Sunday, July 7, 2013

HABARI ZA PWANI



Na John Gagarini, Kibaha
MKUU wa mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza amepongeza utaratibu wa viongozi wa dini za kikristo kufunga siku 40 kwa ajili ya kuombea amani ya nchi ili iweze kuondelea baada ya kutokea matukio yaliyokuwa yakiashiria uvunjifu wa amani.
Akizungumza juzi na viongozi wa madhehebu ya dini mbalimbali na uongozi wa jeshi la polisi mkoani humo, alisema kuwa jambo wanalolifanya ni kubwa na linapaswa kuungwa mkono na wapenda amani.
Mahiza alisema kuwa siku za hivi karibuni kulitokea matukio makubwa ya uvunjifu wa amani hapa nchini ikiwa ni pamoja na kutokea milipuko ya mabomu mkoani Arusha ambapo watu kadhaa walipoteza maisha huku wengine wakijeruhiwa.
“Tukikumbuka hata kule Kusini mkoani Mtwara zilizuka vurugu kubwa ambazo nazo matokeo yake hayakuwa mazuri kwani watu kadhaa walipoteza maisha na mali huku wengine wakijeruhi hivyo kuna haja ya kuwa na mkakati wa kukabilina na hali hiyo ikiwa ni pamoja na kuiombea nchi amani,” alisema mahiza.
Aidha alisema kuwa amani kuipoteza ni rahisi lakini gharama ya kuirudisha ni kubwa sana hivyo lazima kila mtu aangalia ni namna gani anaweza kunusuru hali hiyo.
“Tunaunga mkono jitihada za viongozi wa dini kuamua kufunga na kufanya maombi maalumu ili kuinusuru nchi yetu ili isiingie kwenye machafuko ambayo mara nyingi husababisha vifo na watu kushindwa kufanya shughuli za maendeleo,” alisema Mahiza.
Alisema kuwa sehemu yoyote yenye machafuko maendeleo hakuna hivyo kuna kila sababu ya kuiombea nchi ili iepukane na hayo yanayotaka kujitokeza.
Kwa upande wake katibu wa umoja wa makanisa ya kipentekoste mkoa wa Pwani Mchungaji Gervase masanja alsiema kuwa endapo amani itatoweka hata uhuru wa kumwabudu mungu hautakuwepo.
“Baadhi ya watu wameingiza siasa makanisani jambo ambalo linaweza likawa chanzo cha vurugu hivyo tunawaomba waumini wasiiingize siasa kwenye sehemu za kuabudia kwani ni hatari na ndiyo sababu ya sisi kuamua kufunga kuombea amani iliyopo isivunjike,” alisema Mch Masanja.
Kikao hicho pia kiliwajumuisha wakuu wa wilaya, wakuu wa polisi wa wilaya, vyama vya siasa, vyama vya watu wenye ulemavu na watu maarufu ndani ya jamii kwenye mkoa huo.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MAMLAKA ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (SUMATRA) mkoa wa Pwani imekunjua makucha yake baada ya kumtaka kondakta wa basi la kampuni ya Mbazi kuwarudishia nauli waliyoizidisha tofauti na ile iliyopangwa na serikali.
Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki kwenye stendi ya maili Moja wilayani Kibaha baada ya abiria kulalamika kuwa wamezidishiwa nauli wakati wakikata nauli kwenye kituo cha mabasi cha Ubungo Jijini Dar es Salaam.
Kondakta wa basi hilo ambalo linafanya safari zake kati ya Dar es Salaam na Arusha alijikuta matatani baada ya basi lake kuzuiliwa na kurejesha nauli ambazo zilikuwa zimezidi kwa abiria 19.
