Wednesday, May 21, 2014

MAHIZA APINGA MFUKO WA WENYEVITI WA HALMASHAURI



Na John Gagarini, Kibaha
MKUU wa mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza amezuia bajeti ya fedha iliyokuwa inatengwa kwa ajili ya wenyeviti wa halmashauri za wilaya badala yake fedha hizo zitumike kwenye miradi ya maendeleo ya wananchi.
Fedha hizo ambazo zimekuwa zikitengwa kwenye bajeti za kila mwaka za halmashauri bado hazijaonyeshwa kuwa zinatengwa kwa kanuni gani tofauti na fedha nyingine ndani ya halmashauri.
Akizungumza na wakuu wa wilaya, wenyeviti wa halmashauri, maofisa mipango na waweka hazina wa halmashauri za mkoa huo Mahiza alisema kuwa fedha hizo ni nyingi kwani baadhi ya wenyeviti wamekuwa wakitengewa hadi milioni 11 kw akila bajeti.
Mahiza alifikia kutoa agizo hilo baada ya baadhi ya halmashauri kusema kuwa zimetenga fedha hizo kwa ajili ya wenyeviti wa halmashauri kwa ajili ya matumizi ambayo hayakuwekwa bayana.
“Natoa agizo kuwa mfuko huo wa fedha kwa ajili ya mwenyekiti uondolewe hadi mtakapotoa mwongozo wa mfuko kwani mifuko yote ikiwemo ile ya Jimbo ya Mbunge ipo kisheria na inatambulika je huu umewekwa kwa kufuata sheria ipi,” alisema Mahiza.
Alisema kuwa hana nia mbaya juu ya kuzuia mfuko huo lakini anachotaka ni mwongozo ambao unaelekeza kuwepo kwa fedha hizo ambapo wakurugenzi walishindwa kuonyesha ni sheria gani wanayoitumia kutenga fedha hizo.
“Hadi sasa hakuna anayejua fedha hizi zinatengwa kwa kufuata utaratibu au mwongozo upi hivyo naomba ofisa wa serikali za Mitaa anipatie mwongozo ili mfuko uo uendelee na kama hakuna mwongozo wowote basi fedha ziende kwenye miradi ya maendeleo,” alisema Mahiza.
Aidha alisema hata wakuu wa wilaya hawana fedha kama hizo ambapo wao fedha zao hazizidi zaidi ya milioni tano jambo ambalo liliwashitua watu wengi waliposikia kuhusu mfuko huo wa wenyeviti wa halmashauri.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
ILI kuleta ufanisi wa utendaji kazi kwa wauguzi mkoa wa Pwani utawapatia kiasi cha shilingi 1,000 kwa muuguzi atakayezailisha mama wajawazito kwa usalama.
Pia vituo vya afya na zahanati zinatakiwa kufanya kazi kwa saa 24 ili kuhakikisha wagonjwa wanapata matibabu kwa muda wote tofauti na ili sasa ambapo wahudumu wa afya wanafunga muda wa kazi saa 9:30.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na mkuu wa mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza wakati wa kikao cha kazi ambacho kiliambatana na uingiwaji wa mikataba baina ya wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri za mkoa huo juu ya utendaji kazi kwenye sekta ya afya na makusanyo kwenye bajeti ya mwaka 2014- 2015.
Mahiza alisema kuwa mpango wa kuwapa fedha wauguzi wanaowazalisha mama wajawazito salama ni kuwapa hamasa ili waweze kufanya vizuri katika kuwahudumia akinamama hao.
“Kwa kuwa tayari tumeshaingia mkataba na wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri kwa ajili ya kupunguza vifo vya mama wajawazito, watoto wachanga na watoto wenye umri chini ya miaka mitano lazima tuwape motisha watendaji wa sekta ya afya ili wafanye kazi kwa moyo,” alisema Mahiza.
Aidha Mahiza alisema kuwa kuanzia sasa vituo vya afya na zahanati vifanye kazi kwa saa 24 ili kuweza kufikia malengo ya kupunguza vifo hivyo pamoja na utoaji huduma kwa muda wote kwani ugonjwa hauna saa.



