Sunday, July 27, 2014

MEYA AWATAKA WAISLAMU KUDUMIASHA AMANI NA UPENDO IDDI



Na John Gagarini, Bagamoyo
WAISLAMU kote nchini wametakiwa kusherehekea sikuu ya Eid el Fitr kwa upendo na amani ili funga yao ya mwezi mzima iwe na maana na kuacha kufanya vitendo viovu ambavyo ni kinyume na mapenzi ya Mungu.
Ushauri huo umetolewa jana mjini Bagamoyo na meya wa Mji wa huo Abdul Sharifu, wakati alipokuwa akifuturisha watu wenye mahitaji maalumu na waumini wa dini hiyo kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.
Sharifu alisema kuwa funga hiyo itakuwa na maana endapo waislamu wataisherehekea kwa kuzingatia imani ya dini ya kiislamu na si kinyume na dini inavyosema.
“Baadhi ya waislamu wamekuwa wakiitumia siku hiyo kwa ajili ya kufanya matendo ambayo hayampendezi mwenyezi Mungu hali ambayo inafanya waonekane mbele ya Mwenyezi Mungu kuwa hawakufunga kutokana na kwenda kinyume na imani inavyosema,” alisema Sharifu.
Alisema kuwa pia watumie siku hiyo kwa ajili ya kujitolea kuwasaidia  watu wenye mahitaji maalumu kama vile watu wenye ulemavu, yatima, wajane na wagonjwa na watu wenye shida mbalimbali ili iwe sadaka ambayo itampendeza Mungu.
Sharifu ambaye pia ni mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wilaya ya Bagamoyo aliwataka waumini wa dini hiyo na wale wasio wa imani hiyo kuitumia siku hiyo kwa ajili ya kumtafakari mwenyezi Mungu.
 Wakati huo huo wenye uwezo mkoani Pwani wametakiwa kumtukuza Mungu katika kipindi cha siku kuu ya Eid el Fitr kwa kuwasaidia watu wenye mahitaji ili wapate thawabu mbele ya mwenyezi Mungu.
Hayo yalisemwa jana mjini Kibaha na msaidizi wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Mkoani Pwani, Method Mselewa  ambaye alimwakilisha mbunge huyo Silvestry Koka wakati wa kutoa mkono wa Iddi kwa waumini wa dini ya Kiislamu kutoka misikiti mbalimbali wilayani hapa.
Mselewa alisema kuwa kutoa wakati wa kipindi hichi ni sadaka ambayo ina manufaa makubwa kwa waislamu hivyo wawe na moyo wa kuwasaidia watu wenye uhitaji ili nao wajisikie kama kuna watu wanawajali.
“Mbunge kila mwaka kipindi kama hichi amekuwa akijitolea kwa makundi hayo ambayo ni pamoja na wazee, yatima, wajane na wale wasiojiweza ambapo kila msikiti wanatoka watu 20 ili nao waweze kuandaa futari kwa familia zao,” alisema Mselewa.
Alisema kuwa waumini hao wanatoka kwenye misikiti 64 iliyopo katika Jimbo la Kibaha ambapo kila mmoja anapewa mkono wa Iddi ambao ni mchele kilogramu mbili, sukari kilogramu moja na fedha kwa ajili ya kununulia mboga.
Aidha alisema kuwa mbali ya kuwapatia vitu hivyo pia huwapatia ujumbe wa Iddi wa kudumisha amani, upendo na ushirikiano kwa watu wote katika kipindi hichi na nyakati zingine ambazo si za mfungo.
Alibainisha kuwa mbali ya makundi hayo pia mkono wa Iddi unatolewa kwa viongozi wa chama wakiwemo wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Wilaya, Baraza la Wanawake (UWT), Baraza la Wazazi na Umoja wa Vijana (UVCCM) ambapo jumla ya watu 2,000 watafikiwa.
Mwisho.
     