Baadhi ya abiria ambao waliongea na waandishi wa habari kuhusiana na kuzidishiwa nauli kati yao ni Nagi Nurdin aliyekuwa akienda Moshi alisema kuwa yeye alikatiwa nauli kwa shilingi 29,000 badala ya shilingi 22,700 ambapo alikata kwenye ofisi za basi hilo.
Naye Forida Faustin alisema kuwa yeye naye alikuwa akienda Moshi alitozwa 33,000 huku YUda Nduti akitozwa 30,000 ambapo walianza kumtajia nauli ni shilingi 40,000.
Kwa upande wake ofisa mfawidhi wa SUMATRA Pwani Iroga Nashon alisema kuwa hatua ya kwanza waliyoichukua ni kumwamuru kondakta wa basio hilo lenye namba T 600 APN kuwarejeshea nauli zilizozidi abiria hao.
“Baada ya kurejesha nauli zilizozidi ambazo zilikuwa ni zaidi ya 300,000 pia tuliwapiga faini ya shilingi 250,000 kwa kosa hilo kwa kuzingatia kifungu cha sheria cha 34 na ndipo tuliporuhusu basi hilo kuendelea na safari yake,” alisema Nashon.
Kwa upande wake kondakta wa basi hilo hakuwa tayari kuzungumza na waandishi na kusema kuwa yeye siyo msemaji ambapo alidai abiria hao walikatiwa tiketi stendi ya Ubungo.
Nashon aliwataka abiria kutoa taarifa kuhusiana na wamiliki au makondakta na madereva kuwanyanyasa kwa makusudi huku wakijua sheria za uendeshaji wa mabasi hayo ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kwa wanaokiuka.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MKOA wa Pwani unakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa gari la kunyanyulia vitu vizito (Crane) ikiwemo magari yanayoharibika kwenye barabara za mkoa huo.
Chanagamoto hiyo ilionekana juzi baada ya magari kukwama kwa zaidi ya saa tano baada ya magari mawili kuharibika kwenye daraja linalounganisha mikoa ya Pwani na Dar es Salaam eneo la Kiluvya wilayani Kibaha.
Magari yaliyoharibika ni ya mizigo ambapo la kwanza ni Scania namba T 503 DTJ na Fuso lenye namba za usajili T 515 DSA magari haya yaliziba kabisa barabara hivyo kusababisha magari kushindwa kuingia wala kutoka kwa muda huo.
Akizungumza kwenye eneo la tukio hilo kamanda wa polisi wa kikosi cha usalama barabarani wa mkoa huo Nasoro Sisiwaya alisema kuwa ilibidi watumie nguvu ya ziada kuliondoa gari moja ili magari yaweze kupita kwani lori kubwa liliharibika katikati ya daraja la mto Mpiji.
“Kwa kweli gari la kunyanyua vitu vizito ni changamoto kubwa kwani magari yanayo anguka au kupata ajali yanashindwa kuondolewa kwa wakati kutokana na kukosa huduma ya gari hilo,” alisema Sisiwaya.
Sisiwaya alisema kuwa tayari wameshaiomba serikali na wakala wa barabara TANROADS ili wanunue gari hilo na liwe hapa Kibaha kwani kutegemea litoke Dar es Salaam ni tatizo kubwa.
“Tumeandika sehemu husika kuomba gari hilo ili kukabiliana kwani tukio hili limesababisha usumbufu mkubwa sana kwa magari yanayopita barabara hii ya Morogoro ambayo ndiyo mlango wa kuingilia na kutoka Dar es Salaam.
Aidha alisema wataiomba TANROADS kujenga barabara mbadala kwani kutegemea barabara moja ni tatizo kubwa na kutokana na tukio hili tumeona jinsi gani watu walivyohangaika na kusababisha usumbufu mkubwa.
Mwisho.    

