Sunday, November 1, 2015

Friday, October 30, 2015

RIDHIWANI KIKWETE AWASHUKURU WANACHALINZE KUMCHAGUA TENA

Na John Gagarini, Chalinze
MBUNGE Mteule wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete amesema kuwa hana chuki kwa wale ambao hawakumpigia kura kwenye uchaguzi uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu kwani hizo ni changamoto za uchaguzi.
Aliyasema hayo jana kwenye uwanja wa Miembe Saba Chalinze wilayani Bagamoyo wakati wa mkutano wa hadhara wa kuwashukuru Wanachalinze kwa kumchagua kuwa mbunge kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika Jumapili.
Ridhiwani alisema kuwa licha ya baadhi ya maeneo kutompigia kura za kumchagua kuwa mbunge lakini atawatumikia wananchi wote bila ya kujali kama walimpigia kura au la kwani kila mtu ana haki ya kumpigia kura mgombea yoyote anayempenda.
“Nawashukuru wananchi wote walionipigia kura na hata wale ambao hawakunipigia kura kwani hiyo ndiyo demokrasia nitahakikisha nawahudumia wananchi wote bila ya kuwabagua nitahakikisha napeleka maendeleo kwa watu wote wa jimbo hili,” alisema Ridhiwani.
Alisema kuwa kutopigiwa kura kwa wingi siyo sababu ya kuwagawa wananchi kwani hizo ni changamoto za uchaguzi ambao unakuwa na mambo yake ambapo baadhi ya maeneo walipiga kura kwa kuzingatia ukabila.
“Sitakuwa na chuki wala hasira kwa wale ambao hawakunipigia kura nitashirikiana nao katika suala la maendeleo ili kuhakikisha jimbo letu linakuw ana maendendeleo na wananchi wanaboresha maisha yao ili yasonge mbele,” alisema Ridhiwani.
Aidha alisema kuwa atahakikisha Mji wa Chalinze ambao umekuwa Halmashauri ya Mji Mdogo unajengwa kwa kuwekewa huduma muhimu ili wananchi waweze kuboresha biahara zao hasa ikizingatiwa kuwa mji huo ni wa kibiashara.
“Moja ya mambo nitakayo yafanya ni kufanya Chalinze kuwa makao makuu ya Halmashauri hiyo na baadaye kuwa wilaya kwani mchakato unaendelea na tunaamini baada ya muda tutapewa wilaya hivyo tutaweza kujitegemea na kujiimarisha kiuchumi,” alisema Ridhiwani.
Alibainisha kuwa wananchi wasiwe na wasi wasi kwani kukichagua Chama Cha Mapanduzi CCM ni kuchagua maendeleo hivyo wasubiri kuona jinsi serikali mpya itakavyofanya kazi kwani kwao ni kazi tu.
Kwa upande wake mwenyekiti wa CCM Chalinze Nasa Karama alisema kuwa mbunge huyo ameonyesha uwezo mkubwa kwani kwa kipindi alichochaguliwa cha mwaka mmoja na miezi mitatu ameweza kufanya mambo makubwa ambapo alitumia ziadi ya shilingi bilioni moja na zaidi kwa ajali ya miradi ya maendeleo.
Mwisho.  

