Saturday, August 9, 2014

DEREVA TEXI APOTEA MAZINGIRA YA KUTATANISHA ALIKODISHWA NA WATU



Na John Gagarini, Kibaha
DEREVA wa Texi wa Maili Moja Richard Ponera (36) mkazi wa Mwendapole wilayani Kibaha mkoani Pwani amepotea katika mazingira ya kutatanisha baada ya kukodishwa na watu wasiofahamika.
Ponera alikodishwa na watu wawili ambao hawakufahamika  Agosti 5 mwaka huu majira ya saa 2:30 usiku akiwa anaendesha gari lenye usajili na T 905 BHT aina ya Corolla nyeupe.
Akizungumza na mjini Kibaha kuhusina na tukio hilo katibu wa Umoja wa madereva Texi Kibaha Mjini (KITAGURO) Fadhil Kiroga alisema kuwa dereva huyo tangu alipoondoka siku hiyo hadi leo hakurudi na hakuna taarifa yoyote  iliyopatikana juu yake.
Kiroga alisema kuwa siku ya tukio hilo Ponera alionekana akipatana na watu hao kwa muda kidogo kama dakika 10 hivi kisha akaondoka na watu hao ambao walikuwa wawili.
“Baada ya mapatano licha ya kuwa madereva wengine hawakuweza kujua walichokuwa wakiongea na Ponera waliondoka na alipofika Mlandizi aliwasiliana na mwenzetu ambaye ni Salum Mbawala na kumwambia kuwa kwa sasa yuko Mlandizi,” alisema Kiroga.
Alisema kuwa baada ya hapo simu yake haikuweza kupatikana tena kwani baada ya kuona harudi wenzake walijaribu kumpigia lakini simu yake haikupatikana tena.
“Ponera hapa alikuwa hana muda mrefu tangu aanze kazi na alipata gari hilo ambalo alikuwa amekabidhiwa kama wiki mbili zilizopita na gari lenyewe halikuwa kwenye hali nzuri sana kusema labda ilikuwa ni kishawishi cha watu labda kutaka kuliiba gari hilo, hatujui kilichomtokea mwenzetu,” alisema Kiroga.
Aidha alisema kuwa wamefanya jitihada mbalimbali ambapo walikwenda polisi kutoa taarifa juu ya tukio hilo na kupewa namba KMM/RB/847/2014 pia walitoa taarifa kwenye vituo vya Mlandizi na Tumbi kisha kutembelea maeneo ya Yombo, Miswe na Mzenga bila ya mafanikio.
Kwa uapande wake mke wa dereva huyo Rosemary Urasa (31) alisema kuwa siku ya tukio hilo alikuja naye hadi Maili Moja yeye akenda sokoni kununua vitu vya nyumbani akamwacha stendi kwa ajili ya kuendelea na shughuli zake kama kawaida.
“Nakumbuka majira ya saa 5 asubuhi nilimpigia simu baada ya gari linguine ambalo liko hapa nyumbani lilikuwa linapiga honi lenyewe nikamwambia aje alizime lakini kwa bahati nzuri kuna mtu alifanikiwa kulizima nikamjulisha alikuwa njiani kuja lakini akarudia eneo linaloitwa Picha ya Ndege, toka hapo kila nikipiga simu simpati,” alisema Urasa.
Alibainisha kuwa mumewe ambaye wamezaa naye watoto wawili walihamia Kibaha baada ya kufanikiwa kujenga na kuzaa watoto wawili ambao ni Ruben (14) anayesoma kidato cha kwanza St Anne na Kontrada anayesoma darasa la sita shule ya Msingi Jitegemee.
Aidha alisema kuwa wakati mwingine mumewe hufanya kazi na kukesha hivyo siku hiyo usiku alijua kuwa atakesha lakini ilipofika asubuhi alishangaa kutokumwona kwani endapo anakuwa amekesha asubuhi ni lazima arudi lakini siku hiyo hakumwona ikambidi aje kwenye eneo analopaki lakini alipouliza wakasema tangu alivyoondoka jana hajaonekana tena.
Naye mmiliki wa gari hilo Athuman Kimia alisema kuwa siku hiyo ya tukio aliwasiliana na Ponera ambapo kulikuwa na tatizo la kulipia gari linapokuwa barabarani na kumpa 170,000 kwa ajili ya kulipia.
Kimia alisema kuwa baada ya kama saa moja alimpigia na kumwambia kila kitu kashalipia hivyo mambo mazuri na ndipo alipoendelea na shughuli kama kawaida.
“Tumekubaliana kila baada ya wiki awe ananipa malipo ya kazi lakini nilipigiwa simu kuambiwa kuwa Ponera aonekani na nilipojaribu kumpigia simu yake haipatikani sijui kilichomtokea ninini kwani yeye huwa ananipigia endapo kumetokea tatizo kwani sasa hivi ni wiki ya pili tangu nimkabidhi gari ,” alisema Kimia.
Mwisho.

Monday, August 4, 2014

WASOMI WATUMIE TAALUMA ZAO KULETA MAENDELEO

Na John Gagarini, Chalinze
WASOMI kwenye Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wametakiwa kutumia elimu yao kukabiliana na changamoto za kimaendeleo zilizopo jimboni humo.
Hayo yalisemwa na Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alipokuwa akizindua maktaba ya shule ya sekondari ya Chalinze iliyojengwa na na kampuni ya kutengeneza saruji ya Tanga Simenti huku taasisi ya Read International ikiwa imetoa msaada wa vitabu.
Ridhiwani alisema kuwa jimbo hilo lina changamoto nyingi ambazo nyingine zitatatuliwa na wasomi wanaotoka eneo hilo na wengine kwa lengo la kuleta maendeleo.
“Elimu mnayosoma iwe chachu na ya maana kwa kuleta maendeleo ya jimbo hili kwani wazazi wenu wanajitolea kuwasomesha ili baadaye na nyie muweze kuwa msaada kwa jamii na  elimu ya sasa inaendana na vitendo ambavyo ndiyo tafsiri  kwa vile wanavyokuwa wamejifunza wanafunzi na si kuwa wasomi jina ambao hawana msaada kwa jamii inayowazunguka,” alisema Ridhiwani.
Alibainisha kuwa maktaba ambayo tumeizindua leo iwe chanzo cha nyie kujifunza kwa bidii kwa kujisomea baada ya walimu kuwafundisha kwani Watanzania kwa sasa bila ya elimu ni kazi bure na hataweza kufanya jambo lololote la kimaendeleo.
Kwa upande wake kaimu meneja biashra wa kampuni ya Tanga Simenti Yasin Hussein alisema kuwa wamejenga jengo hilo kwa lengo la kuhakikisha shule hiyo inakabiliana na tatizo la ukosefu wa maktaba ambapo hutoa asilimia moja ya faida ya mapato wanayopata kwa kurudisha kwa jamii kwa kusaidia masuala mbalimbali yakiwemo ya mazingira, elimu na afya.
“Tumetumia kiasi cha shilingi milioni 47 kwa ajili ya ujenzi huu ambapo mpango ni kujenga maktaba kwenye shule za Mingoyo Lindi na Kinyerezi Jijini Dar es Salaam na watatumia zaidi ya shilingi milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa maabara na maktaba kwenye mikoa mbalimbali nchini,” alisema Hussein.
Naye mwalimu mkuu wa shule hiyo Emanuel Kahabi alisema kuwa ufunguzi wa maktaba hiyo utasaidia kukabiliana na changamoto ya maktaba ailiyokuwa inakabili shule yao ambayo ina wanafunzi 879.
Mwisho.

Picha no 1397 Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani akiongea wakati wa ufunguzi wa makataba ya shule ya sekondari ya Chalinze kushoto ni mwenyekiti wa bodi ya shule Mbwana Madeni na kulia ni mkuu wa polisi wilaya ya Chalinze Janeth Magori.

picha no 1389 Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akiweka alama kwenye ukuta kama alama ya kumbukumbu baada ya kuizindua makta ya shule ya sekondari ya Chalinze.

picha no 1369 Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya Chalinze wakimsikiliza Mbunge wa Chalinze Riidhiwani Kikwete maara baada ya kuzindua maktaba ya shule hiyo.

picha no 1391 Mwenyekiti wa bodi ya shule ya sekondari ya Chalinze kushoto Mbwana Madeni akiongea katikakati ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete na katikati mkuu wa polisi kanda maalumu wilaya ya Chalinze Janeth Magori.

picha no 1371 wanafunzi wa shule ya sekondari ya Chalinze wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete wakati wa uzinduzi wa maktaba ya shule.