HABARI ZA PWANI



Na John Gagarini, Kibaha
MKUU wa mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza amepongeza utaratibu wa viongozi wa dini za kikristo kufunga siku 40 kwa ajili ya kuombea amani ya nchi ili iweze kuondelea baada ya kutokea matukio yaliyokuwa yakiashiria uvunjifu wa amani.
Akizungumza juzi na viongozi wa madhehebu ya dini mbalimbali na uongozi wa jeshi la polisi mkoani humo, alisema kuwa jambo wanalolifanya ni kubwa na linapaswa kuungwa mkono na wapenda amani.
Mahiza alisema kuwa siku za hivi karibuni kulitokea matukio makubwa ya uvunjifu wa amani hapa nchini ikiwa ni pamoja na kutokea milipuko ya mabomu mkoani Arusha ambapo watu kadhaa walipoteza maisha huku wengine wakijeruhiwa.
“Tukikumbuka hata kule Kusini mkoani Mtwara zilizuka vurugu kubwa ambazo nazo matokeo yake hayakuwa mazuri kwani watu kadhaa walipoteza maisha na mali huku wengine wakijeruhi hivyo kuna haja ya kuwa na mkakati wa kukabilina na hali hiyo ikiwa ni pamoja na kuiombea nchi amani,” alisema mahiza.
Aidha alisema kuwa amani kuipoteza ni rahisi lakini gharama ya kuirudisha ni kubwa sana hivyo lazima kila mtu aangalia ni namna gani anaweza kunusuru hali hiyo.
“Tunaunga mkono jitihada za viongozi wa dini kuamua kufunga na kufanya maombi maalumu ili kuinusuru nchi yetu ili isiingie kwenye machafuko ambayo mara nyingi husababisha vifo na watu kushindwa kufanya shughuli za maendeleo,” alisema Mahiza.
Alisema kuwa sehemu yoyote yenye machafuko maendeleo hakuna hivyo kuna kila sababu ya kuiombea nchi ili iepukane na hayo yanayotaka kujitokeza.
Kwa upande wake katibu wa umoja wa makanisa ya kipentekoste mkoa wa Pwani Mchungaji Gervase masanja alsiema kuwa endapo amani itatoweka hata uhuru wa kumwabudu mungu hautakuwepo.
“Baadhi ya watu wameingiza siasa makanisani jambo ambalo linaweza likawa chanzo cha vurugu hivyo tunawaomba waumini wasiiingize siasa kwenye sehemu za kuabudia kwani ni hatari na ndiyo sababu ya sisi kuamua kufunga kuombea amani iliyopo isivunjike,” alisema Mch Masanja.
Kikao hicho pia kiliwajumuisha wakuu wa wilaya, wakuu wa polisi wa wilaya, vyama vya siasa, vyama vya watu wenye ulemavu na watu maarufu ndani ya jamii kwenye mkoa huo.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MAMLAKA ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (SUMATRA) mkoa wa Pwani imekunjua makucha yake baada ya kumtaka kondakta wa basi la kampuni ya Mbazi kuwarudishia nauli waliyoizidisha tofauti na ile iliyopangwa na serikali.
Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki kwenye stendi ya maili Moja wilayani Kibaha baada ya abiria kulalamika kuwa wamezidishiwa nauli wakati wakikata nauli kwenye kituo cha mabasi cha Ubungo Jijini Dar es Salaam.
Kondakta wa basi hilo ambalo linafanya safari zake kati ya Dar es Salaam na Arusha alijikuta matatani baada ya basi lake kuzuiliwa na kurejesha nauli ambazo zilikuwa zimezidi kwa abiria 19.
Baadhi ya abiria ambao waliongea na waandishi wa habari kuhusiana na kuzidishiwa nauli kati yao ni Nagi Nurdin aliyekuwa akienda Moshi alisema kuwa yeye alikatiwa nauli kwa shilingi 29,000 badala ya shilingi 22,700 ambapo alikata kwenye ofisi za basi hilo.
Naye Forida Faustin alisema kuwa yeye naye alikuwa akienda Moshi alitozwa 33,000 huku YUda Nduti akitozwa 30,000 ambapo walianza kumtajia nauli ni shilingi 40,000.
Kwa upande wake ofisa mfawidhi wa SUMATRA Pwani Iroga Nashon alisema kuwa hatua ya kwanza waliyoichukua ni kumwamuru kondakta wa basio hilo lenye namba T 600 APN kuwarejeshea nauli zilizozidi abiria hao.
“Baada ya kurejesha nauli zilizozidi ambazo zilikuwa ni zaidi ya 300,000 pia tuliwapiga faini ya shilingi 250,000 kwa kosa hilo kwa kuzingatia kifungu cha sheria cha 34 na ndipo tuliporuhusu basi hilo kuendelea na safari yake,” alisema Nashon.
Kwa upande wake kondakta wa basi hilo hakuwa tayari kuzungumza na waandishi na kusema kuwa yeye siyo msemaji ambapo alidai abiria hao walikatiwa tiketi stendi ya Ubungo.
Nashon aliwataka abiria kutoa taarifa kuhusiana na wamiliki au makondakta na madereva kuwanyanyasa kwa makusudi huku wakijua sheria za uendeshaji wa mabasi hayo ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kwa wanaokiuka.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MKOA wa Pwani unakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa gari la kunyanyulia vitu vizito (Crane) ikiwemo magari yanayoharibika kwenye barabara za mkoa huo.
Chanagamoto hiyo ilionekana juzi baada ya magari kukwama kwa zaidi ya saa tano baada ya magari mawili kuharibika kwenye daraja linalounganisha mikoa ya Pwani na Dar es Salaam eneo la Kiluvya wilayani Kibaha.
Magari yaliyoharibika ni ya mizigo ambapo la kwanza ni Scania namba T 503 DTJ na Fuso lenye namba za usajili T 515 DSA magari haya yaliziba kabisa barabara hivyo kusababisha magari kushindwa kuingia wala kutoka kwa muda huo.
Akizungumza kwenye eneo la tukio hilo kamanda wa polisi wa kikosi cha usalama barabarani wa mkoa huo Nasoro Sisiwaya alisema kuwa ilibidi watumie nguvu ya ziada kuliondoa gari moja ili magari yaweze kupita kwani lori kubwa liliharibika katikati ya daraja la mto Mpiji.
“Kwa kweli gari la kunyanyua vitu vizito ni changamoto kubwa kwani magari yanayo anguka au kupata ajali yanashindwa kuondolewa kwa wakati kutokana na kukosa huduma ya gari hilo,” alisema Sisiwaya.
Sisiwaya alisema kuwa tayari wameshaiomba serikali na wakala wa barabara TANROADS ili wanunue gari hilo na liwe hapa Kibaha kwani kutegemea litoke Dar es Salaam ni tatizo kubwa.
“Tumeandika sehemu husika kuomba gari hilo ili kukabiliana kwani tukio hili limesababisha usumbufu mkubwa sana kwa magari yanayopita barabara hii ya Morogoro ambayo ndiyo mlango wa kuingilia na kutoka Dar es Salaam.
Aidha alisema wataiomba TANROADS kujenga barabara mbadala kwani kutegemea barabara moja ni tatizo kubwa na kutokana na tukio hili tumeona jinsi gani watu walivyohangaika na kusababisha usumbufu mkubwa.
Mwisho.    

