Na John Gagarini, Kibaha
KIJANA Victor Wilfred (29) mkazi wa Keko amekatisha uhai wake kwa kujinyonga kwa kutumia kanga aliyoifunga kwenye dirisha la chumba cha rafiki yake.
Marehemu kabla ya kujinyonga aliacha ujumbe usemao kuwa anaomba samahani ndugu zake kwa kufanya kitendo hicho cha kujitoa uhai hata hivyo hakuweza kuweka wazi kwamba aliamua kujiua kwa sababu gani.
Tukio hilo lilitokea Aprili 30 mwaka huu majira ya asubuhi eneo la Maili Moja Shuleni wilayani Kibaha mkoani Pwani ambapo umati wa watu ulikuwa umejazana kushuhudia tukio hilo la kusikitisha.
Akithibitisha kutokea tukio hilo kamanda wa Polisi mkoani Pwani Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Ulrich Matei alisema kuwa tukio hilo ambalo lilitokea kwenye sebule ya chumba cha Emanuel Lawrance mkazi wa Keko Jijini Dar es Salaam ambaye amepangisha nyumba kwa Emanuel Msengi marehemu alikuwa mgeni kwenye nyumba hiyo na alifika kwa lengo la kutafuta kazi.
"Marehemu aliachwa na rafiki yake ambaye alikuwa amekwenda kazini na kwa kuwa rafiki yake alimuahidi kumtafutia kazi na aliporudi alikuta marehemu kajinyonga kwa kutumia kanga kwenye dirisha la chumba hicho," alisema Kamanda Matei
Hata hivyo marehemu aliacha ujumbe kwenye karatasi lililokutwa pembeni ya mwili wake kuwa kutokanana na kifo chake ana omba samahani na asisumbuliwe mtu yoyote kwani kaamua kujiua yeye mwenyewe.
mwisho.
Wednesday, April 30, 2014
SIMBA YANGA ZAPEWA SOMO
Na John Gagarini, Kibaha
TIMU za soka za Simba na Yanga zimetakiwa kujipanga ili ziweze kupata mafanikio kama ilivyo klabu ya Azam ambayo imepongezwa na Shirikisho la Soka la Miguu la Dunia (FIFA) kwa kuweza kuwa klabu ambayo imepata mafanikio kwa kipindi kifupi tangu kuanzishwa kwake.
Wito huo umetolewa na mdau wa soka wilayani Kibaha mkoani Pwani, Fahim Lardhi alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi na kusema kuwa Azam imeweza kuzipiku Simba na Yanga kwa mafanikio licha ya timu hizo kuanzishwa miaka zaidi ya 50 iliyopita.
Lardhi alisema kuwa Azam imeanzishwa miaka 9 iliyopita lakini imepata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kuwa na uwanja wa kisasa ambao una kidhi haja ya kuwa uwanja ambao unaweza kutumia na timu kubwa kama ilivyo kwa timu za Ulaya.
“Timu za Simba na Yanga zimebaki kuwa timu za malumbano tu badala ya kufikiria masuala ya kimaendeleo kama ilivyo kwa timu ya Azam ambayo ni timu changa katika ramani ya soka hapa nchini na hata barani Afrika,” alisema Lardhi.
Aidha alisema kuwa ili kuleta mafanikio kwenye timu lazima timu hizo zibadili mifumo ya wanachama ili wazichangie timu zao badala ya wao kutaka timu hizo ziwanufaishe hali ambayo inasababisha zishindwe kupata mafanikio.
“Inashangaza kuona timu hizo zinakosa viwanja jambo ambalo linatia aibu ambapo zimebaki kusema tu kuwa zitajenga viwanja matokeo yake yamebaki maneno tu ya kujenga viwanja vyao vya kisasa,” alisema Lardhi.
Alivitaka vilabu hivyo kuwa na mifumo kama ya ulaya ili viweze kupata maendeleo na kuachana na mifumo ambayo haina tija zaidi ya kuleta malumbano na kuzitaka zijifunze kupitia timu ya Azam ambayo inaendeshwa kitaalamu.
Na John Gagarini, Kibaha
MASHINDANO ya kutafuta timu ya wilaya ya Kibaha mkoani Pwani kwa Umoja wa Shule za Sekondari na Sanaa Tanzania (UMISSETA) yanatarajiwa kuanza kutimua vumbi Mei 3 mwaka huu.
Timu hiyo ambayo itaundwa na wachezaji 125 wa michezo mbalimbali inatarajiwa kuchuana kwenye uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha Tumbi ambapo kwa sasa timu hizo zinacheza ngazi ya Kanda ili kupata timu moja ya wilaya.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jana mjini Kibaha mratibu wa mashindano hayo Rajab Kauta alisema kuwa kwa sasa mashindano hayo ya kanda ndogo yanaendelea kwenye vituo vinne ambavyo ni Kibaha Sekondari, Kongowe, Tanita na Kilangalanga.
“Mashindano haya ya kanda ndogo yanshirikisha jumla ya 43 kutoka halmashauri ya Mji wa Kibaha na Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ambapo kila kituo kina wachezaji 125 na baada ya hapo watakutana kupata timu moja ya wilaya,” alisema Kauta
Kauta alisema kuwa michezo hiyo inachezwa kila Jumamosi ili kutoathiri masomo na mara bada ya kumalizika mashindano ya kanda ndogo ndipo wataunda timu moja ili kupata timu ya wilaya hiyo.
“Mashindano ya mkoa yatafanyika Bagamoyo kuanzia Mei 27 na tunaamini tutapata timu nzuri licha ya changamoto zilizojitokeza ikiwa ni pamoja na shule nyingi kutokuwa na viwanja vya michezo, viwanja vingi kujaa maji kutokana na mvua kubwa kunyesha, upungufu wa vifaa vya michezo ,” alisema Kauta.
Aliwaomba wadau kushirikiana na shule ili kusaidia kuboresha viwanja kwenye mashule pmaoja na upatikanaji wa vifaa ili kuweza kupata vijana wenye uwezo.
Mwisho.
TIMU za soka za Simba na Yanga zimetakiwa kujipanga ili ziweze kupata mafanikio kama ilivyo klabu ya Azam ambayo imepongezwa na Shirikisho la Soka la Miguu la Dunia (FIFA) kwa kuweza kuwa klabu ambayo imepata mafanikio kwa kipindi kifupi tangu kuanzishwa kwake.
Wito huo umetolewa na mdau wa soka wilayani Kibaha mkoani Pwani, Fahim Lardhi alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi na kusema kuwa Azam imeweza kuzipiku Simba na Yanga kwa mafanikio licha ya timu hizo kuanzishwa miaka zaidi ya 50 iliyopita.
Lardhi alisema kuwa Azam imeanzishwa miaka 9 iliyopita lakini imepata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kuwa na uwanja wa kisasa ambao una kidhi haja ya kuwa uwanja ambao unaweza kutumia na timu kubwa kama ilivyo kwa timu za Ulaya.
“Timu za Simba na Yanga zimebaki kuwa timu za malumbano tu badala ya kufikiria masuala ya kimaendeleo kama ilivyo kwa timu ya Azam ambayo ni timu changa katika ramani ya soka hapa nchini na hata barani Afrika,” alisema Lardhi.