 Ridhiwani Kikwete

Sunday, October 25, 2015

RAIS DK JAKAYA KIKWETE ASHIRIKI ZOEZI LA KUPIGA KURA MSOGA

Na John Gagarini, Chalinze
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Jakaya Kikwete amesema kuwa mara atakapostaafu nafasi hiyo Novemba 5 mwaka huu anatarajia kuanzisha taasisi ya maendeleo kwa Afrika na Dunia.
Aidha alisema kuwa atarudi Kijijini kwake Msoga Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani ambapo mbali ya kuanzisha taasisi hiyo ya maendeleo pia ataendeleza ufugaji na kilimo cha mananasi.
Dk Kikwete aliyasema hayo jana katika Kijiji cha Msoga mara baada ya kupiga kura yake kwenye uchaguzi mkuu wa kumchagua Rais, Mbunge na Diwani na kusema kuwa amefurahi sana kuona watu wanapiga kura bila ya usumbufu wowote.
Dk Kikwete alisema kuwa mara baada ya kustaafu na baada ya Rais mpya kuapishwa Desemba 5 atajihusisha na masuala hayo kwani hawezi kukaa tu hivi bila ya kuwa na jambo la kufanya kwani ataendelea kuwa na nguvu.
“Natarajia kuwa mfugaji kwani nina shamba la mifugo pia kuwa mkulima wa mananasi huko Kijiji cha Kiwangwa na ninafurahi kupiga kura kwani nimetumia haki yangu na nanishukuru hadi sasa hatujasikia kama kuna tatizo lolote,” alisema Dk Kikwete.
“Nawaomba wananchi wajitokeze kupiga kura na ningependa na vituo vingine viwe na utulivu kama hichi cha hapa na watu washiriki uchaguzi ili baadaye wasije wakahoji kuwa hata fulani kachaguliwa wakati wao hawakupiga kura kumchagua kiongozi ambaye wanamtaka wao,” alisema Dk Kikwete.
Juu ya uchaguzi wa mwaka huu alisema kuwa chaguzi zote zinakuwa na upinzani mkali na anaomba hali ya amani iendelee hivi ili iwe nchi ya mfano kwa kufanya uchaguzi bila ya kuwa na vurugu.
Kwa Upande wake mgombea wa Ubunge wa (CCM) Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alisema kuwa anashukuru kwani hadi sasa zoezi hilo la upigaji kura linaendelea vizuri na hakuna tatizo lolote na anaamini kuwa uchaguzi utakwenda vizuri.
Ridhiwani ambaye naye alipiga kura kwenye kituo cha Kijiji cha Msoga alisema kuwa kuna changamoto ndogondogo zilizojitokeza ikiwa ni pamoja na baadhi ya watu hawakuona majina yao licha ya kuwa walikuwa na vitambulisho vya kupigia kura huko maeneo ya Miono.
Naye mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mathayo Torongey alisema kuwa amepita kwenye vituo vingi hajaona tatizo lakini kuna baadhi ya maeoneo mawakala wao walitishwa.
Torongey alisema kuwa mawakala hao walitishwa kwenye kituo cha Kijiji cha Msoga lakini baada ya makubaliano waliweka mawakala wengine na wakaendelea na zoezi la kusimamia kwenye vituo walivyopangiwa.
Aidha mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo alisema kuwa hadi mchana kulikuwa hakuna tatizo lililoripotiwa licha ya kuwa baadhi ya maeneo watu walikuwa na hofu kwamba zoezi litaenda taratibu lakini hali hiyo iliondoka na utaratibu kwenda vizuri.
Ndikilo alisema kuwa eneo la Vigwaza kulikuwa na hofu ya upungufu wa karatasi kutokana na idadi kubwa ya watu lakini hali hiyo iliwekwa sawa na mambo yanakwenda vizuri na wameweka ulinzi wa kutosha.
Alibainisha kuwa suala la kukaa mita 200 kwa ajili ya kulinda kura halipo kwani sheria imeelekeza vizuri juu ya watu mara baada ya kupiga kura wanaondoka na hakuna mtu aliyebaki kulinda kura kwani wameondoka na kuendelea na shughuli zao.
Mwisho. 

 Rais Dk Jakaya Kikwete akizungumza na mkuu wa mkoa wa Pwani wapili kulia Injinia Evarist Ndikilo , wakati Rais alipokwenda kupiga kura kwenye kituo cha Kijiji cha Msoga Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani kulia ni mkuu wa wilaya hiyo Majid Mwanga

 Rais Dk Jakaya Kikwete akihojiwa na waandishi wa habara mara baada ya kupiga kura kwenye kituo cha Kijiji cha Msoga 

 Rais Dk Jakaya Kikwete kushoto akisubiri kupewa karatasi kwa ajili ya kwenda kupiga kura


 Rais Dk Jakaya Kikwete akiwa amepanga foleni kabla ya kwenda kupiga kura hata hivyo alisimama kwa muda mfupi kabla ya kutimiza zoezi hilo


Rais Dk Jakaya Kikwete akisalimiana na mkuu wa mkoa wa Pwani Evaristi Ndikilo alipowasili kwenye kituo cha kupigia kura kwenye Kijiji cha Msoga



Baadhi ya akinamama wakiwa wanasubiri kupiga kura kwenye kituo cha Kijiji cha Msoga

 Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze kupitia CCM Ridhiwani Kikwete akichukuliwa maelezo kabla ya kupiga kura 

 Ridhiwani Kikwete akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kupiga kura kwenye Kituo cha Kijiji cha Msoga

Thursday, October 22, 2015

johngagariniblog: DK MAGUFULI KUUFANYA MJI WA CHALINZE KUWA WA KISAS...

johngagariniblog: DK MAGUFULI KUUFANYA MJI WA CHALINZE KUWA WA KISAS...: Na John Gagarini, Chalinze MGOMBEA Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk John Magufuli emesema kuwa endapo atachaguliwa kuwa R...