  

WAKAMATWA KWA TUHUMA ZA KULIMA BANGI HEKARI 2

 Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la Polisi mkoani Pwani linawashikilia wakazi wawili wa Kijiji
cha Mwetemo wilaya ya Bagamoyo mkoani humo kwa tuhuma za kulima shamba
la bangi hekari mbili kwenye shamba la mahindi.

Watuhumiwa hao walibainika baada ya askari wa jeshi hilo kufanya doria
ya kusaka makosa mbalimbali wilyani humo ili kukamata wahalifu.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo jana mjini Kibaha kamanda wa
polisi mkoani humo Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa polisi (SACP)
Ulrich Matei alisema kuwa msako huo ni wa kawaida.

Kamanda Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Mei 19 mwaka huu
majira ya saa 9 alasiri huko kijiji cha Mwetemo- Kiwangwa Tarafa ya
Msata wilayani humo.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Musa Zahoro (20) na Asher Mbuya (29)
ambapo watuhumiwa hao watafikishw amahakamani mara upelelezi
utakapokamilika.

Kwenye tukio lingine Jeshi hilo linamshikilia Omary Sultan (32)
mkulima wa mkazi wa Kijiji cha Kauzeni wilaya ya Kisarawe kwa tuhuma
za kupatikana na pombe ya Moshi lita 12 na mtambo wa kutengenezea
pombe hiyo.

Alisema kuwa tukio hilo lilitokea Mei 19 majira ya saa 6:00 Kijijini
hapo na mtuhumiwa anatarajiwa kufikishwa mahakamani mara uchunguzi wa
tukio hilo utakapokamilika.

Mwisho.

MFUKO WA MWENYEKITI WAKATALIWA

Na John Gagarini, Kibaha
MKOA wa Pwani umeingia umeingia mkataba na wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri na wenyeviti wa halmashauri juu ya utekelezaji wa mpango wa kupunguza vifo vya mama wajawazito watoto wachanga na wale wenye umri chini ya miaka mitano.
Pia mkoa umeingia na viongozi hao kwenye mkataba kwa ajili ya makusanyo ya mapato ambayo waliyapitisha kuwa wana uwezo wa kuyakusanya  kwenye halmashauri za wilaya saba za mkoa huo katika kipindi cha bajeti ya mwaka 2014-2015.
Tukio hilo la kihistoria la kusaini mikataba hiyo ya kazi kwa viongozi hao ndani ya mkoa wa Pwani lilifanyika juzi mjini Kibaha na lilisimamiwa na mkuu wa mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza na mwanasheria  wa mkoa Mohamed Magati ambapo viongozi hao endapo watashindwa kufikia malengo yaliyowekwa itawabidi kujieleza.
Wakuu wa wilaya ambao waliingia mikataba hiyo na wilaya zao ni pamoja na Mercy Silla wilaya ya Mkuranga, Fatuma Kimariyo Kisarawe, Nurdin Babu Rufiji, Sauda Mtondoo wilaya ya Mafia, Ahmed Kipozi wilaya ya Bagamoyo  na Halima Kihemba wilaya ya Kibaha.
Akizungumza na watendaji hao kuhusiana na mikata hiyo walioingia na mkoa Mahiza alisema kuwa mikataba hiyo itasaidia uwajibikaji kwa watendaji hao ambao wanawatumikia wananchi katika kuwaletea maendeleo.
“Mikataba hii ni changamoto kwa watendaji wetu hawa na endapo watashindwa kutekeleza majukumu yao kama mkataba unavyoonyesha itabidi wajieleze kwani hata mimi nishaingia mikataba na mamlaka za juu hivyo kila mtu lazima atimize wajibu wake,” alisema Mahiza.
Mahiza alisema kuwa kwa upande wa vifo vya mama wajawazito, watoto wa changa na wale wenye umri chini ya miaka mitano ni tatizo kubwa hivyo mkataba huo utasaidia kupunguza vifo hivyo visivyo vya lazima.
“Kwa upande wa makusanyo kila halmashauri ilileta makadirio yake ya kukusanya mapato kwenye bajeti ya mwaka 2014- 2015 hivyo ni lazima watimize kusudio lao na hakuna sababu ya kusema wameshindwa kuyafikia malengo hayo ya ukusanyaji wa mapato,” alisema Mahiza.
Halmashauri hizo kila moja imejiwekea kiwango chake cha kukusanya kutegemeana na vyanzo vyake vya mapato ambapo Bagamoyo watakusanya bilioni2.6, Kibaha Mjini, bilioni 4.2, Kibaha Vijijini bilioni 2.6, Kisarawe bilioni 3.8, Mafia bilioni 1, Mkuranga bilioni 2.1 na Rufiji bilioni 2.7 ambapo jumla ya makusanyo hayo kwa wilaya zote za mkoa huo itakuwa ni bilioni 8.7
Naye mganga mkuu wa mkoa wa Singida ambaye alishinda tuzo ya Rais ya kupunguza vifo vya makundi hayo Dk Doroth Gwajima alisema kuwa vifo vingi vinatokana na uzembe wa baadhi ya watumishi wasio na maadili ya kazi.
 Dk Gwajima aliwataka wahudumu wa afya kwenye mkoa huo wa Pwani kumtanguliza Mungu wakati wa utendaji wao wa kazi pia kuzingatia maadili ya kazi zao kwani baadhi ya vifo vinatokana na uzembe na si mapenzi ya Mungu. 
Mwisho.