Saturday, July 26, 2014

PICHA MBALIMBALI ZA MATUKIO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU MKOANI PWANI

MWENGE UKIWASILI WILAYA YA MKURANGA
MKUU WA WILAYA YA RUFIJI NURDIN BABU AKIWA AMEBEBA MWENGE

MKUU WA WILAYA YA RUFIJI NURDIN BABU AKIMKABIDHI MWENGE WA UHURU MKUU WA WILAYA YA MKURANGA MERCY SILA


 KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA RACHEL KASANDA AKIWEKA JIWE LA MSINGI KWENYE MOJA YA MIRADI ALIYOIZINDUA

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA RACHEL KASANDA AKIPANDA MTI KWENYE UZINDUZI WA NYUMBA ZA WALIMU WILAYANI MKURANGA

 KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE TAIFA RACHEL KASANDA AKIMWAGILIA MTI BAADA YA KUUPANDA HUKO MKURANGA

 KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA RACHEL KASANDA AKIANGALIA JIWE LA MSINGI BAADA YA KUZINDUA MNADA WA NGOMBE HUKO MKURANGA

 RACHEL KASANDA KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE TAIFA RACHEL KASANDA AKIMWAGIA MAJI KWNYE MTI ALIOUPANDA

 WAMASAI WAKICHEZA KWA FURAHA BAADA YA KUZINDULIWA MNADA WA NGOMBE HUKO MKIU MKURANGA

 MOJA YA WAKIMBIZA MWENGE KITAIFA WITO MNEMWELA AKIWAPA WAZEE MWENGE WAUGUSE HUKO KWENYE KIJIJI CHA MKANOGE WILAYA YA MKURANGA


 BAADHI YA WACHEZA NGOMA WA KIKUNDI KUTOKA WILAYA YA KISARAWE WAKITOA BURUDANI KWENYE MTAA WA KIPANGEGE WILAYA YA KIBAHA

 WATOTO AMBAO NI SKAUTI WA WILAYANI KIBAHA WKIWA WAMESIMAMA KWA UKAKAMAVU KUSUBIRI MWENGE

 KUSHOTO MKUU WA WILAYA YA KISARAWE FATUMA KIMARIO AKIMKABIDHI MWENGE MKUU WA WILAYA YA KIBAHA HALIMA KIHEMBA KULIA KWENYE MTAA WA KIPANGEGE

 MKUU WA WILAYA YA KIBAHA AKIONGEA MBELE YA MBUNGE WA JIMBO LA KIBAHA VIJIJNI ABUU JUMAA, HUKU KUSHOTO KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA RACHEL KASANDA AKISIKILIZA KWA MAKINI KUSHOTO NA KULIA NI MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBAHA TATU SAID

 BAADHI YA WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI KIPANGEGE WILAYANI KIBAHA WAKIPEPERUSHA BENDERA KUUPOKEA MWENGE

 ASKARI MAGEREZA KULIA AKIPOKEA MWENGE ULIPOINGIA WILAYANI KIBAHA

 ASKARI MAGEREZA WA MKOA WA PWANI WAKIJIPANGA KUPOKEA MWENGE WA UHURU ULIPOINGIA WILAYA YA KIBAHA

 KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA AKIJIANDAA KUPOKEA TAARIFA KWA MOJA YA WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI YA RAFSANJANI ILIYOPO WILAYANI KIBAHA

 KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA RACHEL KASANDA AKIWA NA BAADHI YA VIONGOZI WA WILAYA YA KIBAHA KWENYE SHULE YA SEKONDARI RAFSANJANI

 KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA RACHEL KASANDA AKIHUTUBIA WANANCHI WA WILAYA YA MKURANGA

 KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA RACHEL KASANDA KUSHOTO AKIVISHWA SKAFU NA MOJA YA VIJANA WALIPOKUWA WAKIPOKEWA WILAYANI MKURANGA

