Sunday, May 31, 2015

PWANI WAANZISHA WILAYA MPYA YA KIBITI NA MAJIMBO MAPYA


Na John Gagarini, Kibaha

MKOA wa Pwani umepitisha mapendekezo ya kugawanywa kwa Wilaya ya Rufiji kuwa wilaya mbili za Rufiji na Kibiti na kuligawa Jimbo la Chalinze kuwa majimbo mawili ya Chalinze na Saadani.

Mbali ya kupitisha wilaya mpya ya Kibiti na Jimbo la Saadani umepitisha mapendekezo yaliyowasilishwa na Halmashauri ya Kibaha Mji ya kugawa Tarafa ya Kibaha na kuwa na  Tarafa mpya ya Kongowe.

Maamuzi hayo yalifanywa mjini Kibaha kwenye Kiko cha Usahauri cha Mkoa (RCC) kilichokaa mwishoni mwa wiki chini ya kaimu mkuu wa mkoa wa Pwani ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Kibaha Halima Kihemba
Kihemba alisema kuwa mapendekezo hayo yamefuata sheria na taratibu zinazostahili kwa upande wa wilaya na Jimbo ni pamoja na Jimbo kuwa ndani ya wilaya moja ama Halmashauri moja, idadi kubwa ya watu ,upatikanaji wa mawasiliano ikiwemo mitandao ya simu, barabara, huduma za kiuchumi na jiografia ya eneo husika.
Naye Mkuu wa wilaya ya Rufiji Nurdin Babu alisema kuwa anpongeza kikao hicho kuweza kupitisha uanzishwaji wa wilaya mpya ya Kibiti kwani itawasogezea huduma mbalimbali za kijamii karibu.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga alisema kugawanywa kwa Jimbo la Chalinze ni mchakato wa wilaya ya Bagamoyo kugawanywa katika wilaya mbili

Mwanga alisema kuwa endapo utaratibu huo utakuwa umekamilika wilaya hiyo itakuwa na majimbo matatu ya uchaguzi ambayo ni Bagamoyo,Saadani na Chalinze kutokana na ukubwa wa wilaya hiyo.

Jimbo la Bagamoyo litakuwa na kata za Dunda,Magomeni,Nia Njema ,Kisutu, Makurunge, Kiromo,Zinga ,Kerege, Mapinga, Yombo na Fukayosi ambayo itatolewa kutoka jimbo la Chalinze.

Huku Jimbo la Chalinze likiwa na kata za Vigwaza ambayo imeondolewa katika Jimbo la Bagamoyo, Kiwangwa, Msata, Lugoba,Talawanda, Ubena, Pera, Bwiringu na Msoga na Jimbo jipya la Saadani makao makuu yatakuwa Miono na Jimbo hilo likiwa na kata za Kibindu, Mbwewe, Kimange, Mandela, Miono na Mkange.


Mwisho

Friday, May 29, 2015

UMISSETA PWANI

Na John Gagarini, Kibaha
WACHEZAJI wa michezo ya Umoja wa Michezo na Sanaa kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) mkoa wa Pwani wametakiwa kushindana na si kushiriki kwenye michuano hiyo ngazi ya Kanda ili mkoa utoe wachezaji wengi.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na ofisa elimu wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani Benjamini Majoya wakati wa ufungaji wa michezo hiyo ngazi ya mkoa kwenye viwanja vya Filbert Bayi na kusema kuwa ushindani ndiyo unaotakiwa na si ushiriki.
Majoya alisema kuwa mashindano ya Kanda ambayo yatafanyika mkoani Morogoro mwezi ujao ili kupata timu itakayounda kanda ya Mashariki inayoundwa na mikoa ya Pwani na Morogoro kwa ajili ya timu itakayokwenda mkoani Mwanza kwenye mashindano ya Taifa.
“Michezo ni sehemu ya kuendeleza taaluma hivyo lazima mcheze ip[asavyo na si muende kwa ajili ya kushiriki tu lazima mpambane na kuonyesha vipaji vyenu ili muwakilishe vyema mkoa na kutoa wachezaji wengi kuwakilisha kanda ya Mashariki,” alisema Majoya.
Aidha aliwataka wanamichezo hao kuonyesha nidhamu wakati wanacheza michezo kwani nidhamu ndiyo mafanikio ya michezo kwani bila ya kuwa na nidhamu itakuwa vigumu kufanikiwa.
Kwa upande wake ofisa michezo wa mkoa wa Pwani Grace Bureta alisema kuwa michezo hiyo ilihusisha wilaya sita za mkoa huo ambapo jumla ya wachezaji 136 wa michezo mbalimbali walichaguliwa kwa ajili ya kuunda timu ya mkoa.
Bureta alisema kuwa timu hiyo itaingia kambini kwa muda wa siku nne hadi Mei 31 ambapo Juni Mosi wataelekea mkoani Morogoro kwa ajili ya mashindano ya kanda ya Mashariki.
Alisema kuwa wachezaji waliochaguliwa ni wazuri na anategemea watafanya vizuri kwa kutoa wachezaji wengi kuunda timu ya Kanda na kufanikiwa kutetea ubingwa wa jumla wa mashindano hayo kitaifa mjini Mwanza.