Thursday, May 15, 2014

WACHEZAJI WAMIMINIKA RUVU SHOOTING KUOMBA USAJILI



Na John Gagarini, Kibaha
JUMLA ya wachezaji 251 wamejitokeza kufanya majaribio kwenye kikosi cha Ruvu Shooting ya Wilayani Kibaha mkoani Pwani ili kusajiliwa na timu hiyo waweze kupata nafasi kwenye timu hiyo kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu ya Voda Com.
Akizungumza na wachezaji hao kwenye uwanja wa Ruvu Kocha Mkuu Tom Olaba alisema kuwa lengo la kutangaza nafasi hiyo ya kuwaita  wachezaji ni kuwapatia fursa chipukizi wenye uwezo wa kusakata soka ili waweze kutoa mchango wao kwenye kikosi hicho kinachojiandaa na Ligi Kuu ya msimu ujao.
Olaba alisema kuwa wamewaita  wachezaji hao kufanya majaribio ili wataofanikiwa majaribio hayo waweze kupata nafasi ya kukitumikia kikosi chetu ya Ruvu Shooting tayari kwa Ligi Kuu ya Vodacom msimu ujao unaotaraji kuanza kutimua vumbi mwezi wa 8 mwaka huu, hivyo wanapaswa kuonesha uwezo na watakaofaulu watapata nafasi bila ya upendeleo.
“Mazoezi haya yataendelea kwa wiki mbili ambayo yatakuwa yanachezwa kwa mtindo wa bonanza ikiwa na lengo la kuwapatia nafasi nzuri zaidi wachezaji kuonesha uwezo wao wa kucheza soka na hatimye wapatikane wachezaji wenye vipaji,” alisema Olaba.
Naye Mkuu wa Kikosi cha Ruvu kilichopo kikosi hicho Luteni Kanali Charles Mbuge alisema kuwa uongozi huo bado unaendelea kuwataka vijana zaidi wajitokeze kwani lengo ni kuhakikisha wanapata wachezaji wenye uwezo watakaosajiliwa kwa
ajili ya Ligi Kuu na wale wenye chini ya umri wa miaka 20.

"Lengo kubwa ni kuhakikisha tunapata wachezaji ambao wataisaidia timu ili iweze kufanya vyema kwenye ligi ijayo pamoja na kuwaandaa vijana wengine watakaoitumikia timu miaka ya baadaye kwenyeligi zijazo," alisema Luteni Mbuge.
Kanali Mbuge.