Aidha alisema kuwa ili kuleta mafanikio kwenye timu lazima timu hizo zibadili mifumo ya wanachama ili wazichangie timu zao badala ya wao kutaka timu hizo ziwanufaishe hali ambayo inasababisha zishindwe kupata mafanikio.
“Inashangaza kuona timu hizo zinakosa viwanja jambo ambalo linatia aibu ambapo zimebaki kusema tu kuwa zitajenga viwanja matokeo yake yamebaki maneno tu ya kujenga viwanja vyao vya kisasa,” alisema Lardhi.
Alivitaka vilabu hivyo kuwa na mifumo kama ya ulaya ili viweze kupata maendeleo na kuachana na mifumo ambayo haina tija zaidi ya kuleta malumbano na kuzitaka zijifunze kupitia timu ya Azam ambayo inaendeshwa kitaalamu.
Na John Gagarini, Kibaha
MASHINDANO ya kutafuta timu ya wilaya ya Kibaha mkoani Pwani kwa Umoja wa Shule za Sekondari na Sanaa Tanzania (UMISSETA) yanatarajiwa kuanza kutimua vumbi Mei 3 mwaka huu.
Timu hiyo ambayo itaundwa na wachezaji 125 wa michezo mbalimbali inatarajiwa kuchuana kwenye uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha Tumbi ambapo kwa sasa timu hizo zinacheza ngazi ya Kanda ili kupata timu moja ya wilaya.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jana mjini Kibaha mratibu wa mashindano hayo Rajab Kauta alisema kuwa kwa sasa mashindano hayo ya kanda ndogo yanaendelea kwenye vituo vinne ambavyo ni Kibaha Sekondari, Kongowe, Tanita na Kilangalanga.
“Mashindano haya ya kanda ndogo yanshirikisha jumla ya 43 kutoka halmashauri ya Mji wa Kibaha na Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ambapo kila kituo kina wachezaji 125 na baada ya hapo watakutana kupata timu moja ya wilaya,” alisema Kauta
Kauta alisema kuwa michezo hiyo inachezwa kila Jumamosi ili kutoathiri masomo na mara bada ya kumalizika mashindano ya kanda ndogo ndipo wataunda timu moja ili kupata timu ya wilaya hiyo.
“Mashindano ya mkoa yatafanyika Bagamoyo kuanzia Mei 27 na tunaamini tutapata timu nzuri licha ya changamoto zilizojitokeza ikiwa ni pamoja na shule nyingi kutokuwa na viwanja vya michezo, viwanja vingi kujaa maji kutokana na mvua kubwa kunyesha, upungufu wa vifaa vya michezo ,” alisema Kauta.
Aliwaomba wadau kushirikiana na shule ili kusaidia kuboresha viwanja kwenye mashule pmaoja na upatikanaji wa vifaa ili kuweza kupata vijana wenye uwezo.
Mwisho.
Monday, April 28, 2014
AFA KWA MPENZI AKIJARIBU KUTOA MIMBA
Na John Gagarini, Kibaha
MWANAFUNZI wa Chuo cha Eden Hill (EDHICO) kilichopo mtaa wa KwaMfipa
wilayani Kibaha mkoani Pwani Attu Gabriel anayekadiriwa kuwa na umri
kati ya miaka (18) na (19) amekutwa amekufa kwenye nyumba ya mpenzi
wake kwa kile kinachodaiwa kutaka kutoa mimba.
Awali mwanafunzi huyo aliomba ruhusa kwenye uongozi wa chuo hicho
Jumanne ya wiki hii kuwa anakwenda kumuuguza ndugu yake ambaye alikuwa
amelazwa kwenye hospitali ya Amana Jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa mjumbe wa serikali ya mtaa wa Kwamfipa, Emanuel Kilasa
alisema kuwa tukio hilo limetokea jana majira kati ya saa 9 au 10
alfajiri nyumbani kwa mpenzi wake Hafidh Mohamed (22) ambaye alikimbia
mara baada ya tukio hilo.
Kilasa alisema kuwa marehemu alikutwa na mauti ambapo tangu alipoomba
ruhusa hiyo alikuwa kwa mpenzi wake jirani na chuo hicho na kujaribu
kutoa mimba lakini hakufanikiwa.
"Tulipoingia kwenye chumba cha mpenzi wake tulikuta kuna vitu kadhaa
zikiwemo vidonge, chipsi, sukari na inasadikiwa kuwa alikuwa akijaribu
kutoa mimba," alisema Kilasa.
Alisema kuwa mpenzi wa marehemu siku ya tukio alikwenda kwa mama yake
mzazi aitwaye Zaina Said na kumwambia kuwa alilala na mpenzi wake
lakini haamki.
"Mama yake alipofika alimwambia kuwa marehemu ameshakufa hivyo aende
akamwambie mwenyekiti wa serikali ya mtaa ndipo alipokimbia kutokana
na tukio hilo," alisema Kilasa.
Aidha alisem akuwa baada ya tukio hilo walitoa taarifa polisi ambapo
walifika na kuuchukua mwili wa marehemu ambaye alikuwa akiishi hosteli
nyumbani kwao ikiwa ni Makambako mkoani Iringa.
Naye baba mdogo wa kijana ambaye ni mpenzi wa marehemu Lukanda Omary
alisema kuwa yeye alipata taarifa majira ya saa 3 asubuhi lakini awali
kijana huyo alisemekana kabla ya kifo hicho alisikika akiongea na
daktari ambaye bado hajafahamika akimwambia ampe marehemu chai.
"Inasemekana marehemu alikuwa akijaribu kutoa mimba lakini hali ikawa
mbaya na kujaribu kuwasiliana na daktari juu ya nini cha kufanya hivyo
inavyoonekana binti huyo alikuwa kwenye zoezi la utoaji mimba,"
alisema Omary.
Kwa upande wake Kamanda wa polisi mkoani Pwani Kamishna Msaidizi wa
Polisi (SACP) Ulrich Matei alithibitisha kutokea tukio hilo na kusema
kuwa bado yuko hospitali ili kufanya uchunguzi kujua chanzo cha kifo
chake.
mwisho.
MWANAFUNZI wa Chuo cha Eden Hill (EDHICO) kilichopo mtaa wa KwaMfipa
wilayani Kibaha mkoani Pwani Attu Gabriel anayekadiriwa kuwa na umri
kati ya miaka (18) na (19) amekutwa amekufa kwenye nyumba ya mpenzi
wake kwa kile kinachodaiwa kutaka kutoa mimba.
Awali mwanafunzi huyo aliomba ruhusa kwenye uongozi wa chuo hicho
Jumanne ya wiki hii kuwa anakwenda kumuuguza ndugu yake ambaye alikuwa
amelazwa kwenye hospitali ya Amana Jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa mjumbe wa serikali ya mtaa wa Kwamfipa, Emanuel Kilasa
alisema kuwa tukio hilo limetokea jana majira kati ya saa 9 au 10
alfajiri nyumbani kwa mpenzi wake Hafidh Mohamed (22) ambaye alikimbia
mara baada ya tukio hilo.
