Monday, December 5, 2016

ZAIDI YA 15 WAFAULU DARASA LA SABA PWANI

Na John Gagarini, Kibaha

JUMLA ya wanafunzi 15,528 mkoani Pwani wamefaulu kwenda shule za sekondari kwa mwaka 2017 baada ya kufanya mtihani wa kumaliza darasa la saba mwaka huu.

Aidha wanafunzi 9,290 wamefeli sawa na asilimia 37.4 na wanafunzi wote waliofaulu wamechaguliwa kujiunga na elimu ya sekondari ambapo wamefaulu kwa kupata alama zaidi ya 100 kati yao 288 wamepata daraja la A.

Hayo yamesemwa mjini Kibaha na Kaimu ofisa elimu mkoa wa Pwani Modest Tarimo wakati wa uchambuzi wa matokeo ya mtihani wa kuhitimu eilimu ya msingi mwaka 2016 ya mkoa na kusema kuwa wanafunzi waliofanya mtihani walikuwa ni 24,818.

Tarimo amesema kuwa wanafunzi 2,636 walipata daraja B, wanafunzi 12,604 wamepata daraja C na wote waliopata daraja A na C wote wamechaguliwa kujiunga na sekondari

Amesema kuwa wanafunzi waliokuwa wakitarajiwa kufanya mtihani walikuwani 24,913 ambapo waliofanya walikuwa ni 24,818 wavulana wakiwa ni 11,334 na wasichana walikuwa ni 13,484 sawa na asilimia 99.9.

Ameeleza kuwa ufaulu kwa mwaka huu umeshuka kwani ni asilimia 62.5 ikilinganishwa na mwaka 2015 ambapo ufaulu ulikuwa ni asilimia 63.1 matokeo haya hayaridhishi kwani ufaulu badala ya kupanda lakini umeshuka kwa asilimia 0.5 na kwa matokeo hayo mkoa umeshika nafasi ya 21 kitaifa.

Amebainisha kuwa watahiniwa 95 hawakufanya mtihani sawa na asilimia 0.3 kutokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na utoro, wanafunzi 75, mimba mwanafunzi mmoja, vifo 11, ugonjwa wawili na sababu nyingine sita ambapo wadau wanapaswa kupiga vita utoro ambao umepungua 204 ikilinganishwa na mwaka jana.

Kaimu ofisa elimu huyo wa mkoa ambaye ni ofisa taaluma amesema serikali iliweka wastani wa asilimia 80 ya ufaulu kwa shule za msingi ikiwa ni mkakati wa kufikia mpango wa matokeo makubwa sasa BRN ambapo wadau wa elimu wanapaswa kukabiliana na changamoto zinaosababisha ufaulu kushuka.

Naye Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Edward Mwakipesile amesema kuwa wadau wa elimu wanapaswa kushirikiana na idara ya elimu ya mkoa ili kuhakikisha matokea ya wanafunzi yanakuwa mazuri ambapo kwa mwaka huu yanaonekana kushuka.

Mwakipesile amesema kuwa mbali ya changamoto ya matokeo hayo pia changamoto iliyopo ni vyumba vya madarasa ambavyo ni vichache na kusababisha madawati kukosa sehemu ya kukaa baada ya zoezi la utengenezaji madawati kufanikiwa.


Mwisho.

No comments:

Post a Comment