WENYE UWEZO WAWASAIDIE WENYE MAHITAJI



Na John Gagarini, Kibaha
WATU wenye uwezo mkoani Pwani wametakiwa kumtukuza Mungu katika kipindi hichi cha mfungo mtukufu wa Ramadhan kwa kuwasaidia watu wenye mahitaji ili wapate thawabu.
Hayo yalisemwa jana mjini Kibaha na msaidizi wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Mkoani Pwani, Method Mselewa  ambaye alimwakilisha mbunge huyo Silvestry Koka wakati wa kutoa mkono wa Iddi kwa waumini wa dini ya Kiislamu kutoka misikiti mbalimbali wilayani hapa.
Mselewa alisema kuwa kutoa wakati wa kipindi hichi ni sadaka ambayo ina manufaa makubwa kwa waislamu hivyo wawe na moyo wa kuwasaidia watu wenye uhitaji ili nao wajisikie kama kuna watu wanawajali.
“Mbunge kila mwaka kipindi kama hichi amekuwa akijitolea kwa makundi hayo ambayo ni pamoja na wazee, yatima, wajane na wale wasiojiweza ambapo kila msikiti wanatoka watu 20 ili nao waweze kuandaa futari kwa familia zao,” alisema Mselewa.
Alisema kuwa waumini hao wanatoka kwenye misikiti 64 iliyopo katika Jimbo la Kibaha ambapo kila mmoja anapewa mkono wa Iddi ambao ni mchele kilogramu mbili, sukari kilogramu moja na fedha kwa ajili ya kununulia mboga.
“Watu wamekuwa wakifuturisha kwa kuwalisha watu chakula lakini Mbunge kaamua kubadili staili kwa kuwapa vyakula hivyo ambapo wao watenda kuziandalia familia zao tofauti na kuwapa chakula ambapo watakaokula ni wachache tofauti na watakapopeleka nyumbani kuandaa wenyewe kwani yeye hawezi kuja na familia balia atakuja mtu mmoja,” alisema Mselewa.
Aidha alisema kuwa mbali ya kuwapatia vitu hivyo pia huwapatia ujumbe wa Iddi wa kudumisha amani, upendo na ushirikiano kwa watu wote katika kipindi hichi na nyakati zingine ambazo si za mfungo.
Alibainisha kuwa mbali ya makundi hayo pia mkono wa Iddi unatolewa kwa viongozi wa chama wakiwemo wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Wilaya, Baraza la Wanawake (UWT), Baraza la Wazazi na Umoja wa Vijana (UVCCM) ambapo jumla ya watu 2,000 watafikiwa.
Mwisho.
     

Sunday, July 20, 2014

MGOMO WA WACHINJAJI NGOMBE WAISHA



Na John Gagarini, Kibaha
HATIMAYE ule mgomo wa wachinjaji ngombe na wamiliki wa mabucha wilayani Kibaha mkoani Pwani umekwisha baada ya pande mbili zilizokuwa zikitofautia Halmashauri ya Mji wa Kibaha na wamiliki wa mabucha hayo chini ya mkuu wa wilaya ya Kibaha Halima Kihemba kukaa meza moja na kumaliza mgomo huo uliodumu kwa muda wa siku mbili kuanzia Julai 18 hadi 19.
Mgomo huo ambao uliendeshwa na wamiliki hao wa mabucha ambao ndiyo wachinjaji wa ng’ombe kupitia Umoja wa wafanyabiashara wa nyama na mazao yake wilayani Kibaha  (UWABINK) walifanya mgomo wa kuuza nyama kwa mji wa Kibaha na vitongoji vyake kwa madai kuwa machinjio mpya ya Mtakuja waliohamishiwa haina huduma muhimu ikiwemo maji huku wakitaka kutumia ile ya zamani ya Maili Moja.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jana mjini Kibaha kwa njia ya simu mkuu wa wilaya ya Kibaha Kihemba alisema kuwa kulitokea tofauti baina ya pande hizo mbili hali iliyosababisha mgomo huo ambao uliathiri walaji wa nyama wa mji huo na maeneo ya wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam.
Kihemba alisema kuwa suala la maji pande hizo zimekubaliana Halmashauri watanunua maji kwa kipindi cha wiki moja na UWABINK nao watanunua wiki moja hivyo watapeana zamu ya kununua maji hadi suala hilo litakapopatiwa ufumbuzi ambapo halmashauri imetenga kiasi cha shilingi milioni 19 kwa ajili ya kuchimba kisima kirefu cha maji Septemba mwaka huu.
“Muafaka ni kwamba waendelee kuchinja kwenye machinjio ya zamani kwa muda wa siku tatu kuanzia Julai 20 hadi Julai 22 kisha wahamie kule, kwani kwa kipindi hicho taayari marekebisho yatakuwa yamefanywa na maji watashirikiana kununua,” alisema Kihemba.
Aidha alisema kuwa baada ya siku tatu watatakiwa hamie huko machinjio mpya na ile ya zamani itabomolewa ili kupisha shughuli nyingine kwenye eneo hilo hivyo anaamini muafaka huo utaondoa msuguano uliojitokeza.
“Kuhusu zizi walikuwa hawajajenga hivyo wajenge zizi hilo katika kipindi hicho walichokubaliana ambapo waliingia mkataba wa uendeshaji ambapo wao wanachinja halmashauri wao ni wa miliki wa miuondombinu na wao hulipa ushuru kwa kila mwezi ni zaidi ya shilingi milioni moja,” alisema Kihemba.
Kwa upande wake msemaji wa umoja huo Athumani Mkanga alisema waliamua kufanya mgomo huo kupinga kuhamishiwa kwenye machinji hayo ya Mtakuja kutoka yale ya Maili Moja kwani yalikuwa hayajakamilika na hayakuwa na huduma muhimu ikiwemo maji na umeme ambapo ule wa jua hautakidhi mahitaji yao.
Mkanga alisema kuwa walikaa meza moja na halmashauri chini ya mkuu wa wilaya ambaye alikuwa mwenyekiti na kukubaliana kuwa watashirikiana katika masuala mbalimbali kwenye machinjio hayo mapya.
“Tumekubaliana baadhi ya mambo ikiwemo sula la maji ambapo tutayanunua kwa zamu wakati wao wanaendelea na utaratibu wa kuchimba kisima kirefu ili kukabiliana na tatizo la maji na masuala mengine,” alisema Mkanga.
Alibainisha kuwa wamekubaliana na marekebisho hayo lakini wanachokitaka ni kuboreshwa kwa huduma ili waweze kufanya shughuli zao bila ya kikwazo chochote lengo likiwa ni kutoa huduma bora kwa walaji.
Mwisho.