HABARI ZA PWANI



Na John Gagarini, Kibaha
MKUU wa mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza amepongeza utaratibu wa viongozi wa dini za kikristo kufunga siku 40 kwa ajili ya kuombea amani ya nchi ili iweze kuondelea baada ya kutokea matukio yaliyokuwa yakiashiria uvunjifu wa amani.
Akizungumza juzi na viongozi wa madhehebu ya dini mbalimbali na uongozi wa jeshi la polisi mkoani humo, alisema kuwa jambo wanalolifanya ni kubwa na linapaswa kuungwa mkono na wapenda amani.
Mahiza alisema kuwa siku za hivi karibuni kulitokea matukio makubwa ya uvunjifu wa amani hapa nchini ikiwa ni pamoja na kutokea milipuko ya mabomu mkoani Arusha ambapo watu kadhaa walipoteza maisha huku wengine wakijeruhiwa.
“Tukikumbuka hata kule Kusini mkoani Mtwara zilizuka vurugu kubwa ambazo nazo matokeo yake hayakuwa mazuri kwani watu kadhaa walipoteza maisha na mali huku wengine wakijeruhi hivyo kuna haja ya kuwa na mkakati wa kukabilina na hali hiyo ikiwa ni pamoja na kuiombea nchi amani,” alisema mahiza.
Aidha alisema kuwa amani kuipoteza ni rahisi lakini gharama ya kuirudisha ni kubwa sana hivyo lazima kila mtu aangalia ni namna gani anaweza kunusuru hali hiyo.
“Tunaunga mkono jitihada za viongozi wa dini kuamua kufunga na kufanya maombi maalumu ili kuinusuru nchi yetu ili isiingie kwenye machafuko ambayo mara nyingi husababisha vifo na watu kushindwa kufanya shughuli za maendeleo,” alisema Mahiza.
Alisema kuwa sehemu yoyote yenye machafuko maendeleo hakuna hivyo kuna kila sababu ya kuiombea nchi ili iepukane na hayo yanayotaka kujitokeza.
Kwa upande wake katibu wa umoja wa makanisa ya kipentekoste mkoa wa Pwani Mchungaji Gervase masanja alsiema kuwa endapo amani itatoweka hata uhuru wa kumwabudu mungu hautakuwepo.
“Baadhi ya watu wameingiza siasa makanisani jambo ambalo linaweza likawa chanzo cha vurugu hivyo tunawaomba waumini wasiiingize siasa kwenye sehemu za kuabudia kwani ni hatari na ndiyo sababu ya sisi kuamua kufunga kuombea amani iliyopo isivunjike,” alisema Mch Masanja.
Kikao hicho pia kiliwajumuisha wakuu wa wilaya, wakuu wa polisi wa wilaya, vyama vya siasa, vyama vya watu wenye ulemavu na watu maarufu ndani ya jamii kwenye mkoa huo.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MAMLAKA ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (SUMATRA) mkoa wa Pwani imekunjua makucha yake baada ya kumtaka kondakta wa basi la kampuni ya Mbazi kuwarudishia nauli waliyoizidisha tofauti na ile iliyopangwa na serikali.
Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki kwenye stendi ya maili Moja wilayani Kibaha baada ya abiria kulalamika kuwa wamezidishiwa nauli wakati wakikata nauli kwenye kituo cha mabasi cha Ubungo Jijini Dar es Salaam.
Kondakta wa basi hilo ambalo linafanya safari zake kati ya Dar es Salaam na Arusha alijikuta matatani baada ya basi lake kuzuiliwa na kurejesha nauli ambazo zilikuwa zimezidi kwa abiria 19.
