Thursday, January 9, 2025

LICHA YA KUKUTANA NA UKATILI WA KIJINSIA MBONI AUKABILI AWAGARAGAZA WANAUME


KWENYE uchaguzi wa serikali za mitaa ambao ulifanikisha kupatikana kwa wenyeviti na wajumbe baadhi ya wanawake walijitokeza kuwania nafasi hizo na kushindana na wanaume ambapo wanawake baadhi yao walijikuta katika wakati mgumu kwa kukumbana na ukatili wa kijinsia hasa kashfa kutoka kwa wanaume na hata wakati mwingine toka kwa wanawake wenzao.

Hali hiyo inatokana na mfumo dume ambao unamkandamiza mwanamke asiweze kupaza sauti kupitia kwenye nafasi ya uongozi hata hivyo hali hiyo ya mfumo dume kadiri miaka inavyokwenda mbele changamoto hiyo inapungua licha ya kwamba bado haijaisha ndani ya jamii.

Licha ya kuwa mjane na kukumbana na changamoto za kunyanyaswa kijinisa na baadhi ya wagombea na wapiga kura lakini haikumkatisha tamaa, licha ya kwamba maneno aliyokuwa akikashifiwa nayo yalimuumiza sana lakini alivumilia.Huyo siyo mwingine bali ni mwenyekiti wa mtaa wa Bamba Halmashauri ya Mji Kibaha Mkoani Pwani Mboni Mkomwa kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambaye alishinda kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika mwishoni mwa mwaka 2024 ambapo alishinda akiwa ni mgombea pekee kwani hakukuwa na mgombea kutoka vyama vya upinzani.

Mboni alisema kuwa alipata kashfa sana wakati wanaendelea na kampeni ndani ya chama ilifika wakati alitaka hata kujitoa kwenye uchaguzi sababu hakuwahi kupata kashfa kama hizo kwa kama mtu hana moyo anaweza kujitoa ili aepukanane na kashfa kwa kweli uchaguzi una mambo mengi sana ya kukatisha tamaa kuwa mwanamke hawezi kuongoza na mtaa haujawahi kuongozwa na mwanamke hivyo awaachie wanaume.

“Nilishangaa kuona hata baadhi ya wagombea wenzangu wanaume walikuwa wakinitolea maneno ya kashfa lakini nashukuru wananchi hawakujali kashfa hizo lakini walinipa kura za kutosha na kuwashinda wanaumewawili na sisi wanawake tulikuwa wawili ambao tulikuwa tunashindana nao,”alisema Mkomwa.

Kwenye uchaguzi huo wa ndani ya chama Mkomwa alipata kura 269 aliyemfuatia alikuwa mwanaume aliyepata kura 171 huku mwanamke mwenzake akipata kura 93 na kumfanya apate nafasi ya kukiwakilisha chama kwenye uchaguzi wa serikali ya mtaa huo na yeye kuwa mshindi.  

“Suala la rushwa ikiwemo ya ngonio kipindi cha uchaguzi ipo lakini mimi nilifanya kampeni bila ya kutoa fedha niliwaambia wanichague niwaletee maendeleo lakini fedha za kuwapa sina nashukuru walinielewa na kunipa nafasi hiyo na kuwanyima wanaume ambao walijivunia jinsi yao,”alisema Mkomwa.     

Alisema kuwa wakati akiomba kura aliweka vipaumbele ambavyo atavifanyia kazi wakati wa uongozi wake ni pamoja na ujezi wa vyoo vya shule ya sekondari Bamba inakamilika ili mwaka huu 2025 ifunguliwe na kupokea wanafunzi zaidi ya 100 wa mtaa huo ambao wanasoma shule za sekondari za mbali ambapo hutembea umbali wa kilometa sita kwenda na kurudi shuleni. 

Alisema kuwa wanaishukuru serikali ambayo ilitoa kiasi cha shilingi milioni 50 kwa ajili ya ujenzi huo pia wananchi nao walichangia kila kaya 2,000 na kufanikisha ujenzi huo kufikia hapo na kubaki hatua ndogo ili ianze ikiwa ni ukosefu wa matundu nane.

