Na John Gagarini,
Kibaha
CHAMA cha Waigizaji Tanzania
(TFDAA) mkoa wa Pwani kimetoa misaada mbalimbali kwa wagonjwa waliolazwa kwenye
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa huo ya Tumbi iliyopo wilayani Kibaha.
Misaada hiyo kwa ajili
ya wagonjwa ilitolewa na baadhi ya wasanii kwa lengo la kuwafariji ambapo
baadhi hawana ndugu wa kuwafariji.
Akizungumza na
waandishi wa habari mara baada ya kutoa misaada hiyo katibu wa chama hicho
mkoani Pwani Kadnas Nassir alisema kuwa misaada hiyo ni moja ya shughuli
zinazofanywa na kundi hilo.
“Wagonjwa ni wenzetu
na mtu yoyote anaweza kuumwa kwa hiyo tumeona umuhimu wa kuwasaidia misaada kama
sehemu ya kuwajibika kwetu na kuwafariji ili waone kuwa kuwa jamii ya sanaa
nayo iko nao katika hali walizonazo,” alisema Nassir.
Nassir alisema kuwa
misaada hiyo licha ya kwamba siyo mikubwa sana lakini ni faraja kwa wagonjwa
ambao waliwapatia sabuni, dawa za meno nguo za watoto pamoja na mafagio ya
usafi kwa hospitali hiyo pia walifanya usafi.
“Sisi mbali ya kutoa
burudani pia tunajukumu la kuisadia jamii katika masuala mbalimbali ikiwa ni
pamoja na kwenye matatizo na furaha,” alisema Nassir.
Naye moja ya wagonjwa
waliopatiwa msaada huo Beatrice Shirima alisema chama hicho kimeonyesha
ubinaadamu kwani baadhi ya watu wana uwezo lakini hawonyeshi kujali watu wenye
matatizo.
Kwa upande wake
muuguzi wa zamu wa hospitali hiyo ya Tumbi Felisia Mungulele misaada hiyo
imeleta faraja kubwa kwa wagonjwa na wameona kuwa jamii inawajali na watu
wengine wajitokeze kusaidia kama hivyo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment