Monday, December 30, 2024

NYIKA MABINGWA MKOA WA PWANI






TIMU ya soka ya Nyika imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Mkoa wa Pwani kwa kuifunga timu ya Kiduli kwa goli 1-0 kwenye mchezo wa fainali wa ligi daraja la tatu ngazi ya Mkoa.

Mchezo huo ambao ulichezwa kwenye uwanja wa Mwendapole Mjini Kibaha ulihudhuriwa na viongozi wa Chama  Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA), viongozi wa Chama Cha Soka Wilaya ya Kibaha KIBAFA na vyama vya Wilaya zingine na vyama shiriki na mashabiki wengi wa Kibaha.

Mwenyekiti wa COREFA Robert Munis akizungumza mara baada ya mchezo huo amesema kuwa lengo lao ni kuhakikisha mpira unachezwa ili kukuza vipaji vya soka Pwani.

Munis amesema kuwa fainali hiyo ambayo ilionyesha kiwango kikubwa cha wachezaji wa timu hizo zimeonyesha jinsi gani zilivyojiandaa na vijana kuonyesha uwezo mkubwa.

"Lengo letu ni kuhakikisha tunapambania timu zetu angalau zifike kucheza ligi kuu ya NBC angalau timu moja na hilo linawezekana kama tutaunganisha nguvu na kuziunga mkono timu zetu,"amesema Munis.

Kufuatia ushindi huo timu ya Nyika ilipewa kombe na itawakilisha mkoa wa Pwani kwenye mashindano ya Ligi ya mabingwa wa Mikoa (RCL) mwakani.

Saturday, December 28, 2024

JAMII YAWEZESHWA PEMBEJEO KILIMO CHA BUSTANI WILAYA YA KIBAHA








TAASISI ya Anjita Child Development Foundation ya Kibaha imetoa pembejeo za kilimo cha bustani ya mbogamboga zenye thamani ya shilingi milioni 10.8 kwa vikundi vya wakulima wa bustani kwenye Vitongoji vya Mwanabwito na Kidai Kata ya Kikongo kwa ajili ya kuongeza uzalishaji.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi kuwezesha jamii kupitia kilimo cha bustani na kukabidhi pembejeo  kwa vikundi hivyo Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Evelyn Ngwira kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha amesema kuwa mradi huo utakwenda kubadilisha maisha ya jamii kwenye Kata hiyo.  

Ngwira amesema kuwa mradi huo wa uwezeshaji jamii ili kujikwamua kiuchumi na kuboresha afya na utasimamiwa na wanajamii wenyewe na watapaswa kufuata ushauri wa wataalamu wa kilimo.

"Mnapaswa kulima kwa kuzingatia kalenda ili kupata mazao mazuri ambayo yatakuwa na soko zuri na mradi huu utakuwa endelevu na mtasimamia wenyewe hivyo muwe mfano kwa awamu hii ya kwanza,"amesema Ngwira.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Anjita Janeth Malela amesema kuwa mradi huo umeibuliwa na wananchi wenyewe na wataundesha kwa kusimamiwa na taasisi na wataalamu wa kilimo.

Malela amesema kuwa pembejeo hizo ni ufadhili kutoka Ubalozi wa Marekani ukiwa na lengo la kuongaza kipato kwa familia na kuboresha afya kwa wananchi.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kidai Samson Dotto kwa niaba ya diwani wa Kata ya Kikongo amesema kuwa kilimo ni uti wa mgongo kwani wao wanafanya shughuli hizo kando ya Mto Ruvu na utawasaidia kiwasogeza mbele kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine.

Naye ofisa kilimo kata ya Kikongo Fortunatus Ng'itu amesema kuwa hiyo ni fursa muhimu kwa wananchi na wanapaswa kuitumia ili kubadili maisha yao.

Moja ya wanufaika wa mradi huo Eliwaza Kingu amesema kuwa wanaishukuru taasisi hiyo kwa kuwapatia mradi huo kwani utawasaidia kuwapunguzia gharama za kununulia pembejeo ambazo ni kubwa.

Kitongoji cha Mwanabwito ni vikundi  3 ambavyo vina watu 9 na kimoja kina watu 10 kwa Kitongoji cha Kidai kuna vikundi 6 kasoro vikundi 2 wapo  watu 5  wa tano.

TAASISI ya Anjita Child Development Foundation ya Kibaha imetoa pembejeo za kilimo zenye thamani ya shilingi milioni 10.7 kwa vikundi vya wakulima wa bustani kwenye Vitongoji vya Mwanabwito na Kidai Kata ya Kikongo kwa ajili ya kuongeza uzalishaji.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi kuwezesha jamii kupitia kilimo cha bustani na kukabidhi pembejeo  kwa vikundi hivyo Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Evelyn Ngwira kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha amesema kuwa mradi huo utakwenda kubadilisha maisha ya jamii kwenye Kata hiyo.  

