Thursday, June 9, 2016

RC ATAKA MKATABA WA UWEKEZAJI KUPITIWA UPYA

Na John Gagarini, Mafia
MKUU wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo ametaka kupitiwa upya mkataba wa kuuziwa mwekezaji eneo la Magofu ya Chole wilaya ya Mafia mkoani Pwani ambapo kampuni ya Chole Mjini Conservation and Development Ltd imemilikishwa ambapo eneo hilo kuna gereza walilokuwa wanafungwa watumwa enzi za ukoloni wakati wa Utawala wa Wajerumani.
Aidha ameunda tume ya kufuatilia undani wa mkataba huo na amezuia marekebisho yaliyokuwa yanafanywa na kampuni hiyo kwa kipindi cha mwezi mmoja hadi pale ufumbuzi wa kujua namna mkataba huo ulivyoingiwa baina ya Kijiji cha Chole na mwekezaji huyo kama umezingatia taratibu.
Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Chole Mjini kata ya Jibondo kwenye mkutano wa hadhara Ndikilo alisema kuwa mkoa hauna nia mbaya na mwekezaji huyo ambaye amepewa hati miliki ya eneo hilo kwa kipindi cha miaka 33.
Ndikilo alisema kuwa eneo hilo ambalo lina kumbukumbu mbalimbali ambalo liko jirani na Bahari ya Hindi lilikuwa likitumika kwa ajili ya shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na soko la Watumwa pamoja na gereza lina ukubwa wa hekta 3.7 ambapo eneo hilo liko chini ya Wizara ya maliasili na Utalii Idara ya Malikale.
“Mkataba huo ambao ulisainiwa mwaka 2007 shamba namba 2031 baina ya mwekezaji  Dk Jean de Villiers na Kijiji hicho ambapo mwenyekiti wa Kijiji hicho Maburuki Sadiki alisaini kwa niaba ya Kijiji na kushuhudiwa na mkuu wa wilaya wakati ule Manzie Mangochi pasipo kuishirikisha Halmashauri ya wilaya ambayo haipati mapato yoyote kutokana na uwekezaji huo licha ya kutoa huduma za kijamii kwa wakazi wa Kijiji cha Chole” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa kutokana na hali hiyo amemtaka mwekezaji huyo kusimamisha ukarabati na kuunda tume ya kufanya uchunguzi na itatoa majibu baada ya mwezi mmoja ili kujiridhisha na kumilikishwa eneo hilo mtu binafsi eneo la serikali la kihistoria na kujengwa hoteli ya kitalii kwa kukarabati jengo la zamani.
Alibainisha kuwa Wizara ya Maliasili na Utalii ilituma barua ambayo iliyosainiwa na John Kimaro kwa niaba ya katibu mkuu kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia kuhirikiana na mwekezaji na kusema kuwa sheria ya Mambo ya Kale ya mwaka 1964 na marekebisho yake ya mwaka 1979 na sera ya Malikale ya mwaka 2008 inasema Malikale au Magofu yanaweza kumilikiwa na mtu binafs, taasisi na serikali.
Barua hiyo inaendelea kusema kuwa jukumu la serikali (Idara ya Mambo ya Kale) ni kuhakikisha kuwa mmiliki hatabomoa au kufanya chochote katika magofu hayo kinyume cha sheria.
Akitoa maelezo juu ya umiliki wake mkurugenzi wa Chole Mjini Conservation and Development Company Ltd Anne De Villiers amesema kuwa kampuni hiyo iliingia Mafia na kukuta hali ya majengo hayo ya kale yakiwa kwenye hali mbaya ndipo walianza mchakato wa kuyakarabati.
Dk Villiers alisema kuwa lengo la kuchukua eneo hilo ni kuhakikisha uasili wa mahali hapo haupotei kwa kuyafanyia ukarabati magofu hayo ambapo moja lilibaki ukuta mmoja na kutumia fedha nyingi kwa ajili ya ukarabati huo.
Naye mkuu wa wilaya ya Mafia Dk Nasoro Hamid alisema kuwa serikali haishirikishwi jambo lolote wala haijui ni watalii wangapi wanaoingia hapo wala mapato yanayopatikana kwenye eneo hilo.
Dk Hamid amesema kuwa Kijiji cha Chole ndicho kiliingia mkataba na mwekezaji huyo ambapo hugawana asilimia kutokana na watalii wanaoingia kwenye eneo hilo la makumbusho lakini tatizo haijulikani kinachopatikana hapo ni kiasi gani katika mgawanyo huo wa mapato.
Awali baadhi ya wanakijiji wakizungumzia suala hilo wakiongozwa na Ally Sikubali na Hemed Ally walisema kuwa moja ya changamoto iliyokuwepo ni mkataba Kiswahili unasema kuwa endapo kutakuwa na kutoeleweka mkataba wa Kiingereza ndiyo utakaotumika.
Waliomba mkataba huo uangaliwe upya na kufanya marekebisho ili kila upande unufaike kwani kwa sasa inaonekana kuwa pande nyingine hazinufaiki na mkataba huo.     
Mwisho.
   

