Mlandizi-Mzenga kwa kiwango cha lami Dk ambapo kwa sasa upembuzi yakinifu umeshafanyika na kilichobakia ni tathmini ya watakaolipwa fidia ambako itapita barabara pamoja na hatua nyingine ili kupisha mpango huo.
“Utekelezaji wa ujenzi wa barabara hiyo kuwa kwa kiwango cha lami upo katika ilani ya Chama Cha Mapinduzi 2015-2020 na ukamilikaji wake utafungua fursa nyingi za kiuchumi hivyo kuleta maendeleo na kuinua uchumi wa wananchi,” alisema Dk Kawambwa.
Katika hatua nyingine alisema kuwa atahakikisha wakazi wa kata ya Yombo na maeneo ambayo hayajafikiwa umeme kuwa atashirikiana na tanesco kupitia mradi wa wakala wa umeme vijijini (REA) kuondoa tatizo hilo ndani ya miaka mitano ijayo.
"Nitahakikisha nasimamia mipango yote,na ilani ya chama changu ili niweze kupunguza makali ya kero zinazowakabili wana Bagamoyo ikiwemo kwenye afya,maji,nishati ya umeme ,elimu na miundombinu"alisema Dk.Kawambwa.
Kwa upande wake mgombea udiwani kata ya Yombo jimbo la Bagamoyo, kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mohamed Usinga,aliwaahidi wakazi wanaoishi katika vijiji vinavyounda kata hiyo kuwa atahakikisha anamalizia kazi ya kusambaza maji, umeme na kituo cha afya kilichopo katani humo.
Alieleza kuwa pindi wakazi hao wakimpatia ridhaa ya kushika nafasi hiyo atapambana ili kumalizia kazi ambayo ilikuwa imeanzwa na mtangulizi wake Ubwa Idd Mazongera ambaye kwa sasa ametangulia mbele za haki.
Awali akiwanadi wagombea hao,meneja kampeni jimbo la Bagamoyo,AbdulSharif alisema wananchi jimboni hapo wasifanye makosa kuchagua wapinzani bali wawachague wagombea kupitia CCM.

Mwisho