Mwisho.Na John Gagarini, Kibaha
MKOA wa Pwani umechagua jumla ya wanamichezo 136 wa michezo mbalimbali kwa ajili ya kuunda timu ya mkoa ya Umoja wa Michezo na Sanaa kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) kwa ajili ya kushiriki michezo ya Kanda ya Mashariki.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Ofisa Michezo wa mkoa wa Pwani Grace Bureta wakati wa ufungaji wa michezo hiyo ngazi ya wilaya iliyofanyika kwenye viwanja vya shule ya Filbert Bayi.
Bureta alisema kuwa mashindano hayo ambayo yaliwahusisha wachezaji toka kwenye shule za sekondari za wilaya sita za mkoa huo ambazo ni Mafia, Rufiji, Kibaha Mjini na Vijijini, Kisarawe, Mkuranga na Bagamoyo walifanikiwa kupata wachezaji ambao walifanya vizuri.
“Mara baada ya michezo kukamilika na kuchaguliwa wachezaji hao timu itaingia kambini kwa muda wa siku nne hadi Mei 31 ambapo Juni Mosi wataelekea mkoani Morogoro kwa ajili ya mashindano ya kanda ya Mashariki,” alisema Bureta.
Alisema kuwa wachezaji waliochaguliwa ni wazuri na anategemea watafanya vizuri kwa kutoa wachezaji wengi kuunda timu ya Kanda na kufanikiwa kutetea ubingwa wa jumla wa mashindano hayo kitaifa mjini Mwanza.
Benjamini Majoya aliwataka wanamichezo wa mkoa huo kushindana na si kushiriki kwenye michuano hiyo ngazi ya Kanda ili mkoa utoe wachezaji wengi watakaounda kanada hiyo.
Majoya alisema kuwa mashindano ya Kanda ambayo yatafanyika mkoani Morogoro mwezi ujao ili kupata timu itakayounda kanda ya Mashariki inayoundwa na mikoa ya Pwani na Morogoro kwa ajili ya timu itakayokwenda mkoani Mwanza kwenye mashindano ya Taifa.
“Michezo ni sehemu ya kuendeleza taaluma hivyo lazima mcheze ip[asavyo na si muende kwa ajili ya kushiriki tu lazima mpambane na kuonyesha vipaji vyenu ili muwakilishe vyema mkoa na kutoa wachezaji wengi kuwakilisha kanda ya Mashariki,” alisema Majoya.
Aidha aliwataka wanamichezo hao kuonyesha nidhamu wakati wanacheza michezo kwani nidhamu ndiyo mafanikio ya michezo kwani bila ya kuwa na nidhamu itakuwa vigumu kufanikiwa, michezo iliyoshindaniwa ni pamoja na soka, pete, wavu, kikapu, riadha na bao.
Mwisho.

 Na John Gagarini, Kibaha
MKOA wa Pwani umechagua jumla ya wanamichezo 136 wa michezo mbalimbali kwa ajili ya kuunda timu ya mkoa ya Umoja wa Michezo na Sanaa kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) kwa ajili ya kushiriki michezo ya Kanda ya Mashariki.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Ofisa Michezo wa mkoa wa Pwani Grace Bureta wakati wa ufungaji wa michezo hiyo ngazi ya wilaya iliyofanyika kwenye viwanja vya shule ya Filbert Bayi.
Bureta alisema kuwa mashindano hayo ambayo yaliwahusisha wachezaji toka kwenye shule za sekondari za wilaya sita za mkoa huo ambazo ni Mafia, Rufiji, Kibaha Mjini na Vijijini, Kisarawe, Mkuranga na Bagamoyo walifanikiwa kupata wachezaji ambao walifanya vizuri.
“Mara baada ya michezo kukamilika na kuchaguliwa wachezaji hao timu itaingia kambini kwa muda wa siku nne hadi Mei 31 ambapo Juni Mosi wataelekea mkoani Morogoro kwa ajili ya mashindano ya kanda ya Mashariki,” alisema Bureta.
Alisema kuwa wachezaji waliochaguliwa ni wazuri na anategemea watafanya vizuri kwa kutoa wachezaji wengi kuunda timu ya Kanda na kufanikiwa kutetea ubingwa wa jumla wa mashindano hayo kitaifa mjini Mwanza.
Benjamini Majoya aliwataka wanamichezo wa mkoa huo kushindana na si kushiriki kwenye michuano hiyo ngazi ya Kanda ili mkoa utoe wachezaji wengi watakaounda kanada hiyo.
Majoya alisema kuwa mashindano ya Kanda ambayo yatafanyika mkoani Morogoro mwezi ujao ili kupata timu itakayounda kanda ya Mashariki inayoundwa na mikoa ya Pwani na Morogoro kwa ajili ya timu itakayokwenda mkoani Mwanza kwenye mashindano ya Taifa.
“Michezo ni sehemu ya kuendeleza taaluma hivyo lazima mcheze ip[asavyo na si muende kwa ajili ya kushiriki tu lazima mpambane na kuonyesha vipaji vyenu ili muwakilishe vyema mkoa na kutoa wachezaji wengi kuwakilisha kanda ya Mashariki,” alisema Majoya.
Aidha aliwataka wanamichezo hao kuonyesha nidhamu wakati wanacheza michezo kwani nidhamu ndiyo mafanikio ya michezo kwani bila ya kuwa na nidhamu itakuwa vigumu kufanikiwa, michezo iliyoshindaniwa ni pamoja na soka, pete, wavu, kikapu, riadha na bao.
Mwisho.