Kilasa alisema kuwa marehemu alikutwa na mauti ambapo tangu alipoomba
ruhusa hiyo alikuwa kwa mpenzi wake jirani na chuo hicho na kujaribu
kutoa mimba lakini hakufanikiwa.
"Tulipoingia kwenye chumba cha mpenzi wake tulikuta kuna vitu kadhaa
zikiwemo vidonge, chipsi, sukari na inasadikiwa kuwa alikuwa akijaribu
kutoa mimba," alisema Kilasa.
Alisema kuwa mpenzi wa marehemu siku ya tukio alikwenda kwa mama yake
mzazi aitwaye Zaina Said na kumwambia kuwa alilala na mpenzi wake
lakini haamki.
"Mama yake alipofika alimwambia kuwa marehemu ameshakufa hivyo aende
akamwambie mwenyekiti wa serikali ya mtaa ndipo alipokimbia kutokana
na tukio hilo," alisema Kilasa.
Aidha alisem akuwa baada ya tukio hilo walitoa taarifa polisi ambapo
walifika na kuuchukua mwili wa marehemu ambaye alikuwa akiishi hosteli
nyumbani kwao ikiwa ni Makambako mkoani Iringa.
Naye baba mdogo wa kijana ambaye ni mpenzi wa marehemu Lukanda Omary
alisema kuwa yeye alipata taarifa majira ya saa 3 asubuhi lakini awali
kijana huyo alisemekana kabla ya kifo hicho alisikika akiongea na
daktari ambaye bado hajafahamika akimwambia ampe marehemu chai.
"Inasemekana marehemu alikuwa akijaribu kutoa mimba lakini hali ikawa
mbaya na kujaribu kuwasiliana na daktari juu ya nini cha kufanya hivyo
inavyoonekana binti huyo alikuwa kwenye zoezi la utoaji mimba,"
alisema Omary.
Kwa upande wake Kamanda wa polisi mkoani Pwani Kamishna Msaidizi wa
Polisi (SACP) Ulrich Matei alithibitisha kutokea tukio hilo na kusema
kuwa bado yuko hospitali ili kufanya uchunguzi kujua chanzo cha kifo
chake.
mwisho.
AFA KWA KUVUTWA SEHEMU ZA SIRI NA MKEWE
Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la Polisi mkoani Pwani linamshikilia Husna Iddi (16) mkazi wa
Tarafa ya Vikindu kata ya Kisemvule wilaya ya mkuranga mkoani Pwani ka
tuhuma za kusababisha mauaji ya mumewe baada ya kudaiwa kumvuta sehemu
zake za siri.
Inadaiwa kuwa wanandoa hao walikuwa na ugomvi wa kimapenzi hali
iliyosababisha ugomvi kati yao hali iliyosababisha kutokea kwa tukio
hilo la kusikitisha.
Kwa mujibu wa kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msaidizi
Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ulrich Matei alithibitisha kutokea kwa
tukio hilo na alimtaja marehemu kuwa ni Jumanne Mwarami (21).
Kamanda Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Aprili 24 mwaka huu
majira ya saa 2:00 usiku ambapo wakiwa nyumbani na mke wake
kulijitokeza ugomvi kati yao kwa marehemu kumtuhumu mke wake huyo kuwa
siyo mwaminifu katika ndoa yao na ana mahusiano na wanaume wengine
nje.
"Baada ya kutokuwepo kwa maelewano kati yao na ugomvi huo kuwa mkubwa
ndipo mke wake huyo alimshambulia na kumvuta mume wake sehemu zake za
siri hali iliyopelekea kupoteza maisha wakati akipatiwa matibabu
kwenye Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga," alisema Kamanda Matei.
Katika hatua nyingine,Jeshi la Polisi linawashikilia watu watatu kwa
kosa la kukutwa na bangi nusu kilo huko kitongoji cha Mwandege Wilaya
ya Mkuranga.
Watuhumiwa hao ni Seleman Sahdi Ngota (35), KasimuOmari Mlumbita (25)
na Salumu Yusufu Athumani ambao watafikishwa mahakamani mara upelelezi
utakapokamilika.
Mwisho.
JESHI la Polisi mkoani Pwani linamshikilia Husna Iddi (16) mkazi wa
Tarafa ya Vikindu kata ya Kisemvule wilaya ya mkuranga mkoani Pwani ka
tuhuma za kusababisha mauaji ya mumewe baada ya kudaiwa kumvuta sehemu
zake za siri.
Inadaiwa kuwa wanandoa hao walikuwa na ugomvi wa kimapenzi hali
iliyosababisha ugomvi kati yao hali iliyosababisha kutokea kwa tukio
hilo la kusikitisha.
Kwa mujibu wa kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msaidizi
Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ulrich Matei alithibitisha kutokea kwa
tukio hilo na alimtaja marehemu kuwa ni Jumanne Mwarami (21).
Kamanda Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Aprili 24 mwaka huu
majira ya saa 2:00 usiku ambapo wakiwa nyumbani na mke wake
kulijitokeza ugomvi kati yao kwa marehemu kumtuhumu mke wake huyo kuwa
siyo mwaminifu katika ndoa yao na ana mahusiano na wanaume wengine
nje.
"Baada ya kutokuwepo kwa maelewano kati yao na ugomvi huo kuwa mkubwa
ndipo mke wake huyo alimshambulia na kumvuta mume wake sehemu zake za
siri hali iliyopelekea kupoteza maisha wakati akipatiwa matibabu
kwenye Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga," alisema Kamanda Matei.
Katika hatua nyingine,Jeshi la Polisi linawashikilia watu watatu kwa
kosa la kukutwa na bangi nusu kilo huko kitongoji cha Mwandege Wilaya
ya Mkuranga.
Watuhumiwa hao ni Seleman Sahdi Ngota (35), KasimuOmari Mlumbita (25)
na Salumu Yusufu Athumani ambao watafikishwa mahakamani mara upelelezi
utakapokamilika.
Mwisho.
story pwani
John Gagarini, Bagamoyo
KITONGOJI cha Biga kata ya Mkange wilayani Bagamoyo mkoani Pwani ambacho kilikumbwa na mafuriko hivi karibuni kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha hapa nchini kimeomba serikali kuwapatia mbegu za mahindi tani 2.5 kwa ajili ya kupanda tena zao hilo.
Ombi hilo limekuja baada ya hekari 510 za wakazi wa kitongoji hicho kusombwa na maji ya mvua ambazo zilinyesha kabla ya mvua kubwa za mafuriko kunyesha hivi karibuni ambapo kilizungukwa na maji na kuwafanya wakazi wengine kupewa hifadhi ya muda.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi diwani wa kata hiyo ya Mkange Abdala Mwendadi alisema kuwa mazao ya wakazi hao yote yalisombwa na maji hali ambayo itasababisha kitongoji hicho kuwa hatarini kukumbwa na njaa.
"Kutokana na hali hiyo wakazi wa kitongoji hicho wanaomba serikali iwapatie mbegu kwa ajili ya kupanda mahindi mara mvua hizi zitakapokwisha ambapo msimu huo mahindi yake huitwa "Mahindi ya Kitopeni" ambayo hupandwa baada ya mvua kwisha mwezi Mei kiloa mwaka," alisema Mwindadi.