 

Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani akiongea wakati wa ufunguzi wa makataba ya shule ya sekondari ya Chalinze kushoto ni mwenyekiti wa bodi ya shule Mbwana Madeni na kulia ni mkuu wa polisi wilaya ya Chalinze Janeth Magori.
 


Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akiweka alama kwenye ukuta kama alama ya kumbukumbu baada ya kuizindua makta ya shule ya sekondari ya Chalinze.
 

 

Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya Chalinze wakimsikiliza Mbunge wa Chalinze Riidhiwani Kikwete maara baada ya kuzindua maktaba ya shule hiyo.



Mwenyekiti wa bodi ya shule ya sekondari ya Chalinze kushoto Mbwana Madeni akiongea katikakati ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete na katikati mkuu wa polisi kanda maalumu wilaya ya Chalinze Janeth Magori.
 

 

picha no 1371 wanafunzi wa shule ya sekondari ya Chalinze wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete wakati wa uzinduzi wa maktaba ya shule.

Thursday, July 31, 2014

KAMATI ZA MADIWANI SARAKASI TUPU NA DIWANI CHADEMA AONDOLEWA KIKAONI

 Baadhi ya madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani wakiwa kwenye kikao cha baraza hilo kilichofanyika leo mjini Kibaha
 Na John Gagarini, Kibaha
ZOEZI la kuchagua kamati mbalimbali za baraza la madiwani wa
halmashauri ya Mji wa Kibaha wilayani humo mkoani Pwani limekumbwa na
mtafaruku baada ya baadhi ya madiwani kupinga taratibu za kuwachagua
viongozi na wajumbe wa kamati hizo.
Mtafaruku huo ulitokea baada ya baadhi ya madiwani kulalamika kuwa
wengi wao walipewa kamati nzuri kwa upendeleo na kuwaweka madiwani
wengine kwenye kamati ambazo si nzuri.
Sakata hilo lilitokea jana wakati wa kikao cha baraza la madiwani wa
Halmashauri ya Mji huo lililofanyika mjini Kibaha ambapo madiwani hao
walidai kulikuwa na upendeleo wakati wa kuchagua wajumbe na wenyeviti
wa kamati hizo.
Walisema kuwa uchaguzi huo uliambatana na upendeleo mkubwa ambapo
baadhi ya madiwani wamekuwa wakichaguliwa kwenye moja hasa ile ya
Mipango Miji na Mazingira ambapo wako kwenye kamati hiyo kwa vipindi
vinne mfululizo ambapo wao walitaka wabadilishwe na kuwekwa kwenye
kamati zingine.
“Baadhi ya madiwani wamechaguliwa kutokana na urafiki baadhi
tunateuliwa kwenye kamati ambazo si nzuri inasikitisha sana lazima
kuwe na mabadiliko kama vipi sisi wengine tutajitoa kwenye kamati na
kubaki na udiwani pekee,” walisema madiwani hao.
Hata hivyo hali ilikuwa mbaya zaidi ambapo baadhi walidai kuwa wengine
walichaguliwa kwenye kamati hiyo ya mipango miji kama kulipa fadhila
baada ya kumpa mmoja wa viongozi kwenye uchaguzi wa chama.
“Watu walihongwa fedha ili wamchague mtu ushahidi upo sisi hatukubali
tunaona kuwa baada ya uchaguzi ule leo jana wanalipana fedhila
hatutaweza kufanikiwa tunachotakiwa ni kuwahudumia wananchi,” walisema
madiwani hao.
Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri Addhu Mkomambo alisema kuwa
uchaguzi huo haukuwa na upendeleo na kama kuna tatizo wanapaswa
kupeleka ofisini kwake na si kuunda vikundi.
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdala Mdimu alisema kuwa
amesikitishwa na madiwani hao kufikia hatua ya kusema mambo ambayo
hayakupaswa kusemwa hapo badala yake yangepelekwa kwenye chama kwa
hataua.
Mdimu alisema kuwa atakaa na madiwani hao ili kuzungumzia masuala hayo
ambayo yalionekana kumsononesha na kusema kuwa hali hiyo imemsikitisha
sana.
Mwisho.