Aidha Luteni Mbunge alitoa shukrani kwa jopo la makocha mbali ya Olaba na msaidizi wake Seleman Mtungwe ambao wamejipanga vizuri katika kuhakikisha zoezi hilo linakwenda kama lilivyopangwa na hatimaye kupatikana kwa wachezaji bora zaidi watakaoongezea ushindani katika kikosi hicho kwenye kinyang'anyiro kijacho.

MWISHO

MLINZI ANYONGWA



Na John Gagarini, Kibaha
MLINZI Bakari Mape (70) mkazi wa Mlandizi wilaya ya Kibaha mkoa wa Pwani ameuwawa kwa kunyongwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi.
Watu hao ambao idadi yao haikuweza kufahamika mara moja walimwua mlinzi huyo kwa kumvunja shingo kisha kuiba kwenye duka ambalo mlinzi huyo alikuwa akililinda.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Polisi mkoani humo Kamishna Mwandamizi Msaidizi (SACP) Ulrich Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Mei 14 mwaka huu majira ya saa 8 usiku eneo la sokoni Mlandizi wilayani hapa.
Kamanda Matei alisema kuwa watu hao baada ya kumwua marehemu ambaye alikuwa akilinda duka la Conrad Masawe (53) mkazi wa Mtongani Mlandizi, waliiba kiasi cha shilingi milioni 5.2.
"Walipomwua walingoa bati kisha kuingia ndani na kuiba fedha hizo na kutoweka kusikofahamika huku wakimwacha marehemu hapo," alisema Kamanda Matei.
Alisema kuwa kutokana na tukio hilo wanamshikilia mtu mmoja aitwaye Omary Rajabu kuhusiana na suala hilo.
"Mwili wa marehemu ulikabidhiw andugu kwa ajili ya mazishi baada ya uchunguzi wa daktari na tutawasaka watu walihusika na tukio hilo ili mkondo wa sheria uweze kuchukua hatua kwani kitendo hicho ni ukatili ndani ya jamii," alisema Kamanda Matei.
Aidha aliwataka wafanyabiashara waajiri watu weny umri wa kati ili waweze kukabiliana na matukio kama hayo na kuacha kuajiri watu wenye umri mkubwa sana kwani ni vigumu kukabiliana na matukio kama hayo.
mwisho.    