 
   


WATAKA TAARIFA KUHUSU ENEO LA UWEKEZAJI BAADA YA MRADI WA MIWA KUFUTWA

Na John Gagarini, Bagamoyo
HALMASHAURI ya Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani imetakiwa kutoa taarifa rasmi kwenye vijiji vilivyokuwa kwenye mradi wa kilimo cha miwa chini ya kampuni ya Eco Energy uliosimamishwa na serikali ili eneo hilo lisije kuchukuliwa na mtu mwingine ili hali wananchi hao hawajalipwa fidia.
Mradi huo ulisimamishwa kupitia majibu ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa anajibu swali la kiongozi wa kambi ya upinzani Bungeni Freeman Mbowe aliyetaka kujua ni kwanini serikali imeshindwa kuweka jitihada za makusudi ili mradi huo ukamilike ambao ulibainika kuwa ungetumia maji mengi ya Mto Wami na kuathiri usatawi wa wanyama kwenye Mbuga ya Saadani.
Akizungumza na waandishi wa Habari mjini Bagamoyo katibu wa kamati ya ardhi ya Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya Mkombozi Bakari Salum alisema kuwa     kwa kuwa kauli ya Waziri Mkuu ni agizo ni vema Halmashauri ingetoa tangazo rasmi kwa wananchi husika.
“Kwa kuwa wakati anakuja mwekezaji kuchukua maeneo ya wananchi kwa ajili ya mradi huo kulikuwa na taarifa rasmi na wananchi walitoa maeneo yao kwa ajili ya kilimo hicho cha miwa ambacho baadaye kungejengwa kiwanda kwa ajili ya kuzalisha sukari hivyo baada ya kushindikana wangewajulisha wananchi,” alisema Salum
Kwa upande wake mjumbe wa kamati hiyo Jackson Mkango alisema kuwa eneo ambalo lilichukuliwa na mwekezaji ni hekari zaidi ya hekta 22,000 wananchi hao hawajalipwa fidia yoyote licha ya kuwa tathmini kufanyika mwaka 2011 hadi leo hawajalipwa.
Mkango alisema kuwa sheria inasema kuwa tathmini ikifanyika walengwa wanapaswa kulipwa ndani ya kipindi cha miezi sita lakini sasa imepita miaka mitano sasa.
“Tunaiomba Halmashauri kutoa tamko juu ya ardhi hiyo ya wananchi ambayo toka imechukuliwa wananchi hawakufanya chochote licha ya kuwa eneo hilo walikuwa wakitegemea kwa ajili ya kilimo na hawajui hatma yao kwani walitegemea wangelipwa fidia,” alisema Mkango.
Vijiji vilivyokuwa kwenye mpango huo ni Razaba, Matipwili, Kitame, Fukayosi, Makaani na Gongo ambapo kuna jumla ya wananchi zaidi ya 700 ambao walikuwa wakiishi kwenye maeneo hayo yaliyoingizwa kwenye mradi huo ambao ulikuwa na lengo la kukabiliana na upungufu wa sukari hapa nchini.

Mwisho.