Mwindadi alisema kuwa jumla ya kaya 63 zimeathiriwa na mvua hizo ambapo zaidi ya watu 200 wameathirika hivyo kuwafanya kuhama kwenye maeneo hayo na kwenda kwa ndugu jamaa kwa ajili ya hifadhi.
"Wakazi wengi waliokumbwa na mafuriko hayo ni wale waliokuwa wakiishi kwenye mkondo wa maji ambapo kutokana na mvua hizo kumechangia kukumbwa na mafuriko hayo ambayo yamesomba mazao yote yaliyopandwa msimu wa kilimo," alisema Mwindadi.
Aidha diwani huyo wa kata ya Mkange alisema kuwa kutokana na maombi hayo atayapeleka halmashauri ili hatua za kuwasaidia zianze kwani endapo hawatapata msaada huo hali ya chakula kwenye kitongoji hicho itakuwa mbaya.
mwisho.
Na John Gagarini, Bagamoyo
MWENYEKITI wa Kijiji cha Kinzagu William Makumu ameshangzwa na wawekezaji kwenye kijiji hicho kushindwa kuchangia maendeleo hasa kwenye sekta ya barabara kutokana na kuingiza magari makubwa kwa ajili ya kubeba kokoto.
Alisema kuwa kuna wawekezaji wengi ambao wamewekeza kwenye uchimbaji kokoto ambazo zinatumika kwa ajili ya ujenzi wa nyumba na barabara hasa Jijini Dar es Salaam.
Makumu alisema kuwa uwekezaji mkubwa kijijini hapo ni uchimbaji wa kokoto kutokana na kijiji hicho kuzungukwa na milima ya mawe.
"Wamekuwa wakiingiza mamilioni ya fedha kwa ajili ya uchimbaji wa kokoto ambapo magari makubwa ambayo yanafikia hadi uzito wa tani 30 hutumia barabara za kijiji lakini hawazikarabati licha ya wao kufanya uharibifu mkubwa," alisema Mukamu.
Alisema kuwa kabla ya kupewa maeneo kwa ajili ya kuendeshea shughuli zao huomba kupitia mkutano wa Kijiji ambapo hutakiwa kutoa asilimia fulani kutokana na mapato yao pia hutakiwa kutoa nguvu zao kwa ajili ya kufanya kazi za maendeleo.
"Tatizo wao wamekuwa wakiangalia upande wao mfano ni eneo la barabara ambazo zimeharibika sana kutokana na wao kuingiza magari yao ya kubebea kokoto lakini hawako tayari kuzitengeneza licha ya kuwa wao ndiyo watumiaji wakubwa kwa ajili ya kupitisha kokoto kwenda maeneo mengine," alisema Mukamu.
Alibainisha kuwa uchangiaji wa wawekezaji hao ni mdogo sana ikilinganishwa na mapato wanayoyapata na athari wanazoziacha baada ya kupasua mawe kwenye kijiji hicho.
Aliwataka wawekezaji hao kujitahidi kuheshimu mikataba waliyoingia ya kuisadia jamii inayowazunguka ambayo ndiyo iliyowapa ardhi wanayoitumia kwa uwekezaji wao.
mwisho.
Na John Gagarini, Chalinze
HUKU Tarafa ya Chalinze ikiwa kwenye maombi ya kupatiwa wilaya kata ya Bwiringu wilayani Bagamoyo inaendelea na mchakato wa kuhakikisha kuwa inapata nafasi ya kuwa makao makuu ya wilaya hiyo yanakuwa hapo.
Moja ya mambo waliyofanya ni pamoja na kugawa viwanja zaidi ya 11,000 kwa ajili ya makazi na huduma za kijamii kwa wakazi wa kata hiyo iliyopo katikati ya mji huo wa Chalinze.
Hivi karibuni kupitia baraza la Madiwani lilipitisha mpango wa tarafa hiyo kuwa wilaya ambapo suala hilo bado liko kwenye mchakato kwa kupeleka maombi hayo kwenye ngazi husika.
Akizungumza mjini Chalinze diwani wa kata hiyo Nasa Karama alisema kuwa wao wako tayari kufanya hivyo na kuwa makao makuu ya wilaya mpya mara maombi hayo yakapopitishwa na wizara husika.
Karama alisema kuwa moja ya mambo waliyoyafanya kuhakikisha wanapata nafasi hiyo ya kuwa makao makuu ya wilaya ni pamoja na kugawa viwanja hivyo.
"Tumegawa viwanja hivyo kwa kushirikiana na halmashauri ili kuupanga mji wetu uwe kwenye mandhari nzuri na kuepukana na ujenzi holela usiozingatia ramani za mipangomiji," alisema Karama.
Alisema kuwa viwanja hivyo vimetolewa kwa wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo kwenye vijiji vya Mbala, Kibiki na Koo lengo kubwa ikiwa ni kuondokana na ujenzi holela.
"Baadhi ya wadau waliopewa viwanja hivyo tayari wameanza ujenzi huku wengine wakiendelea na michakato ya kuendeleza maeneo yao baadhi yao ni NSSF, wanaotaka kujenga soko la kisasa wakiwa kwenye hatua ya tathmini, ujenzi wa nyumba za watumishi, tume ya utumishi wa umma, ofisi ya Mbunge, TAKUKURU, benki na kituo cha polisi," alisema Nasa.
Aidha alisema kuwa wametoa fidia ya shilingi milioni 98 kwa wananchi kutokana na kuchukua maeneo yao kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya maendeleo.
mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
HOSPITALI Teule ya Rufaa ya mkoa wa Pwani Tumbi imesisitiza kuwa haiuzi damu kama baadhi ya watu wanavyodai kwani hilo ni kosa kisheria.
Akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea hospitali hiyo wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari wa mkoa wa Pwani juu ya hali tete na migogoro iliyoandaliwa na Baraza la habari Tanzania (MCT), mkuu wa kitengo cha maabara Boaz Motto alisema kuwa sera ya afya hairuhusu uuzaji wa damu.
Motto alisema kuwa utaratibu unaonyesha kuwa mgonjwa akipewa damu anapaswa kurejesha ili wagonjwa wengine nao waweze kupata damu wanapokuwa wanahitaji.
"Tatizo huwa linakuwa ni kwa wanafamilia ambapo wanapoambiwa wachangie damu baadhi yao huwa wanashindwa hali ambayo inasababisha kutafuta watu na kuwaomba damu lakini kwa makubaliano ya kuwalipa fedha," alisema Motto.
Alisema kuwa mapatano ya kuuziana damu hayafanyiki hospitalini bali ni makubaliano ya watoa damu na wenye mgonjwa lakini hospitali hutoa damu bure bila ya malipo lakini sharti ni kwamba wenye mgonjwa nao watoe damu ili itumike kwa wengine.
"Hii dhana ya damu kuuzwa imeenea sana lakini sera ya afya hairuhusu hospitali kuuza damu kwa mgonjwa bali ni kwa wanandugu kumtolea damu ambapo watu huwanunua watoa damu na wakifika hospitali hudai kuwa ni ndugu," alisema Motto.