Friday, May 22, 2015

SHULE HATARINI KUANGUKA


WANANCHI wa Kijiji cha Mkoko wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wameiomba Halmashauri kubomoa baadhi ya madarasa ya  shule ya Msingi Mkoko ambayo yananyufa na yako hatarini kuanguka hivyo kufanya wanafunzi kusoma kwa hofu.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo hivi karibuni Muhsin Mkumbi alisema kuwa majengo hayo yako kwenye hali mbaya na wakati wowote yanaweza kuanguka na kuleta madhara.
Mkumbi alisema kuwa madarasa hayo ni mabovu sana na hayastahili kutumika kutokana na ubovu wake hivyo ni vema Halmashauri ikayabomoa na kuyajenga upya ili kuepuka madhara ambayo yanaweza kutokea.
“Madarasa hayo yameharibika sana na yataanguka wakati wowote hivyo tunaiomba halmashauri iyabomoe kwani ni hatari kwa wanafunzi na walimu wanaofundisha shule hiyo, hali ni mbaya sana tunaomba hatua madhubuti zichukuliwe,” alisema Mkumbi.
Alisema kuwa hata baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakiogopa kwenda shule kutokana na hali hiyo ya ubovu wa madarasa hayo ambayo yamewekewa na miti kuyazuia ili yasianguke na tunawasiwasi kwani yakianguka yataleta tatizo.
Kwa upande wake ofisa elimu wa kata ya Msata Rajab Msakam alikiri kuwepo kwa tatizo hilo na kusema kuwa madarasa mengi yana nyufa kutokana na ardhi ya eneo hilo ujenzi wake kuwa mgumu kwani inapasuka na kusababisha nyufa.
Msakamali alisema kuwa talipeleka jambo hilo sehemu husika ili kuangalia namna ya kuikabili hali hiyo ambayo inahatarisha usalama wa wanafunzi pamoja na walimu wanaofundisha madarasa hayo yenye nyufa.
Naye Mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete alisema kuwa tayari suala hilo limepelekwa halmashauri na kinachosubiriwa ni kibali kwa Kijiji kwa ajili ya kuvunja madarasa hayo ambayo yanahatarisha usalama wa wanafunzi na walimu.
Mwisho.

Tuesday, May 19, 2015

RIDHIWANI ATOA MSAADA WA FEDHA NA SARUJI KWENYE ZAHANATI

Na John Gagarini, Chalinze
ADHA ya akinamama wajawazito kujifungua mbele za wanaume kutokana na zahanati ya Kijiji cha Pongwe Kiona wilayani Bagamoyo mkoani Pwani kuwa na chumba kimoja cha matibabu huenda ikaondoka baada ya kuchangiwa kiasi cha shilingi milioni moja na mifuko 70 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya wanawake na wanaume.
Kutokana na zahanati hiyo kuwa na chumba kimoja imesababisha akinamama kujifungua huku kukiwa na wanaume jambo ambalo limesababisha kutokuwa na usiri hivyo utu wa mwanamke kutokuwepo.
Msaada huo umetolewa na Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete ambapo fedha na Saruji  vilikabidhiwa na Katibu wa Mbunge huyo Iddy Swala kwa niaba ya Mbunge.
Akizungumzia changamoto hiyo mwenyekiti wa kijiji hicho Rajab Mgaya alisema kuwa zahanati hiyo ilijengwa mwaka 1964 na ina wodi moja tu.
“Tunamshukuru Mbunge kwani hii ilikuwa changamoto kubwa kwa akinamama wanaojifungua huku kukiwa na akinababa nao wanapata matibabu humo hivyo usiri kutokuwepo kutokana na hali hiyo,” alisema Mgaya.
Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kimange Husein Hadingoka alisema kuwa mbunge huyo ameonyesha upendo wa hali ya juu kwa kutoa vitu hivyo ambavyo vitasaidia ujenzi huo.
Hadingoka alisema kuwa wananchi watafanya ujenzi huo ambapo yeye alitoa 100,000 kwa ajili ya kufanikisha ujenzi huo na kusema atafurahi kuona uujenzi huo unakamilika mapema.
Naye moja ya wakazi wa Kijiji hicho ambaye ni mwanamama Sikudhani Ally alisema kuwa kujifungua huku wanaume wakiwepo ni mtihani mkubwa lakini kwa mpango huo utakuwa umeweka stara ya mwanamke.
Kwa upande wake katibu wa Mbunge Swala alisema kuwa mbunge ametoa msaada huo baada ya kutemebelea hivi karibuni akiwa kwenye ziara zake za kikazi na wananchi kutoa kilio chao juu ya hali hiyo.

