Thursday, April 3, 2025

USSI ATAKA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA MIKOPO ASILIMIA 10 YA HALMASHAURI WAJIKWAMUE KIUCHUMI

VIJANA kwenye Halmashauri ya Mji Kibaha Mkoani Pwani wametakiwa kujiunga kwenye vikundi ili waweze kupata fedha za mikopo asilimia 10 za mapato ya ndani ya Halmashauri ili wajikwamue kiuchumi.

Hayo yamesemwa na kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ussi alipotembelea kikundi cha The Dream kilichopo Mtaa wa Kilimahewa Kata ya Tangini.

Ussi amesema kuwa ili vijana waweze kujitegemea wanapaswa kuwa na shughuli za kufanya za kujiongezea kipato kwa kufanya shughuli za kiuchumi.

"Tuwapongeze vijana hawa kwa kuonyesha mfano mzuri kwa kukopa fedha ambazo matunda yake yanaonekana kwani fedha hizo za Halmashauri zimewanufaisha hivyo vibana wengine waige kikundi hichi,"amesema Ussi.

Akisoma risala mweka hazina wa kikundi hicho kinajishughulisha na utengenezaji wa Clips na Tambi  Neema Shao amesema kuwa walikopa kiasi cha shilingi milioni 15 kutoka Halmashauri Januari mwaka huu.

Shao amesema kuwa kikundi kinauwezo wa kuzalisha pakiti 600 na kwa mwezi pakiti 12,000 zenye thamani ya shilingi milioni 9.6 ambapo uzalishaji hufanyika kwa siku 20 kwa mwezi.

Amesema kuwa wanauwezo wa kupata faida ya shilingi milioni mbili ambapo hadi sasa wamesharejesha kiasi cha shilingi 625,000 na wameweza kununua Toyo ya kusambazia bidhaa zao ambapo zamani walikuwa wakikodisha pikipiki.


KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ISMAIL USSI APONGEZA UJENZI ZAHANATI KILIMAHEWA

MKIMBIZA mbio za Mwenge Kitaifa Ismail Ussi ameweka jiwe la msingi kwenye Zahanati ya Kilimahewa ambayo mara itakapokamilika itahudumia wananchi 68,371 wa Kata tatu.

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ismail Ussi amesema kuwa ujenzi huo ni azma ya Rais anayoitaka ya kuwaondolea adha wananchi ya kupata huduma za afya mbali.

Ussi amesema kuwa anaipongeza Halmashauri na wananchi kwa kufanikisha ujenzi huo ambapo hadi kukamilika kwake unatarajia kutumia kiasi cha shilingi milioni 234.3.

"Tumeambiwa mara itakapokamilika wananchi hawatapata usumbufu kwenda mbali kupata huduma za afya watapata karibu hivyo kupata muda kufanya shughuli za maendeleo,"amesema Ussi

Akisoma taarifa Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Catherine Saguti amesema kuwa ujenzi wa Zahanati hiyo kwa sasa umefikia asilimia 61 ya ujenzi na mradi huo unatarajiwa kukamilika mwaka wa fedha wa 2025/2026.

Saguti amesema kuwa manufaa ni kwa Kata tatu za Tangini, Maili Moja na Pangani zenye jumla ya mitaa 16 ambapo wananchi wataondokana na adha ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya.

Aidha amesema kuwa hadi sasa mradi huo umetumia kiasi cha shilingi milioni 108.3 huku wananchi wakichangia kiasi cha zaidi ya shilingi milioni moja kwa kujaza kifusi.

Naye Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka amesema anaishukuru serikali kuwapatia eneo hilo ambalo lilikuwa mali ya Wizara ya Mifugo na kupangiwa matumizi ya jamii.

Koka amesema kuwa afya ni kipaumbele kikubwa kwa wananchi kwani wakiwa na afya njema wataweza kujiletea maendeleo.


MWENGE WAWEKA JIWE LA MSINGI MRADI SHULE YA AWALI MSINGI YA MCHEPUO WA KIINGEREZA KATA YA SOFU

HALMASHAURI ya Mji Kibaha imetoa kiasi cha shilingi milioni 458.4 kwa ajili ya ujenzi wa shule ya awali na msingi ya Nyerere ya muundo wa Kiingereza iliyopo Mtaa wa Sofu na Kata ya Sofu.

Aidha hadi mradi huo utakapokamilika utatumia kiasi cha shilingi milioni 704.6 ikiwa ni mapato ya ndani ya Halmashauri.

Akisoma taarifa mbele ya kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ismail Ussi, ofisa elimu awali na msingi Theresia Kyara amesema kuwa ujenzi huo uko hatua ta umaliziaji.

Kyara amesema kuwa ujenzi huo umehusisha vyumba tisa vya madarasa, matundu 17 ta vyoo, kichomea taka, jengo la utawala, ununuzi wa samani na madawati.