Alisema kuwa kwa sasa hospitali ina damu ya kutosha na haina upungufu ambapo kuna uniti 150 ambazo watu hujitolea kama vile taasisi za jeshi, watu binafsi, wanafunzi na makundi mbalimbali ndani ya jamii.
"Changamoto tuliyonayo ni vipimo vya damu ambapo hutubidi kupeleka kwenye hospitali ya Muhimbili kwa ajili ya kupimwa kujua ubora wake ili iweze kutumika kwa wagonjwa wanaohitaji damu," alisema Motto.
Aidha alisema kuwa magonjwa yanayoongoza ni pamoja na yale ya msimu wa mvua kama vile kichocho, malaria na minyoo ambapo mazalia yake ni kwenye maji huku wakati wa kiangazi magonjwa ni yale ya kifua kikuu, kukohoa na malaria.
mwisho.
KITONGOJI cha Biga kata ya Mkange wilayani Bagamoyo mkoani Pwani ambacho kilikumbwa na mafuriko hivi karibuni kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha hapa nchini kimeomba serikali kuwapatia mbegu za mahindi tani 2.5 kwa ajili ya kupanda tena zao hilo.
Ombi hilo limekuja baada ya hekari 510 za wakazi wa kitongoji hicho kusombwa na maji ya mvua ambazo zilinyesha kabla ya mvua kubwa za mafuriko kunyesha hivi karibuni ambapo kilizungukwa na maji na kuwafanya wakazi wengine kupewa hifadhi ya muda.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi diwani wa kata hiyo ya Mkange Abdala Mwendadi alisema kuwa mazao ya wakazi hao yote yalisombwa na maji hali ambayo itasababisha kitongoji hicho kuwa hatarini kukumbwa na njaa.
"Kutokana na hali hiyo wakazi wa kitongoji hicho wanaomba serikali iwapatie mbegu kwa ajili ya kupanda mahindi mara mvua hizi zitakapokwisha ambapo msimu huo mahindi yake huitwa "Mahindi ya Kitopeni" ambayo hupandwa baada ya mvua kwisha mwezi Mei kiloa mwaka," alisema Mwindadi.
Mwindadi alisema kuwa jumla ya kaya 63 zimeathiriwa na mvua hizo ambapo zaidi ya watu 200 wameathirika hivyo kuwafanya kuhama kwenye maeneo hayo na kwenda kwa ndugu jamaa kwa ajili ya hifadhi.
"Wakazi wengi waliokumbwa na mafuriko hayo ni wale waliokuwa wakiishi kwenye mkondo wa maji ambapo kutokana na mvua hizo kumechangia kukumbwa na mafuriko hayo ambayo yamesomba mazao yote yaliyopandwa msimu wa kilimo," alisema Mwindadi.
Aidha diwani huyo wa kata ya Mkange alisema kuwa kutokana na maombi hayo atayapeleka halmashauri ili hatua za kuwasaidia zianze kwani endapo hawatapata msaada huo hali ya chakula kwenye kitongoji hicho itakuwa mbaya.
mwisho.
Na John Gagarini, Bagamoyo
MWENYEKITI wa Kijiji cha Kinzagu William Makumu ameshangzwa na wawekezaji kwenye kijiji hicho kushindwa kuchangia maendeleo hasa kwenye sekta ya barabara kutokana na kuingiza magari makubwa kwa ajili ya kubeba kokoto.
Alisema kuwa kuna wawekezaji wengi ambao wamewekeza kwenye uchimbaji kokoto ambazo zinatumika kwa ajili ya ujenzi wa nyumba na barabara hasa Jijini Dar es Salaam.
Makumu alisema kuwa uwekezaji mkubwa kijijini hapo ni uchimbaji wa kokoto kutokana na kijiji hicho kuzungukwa na milima ya mawe.
"Wamekuwa wakiingiza mamilioni ya fedha kwa ajili ya uchimbaji wa kokoto ambapo magari makubwa ambayo yanafikia hadi uzito wa tani 30 hutumia barabara za kijiji lakini hawazikarabati licha ya wao kufanya uharibifu mkubwa," alisema Mukamu.
Alisema kuwa kabla ya kupewa maeneo kwa ajili ya kuendeshea shughuli zao huomba kupitia mkutano wa Kijiji ambapo hutakiwa kutoa asilimia fulani kutokana na mapato yao pia hutakiwa kutoa nguvu zao kwa ajili ya kufanya kazi za maendeleo.
"Tatizo wao wamekuwa wakiangalia upande wao mfano ni eneo la barabara ambazo zimeharibika sana kutokana na wao kuingiza magari yao ya kubebea kokoto lakini hawako tayari kuzitengeneza licha ya kuwa wao ndiyo watumiaji wakubwa kwa ajili ya kupitisha kokoto kwenda maeneo mengine," alisema Mukamu.
Alibainisha kuwa uchangiaji wa wawekezaji hao ni mdogo sana ikilinganishwa na mapato wanayoyapata na athari wanazoziacha baada ya kupasua mawe kwenye kijiji hicho.
Aliwataka wawekezaji hao kujitahidi kuheshimu mikataba waliyoingia ya kuisadia jamii inayowazunguka ambayo ndiyo iliyowapa ardhi wanayoitumia kwa uwekezaji wao.
mwisho.
Na John Gagarini, Chalinze
HUKU Tarafa ya Chalinze ikiwa kwenye maombi ya kupatiwa wilaya kata ya Bwiringu wilayani Bagamoyo inaendelea na mchakato wa kuhakikisha kuwa inapata nafasi ya kuwa makao makuu ya wilaya hiyo yanakuwa hapo.
Moja ya mambo waliyofanya ni pamoja na kugawa viwanja zaidi ya 11,000 kwa ajili ya makazi na huduma za kijamii kwa wakazi wa kata hiyo iliyopo katikati ya mji huo wa Chalinze.
Hivi karibuni kupitia baraza la Madiwani lilipitisha mpango wa tarafa hiyo kuwa wilaya ambapo suala hilo bado liko kwenye mchakato kwa kupeleka maombi hayo kwenye ngazi husika.
Akizungumza mjini Chalinze diwani wa kata hiyo Nasa Karama alisema kuwa wao wako tayari kufanya hivyo na kuwa makao makuu ya wilaya mpya mara maombi hayo yakapopitishwa na wizara husika.
Karama alisema kuwa moja ya mambo waliyoyafanya kuhakikisha wanapata nafasi hiyo ya kuwa makao makuu ya wilaya ni pamoja na kugawa viwanja hivyo.
"Tumegawa viwanja hivyo kwa kushirikiana na halmashauri ili kuupanga mji wetu uwe kwenye mandhari nzuri na kuepukana na ujenzi holela usiozingatia ramani za mipangomiji," alisema Karama.
Alisema kuwa viwanja hivyo vimetolewa kwa wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo kwenye vijiji vya Mbala, Kibiki na Koo lengo kubwa ikiwa ni kuondokana na ujenzi holela.
