ILI kuwapa ufahamu juu ya Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya mwaka (2007) toleo la mwaka 2024 Kamati ya Vijana Wazalendo itafanya makongamano kwenye mikoa 10 hapa nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari mratibu wa Kamati ya Vijana Wazalendo Omary Punzi amesema kuwa Makongamano hayo yatakutanisha makundi ya vijana ambayo yatapatiwa elimu juu ya sera hiyo.
Punzi amesema kuwa sera hiyo ya vijana ni nzuri lakini vijana wengi hawaifahamu hali ambayo inawafanya vijana wengi kutotambua haki zao za msingi na makongamano hayo yatawafikia vijana zaidi ya milioni nane na tisa.
Mwenyekiti wa Kamati ya vijana Wazalendo Farida Kongoi amesema kuundwa kwa sera ya taifa ya maendeleo ya vijana lengo lilikuwa ni vijana wapate mwongozo wa kuendana na masuala ya siasa na kijamii ikiwa ni pamoja na mwelekeo wa kiteknolojia.
Mwanasheria wa Kamati ya vijana Wazalendo Godfrey Kizito amesema pia vijana watafafanuliwa kuhusu Sheria zinazohusu haki na masuala ya vijana.
Naye Mkurugenzi wa Great leaders organization na Mratibu na Mwandaaji wa kongamano la Wazazi na Walezi nchini Dubai Dk Debora Nyamlundwa amesema katika kongamano hilo kuna kujifinza fursa mbalimbali zilizopo katika taifa hilo kuja kuendeleza hapa nchini