Baadhi ya abiria ambao waliongea na waandishi wa habari kuhusiana na kuzidishiwa nauli kati yao ni Nagi Nurdin aliyekuwa akienda Moshi alisema kuwa yeye alikatiwa nauli kwa shilingi 29,000 badala ya shilingi 22,700 ambapo alikata kwenye ofisi za basi hilo.
Naye Forida Faustin alisema kuwa yeye naye alikuwa akienda Moshi alitozwa 33,000 huku YUda Nduti akitozwa 30,000 ambapo walianza kumtajia nauli ni shilingi 40,000.
Kwa upande wake ofisa mfawidhi wa SUMATRA Pwani Iroga Nashon alisema kuwa hatua ya kwanza waliyoichukua ni kumwamuru kondakta wa basio hilo lenye namba T 600 APN kuwarejeshea nauli zilizozidi abiria hao.
“Baada ya kurejesha nauli zilizozidi ambazo zilikuwa ni zaidi ya 300,000 pia tuliwapiga faini ya shilingi 250,000 kwa kosa hilo kwa kuzingatia kifungu cha sheria cha 34 na ndipo tuliporuhusu basi hilo kuendelea na safari yake,” alisema Nashon.
Kwa upande wake kondakta wa basi hilo hakuwa tayari kuzungumza na waandishi na kusema kuwa yeye siyo msemaji ambapo alidai abiria hao walikatiwa tiketi stendi ya Ubungo.
Nashon aliwataka abiria kutoa taarifa kuhusiana na wamiliki au makondakta na madereva kuwanyanyasa kwa makusudi huku wakijua sheria za uendeshaji wa mabasi hayo ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kwa wanaokiuka.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MKOA wa Pwani unakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa gari la kunyanyulia vitu vizito (Crane) ikiwemo magari yanayoharibika kwenye barabara za mkoa huo.
Chanagamoto hiyo ilionekana juzi baada ya magari kukwama kwa zaidi ya saa tano baada ya magari mawili kuharibika kwenye daraja linalounganisha mikoa ya Pwani na Dar es Salaam eneo la Kiluvya wilayani Kibaha.
Magari yaliyoharibika ni ya mizigo ambapo la kwanza ni Scania namba T 503 DTJ na Fuso lenye namba za usajili T 515 DSA magari haya yaliziba kabisa barabara hivyo kusababisha magari kushindwa kuingia wala kutoka kwa muda huo.
Akizungumza kwenye eneo la tukio hilo kamanda wa polisi wa kikosi cha usalama barabarani wa mkoa huo Nasoro Sisiwaya alisema kuwa ilibidi watumie nguvu ya ziada kuliondoa gari moja ili magari yaweze kupita kwani lori kubwa liliharibika katikati ya daraja la mto Mpiji.
“Kwa kweli gari la kunyanyua vitu vizito ni changamoto kubwa kwani magari yanayo anguka au kupata ajali yanashindwa kuondolewa kwa wakati kutokana na kukosa huduma ya gari hilo,” alisema Sisiwaya.
Sisiwaya alisema kuwa tayari wameshaiomba serikali na wakala wa barabara TANROADS ili wanunue gari hilo na liwe hapa Kibaha kwani kutegemea litoke Dar es Salaam ni tatizo kubwa.
“Tumeandika sehemu husika kuomba gari hilo ili kukabiliana kwani tukio hili limesababisha usumbufu mkubwa sana kwa magari yanayopita barabara hii ya Morogoro ambayo ndiyo mlango wa kuingilia na kutoka Dar es Salaam.
Aidha alisema wataiomba TANROADS kujenga barabara mbadala kwani kutegemea barabara moja ni tatizo kubwa na kutokana na tukio hili tumeona jinsi gani watu walivyohangaika na kusababisha usumbufu mkubwa.
Mwisho.    