WAWEKEZAJI WATAKIWA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUDUMISHA AMANI YA NCHI

Na John Gagarini, Mafia
MKUU wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo amewataka wawekezaji kwenye Visiwa vilivyopo Wilayani Mafia kushirikiana na serikali ili kudhibiti usalama wa nchi kukabiliana na wageni wasio waaminifu ambao wanaoweza kuvitumia visiwa hivyo kuhatarisha amani ya nchi.
Aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa ilipotembelea Kisiwa cha Shungimbili kwenye Hoteli ya Thanda ambayo inamilikiwa na raia wa kigeni na kusema kuwa kuna haja ya kuwa na kituo cha kufuatilia wageni wanaoingia na kutoka.
Ndikilo alisema kuwa kutokana na hali ya sasa kuwa mbaya kiusalama kutokana na matukio ya mauaji ya kutisha ambayo yanatokea hapa nchini ni vema ulinzi ukaimarishwa.
“Kuna haja ya kuwa na ushirikiano na baina ya wawekezaji na serfikali ili kukabiliana na wahalifu ambao wanaweza kutumia visiwa kujiingiza hapa nchini na kufanya uhalifu ikiwa ni pamoja na mauaji,” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa dunia ya sasa imebadilika na baadhi ya watu wamekuwa wakitumia njia ya Bahari kupitisha wahamiaji haramu, dawa za kulevya pamoja na uingizwaji wa silaha.
“Serikali haina nia mbaya ya kutaka kujua mambo yanayofanywa na wawekezaji kwa kujua wageni wanaoingia na kutoka na wameleta nini wanatoka na nini na hapa kutakuwa na kituo cha ukaguzi ambacho kitakuwa na polisi kwa ajili ya kulinda eneo la Kisiwa kwani wageni watakuwa wanafika kwa wingi,” alisema Ndikilo
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa Thanda Island Tanzania Ltd Oscar Pucci alisema kuwa hana tatizo na ushirikiano na serikali kwani anashirikiana vizuri na Halmashauri.
Pucci alisema kuwa wamekuwa wakisaidia shughuli za maendeleo kama kuchangia kwenye Hospitali ya wilaya na hata wavuvi wanaovua jirani na hoteli yao.

Mwisho.

TCRA YATOA MAFUNZO KUHUSU KUFUTWA SIMU FEKI

Na John Gagarini, Kibaha
IMEELEZWA Kuwa mawasiliano endapo yatatumika vizuri yana nafasi kubwa ya kuleta maendeleo ikiwa ni pamoja na kuvutia uwekezaji hapa nchini na kusababisha wananchi kutambua fursa za maendeleo zilizopo.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo wakatia akifungua mafunzo ya siku moja ya wadau wa maweasiliano yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) juu ya zoezi la uzimaji simu bandia linalotarajiwa kufanyika katikati ya mwezi huu.
Ndikilo alisema kuwa makampuni na mashirika kuanzia yale ya nje na ndani ya nchi yameweza kuongeza uwekezaji kwenye sekta mbalimbali kupitia mawasiliano yakiwemo ya  Mitandao ya Kijamii ,Simu, Redio, Televisheni na Magazeti.
“Mawasiliano ni chombo cha maendeleo endapo kinatumika vizuri na tumeona faida ya mawasiliano hasa yale ya intaneti ambapo wananchi wameweza kujua fursa mbalimbali za kufanya biashara za ndani na nje nchi nah ii yote imetokana na kuboreshwa suala la mawasiliano,” alisema Ndikilo.
Alisema kupitia mitandao kasi ya maendeleo imekuwa kubwa kup[itia mitandao kwa wale waliotumia vizuri ila kwa wale wanaotumia vibaya imekuwa ni kero kwani baadhi wameitumia kwa kutoa lugha chafu, wizi, utapeli na wizi kwa njia ya mtandao.
“Faida ni nyingi ikilinganishwa na hasara na katika uboreshaji wa kuondoa simu bandia itasaidia kukabiliana na wizi, matumizi mabaya kama vile kashfa na vitendo vibaya vilivyokuwa vinatumika kupitia mitandao kwani hata wale wezi wa kukwapua simu mwisho wao umefika,” alisema Ndikilo.
Kwa upande wake mwakilishi wa mkurugenzi wa TCRA Isaac Mruma alisema kuwa wameamua kutoa elimu hiyo kwa wananchi kabla ya kufikia hatua ya kuzima simu bandia ili wawe wanajua na namna ya kugundua simu hizo ambazo zitasitishwa matumizi yake ifikapo Juni 16 mwaka huu.
Mruma alisema kuwa wametoa elimu hiyo kwa makundi mbalimbali yakiwemo ya mafundi simu, wauzaji wa simu, maofisa wa kamati za ulinzi na usalama, waandishi na wananchi wa kawaida kwenye kanda ambapo kanda ya Mashariki ni ya mwisho ikiwa na mikoa ya Lindi, Pwani, Mtwara, Dar es Salaam na Morogoro.
Naye meneja mradi Injinia Imelda Salum alisema kuwa mbali ya kuondolewa bidhaa bandia za mawasiliano pia zoezi hilo litaambatana na rejesta ya utambulisho wa watumiaji wa wa vifaa vya simu ili kuboresha huduma za mawasiliano.
Salum alisema kuwa kwa mafundi wa simu wanapaswa kutozirekebisha simu hizo ili kuwaaminisha kuwa simu fulani ni aina fulani kwani kufanya hivyo ni kosa la jinai ambapo mhusika anaweza kuchukuliwa hatua ya kisheria.
Mwisho.   
  



Sunday, June 5, 2016

JUMUIYA YA WAZAZI YASISITIZA UBORA WA ELIMU CHUO CHA KILIMO NA MIFUGO

Na John Gagarini, Chalinze
JUMUIYA ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Bagamoyo mkoani Pwani kimesema kuwa kitashirikiana na uongozi wa Chuo Cha Kilimo na Mifugo cha Kaole ili kuhakikisha elimu inayotolewa ina kuwa na manufaa kwa nchi.
Hayo yalisemwa Lugoba wilayani humo na mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Abdul Sharifu wakati wa baraza la Wazazi na kusema kusema kuwa chuo hicho ambacho kinamilikiwa na jumuiya kitaboreshwa masomo yanayotolewa chuoni hapo ili wahitimu wake wabadilishe sekta hiyo na kuleta faida kwa wafugaji na wakulima nchini.
Sharifu alisema kuwa chuo hicho kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo watahakikisha wanaziondoa kwa kushirikiana na makao makuu ya Jumiya hiyo ili kiweze kutoa elimu bora ambayo itasaidia kuboresha ufugaji na kuwa wa kisasa na wenye tija.
“Chuo kinakabiliwa na changamoto lakini tutazikabili kadiri ya uwezo wetu ili tuboreshe elimu inayotolewa chuoni hapo hasa tukizingatia ufugaji ni moja ya chanzo kikubwa cha pato la Taifa na kilimo kwa ajili ya chakula,” alisema Sharifu.
Alisema kuwa chuo hicho kinajijenga upya baada ya awali kubadilishwa na kuwa shule ya sekondari lakini sasa kimerudishwa mikononi mwao hivyo watahakikisha kinakuwa moja ya vyuo bora hapa nchini kwa kutoa elimu inayokubalika.
“Tunaomba wadau mbalimbali kujitokeza kukisaidia chuo chetu ili kiweze kuboresha wasomi ambao watakubalika kule watakakopangiwa hasa ikizingatiwa wahitimu hao watakuwa ni maofisa ugani wataboresha kilimo na ufugaji,” alisema Sharifu.
Kwa upande wake mjumbe wa baraza la jumuiya hiyo Yahaya Msonde alisema kuwa lengo lao ni kutoa elimu itakayokidhi mahitaji ya wakulima na wafugaji ili waboreshe shughuli zao.
Msonde alisema kuwa kilimo ni uti wa mgongo hivyo lazima kiwekewe mikakati ya kuinuliwa kwa kuzalisha wataalamu wenye uweze na mbinu za kisasa na kwa wafugaji nao waweze kukabiliana na ufugaji usiokuwa na tija.

Mwisho.   

WATAKA TAARIFA RASMI MRADI WA MIWA KUFUTWA

Na John Gagarini, Bagamoyo
HALMASHAURI ya Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani imetakiwa kutoa taarifa rasmi kwenye vijiji vilivyokuwa kwenye mradi wa kilimo cha miwa chini ya kampuni ya Eco Energy uliosimamishwa na serikali ili eneo hilo lisije kuchukuliwa na mtu mwingine ili hali wananchi hao hawajalipwa fidia.
Mradi huo ulisimamishwa kupitia majibu ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa anajibu swali la kiongozi wa kambi ya upinzani Bungeni Freeman Mbowe aliyetaka kujua ni kwanini serikali imeshindwa kuweka jitihada za makusudi ili mradi huo ukamilike ambao ulibainika kuwa ungetumia maji mengi ya Mto Wami na kuathiri usatawi wa wanyama kwenye Mbuga ya Saadani.
Akizungumza na waandishi wa Habari mjini Bagamoyo katibu wa kamati ya ardhi ya Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya Mkombozi Bakari Salum alisema kuwa     kwa kuwa kauli ya Waziri Mkuu ni agizo ni vema Halmashauri ingetoa tangazo rasmi kwa wananchi husika.
“Kwa kuwa wakati anakuja mwekezaji kuchukua maeneo ya wananchi kwa ajili ya mradi huo kulikuwa na taarifa rasmi na wananchi walitoa maeneo yao kwa ajili ya kilimo hicho cha miwa ambacho baadaye kungejengwa kiwanda kwa ajili ya kuzalisha sukari hivyo baada ya kushindikana wangewajulisha wananchi,” alisema Salum
Kwa upande wake mjumbe wa kamati hiyo Jackson Mkango alisema kuwa eneo ambalo lilichukuliwa na mwekezaji ni hekari zaidi ya hekta 22,000 wananchi hao hawajalipwa fidia yoyote licha ya kuwa tathmini kufanyika mwaka 2011 hadi leo hawajalipwa.
Mkango alisema kuwa sheria inasema kuwa tathmini ikifanyika walengwa wanapaswa kulipwa ndani ya kipindi cha miezi sita lakini sasa imepita miaka mitano sasa.
“Tunaiomba Halmashauri kutoa tamko juu ya ardhi hiyo ya wananchi ambayo toka imechukuliwa wananchi hawakufanya chochote licha ya kuwa eneo hilo walikuwa wakitegemea kwa ajili ya kilimo na hawajui hatma yao kwani walitegemea wangelipwa fidia,” alisema Mkango.
Vijiji vilivyokuwa kwenye mpango huo ni Razaba, Matipwili, Kitame, Fukayosi, Makaani na Gongo ambapo kuna jumla ya wananchi zaidi ya 700 ambao walikuwa wakiishi kwenye maeneo hayo yaliyoingizwa kwenye mradi huo ambao ulikuwa na lengo la kukabiliana na upungufu wa sukari hapa nchini.

Mwisho.

WAWEKEZAJI WADHIBITI USALAMA WA NCHI

Na John Gagarini, Mafia
MKUU wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo amewataka wawekezaji kwenye Visiwa vilivyopo Wilayani Mafia kushirikiana na serikali ili kudhibiti usalama wa nchi kukabiliana na wageni wasio waaminifu ambao wanaoweza kuvitumia visiwa hivyo kuhatarisha amani ya nchi.
Aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa ilipotembelea Kisiwa cha Shungimbili kwenye Hoteli ya Thanda ambayo inamilikiwa na raia wa kigeni na kusema kuwa kuna haja ya kuwa na kituo cha kufuatilia wageni wanaoingia na kutoka.
Ndikilo alisema kuwa kutokana na hali ya sasa kuwa mbaya kiusalama kutokana na matukio ya mauaji ya kutisha ambayo yanatokea hapa nchini ni vema ulinzi ukaimarishwa.
“Kuna haja ya kuwa na ushirikiano na baina ya wawekezaji na serikali ili kukabiliana na wahalifu ambao wanaweza kutumia visiwa kujiingiza hapa nchini na kufanya uhalifu ikiwa ni pamoja na mauaji,” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa dunia ya sasa imebadilika na baadhi ya watu wamekuwa wakitumia njia ya Bahari kupitisha wahamiaji haramu, dawa za kulevya pamoja na uingizwaji wa silaha.
“Serikali haina nia mbaya ya kutaka kujua mambo yanayofanywa na wawekezaji kwa kujua wageni wanaoingia na kutoka na wameleta nini wanatoka na nini na hapa kutakuwa na kituo cha ukaguzi ambacho kitakuwa na polisi kwa ajili ya kulinda eneo la Kisiwa kwani wageni watakuwa wanafika kwa wingi,” alisema Ndikilo
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa Thanda Island Tanzania Ltd Oscar Pucci alisema kuwa hana tatizo na ushirikiano na serikali kwani anashirikiana vizuri na Halmashauri.
Pucci alisema kuwa wamekuwa wakisaidia shughuli za maendeleo kama kuchangia kwenye Hospitali ya wilaya na hata wavuvi wanaovua jirani na hoteli yao.

Mwisho.