“Tuliomba tena fedha Halmashauri milioni 12 kwa matundu sita ila walituambia kuwa tusubiri na wanafunzi waendelee kusoma huko lakini mara fedha zitakapoingia wanafunzia hao watahamishiwa shuleni hapo ndiyo tunasubiri tunataka wanafunzi wanaotoka kwenye mtaa wetu waanze kusoma hapo pia itasaidia maeneo ya mitaa jirani ambao nao watanufaika,”alisema Mkomwa.

Alisema kuwa changamoto nyingine ambayo iko kwenye mipango yake katika kuitatua ni baadhi ya wakazi wa mtaa wake wapatao 23 hawana huduma ya maji kabisa hali ambayo inawasababisha kupata shida ya kupata maji kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya kawaida.

Alisema kuwa jambo lingine ni kuwa na stendi  ya mabasi kwani sasa hakuna sehemu nzuri ya mabasi kugeuzia ambapo Kongowe ni mwisho wa ruti za baadhi ya mabasi huwa yanageuzia hapo hivyo wanaongea na Wakala wa Barabara Tanzania Tanroads kuwapatia eneo la hifadhi ya barabara kwenye kituo cha mafuta cha Tawaqal kuwa na stendi hapo na ndoto yake pia ni kujenga zahanati kwenye mtaa huo ndiyo ndoto yake kabla hajamaliza uongozi wake.

“Hivi ni baadhi ya vipaumbele ambavyo nilijiwekea na haya yametokana nay ale wananchi waliyokuwa wakiayuliza kipindi cha kampeni ndiyo nimeanza nayo lakini uongozi wangu utakuwa shirikishi kwani wananchi wao ndiyo watakaokubaliana tuende na jambo gani la kimaendeleo,”alisema Mkomwa.

Alisema kuwa yeye alikuwa mjumbe wa serikali ya mtaa huo kwa kipindi cha miaka mitano na alikuwa pia Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) tawi la Bamba na alikuwa akitumiwa akimwakilisha mwenyekiti aliyepita ambaye ni marahemu Majid Kavuta ndiyo aliyemhamasisha kuwa kiongozi na hata watu walikuwa wakimwambia agombee nafasi hiyo.

“Pia Rais Dk Samia Suluhu Hassan alinihamasisha sana kuwa kiongozi kutokana na jinsi anavyoongoza nchi na Spika wa Bunge Tulia Akson naye ni moja ya watu waliokuwa kioo kwangu na moja ya vitu vilivyonifanya nichaguliwe ni jinsi nilivyokuwa nawasaidia wananchi na ilinibidi niingie kwenye siasa baada ya mume wangu kufariki dunia nikasema sasa nitajiliwaza wapi ndiyo kuingia japo ndugu zangu hawakupenda mimi kuingia kwenye siasa,”alisema Mkomwa.

Alibainisha akiwa mjumbe wa serikali ya mtaa na kiongozi wa UWT alisaidia sana wanawake na vijana na watu wenye ulemavu kupata mikopo ya Halmashauri ya asilimia 10 na moyo wa kuwasaidia pindi wajapo ofisini na alikuwa akisaidia vijana ikiwa ni pamoja na kwenye msuala ya michezo na vijana walimwambia wanataka awe mlezi wa mtaa huo ili awasidie.

“Nawasihi wanawake wasiwe na hofu ya kuwania nafasi ya uongozi wapambanie ndoto zao ili kufikia malengo waliyojiwekea na waachane na maneno ya kukatoisha tamaa kwani uongozi hauangalii jinsi bali ni utekelezaji wa majukumu na kufuata miongozo taratibu sheria na kanuni za uongozi zilizowekwa,”alisema Mkomwa.  