Friday, May 9, 2014

VIJANA KUSAIDIWA NA RED CROSS

Na John Gagarini, Kibaha
ASASI isiyo ya Kiserikali ya Amani Development Organization (ADEO) la Kibaha mkoani Pwani limetenga kiasi cha shilingi milioni 10 kwa ajili ya kuwakopesha wasichana waliokuwa wakifanyabiashara ya ngono na matumizi ya dawa za kulevya zaidi ya 20.
Mbali ya kuwakopesha fedha hizo pia shirika hilo linawapatia elimu ya kuepukana na mambo hayo ambayo yamekuwa chanzo cha maambukizi ya magonjwa ukiwemo UKIMWI.
Akizungumza jana mjini Kibaha kwenye mkutano shirikishi wa utekelezaji wa programu ya vijana kupambana na UKIMWI inayofadhiliwa na Sat Tanzania, mratibu wa shirika hilo Jane Apollo alisema kuwa lengo la kuwakopesha fedha hizo ni kuwapatia njia mbadala ili wajiepushe na vitendo hivyo.
Apollo alisema kuwa kupitia mpango huo umeweza kuwafikia vijana wa ndani na nje ya shule 3,817 ambapo kati yao wasichana wanaofanya biashara ya ngono 41 wanaume 11 wanaofanya mapenzi ya jinsia moja, vijana 63 wanaotumia dawa za kulevya na machimbo sita ya mchanga.
"Lengo ni kuwafanya vijana kuachana na vitendo vya matumizi ya dawa za kulevya na biashara ya ngono na kuwafundisha shughuli za ujasiriamali ili kuinua kipato chao na kupunguza umaskini katika maisha yao," alisema Apollo.
Moja ya waischana waliokuwa wakifanya biashaya ya ngono (Subira Hatibu) Jasmini siyo jina halisi alisema kuwa alikuwa akiishi Jijini Dar es Salaam na kujiuza kwa wanaume ambapo kwa siku alikuwa akitembea na wanaume watatu au wanne.
"Nilikuwa nikifanya biashara ya kujiuza kuanzia shilingi 50,000 hadi 30,000 kwa mtu mmoja ambapo nilifanya biashara hii kwa muda mrefu lakini sikuona faida yake zaidi ya kupata matatizo," alisema Jasmini.
Naye kijana aliyejitambulisha kwa jina la Omary Mkumba alisema kuwa alikuwa akijihusisha na uvutaji wa bangi pamoja na dawa za kulevya ambazo zilimsababisha kupata ugonjwa wa kifua kikuu lakini baada ya kupatiwa elimu aliamua kuachana na matumizi hayo.
Shirika hilo lilianzishwa mwaka 2010 na linajihusisha na mapambano dhidi ya dawa za kulevya, UKIMWI, biashara ya ngono, mimba za utotoni, ndoa kwenye umri mdogo na afya ya uzazi.
mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA cha Msalaba Mwekundu mkoani Pwani kimtoa misaada ya viatu na vifaa vya shule kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Nyumbu na vituo vya kulelea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu.
Chama hicho kilitoa misaada hiyo kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi hao waweze kusoma kwa kuwa na mahitaji muhimu ili kufanikisha masomo yao.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mara baada ya sherehe ya siku ya chama hicho inayoadhimishwa kila mwaka ambapo bkitaifa ilifanyika mkoani Mbeya, katibu msaidizi wa msalaba mwekundu mkoani humo, Felisiana Mmasi alisema kuwa waliamua kuadhimisha siku hiyo kwa kuwasaidia wanafunzi.
Mmasi alisema kuwa lengo la chama hicho ni kuwasaidia watu wenye matatizo mbalimbali kwenye jamii ikiwa ni pamoja na kutoa msaada kwenye majanga na maafa yanoyojitokeza ikiwa ni pamoja na ajali, mafuriko na kwenye vita.
"Mbali ya kutoa viatu pia tumetoa madaftari na kalamu ambapo vituo vya watoto waishio kwenye mazingira magumu vya THADEI na Buloma wamenufaika na misaada hiyo," alisema Mmasi.
Naye mratibu wa mradi wa Life kupitia chama hicho Kibaha Mjini Agnes Lubogo alisema kuwa mbali ya kusaidia kutoa misaada mbalimbali pia wanasaidia kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI walio majumbani.
Lubogo alisema kuwa wanahudumia wagonjwa ambao watoro ambao hawapati huduma mahospitalini hivyo kuwafuata huko waliko ambapo wana wahudumu wa nyumbani wapatao 73.
Aliwataka watu kujiunga na chama hicho ili waweze kuisaidia jamii ambayo inahitaji misaada mbalimbali ya kiutu ikiwa ni pamoja na kujitolea damu kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa.
mwisho. 

