UONGOZI wa Mtaa wa Maili Moja A umetimiza ahadi yake ya kujenga ofisi ambapo Diwani wa Kata ya Maili Moja aliizindua ofisi hiyo na kuondokana na ofisi waliyokuwa wamepanga.
UONGOZI wa Mtaa wa Maili Moja A umetimiza ahadi yake ya kujenga ofisi ambapo Diwani wa Kata ya Maili Moja aliizindua ofisi hiyo na kuondokana na ofisi waliyokuwa wamepanga.
WAKALA wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na mkoa huo wametakiwa kuandika ombi maalumu la fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya barabara kwenye maeneo ya uwekezaji.
Hayo yemesemwa Mjini Kibaha na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Denis Londo wakati wa majumuisho ya ziara ya siku moja kutembelea barabara zilizojengwa na Tarura Mkoa huo.
Londo amesema kuwa kutokana na mkoa huo kuwa na uwekezaji mkubwa hasa wa viwanda ambao una manufaa kwa Taifa ni vema wakaomba maombi maalumu ya fedha kwa ajili ya miundombinu ya barabara badala ya kuomba kidogo kidogo.
"Angalieni mahitaji ya barabara zote ambazo zinahitajika kwenye maeneo muhimu ya uwekezaji badala ya kuomba sehemu chache ili muweze kuboresha kwa pamoja,"amesema Londo.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kukiwa na miundombinu mizuri ya barabara kwenye maeneo hayo kutakuwa ni kivutio kwa wawakezaji kuendelea kuwekeza.
Kunenge amesema kuwa Tarura imeweza kujenga barabara yenye urefu wa Kilometa 12.5 kwenye eneo la viwanda la Zegereni yenye thamani ya shilingi bilioni 16.4 ambayo imekamilika kwa sasa ikiwa kwenye muda wa matazamio.
Naye Meneja wa Tarura Mkoa wa Pwani Mhandisi Leopold Runji alisema miradi mitatu ambayo imetembelewa na kamati hiyo ni kutoka barabara ya Morogoro kwenda Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha yenye urefu wa mita 300 na umekamilika unathamani ya shilingi milioni 500.
Runji alisema kuwa barabara nyingine ni Visiga Zegereni ni eneo la viwanda kiwango cha lami kilometa 12.5 tunamshukuru kutoa fedha bilioni 16.4 na umekamilika sasa kipindi cha matazamio barabara nyingine ni ya Picha ya Ndege Boko Timiza kilometa 7.8 ambapo hadi sasa zimekamilika kilometa 1.2 awamu ya kwanza milioni 950 kwa awamu ya kwanza ujenzi huku ukiwa na awamu tatu.
Mjumbe wa Kamati hiyo Saasisha Mafuwe alisema kuwa katika ujenzi wa barabara zinazosimamiwa na Tarura kuwe na kiwango maalum cha gharama za ujenzi ijulikane mfano kwa kilometa na kuwe na bei maalumu siyo kila mtu kujenga kwa utashi ambapo gharama zinatofautiana kutoka sehemu moja hadi nyingine.
Kamati hiyo ilitembelea barabara za Picha ya Ndege-Boko Timiza, barabara kuelekea ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha na Visiga Zegereni na kuridhishwa na ujenzi wa barabara hizo.
IMEELEZWA watu kuoneana aibu ndani ya familia kumesababisha vitendo vya ukatili kuendelea ndani ya jamii ambapo hali hiyo imezipeleka familia pabaya.
Aidha serikali ya Mkoa wa Pwani imesema kuwa itachukua hatua kali kwa watu wanaowafanyia ukatili watoto washindwe kufikia ndoto zao na kukosa haki zao.
Hayo yamesemwa na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Shangwe Twamala wakati wa Siku ya Mtoto wa Afrika kimkoa iliyofanyika Mjini Kibaha.
Twamala amesema kuwa baadhi ya taarifa zinaonyesha kuwa wanaofanya vitendo hivyo ni ndugu wa karibu.
"Ukatili unafanywa na ndugu wa karibu ambapo familia zinashindwa kuchukua hatua sababu ya kuoneana Muhali (Aibu) hili hatulikubali,"amesema Twamala.
Akisoma risala ya watoto wa mkoa wa Pwani Evelin Mhema amesema kuwa baadhi ya changamoto ni pamoja kufanyiwa vitendo vya ukatili mimba za utotoni, ubakaji, vipigo na vitendo vingine vinavyowanyima haki zao.