Amesema kuwa hadi sasa zimetumika kiasi cha shilingi milioni 297.7 kwa awamu ya kwanza huku awamu ya pili ikitumia milioni 157.1 na awamu ya tatu zitatumika kiasi cha shilingi milioni 89 na ujenzi umefikia asilimia 64.5

Kwa upande wake kiongozi huyo wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ussi amesema kuwa shule za msingi za mchepuo wa Kiingereza za serikali ni nzuri katika kuendeleza elimu kwa watoto.

Ussi amesema kuwa shule hizo ni nzuri kwani gharama zake ni nafuu hivyo mradi huo ni mkombozi kwa wanafnzi walioko kwenye maeneo jirani na shule hiyo.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ambaye pia Diwani wa kata ya Sofu Mussa Ndomba amesema kuwa wananchi waliomba mradi huo ambapo na kupelekwa kwenye baraza la madiwani na kupitishwa.

Ndomba amesema hilo lilikuwa hitaji kubwa la wananchi wa Mtaa na Kata hiyo hivyo utakuwa na manufaa makubwa kwa wananchi kwa watoto wao.

KIONGOZI MBIO ZA MWENGE ASIFU MRADI WA MAEGESHO YA MALORI YA MIZIGO

MBIO za Mwenge zimekagua eneo la mradi wa maegesho ya magari makubwa ambao utakapokamilika utaiingizia Halmashauri ya Mji Kibaha kiasi cha shilingi bilioni 3.3 kwa mwaka.

Akikagua na kupata taarifa kwenye mradi huo uliopo Kata ya Misugusugu kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ussi amesema kuwa hicho ni chanzo kizuri cha mapato kwa Halmashauri hiyo.

Ussi amesema kuwa mradi huo wa maegesho hayo ambayo yatakuwa ya kisasa yataifanya Halmashauri kuongeza mapato yake hivyo kuendelea kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.

"Jambo ambalo ni zuri ni kulipa fidia na maendelezo kiasi kikichotengwa ni bilioni 1.8 kwa watu 23 ambapo kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kimelipwa kwa watu 21 hii inaonyesha kuwa wananchi wanalipwa haki zao na hakuna mtu atakaye kosa haki yake,"amesema Ussi.

Kwa upande wake Mthamini wa Halmashsuri ya Mji Kibaha Patrick Kibwana amesema kuwa mradi huo utakuwa wa shilingi bilioni 23 ikiwa ni mapato ya ndani.

Amesema kuwa hadi sasa kiasi cha shilingi milioni 317.8 bado hakijalipwa huku watu wawili wakiendelea na taratibu za kibenki.

Kibwana kuwa mradi utakuwa na nyumba za kulala wageni sehemu ya kuoshea magari kituo cha zimamoto mama lishe hoteli sehemu ya kutengeneza magari mifumo ya miundombinu ya gesi vyoo na mabafu kituo cha mafuta kituo cha polisi fremu za biashara huduma za afya ghala za kuhifadhia mizigo na mizani ya kupimia uzito.

Amesema kuwa mradi amesema kuwa mradi huo utatoa ajira kwa vijana 1,000 ambapo eneo hilo lina ukubwa wa hekari 18 na utaondoa msongamano wa malori kutoka Jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John amesema kuwa maegesho hayo yamejengwa jirani na eneo la viwanda la Zegereni hivyo huduma hiyo inahitajika sana.

John amesema kuwa mradi huo utakuwa ni sehemu ya kuzalisha ajira kwa wananchi hususani vijana kwenye Wilaya hiyo na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano.

 



Wednesday, April 2, 2025

KIONGOZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA AFURAHISHWA MRADI MAEGESHO YA HALMASHAURI YA MJI KIBAHA


MBIO za Mwenge zimekagua eneo la mradi wa maegesho ya magari makubwa ambao utakapokamilika utaiingizia Halmashauri ya Mji Kibaha kiasi cha shilingi bilioni 3.3 kwa mwaka.

Akikagua na kupata taarifa kwenye mradi huo uliopo Kata ya Misugusugu kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ussi amesema kuwa hicho ni chanzo kizuri cha mapato kwa Halmashauri hiyo.

Ussi amesema kuwa mradi huo wa maegesho hayo ambayo yatakuwa ya kisasa yataifanya Halmashauri kuongeza mapato yake hivyo kuendelea kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.

"Jambo ambalo ni zuri ni kulipa fidia na maendelezo kiasi kikichotengwa ni bilioni 1.8 kwa watu 23 ambapo kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kimelipwa kwa watu 21 hii inaonyesha kuwa wananchi wanalipwa haki zao na hakuna mtu atakaye kosa haki yake,"amesema Ussi.

Kwa upande wake Mthamini wa Halmashsuri ya Mji Kibaha Patrick Kibwana amesema kuwa mradi huo utakuwa wa shilingi bilioni 23 ikiwa ni mapato ya ndani.

Amesema kuwa hadi sasa kiasi cha shilingi milioni 317.8 bado hakijalipwa huku watu wawili wakiendelea na taratibu za kibenki.

