Wednesday, March 25, 2015

ABAKA WANAE KWA MIAKA MIWILI MFULULIZO

Na Mwandishi Wetu, Kibaha

MKAZI wa Miembe Saba wilayani Kibaha mkoani Pwani Said Kundum (52) anatuhumiwa kuwabaka watoto wake wawili wa kike kwa kipindi cha miaka miwili na kuwasababishia maumivu makali.

Akizungumza na waandishi wa habari mtoto mkubwa wa mtuhumiwa ambaye anasoma darasa la saba katika Shule ya Msingi ya Miembe Saba jina limehifadhiwa (15) alisema kuwa baba yake alikuwa akimbaka yeye na mdogo wake kwa nyakati tofauti.

Alisema kuwa baba yake alianza kumbaka tangu mwaka 2013 ambapo kwa kipindi chote hicho alipokuwa akiwafanyia vitendo hivyo aliwatishia kuwa atawaua endapo watasema kwa mtu yoyote.

“Baba alikuwa akitubaka kwa nyakati tofauti wakati mama akiwa anaenda sokoni Kariakoo kuuza mboga huku akituacha na baba nyumbani na kutufanyia vietendo hivyo mimi na mdogo wangu ambaye anasoma darasa la tatu shule ya Msingi Tandau akiwa na miaka (12),” alisema Mwanafunzi huyo.

Aidha alisema kuwa wakati wakifanyiwa vitendo hivyo walikuwa wakisikia maumivu makali lakini aliwaambia kuwa wajikaze kwani baadaye watazoea na hawata sikia tena maumivu.

“Tulivumilia kwa kipindi choete hicho lakini Jumamosi Machi 21 ilibidi ni mwambie mama na kusema potelea mbali liwalo na liwe kama ataniua basi lakini hatuwezi kuvumilia vitendo hivyo,” alisema mwanafunzi huyo.

Alibainisha baada ya kumwambia mama yao ilibidi atoe taarifa kwa viongozi wa serikali ya mtaa wa Miembe Saba ambao nao waliwataarifu polisi ambao walimkamata baba yake.

Naye mama mzazi wa watoto hao Rahima  Mshamu alisema kuwa yeye hakujua kinachoendelea kati ya mume wake na watoto wake kwani alikuwa akimuacha na watoto na hakutegemea kama angeweza kuwafanyia watoto wake vitendo hivyo vya ukatili.

Mshamu alisema tangu alipoona na mume wake amekuwa akifanya biashara ya kuuza mboga za majani ambazo huzikusanya nyakati za jioni hadi usiku kisha kuzipeleka sokoni Kariakoo Jijini Dar es Salaam.

“Mume wangu nilikuwa nikimuamini kama baba na sikutegemea kama angeweza kufanya hivyo na huwa nakusanya mboga kwenye maeneo mbalimbali huko mashambani majira ya saa 12 jioni baada ya hapo tunazisafirisha usiku kwenda Kariakoo ambapo kule huwa tunazifikisha usiku wa manane na ifikapo saa 11 alfajiri tunakuwa tumemaliza na tunaanza safari ya kurudi nyumbani,” alisema Mshamu.

Alisema kuwa hayo ndiyo maisha waliyokuwa wakiishi tangu walipohamia kutokea Kibamba mwaka 2012 ambapo kwa kiasi kikubwa yeye amekuwa akiiendesha familia hiyo kwani mume wake hana kazi maalumu.
“Roho inaniuma sana kwani nimekuwa nikihangaika kuhakikisha kuwa familia yangu haipati shida watoto wanakwenda shule na ana mtoto wake ambaye sijazaa naye yuko sekondari namlipia ada na michango mingine na mahitaji yote lakini mume wangu yeye haangaiki kwa chochote tukio hili limeniuma sana nashindwa hata kujizuia,” alisema huku akilia kwa uchungu.

Aidha alisema kuwa kutokana na kumpenda mume wake alimnunulia pikipiki kwa ajili ya kuongeza kipato cha familia lakini aliuza pikipiki hiyo jambo ambalo lilimfanya ashindwe kumwelewa kuwa ana tatizo gani lakini alishangazwa na afya za watoto wake kuumwa magonjwa UTI kila mara.

“Mimi na yeye hatukuwa na ugomvi wowote ambapo hivi karibuni alijaribu kuuza sehemu ya eneo letu na nilipomuuliza alikataa hadi yule mnunuzi alipokuja na kutaka kumalizia fedha zilizobaki ndipo niligundua kuwa aliuza eneo hilo kwa nguvu bila ridhaa yangu na kusema kuwa aliwabaka watoto kuwa tuna ugomvi wa eneo hilo si kweli kwani suala la eneo ni la mwezi Machi huku yeye akiwabaka watoto miaka miwili iliyopita,” alisema Mshamu.

Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa huo Hamis Shomary alisema kuwa baada ya kumhoji mtuhumiwa alikiri kufanya matukio hayo na kusema kuwa aliamua kufanya hivyo kutokana na ugomvi aliokuwa nao na mke wake na kuwa alikuwa akimnyima unyumba.

Shomary alisema kuwa mtuhumiwa alifikishwa polisi kwenye kituo cha Kongowe ambako anashikiliwa kwa hatua zaidi za kisheria ikiwa ni pamoja na kusubiri kupelekwa mahakamani.

Mwalimu mkuu wa shule ya Miembe Saba anayosoma mwanafunzi huyo Rajab Chalamila alisema kuwa mwanafunzi huyo alikuwa anaonekana mnyonge na mawazo mengi.

Chalamila alisema kuwa kutokana na hali ya mwanafunzi huyo alimwita baba mzazi zaidi ya mara mbili na kumwambia kuwa ampeleke hospitali mwanae na alisema alimpeleka na kukutwa na malaria lakini hali bado ilikuwa inajirudia na kuonekana kuwa ameathirika kisaikolojia. Jeshi la polisi limethibitisha kutokea kwa tukio hilo.  


Mwisho.

No comments:

Post a Comment