Ngwira amesema kuwa mradi huo wa uwezeshaji jamii ili kujikwamua kiuchumi na kuboresha afya na utasimamiwa na wanajamii wenyewe na watapaswa kufuata ushauri wa wataalamu wa kilimo.

"Mnapaswa kulima kwa kuzingatia kalenda ili kupata mazao mazuri ambayo yatakuwa na soko zuri na mradi huu utakuwa endelevu na mtasimamia wenyewe hivyo muwe mfano kwa awamu hii ya kwanza,"amesema Ngwira.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Anjita Janeth Malela amesema kuwa mradi huo umeibuliwa na wananchi wenyewe na wataundesha kwa kusimamiwa na taasisi na wataalamu wa kilimo.

Malela amesema kuwa pembejeo hizo ni ufadhili kutoka Ubalozi wa Marekani ukiwa na lengo la kuongaza kipato kwa familia na kuboresha afya kwa wananchi.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kidai Samson Dotto kwa niaba ya diwani wa Kata ya Kikongo amesema kuwa kilimo ni uti wa mgongo kwani wao wanafanya shughuli hizo kando ya Mto Ruvu na utawasaidia kiwasogeza mbele kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine.

Naye ofisa kilimo kata ya Kikongo Fortunatus Ng'itu amesema kuwa hiyo ni fursa muhimu kwa wananchi na wanapaswa kuitumia ili kubadili maisha yao.

Moja ya wanufaika wa mradi huo Eliwaza Kingu amesema kuwa wanaishukuru taasisi hiyo kwa kuwapatia mradi huo kwani utawasaidia kuwapunguzia gharama za kununulia pembejeo ambazo ni kubwa.

Kitongoji cha Mwanabwito ni vikundi  3 ambavyo vina watu 9 na kimoja kina watu 10 kwa Kitongoji cha Kidai kuna vikundi 6 kina watu 6 kasoro vikundi 2 wapo  watu 5  wa tano.


Thursday, December 19, 2024

KAMPUNI YA PPM GROUP YAHAMASISHA NISHATI SAFI NA UTUNZAJI MAZINGIRA

KAMPUNI ya PPM Group inahamasisha wananchi kuwa na matumizi ya nishati safi na kuachana na matumizi ya mkaa na kuni ili kunusuru misitu ambayo inaathiriwa na matumizi kama hayo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa maonyesho ya wiki ya Uwekezaji na Biashara Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya PMM Group Dk Judith Spendi amesema matumizi yanayopaswa kutumika kwa kupikia ni ya nishati safi.

Dk Spendi amesema kuwa Dar es Salaam na Pwani inatumia mkaa tani milioni 2.4 kwa mwaka hali ambayo ni hatari kwa misitu.

"Tunahamasisha matumizi ya majiko sanifu ambapo tutaanza uzalishaji wa majiko sanifu na upandaji miti ili kuepuka mabadiliko ya tabianchi,"amesema Dk Spendi.

Waziri wa Viwanda na Biashara Suleiman Jaffo aliipongeza kampuni ya PPM Group kwa jitihada zake za kukabiliana na uharibifu wa mazingira na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia. 

STAMICO YATAKA WATANZANIA WATAKIWA KUTUMIA NISHATI SAFI NA SALAMA YA MKAA WA RAFIKI BRIQUETTES


KATIKA kuhamasisha matumizi ya nishati safi na salama Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limewataka Watanzania kutumia Mkaa wa Rafiki Briquettes.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na ofisa masoko wa (Stamico) Hope Mahokola wakati wa maonyesho ya Uwekezaji na Biashara ya Mkoa wa Pwani.

Mahokola amesema kuwa mkaa huo ni nishati safi na salama na una uwezo wa kuwaka kwa zaidi ya saa tatu baada ya kuwashwa.

"Tunamuunga mkono Rais Dk Samia Suluhu Hassan kuhamasisha matumizi ya nishati safi ili kulinda mazingira ili kutoharibu uoto wa asili ili usisababishe mabadiliko tabianchi hivyo Watanzania watumie mkaa wa Rafiki Briquettes ili kulinda mazingira,"amesema Mahokola.

Amesema kuwa mkaa huo unatolana na mabaki ya makaa ya mawe hauna moshi na ni safi na salama katika kupikia na unachangia kupunguza mabadiliko ya Tabianchi.

"Mkaa huu unaweza kutumika nyumbani, vyuoni, mashuleni na sehemu nyingine zenye uhitaji wa nishati ya kupikia,"amesema Mahokola.