Mhema amesema kuwa watashirikiana na viongozi wakiwemo walimu ili waweze kufikia ndoto zao walizojiwekea kwa kusoma kwa bidii na kutii wazazi na walezi wao.
Kwa upande wake Said Mwinjuma amesema kuwa matumizi ya dawa za kulevya yamekuwa changamoto kwa vijana na kusababisha mmomonyoko wa maadadili.
Naye Mkurugenzi wa Kituo cha Msaada wa Kisheria Kibaha (KPC) Catherine Mlenga amesema kuwa watoto pia nao wajilinde kwa kutotembea usiku na kwenda kwenye mabanda ya video ma kulindana wao kwa wao.
Mlenga amesema kuwa pia wasipokee zawadi au kuomba fedha kwa watu wasiowafahamu na wazazi wawalinde watoto kwa kutokuwa wakali na
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Picha ya Ndege Grace Jungulu ametoa tofali 300 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya katibu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Kibaha Mjini.
WILAYA ya Kibaha imejiwekea lengo la kukusanya chupa za damu 700 hadi 800 kwa mwaka ili ziweze kusaidia wahitaji wakiwemo akinamama wanaojifungua watoto na majeruhi wa ajali.
Hayo yamesemwa na mratibu wa damu salama wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Nyaisawa Birore alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kwenye zoezi la uchangiaji damu kwenye Kituo cha Afya Mlandizi.
Birore amesema kuwa wamejiwekea malengo ya kukusanya chupa 85 hadi 200 kwa kipindi cha robo mwaka ili ziweze kutumika kwa wagonjwa wenye mahitaji ya damu.
"Matumuzi ya damu kwa mwezi yalikuwa ni chupa 45 lakini yameongezeka na kufikia ni chupa 80 hadi 100 hivyo mahitaji ni makubwa sana na tunawaomba wananchi wajitokeze kwa wingi kujitolea,"amesema Birore.
Moja ya wachangiaji wa damu ambaye ni katibu wa Umoja wa Vijana (UVCCM) Kibaha Vijijini Joel Kijuu amesema ameamua kujitolea ili kusaidia kuokoa maisha ya akinamama na wagonjwa wanaohitaji kuongezewa damu.
Kwa upande wake mhamasishaji uchangiaji damu Mariam Ngamila amesema kuwa baadhi ya wananchi wamekuwa na dhana kuwa damu inayochangwa inauzwa kitu ambacho siyo cha kweli.
Naye mhamasishaji uchangiaji damu Maria Ngamila amesema tone moja la damu linaweza kuokoa maisha ya watu wengi hivyo vijana wahamasike kuchangia damu.
Faudhi Kinanga ambaye yuko kwenye kambi ya uchangiaji damu amesema kuwa wamekuwa wakitoa elimu kwa vijana kushiriki zoezi la uchangiaji damu ili kuisaidia jamii.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amezindua taarifa za utendaji katika Sekta ndogo ya Umeme, Gesi Asilia na Mafuta kwa mwaka 2022/2023 ambapo ametoa maelekezo mahsusi kwa Wizara na Taasisi mbalimbali kufanyia kazi taarifa hizo zinazoonesha mafanikio na changamoto katika Sekta Nishati.
Akizindua taarifa hizo tarehe 14 Juni, 2024 jijini Dodoma, Dkt. Biteko ameagiza Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati pamoja na Wizara ya Mipango na Uwekezaji kusoma taarifa hizo na kuzichambua na changamoto zilizoainishwa zipatiwe majibu ndani ya kipindi cha miezi mitatu.
Aidha ameagiza kuwa, kila aina ya fursa iliyoonekana kwenye taarifa hizo ichukuliwe kwa uzito mkubwa na itambuliwe nani ana uwezo wa kuitumia fursa hiyo ndani ya Serikali na katika taasisi binafsi.
“ Vilevile nawaagiza EWURA mhakikishe kuwa, tathmini ya mwaka ujao ihusishe utendaji wa Nishati Safi ya kupikia ili kuweza kujipima kwa usahihi kuhusu utekelezaji wa ajenda hii inayopewa kipaumbele na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan.” Amesema Dkt. Biteko.
Agizo jingine ni kuwa, matishio yote ya Sekta ya Nishati yaliyoainishwa katika ripoti kati ya mwaka 2023 hadi 2025 yawekewe mabunio ya suluhisho lake ili katika ripoti ijayo changamoto husika zisiwepo ikiwemo suala la kuongezeka kwa mahitaji ya umeme kila mwaka.
