Wednesday, December 26, 2012

TOENI MISAADA KWA WATU WENY UHITAJI NA SI KUFANYA ANASA


Na John Gagarini, Kibaha

JAMII nchini imetakiwa kutoa misaada kwa watu wenye uhitaji katika kipindi cha sikukuu badala ya kuzitumia kwa anasa.

Hayo yalisemwa na Bi Mwajuma Yasini wakati akishukuru kupewa misaada iliyotolewa kwenye sikukuu ya Krismasi kwenye hopsitali ya wilaya ya Kibaha Tumbi.

Bi Yasini alisema kuwa baadhi ya watu wamekuwa wakitumia vibaya fedha kwenye sikukuu kama hizo kwa kufanya vitendo vya kifahari huku watu wenye uhitaji wakiwa hawana msaada.

“Ni vema Watanzania wangetumia sikuu kwa kutoa misaada kwa watu wenye mahitaji wakiwemo watoto waishio kwenye mazingira magumu, yatima na wagonjwa,” alisema.

Aidha alisema kuwa ibaada ya kweli ni kuwakumbuka watu wenye uhitaji ambapo wao kama wagonjwa kwao imekuwa faraja katika sikukuu hii ya Krismasi.

Kwa upande wake mwandishi wa habari na Diwani Viti Maalumu Kibaha Mjini (CCM) Bi Selina Wilson ambaye ndiye aliyetoa misaada hiyo alisema kuwa alitoa ikiwa ni kama ibaada kwa watu wenye mahitaji.

“Niliona niungane na wagonjwa kwa kuwapatia zawadi za Krismasi ili nao wajione kuwa jamii ina wajali na iko pamoja katika hali zote ikiwa ugonjwa na furaha,” alisema Bi Wilson.

Naye muuguzi wa zamu wa hospitali ya Tumbi Bi Ndenisaria Ntuah alisema wagonjwa nao wanahitaji kufarijiwa kwa kupewa misaada mbalimbali.

Misaada hiyo ilitolewa kwenye wodi za watoto, wazazi na wanawake na wanaume wenye magonjwa ya kawaida, misaada iliyotolewa ni sabuni, mafuta ya kujipaka, juisi na biskuti

Mwisho.

Monday, December 24, 2012

WALIONUNUA MAENEO YA WAZI KUSHUGHULIKIWA


Na John Gagarini, Bagamoyo
MJI Mdogo wa Bagamoyo mkoani Pwani umewataka watu wote walionunua maeneo ya wazi kwenye kata ya Magomeni na kujenga nyumba waondoke kabla ya hatua za kisheria kuchukuliwa dhidi yao.
Akizungumza na wakazi wa kitongoji cha Magomeni wilayani humo Meya wa Mji huo Bw Abdul Sharifu alisema kuwa kwa kushirikiana na baadhi ya maofisa wa ardhi wasio waaminfu wamenunua maeneo hayo kinyume cha sheria.
Bw Sharifu alisema kuwa maeneo yote ya wakazi katika kata ya Magomeni yameuzwa yote kinyume cha sheria jambo ambalo linasababisha kata hiyo kushindwa kupewa miradi ya maendeleo kwa ajili ya huduma za kijamii.
“Wale wote walionunua maeneo hayo ya wazi waondoke mara moja kwani endapo hawataondoka wataondolewa kwa nguvu kwani haiwezekani tukakosa eneo kwa ajili ya huduma za kijamii kutokana na watu ambao wanavunja sheria hivyo lazima waondoke,” alisema Bw Sharifu.
Aidha alisema kuwa tayari baraza hilo limewaagiza watu wa ardhi kuyaainisha maeneo yote yale ya wazi ambayo yameuzwa.
“Wilaya ina eneo kubwa lakini cha kushangaza watu wananunua maeneo ya wazi ambayo yametengwa kwa ajili ya huduma za jamii lakini baadhi ya watu wenye kutaka maslahi yao binafsi wanavunja sheria,” alisema Bw Sharifu.
Alisema kwa sasa wanataka kujenga soko na zahanati lakini hakuna eneo la wazi kwa ajili ya kujenga vitu hivyo kutokana na maeneo hayo kuhujumiwa hivyo watu wengi kukosa fursa ya kujengewa miundombinu.
Aliwataka maofisa ardhi watakaotembelea maeneo hayo kuyaanisha maeneo hayo kwa kutumia ramani za zamani ili kubaini watu waliokiuka taratibu za ujenzi kwa kujenga maeneo ya wazi.
Mwisho.
      