Mwisho.

HABARI MOTOMOTO

Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA Cha Wasioona Nchini kimewataka vijana wenye ulemavu huo kuachana na dhana ya kuwa mara wamalizapo elimu mbalimbali ni laziwa waajiriwe badala yake wajiandae kwa kufanya shughuli za kujiajiri wenyewe.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na makamu mwenyekiti wa chama hicho Taifa Robert Bundala wakati wa mafunzo ya sera ya ajira kwa watu wenye ulemavu kwa vijana wanachama wa chama hicho wilayani Kibaha.
Bundala alisema kuwa soko la ajira kwa sasa ni gumu sana hivyo lazima vijana wajiwekee malengo ya kujiajiri wao wenyewe kupitia fursa zilizopo kwenye maeneo yao kuliko kusubiri kuajiriwa serikalini au sekta binafsi.
“Vijana wasioona wanapaswa kuachana na dhana hiyo badala yake wajiajiri kwa kupitia shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na ujasiriamali na si kutegemea kuajiriwa kwani upatikanaji wa ajira kwa sasa ni mgumu,” alisema Bundala.
Alisema kuwa ushindani wa soko la ajira hapa nchini kwa sasa ni mkubwa sana kwani hata watu wasiona na ulemavu wamekuwa wakilalamika hivyo lazima vijana hao watumie mafunzo mbalimbali wanayoyapata ili kujiajiri.
“Kwa sasa ubaguzi umepungua lakini kikubwa kinachoangaliwa ni uwezo wako wa kielimu kwani kwa wale wenye elimu nzuri wamepata ajira lakini lazima wabadili mfumo wa kusubiri ajira badala yake wajiajiri,” alisema Bundala ambaye ni mwalimu wa shule ya msingi.
Naye Mwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye naye ni mlemavu asiyeona Greyson Mlanga alisema kuwa ni vema vijana wakaangalia fursa za ajira zilizopo kwenye maeneo wanayoishi na kuwaondolea fikra kuwa lazima waajiriwe.
Mlanga alisema kuwa kutokana na ugumu wa ajira vijana wasioona wanapaswa kuangalia suala la kujiajiri kwani kutegemea ajira za kuajiriwa itakuwa ni vigumu sana kuweza kufanikiwa kujiletea maendeleo.
 Kwa upande wake moja ya washiriki wa mafunzo hayo Zuhura Omary alisema kuwa changamoto kwao ni nyingi kutokana na hali waliyonayo pia ni kutokana na kutokuwa na elimu ya kutosha hivyo kujikuta wakikosa ajira.
Mafunzo hayo yaliwahusisha vijana wasioona wapatao 60 kutoka kata nne za Misugusugu, Visiga, Kibaha na Kongowe na kufadhiliwa na The Foundation for Civil Society
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WANANCHI wametakiwa kuhakikisha wanazingatia matumizi ya dawa za minyoo kila baada ya miezi mitatu ili kuepukana na athari ikiwa ni pamoja na magonjwa ya Kisukari na Presha.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Ofisa afya Mstaafu Allice Bakari alipozungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa minyoo ni chanzo cha magonjwa hayo makubwa ambayo yanasababisha vifo.
Bakari alisema kuwa kutokana na watu kutotumia kabisa dawa za kuua minyoo kumesababisha watu kupata athari kubwa za kiafya kutokana na ulaji wa vyakula ambao husababisha watu kupata minyoo.
“Minyoo ni chanzo cha magonjwa mengi makubwa yakiwemo moyo kutanuka, kuchanganyikiwa, mba na baadhi ya viuongo vya ndani kuathirika na kushindwa kufanya kazi na hatimaye ni kifo,” alisema Bakari.
Alisema kuwa tatizo la minyoo linazidi kuwa kubwa kutokana na baadhi hata ya wahudumu wa afya kuumwa kutokana na kutotumia dawa za minyoo kutokana na kutotambua ukubwa wa tatizo hilo.