Kibwana kuwa mradi utakuwa na nyumba za kulala wageni sehemu ya kuoshea magari kituo cha zimamoto mama lishe hoteli sehemu ya kutengeneza magari mifumo ya miundombinu ya gesi vyoo na mabafu kituo cha mafuta kituo cha polisi fremu za biashara huduma za afya ghala za kuhifadhia mizigo na mizani ya kupimia uzito.

Amesema kuwa mradi amesema kuwa mradi huo utatoa ajira kwa vijana 1,000 ambapo eneo hilo lina ukubwa wa hekari 18 na utaondoa msongamano wa malori kutoka Jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John amesema kuwa maegesho hayo yamejengwa jirani na eneo la viwanda la Zegereni hivyo huduma hiyo inahitajika sana.

John amesema kuwa mradi huo utakuwa ni sehemu ya kuzalisha ajira kwa wananchi hususani vijana kwenye Wilaya hiyo na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano.

 

Tuesday, April 1, 2025

TAASISI YA BEGA KWA BEGA NA TANZANIA PWANI YACHANGIA DAMU CHUPA 19

TAASISI ya Bega kwa Bega na Tanzania Mkoani Pwani imechangia damu chupa 19 kwenye benki ya damu ajili ya wagonjwa wanaohudumiwa kwenye hospitali Wilayani Kibaha. 

Kiasi hicho cha damu kilipatikana wakati wa bonanza la kuhamasisha wananchi kujitokeza kushiriki kwenye uzinduzi wa mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa Mkoani Pwani 2025 lililofanyika kwenye uwanja wa Bwawani Kibaha.

Mratibu wa taasisi hiyo kitaifa Ruth Mateleka bonanza hilo limefanywa ili kuhamasisha wananchi kushiriki uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru zitakazofanyika leo kwenye uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha.

"Kazi yetu kubwa ni kuhamasisha wananchi kushiriki shughuli za kimaendeleo na kutaja kazi zilizofanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan na tunashukuru watu kujitolea damu ili kusaidia wagonjwa,"amesema Mateleka.

Kwa upande wake Zuhura Sekelela ambaye ni mratibu wa taasisi hiyo Mkoa wa Pwani alisema kuwa upatikanaji wa damu hiyo kutasaidia benki ya damu kuwa na damu ili kusaidia wagonjwa.

Sekelela alisema kuwa shughuli nyingine ambazo wanazifanya ni kupanda miti, kufanya usafi kwenye taasisi za umma ikiwa ni pamoja na shuleni, hoapitali na maeneo mbalimbali pamoja na kusaidia watoto waishio kwenye mazingira magumu.

Naye Mchungaji Josephine Mwalusama amesema kuwa yeye kama Mchungaji anamshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuhimiza wanawake kushika nafasi za uongozi.

Mwalusama amesema kuwa Rais amefanya kazi kubwa na zinaonekana na ameshukuru Mwenge kuwashiwa Mkoani Pwani kwani utautangaza Mkoa na wajasiriamali watanufaika kwa kuwashwa mwenge huo wa uhuru.

Naye Mwenyekiti wa Vijana kutoka taasisi hiyo ya Bega kwa Bega na Tanzania Mkoa wa Pwani Athuman Lusambi  amesema kuwa wanawahamasisha vijana kushiriki kwenye Mwenge ili wawe wazalendo na nchi yao.

Monday, March 31, 2025

NMB KUTUMIA ZAIDI YA BILIONI 6 MIRADI YA MAENDELEO

BENKI ya inatarajia kutumia kiasi cha shilingi bilioni 6.4 kwa ajili ya kuchangia shughuli za maendeleo kwa mwaka wa 2025.

Hayo yalisemwa na Meneja wa benki hiyo Kanda ya Dar es Salaam ambaye aliwakilishwa na meneja wa tawi la Mlandizi Wilayani Kibaha William Marwa wakati wa Kongamano la Vijana juu ya umuhimu wa kushiriki mbio za mwenge mkoa wa Pwani 2025.

Alisema vijana wanapaswa kujua historia ya mbio za mwenge wa uhuru na fursa zilizopo kupitia mwenge ambao ni alama ya mshikamano wa kuleta maendeleo ya nchi.

"Tangu mwenge umeanza mbio zake kwa sasa ni miaka 61 na pia tunakumbuka kifo cha mwasisi wa Taifa letu miaka 26 iliyopita lazima tumjue kwani aliifanyia nchi hii mambo makubwa,"alisema Marwa. 

Akizungumzia benki hiyo ambayo ni kubwa kuliko zote nchini imekuwa ikichangia maendeleo na ni chachu kwa kuchangia kwenye sekta ya afya, elimu na kutoa mkono wa pole kwa wananchi wanaopata majanga.

"Benki imekuwa ikirudisha sehemu ya faida kwa kuchangia suala la maendeleo kupitia sekta mbalimbali kwani wao ni sehemu ya wateja kwani ina matawi wilaya zote nchini,"alisema Marwa.

Alisema kuwa benki hiyo ina matawi 241 Atm 720 mawakala 50,000 na wateja milioni 8.7 kote nchini na bado inaendelea kuboresha huduma zake kimtandao.