"Baadhi ya wadau waliopewa viwanja hivyo tayari wameanza ujenzi huku wengine wakiendelea na michakato ya kuendeleza maeneo yao baadhi yao ni NSSF, wanaotaka kujenga soko la kisasa wakiwa kwenye hatua ya tathmini, ujenzi wa nyumba za watumishi, tume ya utumishi wa umma, ofisi ya Mbunge, TAKUKURU, benki na kituo cha polisi," alisema Nasa.
Aidha alisema kuwa wametoa fidia ya shilingi milioni 98 kwa wananchi kutokana na kuchukua maeneo yao kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya maendeleo.
mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
HOSPITALI Teule ya Rufaa ya mkoa wa Pwani Tumbi imesisitiza kuwa haiuzi damu kama baadhi ya watu wanavyodai kwani hilo ni kosa kisheria.
Akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea hospitali hiyo wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari wa mkoa wa Pwani juu ya hali tete na migogoro iliyoandaliwa na Baraza la habari Tanzania (MCT), mkuu wa kitengo cha maabara Boaz Motto alisema kuwa sera ya afya hairuhusu uuzaji wa damu.
Motto alisema kuwa utaratibu unaonyesha kuwa mgonjwa akipewa damu anapaswa kurejesha ili wagonjwa wengine nao waweze kupata damu wanapokuwa wanahitaji.
"Tatizo huwa linakuwa ni kwa wanafamilia ambapo wanapoambiwa wachangie damu baadhi yao huwa wanashindwa hali ambayo inasababisha kutafuta watu na kuwaomba damu lakini kwa makubaliano ya kuwalipa fedha," alisema Motto.
Alisema kuwa mapatano ya kuuziana damu hayafanyiki hospitalini bali ni makubaliano ya watoa damu na wenye mgonjwa lakini hospitali hutoa damu bure bila ya malipo lakini sharti ni kwamba wenye mgonjwa nao watoe damu ili itumike kwa wengine.
"Hii dhana ya damu kuuzwa imeenea sana lakini sera ya afya hairuhusu hospitali kuuza damu kwa mgonjwa bali ni kwa wanandugu kumtolea damu ambapo watu huwanunua watoa damu na wakifika hospitali hudai kuwa ni ndugu," alisema Motto.
Alisema kuwa kwa sasa hospitali ina damu ya kutosha na haina upungufu ambapo kuna uniti 150 ambazo watu hujitolea kama vile taasisi za jeshi, watu binafsi, wanafunzi na makundi mbalimbali ndani ya jamii.
"Changamoto tuliyonayo ni vipimo vya damu ambapo hutubidi kupeleka kwenye hospitali ya Muhimbili kwa ajili ya kupimwa kujua ubora wake ili iweze kutumika kwa wagonjwa wanaohitaji damu," alisema Motto.
Aidha alisema kuwa magonjwa yanayoongoza ni pamoja na yale ya msimu wa mvua kama vile kichocho, malaria na minyoo ambapo mazalia yake ni kwenye maji huku wakati wa kiangazi magonjwa ni yale ya kifua kikuu, kukohoa na malaria.
mwisho.
Wednesday, April 23, 2014
HABARI MCHANGANYIKO
John Gagarini, Bagamoyo
KITONGOJI cha Biga kata ya Mkange wilayani Bagamoyo mkoani Pwani ambacho kilikumbwa na mafuriko hivi karibuni kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha hapa nchini kimeomba serikali kuwapatia mbegu za mahindi tani 2.5 kwa ajili ya kupanda tena zao hilo.
Ombi hilo limekuja baada ya hekari 510 za wakazi wa kitongoji hicho kusombwa na maji ya mvua ambazo zilinyesha kabla ya mvua kubwa za mafuriko kunyesha hivi karibuni ambapo kilizungukwa na maji na kuwafanya wakazi wengine kupewa hifadhi ya muda.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi diwani wa kata hiyo ya Mkange Abdala Mwendadi alisema kuwa mazao ya wakazi hao yote yalisombwa na maji hali ambayo itasababisha kitongoji hicho kuwa hatarini kukumbwa na njaa.
"Kutokana na hali hiyo wakazi wa kitongoji hicho wanaomba serikali iwapatie mbegu kwa ajili ya kupanda mahindi mara mvua hizi zitakapokwisha ambapo msimu huo mahindi yake huitwa "Mahindi ya Kitopeni" ambayo hupandwa baada ya mvua kwisha mwezi Mei kiloa mwaka," alisema Mwindadi.
Mwindadi alisema kuwa jumla ya kaya 63 zimeathiriwa na mvua hizo ambapo zaidi ya watu 200 wameathirika hivyo kuwafanya kuhama kwenye maeneo hayo na kwenda kwa ndugu jamaa kwa ajili ya hifadhi.
"Wakazi wengi waliokumbwa na mafuriko hayo ni wale waliokuwa wakiishi kwenye mkondo wa maji ambapo kutokana na mvua hizo kumechangia kukumbwa na mafuriko hayo ambayo yamesomba mazao yote yaliyopandwa msimu wa kilimo," alisema Mwindadi.
Aidha diwani huyo wa kata ya Mkange alisema kuwa kutokana na maombi hayo atayapeleka halmashauri ili hatua za kuwasaidia zianze kwani endapo hawatapata msaada huo hali ya chakula kwenye kitongoji hicho itakuwa mbaya.
mwisho.
Na John Gagarini, Bagamoyo
MWENYEKITI wa Kijiji cha Kinzagu William Makumu ameshangzwa na wawekezaji kwenye kijiji hicho kushindwa kuchangia maendeleo hasa kwenye sekta ya barabara kutokana na kuingiza magari makubwa kwa ajili ya kubeba kokoto.
Alisema kuwa kuna wawekezaji wengi ambao wamewekeza kwenye uchimbaji kokoto ambazo zinatumika kwa ajili ya ujenzi wa nyumba na barabara hasa Jijini Dar es Salaam.
Makumu alisema kuwa uwekezaji mkubwa kijijini hapo ni uchimbaji wa kokoto kutokana na kijiji hicho kuzungukwa na milima ya mawe.
"Wamekuwa wakiingiza mamilioni ya fedha kwa ajili ya uchimbaji wa kokoto ambapo magari makubwa ambayo yanafikia hadi uzito wa tani 30 hutumia barabara za kijiji lakini hawazikarabati licha ya wao kufanya uharibifu mkubwa," alisema Mukamu.
Alisema kuwa kabla ya kupewa maeneo kwa ajili ya kuendeshea shughuli zao huomba kupitia mkutano wa Kijiji ambapo hutakiwa kutoa asilimia fulani kutokana na mapato yao pia hutakiwa kutoa nguvu zao kwa ajili ya kufanya kazi za maendeleo.
"Tatizo wao wamekuwa wakiangalia upande wao mfano ni eneo la barabara ambazo zimeharibika sana kutokana na wao kuingiza magari yao ya kubebea kokoto lakini hawako tayari kuzitengeneza licha ya kuwa wao ndiyo watumiaji wakubwa kwa ajili ya kupitisha kokoto kwenda maeneo mengine," alisema Mukamu.
Alibainisha kuwa uchangiaji wa wawekezaji hao ni mdogo sana ikilinganishwa na mapato wanayoyapata na athari wanazoziacha baada ya kupasua mawe kwenye kijiji hicho.
