Thursday, January 9, 2025
LICHA YA KUKUTANA NA UKATILI WA KIJINSIA MBONI AUKABILI AWAGARAGAZA WANAUME
Monday, January 6, 2025
MTAA WA MIEMBE SABA WAWEKA VIFUSI KUBORESHA BARABARA YA MTAA
MTAA wa Miembe Saba B Wilayani Kibaha Mkoani Pwani umezanza zoezi la kuweka vifusi kwenye barabara ya Mtaa ili kuwaondolea kero wananchi wa Mtaa huo.
Sunday, January 5, 2025
WAHUKUMIWA MAISHA NA MIAKA 20 KWA UKATILI WA KIJINSIA
WATUHUMIWA wawili Mkoani Pwani waliokuwa wanakabiliwa kwa kesi za ukatili wa kijinsia wamehukimiwa vifungo tofauti ambapo mmoja amefungwa kifungo cha maisha jela na mwingine amefungwa kifungo cha miaka 20 jela.
Aidha jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani lilipeleka Mahakamani kesi 125 za makosa mbalimbali ambapo kati ya kesi hizo 47 zimepata mafanikio kwa watuhumiwa kuhukumiwa vifungo mbalimbali.
Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani ACP Salim Morcase alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya mafanikio ya jeshi hilo kwa kipindi cha mwezi Disemba 2024.
Morcase amesema kuwa jumla ya kesi za ukatili wa kijinsia kulikuwa na kesi tano za makosa ya kubaka na kulawiti.
"Watuhumiwa hao wawili walipata adhabu hizo ambapo wa kwanza alipatikana na hatia ya kubaka na kulawiti na wa pili alikutwa na hatia ya unyanyasaji wa kingono,"amesema Morcase.
Amesema kuwa watuhumiwa 52 wamehukumiwa vifungo tofauti tofauti kutokana na aina ya makosa yaliyokuwa yakiwakabili.
MADEREVA 11 MKOANI PWANIWAFUNGIWA LESENI
COREFA KUJENGA OFISI UWANJA WAKE
COREFA KUANDAA VIJANA KWENYE VITUO KILA WILAYA
CHAMA Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) kimesema kitahakikisha kila Wilaya inakuwa na kituo cha kuandaa vijana ili kuzalisha wachezaji watakaokuja kulitumikia Taifa.
COREFA KUANDAA VIJANA KUPITIA VITUO KILA WILAYA
CHAMA Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) kimesema kitahakikisha kila Wilaya inakuwa na kituo cha kuandaa vijana ili kuzalisha wachezaji watakaokuja kulitumikia Taifa.