Picha zikionyesha machinjio mpya ya Mtakuja iliyopo kata ya Pangani wilayani Kibaha mkoani Pwani ambayo wachinjaji na wamiliki wa mabucha mjini Kibaha waliigomea wakidai kuwa baadhi ya miundombinu yake haijakamilika ikiwemo maji.

Friday, July 18, 2014

RIDHIWANI ATOA MSAADA POLISI



Na John Gagarini, Chalinze

KATIKA kuhakikisha Jeshi la Polisi linafanya kazi kwa teknolojia ya kisasa Mbunge wa jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani  Ridhiwani Kikwete ametoa msaada wa kompyuta na mashine za kutolea kopi zenye thamani ya shilingi milioni 11 kwa kanda maalumu ya kipolisi ya Wilaya ya Chalinze.

Msaada huo wa kompyuta, na mashine ya kutolea kopi utasaidia kuhifadhi nyaraka za kipolisi na pia kuachana na usumbufu wa kutumia steshenari zilizopo nje ya ofisi yao.

Akikabidhi msaada huo wa kompyuta pamoja na fedha taslimu kwa kamanda wa polisi wa mkoa wa Pwani Ulrich Matei, Ridhiwani alisema lengo ni uboreshaji wa vituo vya polisi katika jimbo hilo.

“Kwa kuwa kituo hichi cha polisi Chalinze kimepandishwa hadhi na kuwa cha wilaya bado kinakabiliwa na changamoto ya uwepo wa ofisi ndogo ambayo haikidhi mahitaji na kusababisha kutumia kontena kufanyia kazi nyingine za kiofisi nimetoa kwa ajili ya siri za kiofisi badala ya kufanyia kazi nje ya kituo,” alisema Ridhiwani.

Ridhiwani alisema kuwa siri nyingi za ofisi zilikuwa zikivuja kutokana na kazi kufanyiwa nje ya ofisi jambo ambalo lilikuwa likisababisha uvujaji wa taarifa hivyo kushindwa kufanikiwa kudhibiti uhalifu kikamilifu.

Kwa upande wake  Kamanda Matei  alimshukuru mbunge huyo na kusema kuwa kituo cha Chalinze ambacho kimepandishwa hadhi na kuwa cha kiwilaya kwasasa ni kipya na
hivyo kinahitaji maboresho mengi ambapo aliahidi kudumisha ushirikiano ili kusaidiana katika kutatua changamoto nyingine za vituo hivyo.

Naye Diwani wa kata ya Bwilingu Nasa Karama alimueleza mbunge huyo kuwa  tangu kituo hicho kipandishwe hadhi na kuwa cha wilaya, shughuli nyingi zimeongezeka na hivyo kuwa na kazi kubw aya kuzuia uhalifu

“Tunashukuru kwa msaada huu pia tunaomba msaada wa kujengewa nyumba kwa ajili askari kwani wengi wa kituo hicho hawana nyumba za kuishi na hivyo kulazimika kupanga uraiani na kusababisha utendaji kazi kupungua.

Misaada iliyokabidhiwa kwa jeshi hilo ni pamoja na shilingi Milioni
tatu kwa ajili ya kituo cha polisi Mbwewe, mifuko ya saruji 20 na
shilingi 350,000 kwa ajili ya kuharakisha ujenzi wa kituo cha polisi
Kiwangwa pamoja na kompyuta na mashine ya kutolea kopi kwa ajili ya
kituo cha Chalinze.

Mwisho.