Dkt. Biteko pia ameitaka EWURA kupima uhusiano wa rasilimali zilizopo na mafanikio ya watu ambapo amesisitiza kuwa mafanikio ya sekta lazima yaendane na mabadiliko ya maisha ya watu.
Pia ametaka mifumo ya uagizaji mafuta iendelee kuboreshwa baada ya kufanyika utafiti wa kina na kueleza kwamba miundombinu ya mafuta bado inahitajika huku akisisitiza kuwa urasimu usiwepo kwenye Sekta ya Nishati.
Ameipongeza EWURA kwa tathmini ambayo inaonesha kuwa Sekta ya Nishati inaendelea kuimarika, akitolea mfano kutolewa kwa leseni ya kuchimba gesi asilia katika kisima cha Ntorya kilichopo mkoani Mtwara kitakachotoa gesi futi za ujazo milioni 140 kwa siku ambapo leseni ya mwisho ya kuchimba gesi ilitolewa mwaka 2006.
Kuhusu sekta ndogo ya umeme amesema amesema Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kuiboresha ambapo leo ametoa taarifa kuwa mradi wa Julius Nyerere (JNHPP) umeingiza mtambo wa pili katika gridi ya Taifa kupitia mtambo namba 8 na hivyo kufanya mradi huo kuingiza megawati 470 katika gridi.
Kuhusu sekta binafsi amesema, “Sekta binafsi imetutoa kimasomaso, Serikali haiwezi kufanya kila kitu, wamefanya kazi kubwa mno kwenye mafuta, gesi na hata kwenye uzalishaji umeme, wito wangu kwenu msibaki nyuma changamkieni fursa, na kwa taasisi zilizo chini ya Wizara msione sekta binafsi kama watu wajanjawajanja, tuwape kipaumbele.” Amesema Dkt. Biteko
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, amemshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiimarisha Sekta ya Nishati na kusema kuwa Dodoma imeshuhudia matunda ya uimarishaji huo wa sekta kwani sasa umeme haukatiki.
Pia amepongeza utashi mkubwa wa uongozi wa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ambao unachangia kwa kiasi kikubwa katika kuiimarisha Sekta kwa ujumla.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba amesema kuwa katika tathmini iliyozinduliwa inaonesha Sekta ya Nishati imepiga hatua kwenye maeneo megi ikiwemo uhakika wa upatikanaji umeme, upatikanaji na usambazaji wa mafuta kuimarika hasa baada ya Mhe. Dkt. Doto Biteko kuanza kuongoza Wizara ya Nishati, aidha upatikanaji na uwekezaji wa gesi unaendelea kuimarika na hii ikijumuisha usambazaji gesi kwenye maeneo mbalimbali kama katika magari, majumbani na viwandani.
Ameongeza kuwa, taarifa ya Benki ya Dunia kwa nchi za Dunia ya Tatu zinazofadhiliwa na Benki hiyo inaonesha kuwa Sekta ya Nishati kwa Tanzania inafanya vizuri zaidi katika nchi zote zinazoendelea na Bara la Afrika kwa ujumla na hii ni matunda ya usimamizi madhubuti wa Mhe.Dkt. Doto Biteko ambapo eneo lililofanya vizuri zaidi ni usambazaji umeme vijijini na miradi mingine ya nishati kama JNHPP na mradi wa TAZA.
Ameongeza kuwa Benki ya Dunia imeidhinisha Dola.za Marekani milioni 300 ili ziendeleze sekta ya umeme kutokana na ufanisi huo wa Tanzania.
Akitoa taarifa za utendaji katika Sekta ya Nishati, Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Andilile alisema kuwa Sekta ya Nishati inaendelea kuimarika ikiwemo uwekezaji kwenye miundombinu ya mafuta, uwekezaji wa vituo vya mafuta na maghala umeongezeka, kuna ongezeko la uagizaji wa Gesi ya Mitungi (LPG) kwa asilimia 16 na ongezeko la uagizaji wa mafuta kwa asilimia 8.
Amesema kuwa katika Sekta ya umeme uwekezaji umeongezeka katika uzalishaji, usafirishaji na usambazaji, upotevu wa umeme unazidi kupungua na wateja wa umeme wameongezeka kutoka milioni 3.8 mwaka 2021/22 hadi milioni 4.4 mwaka 2022/2023.
Baadhi ya changamoto zilizoainishwa kwenye taarifa katika sekta ya umeme ni uchakavu wa miundombinu ambao unaendelea kufanyiwa kazi na uwekezaji endelevu kwenye sekta.