BAGAMOYO YAKABILIWA NA UHABA WA MADAWATI


Na John Gagarini, Bagamoyo
KATA ya Talawanda wilayani Bagamoyo mkoani Pwani imetenga hekta 13,000 kwa ajili ya matumizi bora ya ardhi kwa wakulima na wafugaji ili kuondoa migogoro baina ya pande mbili hizo.
Hayo yalisema na diwani wa kata hiyo Bw Said Zikatimu kwenye Kijiji cha Talawanda wakati wa mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Jumuiya ya Wazazi ya wilaya hiyo kujua kero zinazowakabili wakazi wa kata hiyo.
Bw Zikatimu alisema kuwa maeneo hayo yalitengwa na halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo katika mpango wa matumizi bora ya ardhi ili kupunguza vurugu zinazotokea mara kwa mara.
“Kati ya hekta hizo 13,000 wafugaji wametengewa hekta 5,800 huku wakulima wakitengewa hekta 9,200 kupitia mpango huo ambao utawafanya makundi hayo kuishi kwa amani,” alisema Bw Zikatimu.
Alisema mpango huo uko kwenye vijiji vya Talawanda na Magulumatali ambapo utaeneo kwenye vijiji vingine kadri suala la fedha litakapokuwa liko sawa.
“Kutokana na mpango huu wafugaji wamepewa muda wa miezi mitatu kuondoka na kwenda kwenye eneo lao lililotengwa na serikali na endapo watashindwa kuondoka wataondolewa kwa nguvu,” alisema Bw Zikatimu.
Aidha alisema wafugaji walioingia kwenye kata hiyo kwa ajili ya malisho kuondoka haraka ili kuondoa migogoro baina ya wakulima na wafugaji.
Aliwataka wakulima na wafugaji kila moja akae kwenye eneo lililopangwa kwa lengo la kuondoa mizozo isiyona na lazima.
Mwisho.

Na John Gagarini, Bagamoyo
KATA ya Talawanda wilayani Bagamoyo mkoani Pwani imetenga hekta 13,000 kwa ajili ya matumizi bora ya ardhi kwa wakulima na wafugaji ili kuondoa migogoro baina ya pande mbili hizo.
Hayo yalisema na diwani wa kata hiyo Bw Said Zikatimu kwenye Kijiji cha Talawanda wakati wa mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Jumuiya ya Wazazi ya wilaya hiyo kujua kero zinazowakabili wakazi wa kata hiyo.
Bw Zikatimu alisema kuwa maeneo hayo yalitengwa na halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo katika mpango wa matumizi bora ya ardhi ili kupunguza vurugu zinazotokea mara kwa mara.
“Kati ya hekta hizo 13,000 wafugaji wametengewa hekta 5,800 huku wakulima wakitengewa hekta 9,200 kupitia mpango huo ambao utawafanya makundi hayo kuishi kwa amani,” alisema Bw Zikatimu.
Alisema mpango huo uko kwenye vijiji vya Talawanda na Magulumatali ambapo utaeneo kwenye vijiji vingine kadri suala la fedha litakapokuwa liko sawa.
“Kutokana na mpango huu wafugaji wamepewa muda wa miezi mitatu kuondoka na kwenda kwenye eneo lao lililotengwa na serikali na endapo watashindwa kuondoka wataondolewa kwa nguvu,” alisema Bw Zikatimu.
Aidha alisema wafugaji walioingia kwenye kata hiyo kwa ajili ya malisho kuondoka haraka ili kuondoa migogoro baina ya wakulima na wafugaji.
Aliwataka wakulima na wafugaji kila moja akae kwenye eneo lililopangwa kwa lengo la kuondoa mizozo isiyona na lazima.
Mwisho.