DK MAGUFULI KUUFANYA MJI WA CHALINZE KUWA WA KISASA

Na John Gagarini, Chalinze
MGOMBEA Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk John Magufuli emesema kuwa endapo atachaguliwa kuwa Rais atahakikisha mji wa Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani unakuwa moja ya miji ya kisasa na wa uwekezaji ambapo utakuwa na barabara za juu Fly Over.
Aidha ujenzi huo ambao utakuwa wa barabara sita hadi jijini Dar es Salaam utagharimu kiasi cha shilingi trilioni 2.3 na Chalinze itakuwa kiunganishi cha njia hizo kwenda mikoa ya Kasakazini na mikoa ya Kati ambapo tayari wataalamu wa upembuzi wa ujenzio huo wamelipwa kiaisi cha shilingi billion 7.7.
Aliyasema hayo kwenye mkutano wa kampeni kwenye Jimbo la Chalinze mkoani humo ambapo alisema kuwa atahakikisha mji huo unakuwa wa kisasa na huduma zote muhimu zinapatikana hapo na kuwa mji mbadala wa Dar es Salaam.
Dk Magufuli ambaye ni Waziri wa Ujenzi na Miundombinu alisema kuwa mji huo utakuwa kituo kikubwa cha uwekezaji hapa nchini kwani faida nyingine iliyopo ni kugunduliwa gesi eneo la Ruvu hivyo kufanya uchumi wa mji huo kuwa juu na wananchi wataboresha maisha yao na kuwa na maisha bora.
“Msiuze kiholela maeneo yenu kwani baadhi ya watu wanauza maeneo kwa bei ndogo lakini watakao nunua watakuja kuuza kwa bei kubwa hivyo huu ni moja ya miji itakayokuwa ya kisasa hapa nchini na sasa maisha bora yanakuja na sitawaangusha naomba mnipigie kura nyingi za kutosha ili niweze kuwa Rais,” alisema Dk Magufuli.
Alisema kuwa kuhusu changamoto ya maji kwenye mji huo alisema kuwa atahakikisha suala hilo linakwisha ambapo aliipongeza awamu ya tatu na nne ambazo zimejitahidi angalau maji yanapatikana kwani mji huo ulikuwa na tatizo kubwa la maji.
Katika hatua nyingine amesema anashangazwa na baadhi ya wanasiasa kusema kuwa fedha zilizokuwa zijenge bandari ya Tanga zimepelekwa Bagamoyo kisa ni wilaya anayotoka Rais Dk Jakaya Kikwete.
“Kauli kama hizo ni za uchonganishi kwani kila eneo limetengewa fedha zake kwa ajili ya ujenzi wa Bandari kuanzia Tanga, Mtwara na Mwanza kote kutajengwa bandari hizo na Bagamoyo ni uwekezaji wa watu binafsi hivyo hakuna sababu ya kuwachonganisha watu kwa maneno ya uongo,” alisema Dk Magufuli.
Alibainisha kuwa hizo ni hoja hafifu na hazina msingi wowote zaidi ya kuleta uchonganishi kwani wanapaswa kutangaza sera zao na si kuongopa hali ambayo inajenga chuki baina ya wananchi wa eneo fulani na eneo jingine.
Alisisitiza kuwa endapo atapata ridhaa ya kuongoza atahakikisha ushuru mdogomdogo unaondolewa ili kuwaondolea kero wananchi ambao wanataka kujiongezea kipato kutokana na shughuli zao za ujasiriamali.
Kwa upande wake mgombea Ubunge wa Jimbo hilo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alimshukuru Dk Magufuli kwa mipango hiyo na kusema kuwa changamoto iliyopo ni ujenzi wa kituo cha afya kikub wa ili kukabiliana na uwingi wa wagonjwa pamoja na majeruhi kwenye kituo cha afya chya Chalinze.
Ridhiwani alisema kuwa changamoto nyingine ni maji ambayo licha ya kupatikana bado kuna baadhi ya maeneo hayapati maji hasa kwenye makmao makuu ya vitongoji ambapo kwa makao makuu ya vijiji yote yanapata maji kwa asilimia 94 ambapo Dk Magufuli alisema atashughulikia changamoto hizo endapo atachaguliwa kuwa Rais.
Mwisho   

 Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk John Magufuli kulia na mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze wilayani Bagtamoyo mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete wakiteta jambo wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo mchana kwenye uwanja wa Miembe Saba Chalinze


 Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kushoto katikati ni mwenyekiti wa CCM mkoa Mwinshehe Mlao na kulia ni mwenyekiti wa CCM wilaya ya bagamoyo Almasa Maskuzi wakijadili wakati wakimsubiri mgombea Urais wa CCM Dk John Magufuli kwenye uwanja wa Miembe Saba Chalinze.

 Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze CCM Ridhiwani Kikwete kulia akisalimiana na moja ya wanachama waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni wa Dk John Magufuli kwenye uwanja wa Miembe Saba Chalinze

 Ridhiwani Kikwete akisalimiana na mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Josia Jackson 

Add caption



 Wagombea Ubunge kupitia CCM Ridhiwani Kikwete Jimbo la Chalinze kulia na Amoud Jumaa Jimbo la Kibaha Vijijini wakifurahi kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea Urais kupitia chama hicho Dk John Magufuli. 

 Ridhiwani Kikwete na Dk John Magufuli wakiteta kabla ya kuanza mkutano wa kampeni uliofanyika uwanja wa Miembe Saba Chalinze

 Ridhiwani Kikwete katikati akiteta jambo na mgombea Urais CCM Dk John Magufuli kushoto ni Amoud Jumaa mgombea ubunge Jimbo la Kibaha Vijijini

 Dk Magufuli katikati wakitetea na Ridhiwani Kikwete kushoto na mjumbe wa kampeni Taifa CCM Abdala Bulembo 

 Abdala Bulembo akiwaonyesha wananchi wa Chalinze hawapo pichani namna ya kuwapigia kura wagombea wa CCM ngazi ya Urais

 Ridhiwnai Kikwete akizungumza kwenye mkutano huo wa kampeni

 Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dk John Magufuli akiongea

 Baadhi ya wagombea udiwani wa CCM kwenye Majimbo ya Chalinze na Bagamoyo wakitambulishwa kwenye mkutano huo wa kampeni

 Dk John Magufuli akifurahi jambo na Ridhiwani Kikwete wakifurahia jambo wakati wa mkutano wa kampeni 

 Baadhi ya wanachama wa CCM wakiwa wamejazana kwenye uwanja wa  Miembe Saba Chalinze kumsikiliza mgombea Urais wa chama hicho Dk John Magufuli

 Sehemu ya umati wa wanachama na wananchi wa Chalinze wakiwa wanawasikiliza wagombea mbalimbali wa CCM 

 Wanachama wa CCM wakiwa wamefurika uwanja wa Miembe Saba Chalinze

 Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dk John Magufuli kulia na Ridhiwani Kikwete kushoto wakiombewa duwa mara baada ya mkutano wa kampeni kwenye uwanja wa Miembe Saba Chalinze