PIMENI MAENEO YA SHULE ILI YAPATE HATI MILIKI

Na John Gagarini, Kibaha
HALMASHAURI kote nchini zimetakiwa kupima maeneo ya shule ili kuepuka
kuvamiwa kwani hazina hati za kumiliki maeneo hayo kisheria na kuepuka
wavamizi.
Akizungumza wakati wa kufunga mashindano ya Umoja wa Michezo na
Taaluma kwa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) Waziri wa Tawala za
Mikoa n Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Hawa Ghasia alisema kuwa maeneo
mengi ya shule hayajapimwa.
Ghasia asliema kuwa anashangaa ni kwa nini halmashauri hazipimi maeneo
ya shule hivyo kuwa rahisi kuvamiwa na watu kwa ajili ya kuyatumia kwa
shughuli za kimaendeleo.
“Inashangaza kuona kuwa maeneo mengi ya shule hayajapimwa na
halmashauri zinaangali tu hali hii ni mbaya kwani mtu anaweza kuvamia
bila ya woga na kwa kuwa hakuna hati miliki hivyo ni rahisi kuichukua
ardhi ya shule,” alisema Ghasia.
Alisema kuwa maeneo hayo nayo yanapaswa kuwa na hati miliki kama
ilivyo umiliki wa watu binafsi au taasisi za serikali.
“Nawaomba wakurugenzi kutekeleza hili ili kuondoa uporwaji wa maeneo
ya shule kwani kwa sasa migogoro ni mingi baina ya mashule na wananchi
ambao wanavamia maeneo hayo,” alisema Ghasia.
Aidha alsiema kuwa halmashauri ziepukane na mawazo ya kuyatoa maeneo
hayo kwa wawekezaji kwa ajili ya kufanyia shughuli za biashara au
matumizi mengine.
“Maeneo kwenye halmashauri yako mengi kwa nini waone maeneo ya shule
ndiyo sehemu ya kuwekeza hilo ni kosa kama wanahitaji maeneo wapewe
maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya uwekezaji,” alisema Ghasia.
Alizitaka halmashauri kuyalinda maeneo ya shule ambayo yamekuwa
yakivamiwa na watu bila ya kuwa na woga wowote licha ya kuwa ni
kinyume cha sheria.
Mwisho.