Aliwataka wawekezaji hao kujitahidi kuheshimu mikataba waliyoingia ya kuisadia jamii inayowazunguka ambayo ndiyo iliyowapa ardhi wanayoitumia kwa uwekezaji wao.
mwisho.
Na John Gagarini, Chalinze
HUKU Tarafa ya Chalinze ikiwa kwenye maombi ya kupatiwa wilaya kata ya Bwiringu wilayani Bagamoyo inaendelea na mchakato wa kuhakikisha kuwa inapata nafasi ya kuwa makao makuu ya wilaya hiyo yanakuwa hapo.
Moja ya mambo waliyofanya ni pamoja na kugawa viwanja zaidi ya 11,000 kwa ajili ya makazi na huduma za kijamii kwa wakazi wa kata hiyo iliyopo katikati ya mji huo wa Chalinze.
Hivi karibuni kupitia baraza la Madiwani lilipitisha mpango wa tarafa hiyo kuwa wilaya ambapo suala hilo bado liko kwenye mchakato kwa kupeleka maombi hayo kwenye ngazi husika.
Akizungumza mjini Chalinze diwani wa kata hiyo Nasa Karama alisema kuwa wao wako tayari kufanya hivyo na kuwa makao makuu ya wilaya mpya mara maombi hayo yakapopitishwa na wizara husika.
Karama alisema kuwa moja ya mambo waliyoyafanya kuhakikisha wanapata nafasi hiyo ya kuwa makao makuu ya wilaya ni pamoja na kugawa viwanja hivyo.
"Tumegawa viwanja hivyo kwa kushirikiana na halmashauri ili kuupanga mji wetu uwe kwenye mandhari nzuri na kuepukana na ujenzi holela usiozingatia ramani za mipangomiji," alisema Karama.
Alisema kuwa viwanja hivyo vimetolewa kwa wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo kwenye vijiji vya Mbala, Kibiki na Koo lengo kubwa ikiwa ni kuondokana na ujenzi holela.
"Baadhi ya wadau waliopewa viwanja hivyo tayari wameanza ujenzi huku wengine wakiendelea na michakato ya kuendeleza maeneo yao baadhi yao ni NSSF, wanaotaka kujenga soko la kisasa wakiwa kwenye hatua ya tathmini, ujenzi wa nyumba za watumishi, tume ya utumishi wa umma, ofisi ya Mbunge, TAKUKURU, benki na kituo cha polisi," alisema Nasa.
Aidha alisema kuwa wametoa fidia ya shilingi milioni 98 kwa wananchi kutokana na kuchukua maeneo yao kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya maendeleo.
mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
HOSPITALI Teule ya Rufaa ya mkoa wa Pwani Tumbi imesisitiza kuwa haiuzi damu kama baadhi ya watu wanavyodai kwani hilo ni kosa kisheria.
Akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea hospitali hiyo wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari wa mkoa wa Pwani juu ya hali tete na migogoro iliyoandaliwa na Baraza la habari Tanzania (MCT), mkuu wa kitengo cha maabara Boaz Motto alisema kuwa sera ya afya hairuhusu uuzaji wa damu.
Motto alisema kuwa utaratibu unaonyesha kuwa mgonjwa akipewa damu anapaswa kurejesha ili wagonjwa wengine nao waweze kupata damu wanapokuwa wanahitaji.
"Tatizo huwa linakuwa ni kwa wanafamilia ambapo wanapoambiwa wachangie damu baadhi yao huwa wanashindwa hali ambayo inasababisha kutafuta watu na kuwaomba damu lakini kwa makubaliano ya kuwalipa fedha," alisema Motto.
Alisema kuwa mapatano ya kuuziana damu hayafanyiki hospitalini bali ni makubaliano ya watoa damu na wenye mgonjwa lakini hospitali hutoa damu bure bila ya malipo lakini sharti ni kwamba wenye mgonjwa nao watoe damu ili itumike kwa wengine.
"Hii dhana ya damu kuuzwa imeenea sana lakini sera ya afya hairuhusu hospitali kuuza damu kwa mgonjwa bali ni kwa wanandugu kumtolea damu ambapo watu huwanunua watoa damu na wakifika hospitali hudai kuwa ni ndugu," alisema Motto.
Alisema kuwa kwa sasa hospitali ina damu ya kutosha na haina upungufu ambapo kuna uniti 150 ambazo watu hujitolea kama vile taasisi za jeshi, watu binafsi, wanafunzi na makundi mbalimbali ndani ya jamii.
"Changamoto tuliyonayo ni vipimo vya damu ambapo hutubidi kupeleka kwenye hospitali ya Muhimbili kwa ajili ya kupimwa kujua ubora wake ili iweze kutumika kwa wagonjwa wanaohitaji damu," alisema Motto.
Aidha alisema kuwa magonjwa yanayoongoza ni pamoja na yale ya msimu wa mvua kama vile kichocho, malaria na minyoo ambapo mazalia yake ni kwenye maji huku wakati wa kiangazi magonjwa ni yale ya kifua kikuu, kukohoa na malaria.
mwisho.
KITONGOJI cha Biga kata ya Mkange wilayani Bagamoyo mkoani Pwani ambacho kilikumbwa na mafuriko hivi karibuni kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha hapa nchini kimeomba serikali kuwapatia mbegu za mahindi tani 2.5 kwa ajili ya kupanda tena zao hilo.
Ombi hilo limekuja baada ya hekari 510 za wakazi wa kitongoji hicho kusombwa na maji ya mvua ambazo zilinyesha kabla ya mvua kubwa za mafuriko kunyesha hivi karibuni ambapo kilizungukwa na maji na kuwafanya wakazi wengine kupewa hifadhi ya muda.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi diwani wa kata hiyo ya Mkange Abdala Mwendadi alisema kuwa mazao ya wakazi hao yote yalisombwa na maji hali ambayo itasababisha kitongoji hicho kuwa hatarini kukumbwa na njaa.
"Kutokana na hali hiyo wakazi wa kitongoji hicho wanaomba serikali iwapatie mbegu kwa ajili ya kupanda mahindi mara mvua hizi zitakapokwisha ambapo msimu huo mahindi yake huitwa "Mahindi ya Kitopeni" ambayo hupandwa baada ya mvua kwisha mwezi Mei kiloa mwaka," alisema Mwindadi.
Mwindadi alisema kuwa jumla ya kaya 63 zimeathiriwa na mvua hizo ambapo zaidi ya watu 200 wameathirika hivyo kuwafanya kuhama kwenye maeneo hayo na kwenda kwa ndugu jamaa kwa ajili ya hifadhi.
"Wakazi wengi waliokumbwa na mafuriko hayo ni wale waliokuwa wakiishi kwenye mkondo wa maji ambapo kutokana na mvua hizo kumechangia kukumbwa na mafuriko hayo ambayo yamesomba mazao yote yaliyopandwa msimu wa kilimo," alisema Mwindadi.
Aidha diwani huyo wa kata ya Mkange alisema kuwa kutokana na maombi hayo atayapeleka halmashauri ili hatua za kuwasaidia zianze kwani endapo hawatapata msaada huo hali ya chakula kwenye kitongoji hicho itakuwa mbaya.
mwisho.