“Hata baadhi ya madaktari wameathiriwa na hali hiyo kutokana na kutoona kuwa minyoo ni tatizo lakini ukweli ni kwamba hili ni tatizo kubwa sana na inabidi wahudumu wa afya kulifuatilia kwa umakini ili kuwanusuru watu,” alisema Bakari.
Ofisa afya huyo ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye hospitali ya Tumbi iliyopo wilayani Kibaha alisema kuwa minyoo inapokuwa imekithiri mwilini hushambulia viungo mbalimbali vya ndani ya mwili na kuleta athari hizo.
“Ushauri ni kwamba madaktari wanapaswa kuwa makini kwa kuwashauri wagonjwa kutumia dawa za kuwaua wadudu hao kwa kujua kuwa endapo walishawahi kutumia dawa kwani watu wanafikiri minyoo ni kwa watoto pekee,” alisema Bakari.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MRADI mkubwa wa Maji wilayani Kibaha mkoani Pwani unatarajiwa kukamilika Agosti mwaka huu na kuondoa tatizo la ukosefu wa maji ambapo baadhi ya vitongoji wananchi wameanza kukimbia bili za maji.
Akizungumza na wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa uzinduzi wa matawi ya chamaa hicho Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema kuwa mara mradi huo utakapokamilika tatizo hilo itakuwa ni historia.
Koka alisema kuwa mradi huo wa maji ambao chanzo chake ni mto Ruvu utapitia kwenye mitaa yote ya Jimbo hilo ambapo kwa kipindi kirefu wananchi wamekuwa wakilalamika upatikanaji wa maji.
“Tunashukuru kuwa kwenye mradi uliotokea wilaya ya Bagamoyo baadhi ya mitaa ikiwemo ya Vikawe, Vikawe shule maji yanapatikana kwa wingi ambapo sasa watu wanakimbia bili kutokanana kushindwa kulipa kwani awali walikuwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa maji,” alisema Koka.
Alisema kwa sasa maji yamesambazwa kwenye mitaa 14 na mara mradi huo utakapokamilika wakazi wa Kibaha hawatanyanganyana maji na Jiji la Dar es Salaam ambao wanategemea chanzo kimoja hivyo maji kuwa ya mgao.
“Nawaomba msiwe na wasiwasi kwani mradi huo unaendelea vizuri ambapo kwa sasa wanatandaza mabomba ambayo kwa sasa yamefika eneo la Kongowe kilometa 10 kutoka hapa mjini hivyo Mungu akipenda wakati huo uliotajwa maji yatapatikana,” alisema Koka.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WANAWAKE wajawazito wilayani Kibaha mkoani Pwani wametakiwa kuacha kutumia dawa za kienyeji za kuongeza uchungu ili kupunguza vifo vya watoto wachanga.
Hayo yalisemwa na ofisa muuguzi wa kituo cha afya cha Mkoani, Prisca Nyambo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea kituo hicho hivi karibuni na kusema kuwa dawa hizo zianasababisha watoto kufia tumboni.
Nyambo alisema kuwa dawa hizo za kuongeza uchungu za kienyeji ni mbaya kwa watoto waliotumboni kwani wengi wamekuwa wakipoteza maisha.
“Tatizo la watoto kufia tumboni kwa sasa ni kubwa kutokana na wajawazito kutumia dawa hizo ili waweze kujifungua endapo muda umefika na hakuna dalili za kufanya hivyo,” alisema Nyambo.
Alisema kuwa wajawazito wanapaswa kwenda hospitali wanapoona muda wa kujifungua umefika lakini hawajifungui kuliko kutumia dawa hizo ambazo zinasabisha vifo vya watoto.
Aidha alisema vifo vya watoto wachanga ni kati ya saba na tisa kwa kila mwezi kutokana na sababu mbalimbali mojawapo ikiwa ni matumizi ya dawa hizo za kienyeji za kuongeza uchungu ambapo wastani wa wanawake wanaojifungua kwa kipindi hicho ni zaidi ya 300.
Alibainisha kuwa akinamama wajawazito wanaokwenda kujifungua hapo ni wengi kwani baadhi yao wanatoka maeneo ya Jiji la Dar es Salaam kama vile Mbezi, Kibamba, Kimara na Ilala kutokana na ukaribu.
Mwisho.




