Wednesday, December 14, 2016

CCM WAANZA MCHAKATO WA KUMPATA MGOMBEA UDIWANI MISUGUSUGU

Na John Gagarini, Kibaha

RAMADHAN Bogas ameshinda kura za maoni za kumpata mgombea udiwani kata ya Misugusugu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya kupata kura 43 huku aliyeshinda udiwani kabla ya mahakama kutengua matokeo Addhu Mkomambo akiambulia kura mbili.

Uchaguzi huo ambao ulifanyika Misugusugu ulisimamiwa na Yusuph Mbonde, Selina Wilson na Mohamed Mpaki ambao ni wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya, ulihusisha wagombea saba.

Akizungumza na waandishi wa habari katibu wa CCM Kibaha Mjini Abdala Mdimu alisema kuwa kura zilizopigwa zilikuwa 115 na hakuna kura iliyoharibika.
Mdimu akitaja matokeo alisema kuwa mshindi wa pili alikuwa Eliasi Masenga aliyepata kura 37, Ramadhan Mataula aliyepata kura 15 huku Salumu Mkali akipata kura 14, huku watano akiwa Mkomambo aliyepata kura mbili, Francis Alinamiswe alipata kura mbili na Laurence Likuda naye kura mbili.

Alisema kuwa bado vikao mapendekezo vinaendelea kukaa ambapo jana kilitarajiwa kukaa kikao cha kamati ya siasa ya kata ambapo leo kikao cha kamati ya Usalama na maadili wilaya kinakaa.

“Desemba 16 kamati ya siasa ya wilaya itakaa na baadaye vitaendelea vikao vya mkoa na Desemba 19 Halmashauri Kuu ya mkoa itafanya uteuzi wa mwisho wa mgombea atakayekiwakilisha chama kwenye uchaguzi huo,”alisema Mdimu.

Uchaguzi huo mdogo wa udiwani unarudiwa baada ya mahakama ya mkoa kutengua matokeo kutokana na malalamiko yaliyotolewa na diwani wa Chadema ambapo mgombea wa CCM Addhu Mkomambo alikuwa ameshinda.

Mwisho.      




No comments:

Post a Comment