 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Addhu Mkomambo kulia akihutubia kwenye kikao hicho kushoto ni mkurugenzi wa halmashuri hiyo Jenifa Omolo
Na John Gagarini, Kibaha
DIWANI wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kata ya  Tumbi
Mbena  Makala jana aliondolewa kwenye kikao cha madiwani wa baraza la
madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha wilayani Kibaha mkoani Pwani
kutokana na utovu wa nidhamu.
Kikao hicho cha kawaida cha robo tatu ya mwaka ambacho kilifanyika
jana ilimbidi mwenyekiti wa Halmashauri Addhu Mkomambo kumtoa nje ya
ukumbi baada ya kumtaka diwani huyo kukaa chini baada ya hoja yake
kutakiwa kupatiwa ufumbuzi wakati mwingine na si kwenye kaikao hicho.
Diwani huyo alitoa hoja ambapo alisema kuwa wananchi wake walikuwa
wakihitaji eneo kwa ajili ya kufanya soko huku eneo hilo likitakiwa
kufanyiwa jambo jingine na si soko na watafute sehemu nyingine na hapo
patawekwa kitega uchumi kingine.
“Wananchi walikubaliana eneo hilo la (Community Centre) lijengwe soko
kutokana na kata hiyo kutokuwa na soko ambapo wananchi mbali ya
kuliandaa pia walichanga fedha kwa ajili ya kulirekebisha kwa ajili ya
shughuli hiyo,” alisema Makala.
Makala alisema kuwa wananchi walishakubaliana juu ya eneo hilo
kufanywa ujenzi wa soko lakini cha kushangaza Halmashauri inakataa na
kuwataka watafute sehemu nyingine.
Akijibu hoja hiyo Mwenyekiti Mkomambo alisema kuwa eneo hilo haliwezi
kuwekwa soko na badala yake kiwekwe kitega uchumi kingine hivyo
watafute eneo mbadala kwa ajili ya shughuli hiyo ya soko na nyumba
zilizopo hapo zibomolewe.
Kutokana na majibu hayo ndipo diwani huyo alipoamka na kusema kuwa
miezi michache iliyopita Mwenyekiti alikuwa kwenye ziara na kusema
kuwa soko litajengwa iweje leo anakana kauli yake hivyo hawezi
kukubaliana na maelezo hayo.
Mwenyekiti huyo baada ya maelezo kutoafikiwa na diwani huyo alimwambia
kuwa suala hilo alipeleke kwenye kamati ya mipango miji na mazingira
ili lipatiwe majibu na majibu hayataweza kutolewa hapo.
“Ni kweli nilikuja kwenye kata yako lakini masuala haya itabidi
uyapeleke kwenye kamati ya mipango miji naamini utapata majibu pia
sasa imepita miezi saba tangu nilipotembelea kwanini hukuleta hoja
hizo mapema leo ndiyo unataka majibu hapa ili upate majibu ya uhakika
fuata hizo taratibu nilizokuambia,” alisema Mkomambo.
Kutokana na majibu hayo diwani huyo aliendelea kutoa maneno na
kutakiwa akae lakini alikataa na ndipo mwenyekiti alipomwamuru atoke
nje hadi pale atakapojirekebisha jambo ambalo lilimfanya diwani huyo
atoke nje na kuondoka kabisa eneo la viwanja vya halmashauri.
Mwisho.