Monday, October 19, 2015

WANAFUNZI HATARINI KUOZWA

Na John Gagarini, Chalinze
WANAFUNZI wawili wa kidato cha tatu waliokuwa wakisoma shule ya sekondari Msata wilayani Bagamoyo mkoani Pwani ambao mwanzoni mwa mwaka jana walilamikiwa na wanafunzi wenzao kuwa wanajihusisha na vitendo vya ushirikina shuleni hapo hali iliyosababisha washindwe kuendelea na masomo wako katika hatari ya kukatishwa masomo kufuatia taarifa kuwa mmoja kaozeshwa kwa mwanaume na mwingine yuko kwenye mipango ya kuolewa.
Wanafunzi hao ambao wanatoka kijiji cha Mkoko kata ya Msata wilayani humo  wanadaiwa kuwa wako kwenye hatua hizo baada ya wazazi wao na walezi kushindwa kuwafanyia uhamisho kwenda shule nyingine baada ya wanafunzi wenzao kuwakataa kutokana na madai hayo ya ushirikina.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi moja ya wakazi wa kijiji hicho ambaye hakutaka kutajwa jina lake kutajwa alisema kuwa mwanafunzi wa kwanza (17) anaishi na mwanaume baada ya baba yake kumwoza.
Alisema kuwa baba wa mwanafunzi huyo Damian Joseph alifikia hatua hiyo baada ya mwanae kugoma kuendelea kusoma kwenye shule hiyo na kutaka ahamishiwe shule nyingine kutokana na wenzake kumtuhumu kuwa ni mshirikina.
Baba wa mwanafunzi huyo Joseph alipoulizwa juu ya suala hilo alikanusha na kusema kuwa hajamwoza mwanaye na hana mpango wa kumwozesha kwa kuwa bado ni mwanafunzi ila tatizo lilikuwa ni uhamisho na kufiwa na mkewe.
Akielezea juu ya tatizo la mwanae alisema kuwa mwanawe alikuwa ni mnyonge na kukata tamaa ya kusoma kutokana na wanafunzi wenzake kumtuhumu kuwa ni mchaawi na anawaloga wanafunzi wenzake yeye na mwenzake ambao wanatoka Kijiji kimoja hivyo walishindwa kwenda shule na yeye alikataa kurudi shuleni vinginevyo ahamishiwe shule nyingine.
Joseph alisema kuwa jambo lililomfanya ashindwe kumhamisha mwanae ni kutokana na msiba wa mkewe uliomfanya achanganyikiwe hivyo kusimamisha taratibu za kumhamisha shule hata hivyo amesema kuwa atahakikisha mwanae anawekwenda shule.
Kwa upande wa mwanafunzi (17) ambaye alidaiwa yuko kwenye mchakato wa kutolewa mahari na mwanaume kaka wa mwanafunzi huyo Ramadhan Ndege alikanusha taarifa hizo na kusema kuwa mdogo wake yuko kwa bibi yake mzaa mama ambapo kwa sasa anazaidi ya miezi sita hajaenda shule kutokana na kuwa na matatizo ya mapepo.
Ndege alisema kuwa si kweli kuwa mdogo wake yuko kwenye mpango wa kuozeshwa ila yuko kwa bibi yake akipatiwa matibabu ambapo akienda shule hali inakuwa mbaya kutokana na mapepo kumsumbua.
“Changamoto nyingine ni kukosa fedha kwa ajili ya kumfanyia uhamisho kiasi cha shilingi 250,000 ambazo ni gharama zote kuanzia ufuatiliaji pamoja na sare, vitabu na vifaa vinavyotakiwa kwenye shule anayokwenda ya Changarikwa ambayo ni jirani na kijiji hicho,” alisema Ndege.
Alisema kuwa tatizo kubwa linalowasumbua ni ukosefu wa fedha kwani kipato chao ni kidogo na hawawezi kupata fedha hizo kwa mara moja na msaada ni mdogo kwani wazazi wao walishafariki nakuomba kama kuna wafadhili wanaoweza kuwasaidia wajitokeze ili kuwasaidia kumpeleka shule ndugu yao.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Kijiji hicho Hamis Buzoza alisema kuwa mambo hayo yalikuwa yakifanywa kifamilia zaidi lakini masuala hayo hayajapelekwa ofisini kwake ila aliwataka wazazi wa familia hizo kutofanya hivyo kwani hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Mwisho.   
  

WAFUGAJI WALIOINGIA KINYEMELA BAGAMOYO KUONDOLEWA


Na John Gagarini, Chalinze

 

WILAYA ya Bagamoyo imesema kuwa itawaondoa wafugaji wote walioingia kinyemela kwenye wilaya hiyo ili kuepusha migogoro ya wakulima na wafugaji.

 

Hayo yalisemwa na mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Hemed Mwanga, wakati akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Kihangaiko wilayani humo.

 

Mwanga alisema kuwa kuna baadhi ya wafugaji wameingia kinyemela kwenye wilaya hiyo jambo ambalo ni kinyume cha taratibu.

 

“Tuna taarifa tunazo kuwa kuna baadhi ya wafugaji wanaingia kinyume cha taratibu hali ambayo inaweza kusababisha vurugu baina ya wakulima na wafugaji,” alisema Mwanga.

 

Alisema kuwa wafugaji wote walioingia kwa njia za panya wataondolewa kwani kila mahali kuna taratibu zake na kama walikuwa wanataka kuingia walipaswa kufuata taratibu.

 

“Wafugaji walioingia kinyume cha utaratibu wataondolewa na tumepata taarifa kuwa baadhi ya mgambo wamekuwa wakihusika kuwaingiza wafugaji hao kinyume cha utaratibu pale Mto Wami,” alisema Mwanga.

 

Aidha alisema kuwa wale wote wanaohusika kuwaingiza wafugaji hao kinyume cha utaratibu watashughulikiwa kwani wanataka kutoletea matatizo.

 

Mwisho.