   

    

HABARI MOTOMOTO

Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA Cha Wasioona Nchini kimewataka vijana wenye ulemavu huo kuachana na dhana ya kuwa mara wamalizapo elimu mbalimbali ni laziwa waajiriwe badala yake wajiandae kwa kufanya shughuli za kujiajiri wenyewe.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na makamu mwenyekiti wa chama hicho Taifa Robert Bundala wakati wa mafunzo ya sera ya ajira kwa watu wenye ulemavu kwa vijana wanachama wa chama hicho wilayani Kibaha.
Bundala alisema kuwa soko la ajira kwa sasa ni gumu sana hivyo lazima vijana wajiwekee malengo ya kujiajiri wao wenyewe kupitia fursa zilizopo kwenye maeneo yao kuliko kusubiri kuajiriwa serikalini au sekta binafsi.
“Vijana wasioona wanapaswa kuachana na dhana hiyo badala yake wajiajiri kwa kupitia shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na ujasiriamali na si kutegemea kuajiriwa kwani upatikanaji wa ajira kwa sasa ni mgumu,” alisema Bundala.
Alisema kuwa ushindani wa soko la ajira hapa nchini kwa sasa ni mkubwa sana kwani hata watu wasiona na ulemavu wamekuwa wakilalamika hivyo lazima vijana hao watumie mafunzo mbalimbali wanayoyapata ili kujiajiri.
“Kwa sasa ubaguzi umepungua lakini kikubwa kinachoangaliwa ni uwezo wako wa kielimu kwani kwa wale wenye elimu nzuri wamepata ajira lakini lazima wabadili mfumo wa kusubiri ajira badala yake wajiajiri,” alisema Bundala ambaye ni mwalimu wa shule ya msingi.
Naye Mwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye naye ni mlemavu asiyeona Greyson Mlanga alisema kuwa ni vema vijana wakaangalia fursa za ajira zilizopo kwenye maeneo wanayoishi na kuwaondolea fikra kuwa lazima waajiriwe.
Mlanga alisema kuwa kutokana na ugumu wa ajira vijana wasioona wanapaswa kuangalia suala la kujiajiri kwani kutegemea ajira za kuajiriwa itakuwa ni vigumu sana kuweza kufanikiwa kujiletea maendeleo.
 Kwa upande wake moja ya washiriki wa mafunzo hayo Zuhura Omary alisema kuwa changamoto kwao ni nyingi kutokana na hali waliyonayo pia ni kutokana na kutokuwa na elimu ya kutosha hivyo kujikuta wakikosa ajira.
Mafunzo hayo yaliwahusisha vijana wasioona wapatao 60 kutoka kata nne za Misugusugu, Visiga, Kibaha na Kongowe na kufadhiliwa na The Foundation for Civil Society
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WANANCHI wametakiwa kuhakikisha wanazingatia matumizi ya dawa za minyoo kila baada ya miezi mitatu ili kuepukana na athari ikiwa ni pamoja na magonjwa ya Kisukari na Presha.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Ofisa afya Mstaafu Allice Bakari alipozungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa minyoo ni chanzo cha magonjwa hayo makubwa ambayo yanasababisha vifo.
Bakari alisema kuwa kutokana na watu kutotumia kabisa dawa za kuua minyoo kumesababisha watu kupata athari kubwa za kiafya kutokana na ulaji wa vyakula ambao husababisha watu kupata minyoo.
“Minyoo ni chanzo cha magonjwa mengi makubwa yakiwemo moyo kutanuka, kuchanganyikiwa, mba na baadhi ya viuongo vya ndani kuathirika na kushindwa kufanya kazi na hatimaye ni kifo,” alisema Bakari.
Alisema kuwa tatizo la minyoo linazidi kuwa kubwa kutokana na baadhi hata ya wahudumu wa afya kuumwa kutokana na kutotumia dawa za minyoo kutokana na kutotambua ukubwa wa tatizo hilo.