Sunday, December 23, 2012

johnnygagarini@yahoo.co.uk
Na John Gagarini, Bagamoyo
WAFUGAJI wote waliovamia kwenye vijiji mbalimbali kwa ajili ya malisho ya mifugo wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wametakiwa kuondoka ili kuepusha migogoro baina ya wakulima na wafugaji.
Hayo yalisemwa na Meya wa Mji Mdogo wa Bagamoyo Bw Abdul Sharifu kwenye Kijiji cha Kwamduma wakati wa ziara yake kutembelea wilaya hiyo kubaini changamoto zinazowakabili wakazi wa wilaya hiyo, kupitia Jumuiya ya Wazazi (CCM) ya wilaya.
Bw Sharifu alisema kuwa kero ya wafugaji kuingia wilayani humo imekuwa kubwa na kusababisha migogoro kutokana na wafugaji kulisha mifugo kwenye mashamba ya wakulima.
“Kuanzia sasa wale wafugaji wote walioingia katika wilaya hii kwa ajili ya kutafuta malisho waondoke ili kuepusha vurugu ambazo zimekuwa zikitokea mara kwa mara kwa mazao kuharibiwa na mifugo hiyo,” alisema Bw Sharifu.
Alisema kuwa kila kijiji alichotembelea kilio kimekuwa ni wafugaji ambao wamekuwa wakiingiza makundi makubwa ya mifugo hasa ngombe wakitokea mikoa mingine.
“Huko tunakoelekea hali ya amani inaweza kuvurugika kutokana na ngombe kuharibu mazao ya wakulima ambapo wafugaji ambao wamevamia wilaya hii wakitafuta malisho lakini hata hivyo hawathamini wakulima,” alisema Bw Sharifu.
Meya huyo ambaye pia ni mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Bagamoyo alisema kuwa suala la mifugo ndani ya wilaya hiyo limekuwa chanagamoto kubwa kwa viongozi wa wilaya hiyo.
Aidha alisema katika kukabuilina na changamoto hiyo halmashauri imeanzisha mpango wa matumizi bora ya ardhi kwa baadhi ya vijiji ambapo yametengwa maoeneo ya wakulima na wafugaji.
Mwisho.   

WAFUGAJI WATAKIWA KUONDOKA


Na John Gagarini, Bagamoyo
WAFUGAJI wote waliovamia kwenye vijiji mbalimbali kwa ajili ya malisho ya mifugo wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wametakiwa kuondoka ili kuepusha migogoro baina ya wakulima na wafugaji.
Hayo yalisemwa na Meya wa Mji Mdogo wa Bagamoyo Bw Abdul Sharifu kwenye Kijiji cha Kwamduma wakati wa ziara yake kutembelea wilaya hiyo kubaini changamoto zinazowakabili wakazi wa wilaya hiyo, kupitia Jumuiya ya Wazazi (CCM) ya wilaya.
Bw Sharifu alisema kuwa kero ya wafugaji kuingia wilayani humo imekuwa kubwa na kusababisha migogoro kutokana na wafugaji kulisha mifugo kwenye mashamba ya wakulima.
“Kuanzia sasa wale wafugaji wote walioingia katika wilaya hii kwa ajili ya kutafuta malisho waondoke ili kuepusha vurugu ambazo zimekuwa zikitokea mara kwa mara kwa mazao kuharibiwa na mifugo hiyo,” alisema Bw Sharifu.
Alisema kuwa kila kijiji alichotembelea kilio kimekuwa ni wafugaji ambao wamekuwa wakiingiza makundi makubwa ya mifugo hasa ngombe wakitokea mikoa mingine.
“Huko tunakoelekea hali ya amani inaweza kuvurugika kutokana na ngombe kuharibu mazao ya wakulima ambapo wafugaji ambao wamevamia wilaya hii wakitafuta malisho lakini hata hivyo hawathamini wakulima,” alisema Bw Sharifu.
Meya huyo ambaye pia ni mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Bagamoyo alisema kuwa suala la mifugo ndani ya wilaya hiyo limekuwa chanagamoto kubwa kwa viongozi wa wilaya hiyo.
Aidha alisema katika kukabuilina na changamoto hiyo halmashauri imeanzisha mpango wa matumizi bora ya ardhi kwa baadhi ya vijiji ambapo yametengwa maoeneo ya wakulima na wafugaji.
Mwisho.