   
Na John Gagarini, Kibaha
ASASI isiyo ya Kiserikali ya Amani Development Organization (ADEO) la Kibaha mkoani Pwani limetenga kiasi cha shilingi milioni 10 kwa ajili ya kuwakopesha wasichana waliokuwa wakifanyabiashara ya ngono na matumizi ya dawa za kulevya zaidi ya 20.
Mbali ya kuwakopesha fedha hizo pia shirika hilo linawapatia elimu ya kuepukana na mambo hayo ambayo yamekuwa chanzo cha maambukizi ya magonjwa ukiwemo UKIMWI.
Akizungumza jana mjini Kibaha kwenye mkutano shirikishi wa utekelezaji wa programu ya vijana kupambana na UKIMWI inayofadhiliwa na Sat Tanzania, mratibu wa shirika hilo Jane Apollo alisema kuwa lengo la kuwakopesha fedha hizo ni kuwapatia njia mbadala ili wajiepushe na vitendo hivyo.
Apollo alisema kuwa kupitia mpango huo umeweza kuwafikia vijana wa ndani na nje ya shule 3,817 ambapo kati yao wasichana wanaofanya biashara ya ngono 41 wanaume 11 wanaofanya mapenzi ya jinsia moja, vijana 63 wanaotumia dawa za kulevya na machimbo sita ya mchanga.
"Lengo ni kuwafanya vijana kuachana na vitendo vya matumizi ya dawa za kulevya na biashara ya ngono na kuwafundisha shughuli za ujasiriamali ili kuinua kipato chao na kupunguza umaskini katika maisha yao," alisema Apollo.
Moja ya waischana waliokuwa wakifanya biashaya ya ngono (Subira Hatibu) Jasmini siyo jina halisi alisema kuwa alikuwa akiishi Jijini Dar es Salaam na kujiuza kwa wanaume ambapo kwa siku alikuwa akitembea na wanaume watatu au wanne.
"Nilikuwa nikifanya biashara ya kujiuza kuanzia shilingi 50,000 hadi 30,000 kwa mtu mmoja ambapo nilifanya biashara hii kwa muda mrefu lakini sikuona faida yake zaidi ya kupata matatizo," alisema Jasmini.
Naye kijana aliyejitambulisha kwa jina la Omary Mkumba alisema kuwa alikuwa akijihusisha na uvutaji wa bangi pamoja na dawa za kulevya ambazo zilimsababisha kupata ugonjwa wa kifua kikuu lakini baada ya kupatiwa elimu aliamua kuachana na matumizi hayo.
Shirika hilo lilianzishwa mwaka 2010 na linajihusisha na mapambano dhidi ya dawa za kulevya, UKIMWI, biashara ya ngono, mimba za utotoni, ndoa kwenye umri mdogo na afya ya uzazi.
mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA cha Msalaba Mwekundu mkoani Pwani kimtoa misaada ya viatu na vifaa vya shule kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Nyumbu na vituo vya kulelea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu.
Chama hicho kilitoa misaada hiyo kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi hao waweze kusoma kwa kuwa na mahitaji muhimu ili kufanikisha masomo yao.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mara baada ya sherehe ya siku ya chama hicho inayoadhimishwa kila mwaka ambapo bkitaifa ilifanyika mkoani Mbeya, katibu msaidizi wa msalaba mwekundu mkoani humo, Felisiana Mmasi alisema kuwa waliamua kuadhimisha siku hiyo kwa kuwasaidia wanafunzi.
Mmasi alisema kuwa lengo la chama hicho ni kuwasaidia watu wenye matatizo mbalimbali kwenye jamii ikiwa ni pamoja na kutoa msaada kwenye majanga na maafa yanoyojitokeza ikiwa ni pamoja na ajali, mafuriko na kwenye vita.
"Mbali ya kutoa viatu pia tumetoa madaftari na kalamu ambapo vituo vya watoto waishio kwenye mazingira magumu vya THADEI na Buloma wamenufaika na misaada hiyo," alisema Mmasi.
Naye mratibu wa mradi wa Life kupitia chama hicho Kibaha Mjini Agnes Lubogo alisema kuwa mbali ya kusaidia kutoa misaada mbalimbali pia wanasaidia kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI walio majumbani.
Lubogo alisema kuwa wanahudumia wagonjwa ambao watoro ambao hawapati huduma mahospitalini hivyo kuwafuata huko waliko ambapo wana wahudumu wa nyumbani wapatao 73.
Aliwataka watu kujiunga na chama hicho ili waweze kuisaidia jamii ambayo inahitaji misaada mbalimbali ya kiutu ikiwa ni pamoja na kujitolea damu kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa.
mwisho.