Monday, July 1, 2013

TAPELI AWACHIMBISHA KABURI WATU, ATOWEKA NA SIMU ZAO NA KAMERA

Na John Gagarini, Kibaha
MTU mmoja aliyetambuliwa kwa jina la Abdul Ramadhan (35) amewatapeli baadhi ya wakazi wa Kwa Mathias wilayani Kibaha mkoani Pwani kwa kuwachimbisha kaburi kisha kutoweka na kuwaachia kaburi tupu bila ya kuzikwa marehemu kama alivyowaomba azike ndugu yake.
Tukio hilo lilitokea juzi kwenye mtaa huo baada ya mtu huyo kufika hapo na kuomba kusaidiwa kumzika mfanyakazi wake ambaye alidai kuwa hana uwezo wa kumsafirisha kwani kwao ni mbali.
Mbali ya kuwachimbisha kaburi wakazi hao pia alifanikiwa kuwaibia simu mbili pamoja na kamera moja pamoja na kuacha deni kwenye vyakula ambavyo vilitumiwa na wachimba kaburi huku kingine kikiwa kimeandaliwa bila ya kuliwa.
Akielezea mkasa huo Ustaadhi wa Masjid Kadiriya uliopo Kwa Mathias Said Omary alisema kuwa mtu huyo alifika msikitini hapo na kukutana na kiongozi kasha kuomba kuwa asaidiwe kuzikiwa mfanyakazi wake, msikiti ukamkubalia na taratibu zikaanza kufanyika.
Omary alisema kuwa baada ya kuelekezwa na mkuu wake alitakiwa ashughulikie suala hilo na kwenda na mtu huyo kwenye makaburi ya mambo akiwa na watu wengine watatu kwa ajili ya kuchimba kaburi kwa ajili ya kumsitiri marehemu.
“Tulikwenda makaburini na wachimbaji wakaanza kazi ya kuchimba kaburi akawaletea chain a maandazi 20 wakanywa wakaendelea na kazi yao mimi akaniambia twende hospitali ya Tumbi aliko marehemu kwa ajili ya kumwandaa,” alisema Omary.
Alisema wakiwa njiani alimwambia kuwa anaomba simu yake ili awasiliane na ndugu zake kwani ya kwake imeisha chaji pia amtafutie mpiga picha kwa ajili ya tukio hilo kwa ajili ya kuwaonyesha ndugu juu ya mazishi hayo.
“Tulikwenda kwa mpiga picha wakakubaliana apige picha akasema kabla ya kwenda Tumbi wakachukue nyama na vitu vingine kwa ajili ya msiba huo na walipofika Maili Moja wakachukua nyama kilogramu 25 na,”alisema Omary.
Aliongeza kuwa  wakati wameshapima nyama aliwaambia ngoja akanunue viungo vingine lakini hakurudi tena na kutoweka kusikojulikana huku kaburi likiwa limeshachimbwa na liko wazi hadi sasa.
Kwa upande wake mpiga picha Jum Said ambaye yeye aliibiwa kamera na simu alisema kuwa walikubaliana apige picha 36 hadi 40 ambazo gharama yake ni sawa na shilingi 36,000 au 40,000.
Alisema wakati wako kwenye harakati ya kunua nyanya alimwachia begi likiwa na kamera na simu lakini aliporudi hakumkuta akiwa yeye na Ustaadhi na dereva wa teksi ambayo aliikodisha kwa shughuli za mazishi hayo.
“Alituacha mimi na ustaadhi tukiwa na nyama huku tukimsubiria hali amabyo ilitufanya tuingie matatani kwani wauzaji nyama ilibidi watubana ndipo tulipowaelewesha juu ya hali halisi ndiyo ikawa salama kwetu na kuondoka,” alisema.
Watu waliokumbwa na hali hiyo walisema kuwa mbali ya kudanganya mambo yote hayo pia aliweka oda ya chakula sahani 20 kwenye hoteli lakini hakuonekana tena, katika kufuatilia walibaini jina la mtu huyo kwani siku moja kabla ya tukio hilo alilala kwenye nyumba ya kulala wageni ya Iwawa iliyopo mtaa wa Kwa Mbonde jirani na hapo wakazi hao walitoa taarifa kwenye kituo cha polisi Kwa Mathias juu ya tukio hilo.
Mwisho.

