Na Mwandishi
Wetu, Kibaha
MKAZI wa
Miembe Saba wilayani Kibaha mkoani Pwani Said Kundum (52) anatuhumiwa kuwabaka
watoto wake wawili wa kike kwa kipindi cha miaka miwili na kuwasababishia
maumivu makali.
Akizungumza
na waandishi wa habari mtoto mkubwa wa mtuhumiwa ambaye anasoma darasa la saba
katika Shule ya Msingi ya Miembe Saba jina limehifadhiwa (15) alisema kuwa baba
yake alikuwa akimbaka yeye na mdogo wake kwa nyakati tofauti.
Alisema kuwa
baba yake alianza kumbaka tangu mwaka 2013 ambapo kwa kipindi chote hicho
alipokuwa akiwafanyia vitendo hivyo aliwatishia kuwa atawaua endapo watasema
kwa mtu yoyote.
“Baba
alikuwa akitubaka kwa nyakati tofauti wakati mama akiwa anaenda sokoni Kariakoo
kuuza mboga huku akituacha na baba nyumbani na kutufanyia vietendo hivyo mimi
na mdogo wangu ambaye anasoma darasa la tatu shule ya Msingi Tandau akiwa na
miaka (12),” alisema Mwanafunzi huyo.
Aidha alisema
kuwa wakati wakifanyiwa vitendo hivyo walikuwa wakisikia maumivu makali lakini
aliwaambia kuwa wajikaze kwani baadaye watazoea na hawata sikia tena maumivu.
“Tulivumilia
kwa kipindi choete hicho lakini Jumamosi Machi 21 ilibidi ni mwambie mama na
kusema potelea mbali liwalo na liwe kama ataniua basi lakini hatuwezi kuvumilia
vitendo hivyo,” alisema mwanafunzi huyo.
Alibainisha
baada ya kumwambia mama yao ilibidi atoe taarifa kwa viongozi wa serikali ya
mtaa wa Miembe Saba ambao nao waliwataarifu polisi ambao walimkamata baba yake.
Naye mama
mzazi wa watoto hao Rahima Mshamu
alisema kuwa yeye hakujua kinachoendelea kati ya mume wake na watoto wake kwani
alikuwa akimuacha na watoto na hakutegemea kama angeweza kuwafanyia watoto wake
vitendo hivyo vya ukatili.
Mshamu alisema
tangu alipoona na mume wake amekuwa akifanya biashara ya kuuza mboga za majani
ambazo huzikusanya nyakati za jioni hadi usiku kisha kuzipeleka sokoni Kariakoo
Jijini Dar es Salaam.
“Mume
wangu nilikuwa nikimuamini kama baba na sikutegemea kama angeweza kufanya hivyo
na huwa nakusanya mboga kwenye maeneo mbalimbali huko mashambani majira ya saa
12 jioni baada ya hapo tunazisafirisha usiku kwenda Kariakoo ambapo kule huwa
tunazifikisha usiku wa manane na ifikapo saa 11 alfajiri tunakuwa tumemaliza na
tunaanza safari ya kurudi nyumbani,” alisema Mshamu.
Alisema kuwa
hayo ndiyo maisha waliyokuwa wakiishi tangu walipohamia kutokea Kibamba mwaka
2012 ambapo kwa kiasi kikubwa yeye amekuwa akiiendesha familia hiyo kwani mume
wake hana kazi maalumu.
“Roho
inaniuma sana kwani nimekuwa nikihangaika kuhakikisha kuwa familia yangu
haipati shida watoto wanakwenda shule na ana mtoto wake ambaye sijazaa naye
yuko sekondari namlipia ada na michango mingine na mahitaji yote lakini mume
wangu yeye haangaiki kwa chochote tukio hili limeniuma sana nashindwa hata
kujizuia,” alisema huku akilia kwa uchungu.
Aidha alisema
kuwa kutokana na kumpenda mume wake alimnunulia pikipiki kwa ajili ya kuongeza
kipato cha familia lakini aliuza pikipiki hiyo jambo ambalo lilimfanya ashindwe
kumwelewa kuwa ana tatizo gani lakini alishangazwa na afya za watoto wake
kuumwa magonjwa UTI kila mara.
“Mimi na
yeye hatukuwa na ugomvi wowote ambapo hivi karibuni alijaribu kuuza sehemu ya
eneo letu na nilipomuuliza alikataa hadi yule mnunuzi alipokuja na kutaka
kumalizia fedha zilizobaki ndipo niligundua kuwa aliuza eneo hilo kwa nguvu
bila ridhaa yangu na kusema kuwa aliwabaka watoto kuwa tuna ugomvi wa eneo hilo
si kweli kwani suala la eneo ni la mwezi Machi huku yeye akiwabaka watoto miaka
miwili iliyopita,” alisema Mshamu.
Kwa upande
wake mwenyekiti wa mtaa huo Hamis Shomary alisema kuwa baada ya kumhoji
mtuhumiwa alikiri kufanya matukio hayo na kusema kuwa aliamua kufanya hivyo
kutokana na ugomvi aliokuwa nao na mke wake na kuwa alikuwa akimnyima unyumba.
Shomary alisema
kuwa mtuhumiwa alifikishwa polisi kwenye kituo cha Kongowe ambako anashikiliwa
kwa hatua zaidi za kisheria ikiwa ni pamoja na kusubiri kupelekwa mahakamani.
Mwalimu mkuu
wa shule ya Miembe Saba anayosoma mwanafunzi huyo Rajab Chalamila alisema kuwa
mwanafunzi huyo alikuwa anaonekana mnyonge na mawazo mengi.
Chalamila
alisema kuwa kutokana na hali ya mwanafunzi huyo alimwita baba mzazi zaidi ya
mara mbili na kumwambia kuwa ampeleke hospitali mwanae na alisema alimpeleka na
kukutwa na malaria lakini hali bado ilikuwa inajirudia na kuonekana kuwa
ameathirika kisaikolojia. Jeshi la polisi limethibitisha kutokea kwa tukio
hilo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment