MTANZANIA ambaye alipata Tuzo ya Malkia Elizabeth || wa Uingereza, Prudence Kimiti amesema kuwapa hadhi maalum Diaspora itasaidia waweze kuwekeza nchini.
Sunday, December 31, 2023
ALIYEESHINDA TUZO YA MALKIA WA UINGEREZA ATAKA DIASPORA WAPEWE HADHI MAALUM WAWEZE KULETA MAENDELEO NCHINI.
Saturday, December 30, 2023
SIKU YA LISHE YA KIJIJI GAIRO DC
GAIRO DC
SIKU YA AFYA NA LISHE YA KIJIJI
NIMEPATA FURSA YA KUZUNGUMZA NA WAKINA MAMA.
NIMESISITIZA KUHUSU LISHE, NIMEWAKUMBUSHA MALEZI YA WATOTO KWA KUWALINDA DHIDI YA UKATILI. UZOEFU UNAONESHA KUWA MATUKIO MENGI YA UKATILI YANAANZIA KWENYE NYUMBA ZETU KWA KUWAAMINI NDUGU TUNAOWAKARIBISHA HADI KUWALAZA KITANDA KIMOJA NA WATOTO WETU.
GAIRO DC - KAZI INAENDELEA
@ortamisemi
@wizara_afyatz
@rs_morogoro
@jabiri_makame
Thursday, December 28, 2023
WATU WATATU WAMEFARIKI DUNIA BAADA YA GARI WALILOKUWA WAKISAFIRIA KULIGONGA GARI LINGINE KWA NYUMA
ReplyReply allForward Add reaction |
Saturday, December 16, 2023
ATFT KUENDELEZA VIPAJI KUPITIA KIPAJI BILA MIPAKA
KITUO cha kuendeleza vipaji Africa Talent Forum-TZ (ATFT) cha Mkoani Pwani imewakutanisha wasanii wa fani mbalimbali ili kujadili namna ya kuendeleza vipaji vya wasanii ili viweze kutoa ajira.
Wednesday, December 6, 2023
TPFNET CHALINZE WATOA MSAADA KITUO CHA WATOTO DOLPHINE.
Jeshi la Polisi Wilaya ya Kipolisi Chalinze, Mkoa wa Pwani, Disemba 05, 2023 wametoa msaada kwa watoto wenye uhitaji katika kituo cha Dolphine kilichopo Kijiji cha Kipera, Kitongoji cha Mwanabele Wilayani humo.
Akizungumza akiwa kituoni hapo, Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kipolisi Chalinze, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Sophia Lyidenge alisema jukumu la ulezi wa watoto wenye uhitaji na kuwatunza ni la jamii nzima hivyo wao wakiwa ni sehemu ya wazazi wameguswa katika siku 16 za maadhimisho ya kupinga ukatili wa Kijinsia kufikia kwa watoto hao wenye uhitaji na kuweza kutoa msaada wa vitu mbalimbali.
"Jamii inapaswa kutambua malezi ya watoto na kuwatunza na kuwatembelea mara kwa mara kujua changamoto walizonazo na kuzitafutia ufumbuzi watoto wenye uhitaji kwenye vituo vya malezi ni la watu wote na kufanya hivyo ni kuwapa faraja watoto walio kwenye vituo hivyo kuona jamii ina wajali na kuwathamini".Alisema Lyidenge.
Lyidenge amewapongeza wasimamizi wa kituo hicho kwa malezi ya watoto hao akiweka wazi kuwa jambo wanalolifanya la kuwalea watoto kwenye maadili mema ni kubwa sana mbele ya Mungu na la kupongezwa.
Amesema kuwa watoto hao endapo wangeachwa bila ulezi kwenye kituo hiki wangeweza kuwa katika makuzi mabaya hivyo kutumbukia kwenye makundi ya kihalifu na hivyo kupeleka Jamii kuwa na kizazi kisichokuwa na maadili.
Aidha, Lyidenge amewaasa watoto hao kuwa wasikivu kwa walezi wao na kutambua kuwa wao ni taifa la kesho akiwasisitiza kusoma kwa bidii ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa za changamoto walizonazo kwa walezi wao bila woga ili ziweze kupatiwa ufumbuzi kwa wakati.
Kwa upande wake Afisa Ustawi wa jamii Bi. Linna Jackson Mlay ameahidi kuendeleza ushirikiano na walezi wa kituo hicho katika kutatua changamoto mbalimbali walizonazo.
Nae msimamizi wa kituo hicho Anna Munisi amelishukuru Jeshi la Polisi Wilaya ya Kipolisi Chalinze kwa msaada waliowapatia na kuomba wananchi wengine kuendelea kusaidia kituo hiko kwani uhitaji ni mkubwa katika maelezi ya watoto waliopo kituoni hapo.
Msaada uliotolewa na Jeshi la Polisi kituoni hapo ni unga wa sembe, mchele, sabuni, madaftari, kalamu na taulo za watoto.
Monday, December 4, 2023
TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE MKOA WA PWANI YAWATAKA WANAWAKE KUMUENZI BIBI TITI MOHAMED KWA KULETA MAENDELEO
Aidha amewataka kuunga mkono jitihada za Rais Dk Samia Suluhu Hassan kuwaletea maendeleo wananchi kwa kuwapatia fursa mbalimbali za kujiletea maendeleo.
TASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE MKOA WA PWANI YAWAPONGEZA WAANDAJI WA MAFUNZO YA IJUE KESHO YAKO KWA WANAWAKE MLANDIZI KIBAHA