Na John Gagarini, Bagamoyo
MWENYEKITI wa Kijiji cha Kinzagu William Makumu ameshangzwa na wawekezaji kwenye kijiji hicho kushindwa kuchangia maendeleo hasa kwenye sekta ya barabara kutokana na kuingiza magari makubwa kwa ajili ya kubeba kokoto.
Alisema kuwa kuna wawekezaji wengi ambao wamewekeza kwenye uchimbaji kokoto ambazo zinatumika kwa ajili ya ujenzi wa nyumba na barabara hasa Jijini Dar es Salaam.
Makumu alisema kuwa uwekezaji mkubwa kijijini hapo ni uchimbaji wa kokoto kutokana na kijiji hicho kuzungukwa na milima ya mawe.
"Wamekuwa wakiingiza mamilioni ya fedha kwa ajili ya uchimbaji wa kokoto ambapo magari makubwa ambayo yanafikia hadi uzito wa tani 30 hutumia barabara za kijiji lakini hawazikarabati licha ya wao kufanya uharibifu mkubwa," alisema Mukamu.
Alisema kuwa kabla ya kupewa maeneo kwa ajili ya kuendeshea shughuli zao huomba kupitia mkutano wa Kijiji ambapo hutakiwa kutoa asilimia fulani kutokana na mapato yao pia hutakiwa kutoa nguvu zao kwa ajili ya kufanya kazi za maendeleo.
"Tatizo wao wamekuwa wakiangalia upande wao mfano ni eneo la barabara ambazo zimeharibika sana kutokana na wao kuingiza magari yao ya kubebea kokoto lakini hawako tayari kuzitengeneza licha ya kuwa wao ndiyo watumiaji wakubwa kwa ajili ya kupitisha kokoto kwenda maeneo mengine," alisema Mukamu.
Alibainisha kuwa uchangiaji wa wawekezaji hao ni mdogo sana ikilinganishwa na mapato wanayoyapata na athari wanazoziacha baada ya kupasua mawe kwenye kijiji hicho.
Aliwataka wawekezaji hao kujitahidi kuheshimu mikataba waliyoingia ya kuisadia jamii inayowazunguka ambayo ndiyo iliyowapa ardhi wanayoitumia kwa uwekezaji wao.
mwisho.
Na John Gagarini, Chalinze
HUKU Tarafa ya Chalinze ikiwa kwenye maombi ya kupatiwa wilaya kata ya Bwiringu wilayani Bagamoyo inaendelea na mchakato wa kuhakikisha kuwa inapata nafasi ya kuwa makao makuu ya wilaya hiyo yanakuwa hapo.
Moja ya mambo waliyofanya ni pamoja na kugawa viwanja zaidi ya 11,000 kwa ajili ya makazi na huduma za kijamii kwa wakazi wa kata hiyo iliyopo katikati ya mji huo wa Chalinze.
Hivi karibuni kupitia baraza la Madiwani lilipitisha mpango wa tarafa hiyo kuwa wilaya ambapo suala hilo bado liko kwenye mchakato kwa kupeleka maombi hayo kwenye ngazi husika.
Akizungumza mjini Chalinze diwani wa kata hiyo Nasa Karama alisema kuwa wao wako tayari kufanya hivyo na kuwa makao makuu ya wilaya mpya mara maombi hayo yakapopitishwa na wizara husika.
Karama alisema kuwa moja ya mambo waliyoyafanya kuhakikisha wanapata nafasi hiyo ya kuwa makao makuu ya wilaya ni pamoja na kugawa viwanja hivyo.
"Tumegawa viwanja hivyo kwa kushirikiana na halmashauri ili kuupanga mji wetu uwe kwenye mandhari nzuri na kuepukana na ujenzi holela usiozingatia ramani za mipangomiji," alisema Karama.
Alisema kuwa viwanja hivyo vimetolewa kwa wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo kwenye vijiji vya Mbala, Kibiki na Koo lengo kubwa ikiwa ni kuondokana na ujenzi holela.
"Baadhi ya wadau waliopewa viwanja hivyo tayari wameanza ujenzi huku wengine wakiendelea na michakato ya kuendeleza maeneo yao baadhi yao ni NSSF, wanaotaka kujenga soko la kisasa wakiwa kwenye hatua ya tathmini, ujenzi wa nyumba za watumishi, tume ya utumishi wa umma, ofisi ya Mbunge, TAKUKURU, benki na kituo cha polisi," alisema Nasa.
Aidha alisema kuwa wametoa fidia ya shilingi milioni 98 kwa wananchi kutokana na kuchukua maeneo yao kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya maendeleo.
mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
HOSPITALI Teule ya Rufaa ya mkoa wa Pwani Tumbi imesisitiza kuwa haiuzi damu kama baadhi ya watu wanavyodai kwani hilo ni kosa kisheria.
Akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea hospitali hiyo wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari wa mkoa wa Pwani juu ya hali tete na migogoro iliyoandaliwa na Baraza la habari Tanzania (MCT), mkuu wa kitengo cha maabara Boaz Motto alisema kuwa sera ya afya hairuhusu uuzaji wa damu.
Motto alisema kuwa utaratibu unaonyesha kuwa mgonjwa akipewa damu anapaswa kurejesha ili wagonjwa wengine nao waweze kupata damu wanapokuwa wanahitaji.
"Tatizo huwa linakuwa ni kwa wanafamilia ambapo wanapoambiwa wachangie damu baadhi yao huwa wanashindwa hali ambayo inasababisha kutafuta watu na kuwaomba damu lakini kwa makubaliano ya kuwalipa fedha," alisema Motto.
Alisema kuwa mapatano ya kuuziana damu hayafanyiki hospitalini bali ni makubaliano ya watoa damu na wenye mgonjwa lakini hospitali hutoa damu bure bila ya malipo lakini sharti ni kwamba wenye mgonjwa nao watoe damu ili itumike kwa wengine.
"Hii dhana ya damu kuuzwa imeenea sana lakini sera ya afya hairuhusu hospitali kuuza damu kwa mgonjwa bali ni kwa wanandugu kumtolea damu ambapo watu huwanunua watoa damu na wakifika hospitali hudai kuwa ni ndugu," alisema Motto.
Alisema kuwa kwa sasa hospitali ina damu ya kutosha na haina upungufu ambapo kuna uniti 150 ambazo watu hujitolea kama vile taasisi za jeshi, watu binafsi, wanafunzi na makundi mbalimbali ndani ya jamii.
"Changamoto tuliyonayo ni vipimo vya damu ambapo hutubidi kupeleka kwenye hospitali ya Muhimbili kwa ajili ya kupimwa kujua ubora wake ili iweze kutumika kwa wagonjwa wanaohitaji damu," alisema Motto.
Aidha alisema kuwa magonjwa yanayoongoza ni pamoja na yale ya msimu wa mvua kama vile kichocho, malaria na minyoo ambapo mazalia yake ni kwenye maji huku wakati wa kiangazi magonjwa ni yale ya kifua kikuu, kukohoa na malaria.
mwisho.
Subscribe to:
Posts (Atom)