Wednesday, July 30, 2014

COPA COCA COLA KUCHUJANA AGOSTI 16



Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA cha soka Kibaha Vijijini wilayani Kibaha mkoani Pwani (KIVIFA) kinatarajia kuchagua timu ya vijana wenye umri wa miaka 15 ya Copa Coca Cola Agosti 16 mwaka huu.
Kwa mujibu wa mwenyekiti wa wa mashinadano wa (KIVIFA) Mohamed Msamati amesema kuwa tayari wameshakaa na vilabu 11ili kuwaelekeza namna ya kufanya mashindano hayo.
Msamati amesema mashindano hayo yatafanyika ili kutekeleza agizo la Chama Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA), kila wilaya kuhakikisha inapata timu ya vijana kwa ajili ya mashindano ya mkoa.
Amesema kuwa kuwa kwa sasa wako kwenye maandalizi ya michuano hiyo ambayo itashirikisha timu zote za Kibaha Vijijini na kuzitaka timu kujiandaa na mashindano.
Aidha amesema kuwa Kila timu inapaswa kuandaa wachezaji wake kwa kufanya mazoezi ya kutosha ili kuhakikisha wilaya inapata wachezaji wazuri watakaowakilisha kwenye mashindano ya mkoa.
Amebainisha kuwa watahakikisha mashindano hayo yanatumia wachezaji ambao wana umri unaopaswa na kuepukana na kutumia wachezaji ambao wana umri mkubwa maarufu kama vijeba.
Kwa upande wake mwenyekiti wa KIVIFA Meja Mstaafu Deus Makwaya amesema wamejipanga vizuri katika kuhakikisha mashindano hayo yanafanikiwa na kupata timu bora.
Meja Makwaya amesema kuwa tayari wameteua viongozi kwa ajili ya kusimamia mashindano hayo ya Copa Cola Cola ambao ni Dk Musa Sama ambaye ni mwenyekiti, Juma Likali katibu na God Mwafulilwa meneja.
Amewataja wajumbe kuwa ni Hija Matitu, Juma Kisebengo, Said Kidile huku walimu wakiwa ni Said Shaban na Mtoso ambao ni timu ya ushindi ya kuandaa vijana hao.
Mwisho.

Monday, July 28, 2014

AMWUA MKEWE KWA WIVU WA MAPENZI



KIJANA aliyetambuliwa kwa jina la Omary Molel mkazi wa Kijiji cha Mwanabwito kata ya Ruvu wilayani Kibaha mkoani Pwani anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka (25) anatuhumiwa kumwua mchumba wake Sina Hamis (21) kwa kumchoma kisu kutokana na wivu wa mapenzi.

Mtuhumiwa huyo ambaye alikuwa akifanya kazi ya kusimamia shamba la mtu pamoja na kufanya kazi ya bodaboda anatuhumiwa kufanya mauaji hayo nyumbani kwa wakwe zake baada ya kuona kuwa mkewe amegoma kwenda kwake kutokana na ugomvi uliokuwepo baina yao.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu mwenyekiti wa Kijiji cha Boko Mnemela Hassan Mohamed amesema kuwa tukio hilo limetokea Julai 27 majira ya saa mbili asubuhi.

Mohamed amesema kuwa siku moja kabla ya tukio hilo Julai 26 mtuhumiwa huyo akiwa na amesindikizwa na mtu mmoja ambaye jina lake bado halijapatikana walikuwa na kikao cha kusuluhishwa baada ya kuhitilafiana  na kikao hicho kilifanyika nyumbani kwa wazazi wa marehemu.

Amesema kuwa Kwa mujibu wa watu waliohudhuria kikao hicho wamesema kuwa kikao hicho kilifanyika kuanzia majira ya saa 2 usiku hadi saa 5 usiku ambapo hata hivyo mwafaka haukuweza kufikiwa kwani marehemu alikataa kwenda kwa mume wake.

Aidha amessema kuwa siku iliyofuata watu waliokuwa wakihusika kusuluhisha waliondoka na yeye pamoja na mtu aliyeambatana naye waliondoka lakini ghafla alirudi akidai kuwa anafuata betri ya simu aliyoisahau nyumbani kwao na marehemu.

Alimkuta mkewe akipepeta mchele jikoni na kuanza kumbembeleza lakini inaonekana aligoma kabisa kurudi kwa mumewe hali ambayo ili mkasirisha mumewe na kuanza kumchoma kwa kutumia kisu huko jikoni kisha wakatoana nje huku marehemu akipiga kelele.

Ameongeza kuwa Mtuhumiwa alimchoma marehemu kwenye ziwa la upande wa kulia na kwenye uti wa mgongo karibu na bega la upande wa kushoto na alimchoma kisu mbele ya bibi yake mama yake wa kufikia na mdogo wake ambao walipiga kelele na kushindwa kumsaidia ambapo mtuhumiwa huyo alikimbia maporini.

Mwenyekiti huyo alipoulizwa juu ya chanzo cha mauaji hayo amesema kuwa kwa mujibu wa watu waliokuwa wakijua ugomvi wao walisema kuwa mtuhumiwa alikerwa na tabia ya mkewe kurudishiwa zaidi chenchi anapokwenda kwenye duka lililopo kijijini hapo.