Aidha amesema kuwa mkaa huo ni rafiki kwa matimizi, mazingira na gharama na mkaa huo unatokana na makaa ya mawe yanayochimbwa kwenye mgodibwa Kiwira-Kabulo Mkoani Songwe.

TAASISI YA ANJITA YATAKA USHIRIKIANO KUKABILIANA NA UKATILI WA KIJINSIA










TAASISI ya Anjita Child Development Foundation iliyopo Halmashauri ya Mji Kibaha imeomba wadau wa kupinga ukatili kushirikiana ili kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia kwenye jamii.

Akizungumza wakati wa kuhitimisha siku 16 za kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia Mkurugenzi wa Taasisi hiyo ya Anjita Janeth Malela amesema kuwa ili kufikia hatua ya kupunguza matukio hayo lazima watu, taasisi na mashirika waungane kukabili vitendo hivyo.

Malela amesema kuwa kabla ya kufikia hitimisho la siku hizo 16 za kupinga ukatili walitoa elimu kwa jamii juu ya kukabiliana na vitendo hivyo ambapo jamii imepata uelewa kwani wamejengewa uwezo.

"Tumetoa elimu hiyo na imeonyesha kuwa ndani ya jamii bado matukio kama hayo yanajitokeza hivyo tumewapatia uelewa na namna ya kuripoti mara waonapo matukio kama hayo ili hatua stahiki zichukuliwe,"amesema Malela.

Amesema kuwa ili kupunguza au kutokomeza vitendo hivyo lazima wadau waungane kwa pamoja kwa kutoa elimu kwa jamii ili kukabili vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Taasisi ya Anjita inashughulisha zinazohusiana na watoto na vijana pia kundi la watu wazima kupitia elimu ya malezi changamshi  kwa wazazi na walezi kupitia mradi wa Mtoto Kwanza.

Katika kuhitimisha kilele hicho cha siku 16 za kupinga vitendo vya ukatili Taasisi ya Anjita ilipewa cheti cha pongezi na ófisi ya mkuu wa Mkoa wa Pwani cha kushiriki kikamilifu katika kutoa elimu ya kupambana na ukatili wa kijinsia maeneo mbalimbali ya Mji wa Kibaha.

Wednesday, December 18, 2024

KINGLION KUTOA AJIRA



KIWANDA cha kuzalisha malighafi zitumikazo kwenye uzalishaji vyuma na mabati na usambazaji wa pikipiki cha Kinglion kinatarajia kutoa ajira kwa watu 1,500 ajira za kudumu na ajira za muda zaidi ya 5,000.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa wiki ya maonyesho  ya Biashara na Viwanda ya Mkoa wa Pwani meneja wa kiwanda hicho Anold Lyimo amesema kuwa kiwanda hicho kitafunguliwa muda siyo mrefu.

Lyimo amesema kuwa mara kiwanda hicho kitakapoanza uzalishaji vijana wengi watapata ajira na kuongeza pato la Taifa kwani kitakuwa kiwanda kikubwa na kitauza bidhaa zake hadi nje ya Tanzania yaani nchi jirani.

"Kiwanda kilikuwa kianze uzalishaji mwaka huu lakini kuna changamoto kidogo ikiwa ni pamoja na barabara na gesi ambavyo serikali inavifanyia kazi ili kukabili changamoto hizo,"amesema Lyimo.

Aidha alisema kuwa wanatarajia kiwansa kitakapoanza kazi kitakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 35,000 kwa mwaka.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini Tanzania (TARURA) wataijenga barabara ya kuelekea kiwandani huko yenye urefu wa kilometa 2.5.

Kunenge amesema kuwa pia wanatarajia kusambaziwa gesi kwenye eneo la viwanda la Zegereni ikiwemo kwenye kiwanda hicho cha Kinglion.

MLEZI WA KAMATI YA USALAMA BARABARANI ACP MORCASE AONGOZA KIKAO CHA KAMATI


Mlezi wa Kamati ya usalama barabarani Mkoa wa Pwani, Kamishina Msaidizi wa Polisi Salim Morcase Disemba 17 amekiongoza kikao cha kamati ya usalama barabarani ambacho kimejadili maswala mbalimbali ikiwemo kuondoa msongamano wa foleni kwenye barabara kuu za Mkoa wa Pwani na kuweka mikakati ya pamoja ya kumaliza foleni hizo ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua kali kwa madereva watakaobainika kupandisha nauli za mabasi kwenye kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka pamoja na madereva wanaokaidi kutii Sheria za usalama barabarani kwa watumiaji wengine wa barabara.