Friday, June 7, 2013

SUMATRA KUDHIBITI MADEREVA PWANI

Na John Gagarini, Kibaha
MAMLAKA ya Udhibiti wa usafiri Majini na Nchini Kavu (SUMATRA) imefungua ofisi yake mkoani Pwani na kuwataka wananchi kutoa taarifa za mabasi yanayokatisha ruti na kutotoa tiketi kwa abiria.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake ofisa mwandamizi wa SUMATRA wa mkoa Iroga Nashoni alisema kuwa abiria wanapaswa kukitumia chombo hicho ili kuondoa kero kwa wasafiri.
Iroga alisema kuwa ofisi hiyo imefunguliwa mwezi uliopita kwa lengo la kusogeza huduma kwa wateja wao ambapo inaendelea kujitanua kwenye mikoa, mingine ikiwa ni Singida, Iringa, Musoma na Rukwa.
Alisema kuwa changamoto kubwa waliyoiona ni mabasi mengi ya abiria kushindwa kumalizia safari zao Kukatisha Ruti) na kutotoa tiketi kwa abiria jambo ambalo ni kinyume cha sheria ambapo watawapiga faini hata ikibidi kuwafungia leseni madereva watukutu.
“Changamoto hiyo inakuwa kubwa kutokana na abiria wengi kutokuwa na elimu ya kujua haki zao za msingi wanapokuwa wanasafiri hivyo kuwapa mwanya madereva kufanya watakavyo,” alisema Iroga.
Aliongeza kuwa wataendelea kutoa elimu kwa pande zote ikiwa ni pamoja na abiria, madereva na wamiliki wa mabasi hayo ili waweze kufuata sheria bila ya kushurutishwa.
“Jana tulifanya operesheni kukamata magari yenye makosa mbalimbali ambapo magari manne yamekutwa na makosa na kupigwa faini kutegemea na makosa,” alisema Iroga.
Alibainisha kuwa wataendelea kufanya operesheni za kushtukiza za mara kwa mara ili kukabiliana na madereva wengi kukiuka sheria za barabarani na kuwataka wananchi kutoa taarifa na si kulalamika bali wachukue hatua.
Mwisho.

MBUNGE AMWAGA VIFAA TIMU YA UMISSETA

Na John Gagarini, Kibaha
MBUNGE wa Jimbo la Kibaha mkoani Pwani Silvestry Koka ametoa seti za
jezi kwa timu za mpira wa pete na soka za mkoa huo zinazojiandaa na
mashindano ya Umoja wa Michezo na Sanaa kwa Shule za Sekondari
Tanzania (UMISSETA) Kanda ya Mashariki inayotarajiwa kutimua vumbi
hivi karibuni mjini Kibaha.
Jezi hizo zimekabidhiwa kwa timu hiyo na mke wa mbunge huyo Selina
Koka kwenye kambi ya timu hiyo iliyopo kwenye shule ya Filbert Bayi
iliyopo wilayani Kibaha.
Mbali ya jezi hizo pia timu ya mkoa iliahidiwa kupatiwa mipira ya
michezo hiyo, mchele, kilogramu 100, mafuta ya kupikia, maji na sukari
pamoja na kumkabidhi mwalimu wa timu hiyo Loyd Mgombele kiasi cha
shilingi 100,000 kwa ajili ya shughuli za kuratibu timu hiyo.
Akiwakabidhi manahodha wa timu ya mpira wa pete na mpira wa miguu Koka
alisema kuwa lengo la kutoa vitu hivyo ni kuhamasisha timu hiyo ili
iweze kufanya vizuri kwenye michezo yake dhidi ya mkoa wa Morogoro ili
kuunda timu ya Kanda.
Koka alisema kuwa mkoa wa Pwani ni wenyeji wa mashindano hayo
wanapaswa kuwa na maandalizi mazuri ili kuweza kuwakilisha vema mkoa
na baadaye Taifa ambapo michuano hiyo itafanyika kwenye viwanja vya
Shirika la Elimu Kibaha Tumbi.
Aliwataka wachezaji hao kujituma kuzingatia yale wanayofundishwa na
walimu wao ili kuhakikisha wanafanya vyema na kutoa wachezaji wazuri
ili kuunda timu ya Kanda inayoundwa na mikoa ya Pwani na Morogoro.
Kwa upande wake ofisa elimu taaluma mkoa wa Pwani Godwin Mkaruka
ambaye aliwakilisha mkoa huo alisema kuwa ana mpongeza mbunge huyo kwa
kuisaidia timu ya mkoa ili iweze kuwakilisha vema mkoa huo.
Aliwataka wadau mbalimbali kujitokeza kuisaidia timu hiyo kwa hali na
mali kama alivyojitolea Mbunge huyo ili iweze kuuletea mkoa ushindi
katika michuano hiyo ambayo hufanyika wilayani humo kila mwaka.
Mwisho.
3 attachments — Download all attachments   View all images   Share all images  
E89A0881.jpgE89A0881.jpg
1311K   View   Share   Download  
E89A0882.jpgE89A0882.jpg
1162K   View   Share   Download  
E89A0874.jpgE89A0874.jpg
1