“Hata baadhi ya madaktari wameathiriwa na hali hiyo kutokana na kutoona kuwa minyoo ni tatizo lakini ukweli ni kwamba hili ni tatizo kubwa sana na inabidi wahudumu wa afya kulifuatilia kwa umakini ili kuwanusuru watu,” alisema Bakari.
Ofisa afya huyo ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye hospitali ya Tumbi iliyopo wilayani Kibaha alisema kuwa minyoo inapokuwa imekithiri mwilini hushambulia viungo mbalimbali vya ndani ya mwili na kuleta athari hizo.
“Ushauri ni kwamba madaktari wanapaswa kuwa makini kwa kuwashauri wagonjwa kutumia dawa za kuwaua wadudu hao kwa kujua kuwa endapo walishawahi kutumia dawa kwani watu wanafikiri minyoo ni kwa watoto pekee,” alisema Bakari.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MRADI mkubwa wa Maji wilayani Kibaha mkoani Pwani unatarajiwa kukamilika Agosti mwaka huu na kuondoa tatizo la ukosefu wa maji ambapo baadhi ya vitongoji wananchi wameanza kukimbia bili za maji.
Akizungumza na wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa uzinduzi wa matawi ya chamaa hicho Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema kuwa mara mradi huo utakapokamilika tatizo hilo itakuwa ni historia.
Koka alisema kuwa mradi huo wa maji ambao chanzo chake ni mto Ruvu utapitia kwenye mitaa yote ya Jimbo hilo ambapo kwa kipindi kirefu wananchi wamekuwa wakilalamika upatikanaji wa maji.
“Tunashukuru kuwa kwenye mradi uliotokea wilaya ya Bagamoyo baadhi ya mitaa ikiwemo ya Vikawe, Vikawe shule maji yanapatikana kwa wingi ambapo sasa watu wanakimbia bili kutokanana kushindwa kulipa kwani awali walikuwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa maji,” alisema Koka.
Alisema kwa sasa maji yamesambazwa kwenye mitaa 14 na mara mradi huo utakapokamilika wakazi wa Kibaha hawatanyanganyana maji na Jiji la Dar es Salaam ambao wanategemea chanzo kimoja hivyo maji kuwa ya mgao.
“Nawaomba msiwe na wasiwasi kwani mradi huo unaendelea vizuri ambapo kwa sasa wanatandaza mabomba ambayo kwa sasa yamefika eneo la Kongowe kilometa 10 kutoka hapa mjini hivyo Mungu akipenda wakati huo uliotajwa maji yatapatikana,” alisema Koka.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WANAWAKE wajawazito wilayani Kibaha mkoani Pwani wametakiwa kuacha kutumia dawa za kienyeji za kuongeza uchungu ili kupunguza vifo vya watoto wachanga.
Hayo yalisemwa na ofisa muuguzi wa kituo cha afya cha Mkoani, Prisca Nyambo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea kituo hicho hivi karibuni na kusema kuwa dawa hizo zianasababisha watoto kufia tumboni.
Nyambo alisema kuwa dawa hizo za kuongeza uchungu za kienyeji ni mbaya kwa watoto waliotumboni kwani wengi wamekuwa wakipoteza maisha.
“Tatizo la watoto kufia tumboni kwa sasa ni kubwa kutokana na wajawazito kutumia dawa hizo ili waweze kujifungua endapo muda umefika na hakuna dalili za kufanya hivyo,” alisema Nyambo.
Alisema kuwa wajawazito wanapaswa kwenda hospitali wanapoona muda wa kujifungua umefika lakini hawajifungui kuliko kutumia dawa hizo ambazo zinasabisha vifo vya watoto.
Aidha alisema vifo vya watoto wachanga ni kati ya saba na tisa kwa kila mwezi kutokana na sababu mbalimbali mojawapo ikiwa ni matumizi ya dawa hizo za kienyeji za kuongeza uchungu ambapo wastani wa wanawake wanaojifungua kwa kipindi hicho ni zaidi ya 300.
Alibainisha kuwa akinamama wajawazito wanaokwenda kujifungua hapo ni wengi kwani baadhi yao wanatoka maeneo ya Jiji la Dar es Salaam kama vile Mbezi, Kibamba, Kimara na Ilala kutokana na ukaribu.
Mwisho.