Ameongeza kuwa Marehemu alikuwa akimjulisha mumewe juu ya hali hiyo ambapo inasemekana aligoma kurudi kutokana na kuambulia vipigo na kutishiwa kuuwawa na mwanaume huyo na kupelekea kufanyika kikao cha usuluhishi na muuza duka kifanyika ili kupata mwafaka lakini ikashindikana na kutokea mauaji hayo ya kusikitisha.

Kwa upande wa kamanda wa Polisi mkoani Pwani Kamishna Msaidizi Mwanadamizi wa Polisi (SACP) Ulrich Matei amekiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mtuhumiwa huyo anatafutwa ambapo jitihada hizo bado hazijazaa matunda.

 

  

Sunday, July 27, 2014

ATUHUMIWA KUMWUA MKEWE KWA KUMCHOMA KISU KUTOKANA NA WIVU WA KIMAPENZI



Na John Gagarini, Kibaha
KIJANA aliyetambuliwa kwa jina la Omary Iddi mkazi wa Kijiji cha Mwanabwito kata ya Ruvu wilayani Kibaha mkoani Pwani anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka (25) anatuhumiwa kumwua mkewe kwa kumchoma kisu kutokana na wivu wa mapenzi.
Mtuhumiwa huyo ambaye alikuwa akifanya ya kusimamia shamba la mtu pamoja na kufanya kazi ya bodaboda anatuhumiwa kufanya mauaji hayo nyumbani kwa wakwe zake baada ya kuona kuwa mkewe amegoma kwenda kwake kutokana na ugomvi uliokuwepo baina yao.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu mwenyekiti wa Kijiji cha Boko Mnemela Hassan Mohamed alisema kuwa tukio hilo limetokea Julai 27 majira ya saa mbili asubuhi.
Mohamed alisema kuwa siku moja kabla ya tukio hilo Julai 26 mtuhumiwa huyo akiwa na amesindikizwa na mtu mmoja ambaye jina lake bado halijapatikana walikuwa na kikao cha kusuluhishwa baada ya kuhitilafiana  na kikoa hicho kilifanyika nyumbani kwa wazazi wa marehemu.
“Kwa mujibu wa watu waliohudhuria kikao hicho walisema kuwa kikao hicho kilifanyika kuanzia majira ya saa 2 usiku hadi saa 5 usiku ambapo hata hivyo mwafaka haukuweza kufikiwa kwani marehemu alikataa kwenda kwa mume wake,” alisema Mohamed.
Alisema kuwa siku iliyofuata watu waliokuwa wakihusika kusuluhisha waliondoka na yeye pamoja na mtu aliyeambatana naye waliondoka lakini ghafla alirudi akidai kuwa anafuata betri ya simu aliyoisahau nyumbani kwao na marehemu.
“Alimkuta mkewe akipepeta mchele jikoni na kuanza kumbembeleza lakini inaonekana aligoma kabisa kurudi kwa mumewe hali ambayo ili mkasirisha mumewe na kuanza kumchoma kwa kutumia kisu huko jikoni kisha wakatoana nje huku marehemu akipiga kelele,” alisema Mohamed.
“Mtuhumiwa alimchoma marehemu kwenye ziwa la upande wa kulia na kwenye uti wa mgongo karibu na bega la upande wa kushoto na alimchoma kisu mbele ya bibi yake mama yake wa kufikia na mdogo wake ambao walipiga kelele na kushindwa kumsaidia ambapo mtuhumiwa huyo alikimbia maporini,” alisema Mohamed.
Mwenyekiti huyo alipoulizwa juu ya chanzo cha mauaji hayo alisema kuwa kwa mujibu wa watu waliokuwa wakijua ugomvi wao walisema kuwa mtuhumiwa alikerwa na tabia ya mkewe kurudishiwa zaidi chenchi anapokwenda kwenye duka lililopo kijijini hapo.
“Marehemu alikuwa akimjulisha mumewe juu ya hali hiyo ambapo inasemekana aligoma kurudi kutokana na kuambulia vipigo na kutishiwa kuuwawa na mwanaume huyo na kupelekea kufanyika kikao cha usuluhishi na muuza duka kifanyike ili kupata mwafaka lakini ikashindikana na kutokea mauaji hayo ya kusikitisha,” alisema Mohamed.
Jitihada za kumpata kamanda wa Polisi mkoani Pwani Kamishna Msaidizi Mwanadamizi wa Polisi Ulrch Matei hazikuweza kuzaa matunda ili aweze kuzungumzia tukio hilo.
Mwisho.