   

    

HABARI MOTOMOTO

Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA Cha Wasioona Nchini kimewataka vijana wenye ulemavu huo kuachana na dhana ya kuwa mara wamalizapo elimu mbalimbali ni laziwa waajiriwe badala yake wajiandae kwa kufanya shughuli za kujiajiri wenyewe.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na makamu mwenyekiti wa chama hicho Taifa Robert Bundala wakati wa mafunzo ya sera ya ajira kwa watu wenye ulemavu kwa vijana wanachama wa chama hicho wilayani Kibaha.
Bundala alisema kuwa soko la ajira kwa sasa ni gumu sana hivyo lazima vijana wajiwekee malengo ya kujiajiri wao wenyewe kupitia fursa zilizopo kwenye maeneo yao kuliko kusubiri kuajiriwa serikalini au sekta binafsi.
“Vijana wasioona wanapaswa kuachana na dhana hiyo badala yake wajiajiri kwa kupitia shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na ujasiriamali na si kutegemea kuajiriwa kwani upatikanaji wa ajira kwa sasa ni mgumu,” alisema Bundala.
Alisema kuwa ushindani wa soko la ajira hapa nchini kwa sasa ni mkubwa sana kwani hata watu wasiona na ulemavu wamekuwa wakilalamika hivyo lazima vijana hao watumie mafunzo mbalimbali wanayoyapata ili kujiajiri.
“Kwa sasa ubaguzi umepungua lakini kikubwa kinachoangaliwa ni uwezo wako wa kielimu kwani kwa wale wenye elimu nzuri wamepata ajira lakini lazima wabadili mfumo wa kusubiri ajira badala yake wajiajiri,” alisema Bundala ambaye ni mwalimu wa shule ya msingi.
Naye Mwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye naye ni mlemavu asiyeona Greyson Mlanga alisema kuwa ni vema vijana wakaangalia fursa za ajira zilizopo kwenye maeneo wanayoishi na kuwaondolea fikra kuwa lazima waajiriwe.
Mlanga alisema kuwa kutokana na ugumu wa ajira vijana wasioona wanapaswa kuangalia suala la kujiajiri kwani kutegemea ajira za kuajiriwa itakuwa ni vigumu sana kuweza kufanikiwa kujiletea maendeleo.
 Kwa upande wake moja ya washiriki wa mafunzo hayo Zuhura Omary alisema kuwa changamoto kwao ni nyingi kutokana na hali waliyonayo pia ni kutokana na kutokuwa na elimu ya kutosha hivyo kujikuta wakikosa ajira.
Mafunzo hayo yaliwahusisha vijana wasioona wapatao 60 kutoka kata nne za Misugusugu, Visiga, Kibaha na Kongowe na kufadhiliwa na The Foundation for Civil Society
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WANANCHI wametakiwa kuhakikisha wanazingatia matumizi ya dawa za minyoo kila baada ya miezi mitatu ili kuepukana na athari ikiwa ni pamoja na magonjwa ya Kisukari na Presha.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Ofisa afya Mstaafu Allice Bakari alipozungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa minyoo ni chanzo cha magonjwa hayo makubwa ambayo yanasababisha vifo.
Bakari alisema kuwa kutokana na watu kutotumia kabisa dawa za kuua minyoo kumesababisha watu kupata athari kubwa za kiafya kutokana na ulaji wa vyakula ambao husababisha watu kupata minyoo.
“Minyoo ni chanzo cha magonjwa mengi makubwa yakiwemo moyo kutanuka, kuchanganyikiwa, mba na baadhi ya viuongo vya ndani kuathirika na kushindwa kufanya kazi na hatimaye ni kifo,” alisema Bakari.
Alisema kuwa tatizo la minyoo linazidi kuwa kubwa kutokana na baadhi hata ya wahudumu wa afya kuumwa kutokana na kutotumia dawa za minyoo kutokana na kutotambua ukubwa wa tatizo hilo.
“Hata baadhi ya madaktari wameathiriwa na hali hiyo kutokana na kutoona kuwa minyoo ni tatizo lakini ukweli ni kwamba hili ni tatizo kubwa sana na inabidi wahudumu wa afya kulifuatilia kwa umakini ili kuwanusuru watu,” alisema Bakari.
Ofisa afya huyo ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye hospitali ya Tumbi iliyopo wilayani Kibaha alisema kuwa minyoo inapokuwa imekithiri mwilini hushambulia viungo mbalimbali vya ndani ya mwili na kuleta athari hizo.
“Ushauri ni kwamba madaktari wanapaswa kuwa makini kwa kuwashauri wagonjwa kutumia dawa za kuwaua wadudu hao kwa kujua kuwa endapo walishawahi kutumia dawa kwani watu wanafikiri minyoo ni kwa watoto pekee,” alisema Bakari.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MRADI mkubwa wa Maji wilayani Kibaha mkoani Pwani unatarajiwa kukamilika Agosti mwaka huu na kuondoa tatizo la ukosefu wa maji ambapo baadhi ya vitongoji wananchi wameanza kukimbia bili za maji.
Akizungumza na wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa uzinduzi wa matawi ya chamaa hicho Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema kuwa mara mradi huo utakapokamilika tatizo hilo itakuwa ni historia.
Koka alisema kuwa mradi huo wa maji ambao chanzo chake ni mto Ruvu utapitia kwenye mitaa yote ya Jimbo hilo ambapo kwa kipindi kirefu wananchi wamekuwa wakilalamika upatikanaji wa maji.
“Tunashukuru kuwa kwenye mradi uliotokea wilaya ya Bagamoyo baadhi ya mitaa ikiwemo ya Vikawe, Vikawe shule maji yanapatikana kwa wingi ambapo sasa watu wanakimbia bili kutokanana kushindwa kulipa kwani awali walikuwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa maji,” alisema Koka.
Alisema kwa sasa maji yamesambazwa kwenye mitaa 14 na mara mradi huo utakapokamilika wakazi wa Kibaha hawatanyanganyana maji na Jiji la Dar es Salaam ambao wanategemea chanzo kimoja hivyo maji kuwa ya mgao.
“Nawaomba msiwe na wasiwasi kwani mradi huo unaendelea vizuri ambapo kwa sasa wanatandaza mabomba ambayo kwa sasa yamefika eneo la Kongowe kilometa 10 kutoka hapa mjini hivyo Mungu akipenda wakati huo uliotajwa maji yatapatikana,” alisema Koka.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WANAWAKE wajawazito wilayani Kibaha mkoani Pwani wametakiwa kuacha kutumia dawa za kienyeji za kuongeza uchungu ili kupunguza vifo vya watoto wachanga.
Hayo yalisemwa na ofisa muuguzi wa kituo cha afya cha Mkoani, Prisca Nyambo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea kituo hicho hivi karibuni na kusema kuwa dawa hizo zianasababisha watoto kufia tumboni.
Nyambo alisema kuwa dawa hizo za kuongeza uchungu za kienyeji ni mbaya kwa watoto waliotumboni kwani wengi wamekuwa wakipoteza maisha.
“Tatizo la watoto kufia tumboni kwa sasa ni kubwa kutokana na wajawazito kutumia dawa hizo ili waweze kujifungua endapo muda umefika na hakuna dalili za kufanya hivyo,” alisema Nyambo.
Alisema kuwa wajawazito wanapaswa kwenda hospitali wanapoona muda wa kujifungua umefika lakini hawajifungui kuliko kutumia dawa hizo ambazo zinasabisha vifo vya watoto.
Aidha alisema vifo vya watoto wachanga ni kati ya saba na tisa kwa kila mwezi kutokana na sababu mbalimbali mojawapo ikiwa ni matumizi ya dawa hizo za kienyeji za kuongeza uchungu ambapo wastani wa wanawake wanaojifungua kwa kipindi hicho ni zaidi ya 300.
Alibainisha kuwa akinamama wajawazito wanaokwenda kujifungua hapo ni wengi kwani baadhi yao wanatoka maeneo ya Jiji la Dar es Salaam kama vile Mbezi, Kibamba, Kimara na Ilala kutokana na ukaribu.
Mwisho.