Akizungumzia juu ya mwenyekiti huyo Simon Mbelwa alisema kuwa mtaa huo umepata kiongozi mzuri na alikuwa karibu na wananchi hivyo wamepata kiozi sahihi kwani ni msikivu na mpenda maendeleo anaamini kuwa ataufiukisha mbali mtaa huo.

Mbelwa alisema kuwa kiongozi huyo ana uzoefu mkubwa kwani kabla ya ksuhika nafasi hiyo alikuwa mjumbe hivyo anajua changamoto za wananchi na jinsi gani atazitatua kwa kupitia mipango na ushirikishaji wananchi kupitia vikao vya mtaa.

Kwa upande wake Swaiba Kazi alisema kuwa wanawake ni viongozi wenye uwezo mkubwa na dhana kuwa mwanamke hana uwezo si ya kweli na haipaswi kuungwa mkono na wanaweke wameonyesha gani kiongozi anatakiwa afanye.Kazi alisema kuwa wanwake wana uwezo mzuri wa kuongoza na ndiyo sababu wameaminika na kupewa nafasi hizo za juu kuanzia ngazi za chini hadi Uras hivyo wanapaswa kuungwa mkono na siyo kuwavunja moyo na mtaa huo una jumla ya wananchi 7,546 ana watoto watatu na ni mjasiriamali.    Mwisho.  

Monday, January 6, 2025

MTAA WA MIEMBE SABA WAWEKA VIFUSI KUBORESHA BARABARA YA MTAA


MTAA wa Miembe Saba B Wilayani Kibaha Mkoani Pwani umezanza zoezi la kuweka vifusi kwenye barabara ya Mtaa ili kuwaondolea kero wananchi wa Mtaa huo.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mwenyekiti wa Mtaa huo Nuru Awadhi amesema kuwa barabara hiyo yenye urefu wa kilometa saba imeharibika sana kutokana na kuharibiwa na mvua kubwa zilizonyesha mwaka jana.

Awadhi amesema kuwa wameanza kusambaza vifusi hivyo ambavyo wameviomba kutoka kwa wadau mbalimbali wa maendeleo wa mtaa huo ili kufanikisha uboreshaji wa barabara hiyo ya vumbi.

"Nawashukuru wadau wa maendeleo katika mtaa ambao wamejitolea kupatikana kwa kifusi hichi ambacho kitatusaidia ili kupunguza kero kwa wananchi wanayoitumia barabara hii,"amesema Awadhi.

Amesema kuwa wameweka kifusi sehemu na bado kinahitajika kifusi zaidi ambapo tunaweka kwanza kwenye maeneo korofi ili kupunguza changamoto ya ubovu wa barabara.

"Tumepata changamoto kubwa ya ubovu wa barabara kwani sisi kwa bahati mbaya barabara yetu haikuchongwa kama baadhi ya barabara za mitaa mingine zilibahatika kuchongwa hivyo kupunguza athari za ubovu tofauti na kwetu,"amesema Awadhi.

Aidha amesema kuwa wanaendelea kuwahamasisha wananchi kuendelea kusaidia ili wakabiliane na changamotro hiyo ili kuongeza vifusi zaidi ili kuweza kuvisambaza kwenye barabara yote.

"Tuliongea na diwani ambapo alisema watafanya mpango wa kutuletea greda lakini majibu ni kuwa ni bovu hivyo tutatasubiri hadi litengenezwe ndipo tulilete kwetu lakini hiyo itakuwa ni muda mrefu ndipo tukaona njia ya haraka ni kumwaga kwanza kifusi kwenye sehemu korofi,"amesema Awadhi.

Aliongeza kuwa wao walipata bahati mbaya kutochongewa barabara yao lakini mitaa mingine ilichongewa barabara zao ambazo zilichongwa mwaka jana angalau imepunguza changamoto za ubovu.

"Mtaa wetu una wananchi zaidi ya 4,000 hivyo kila mmoja wetu akipambana tutaweza kuboresha miundombinu yetu ya barabara ambapo kuna shule za Msingi tatu na moja ya sekondari hivyo inaonyesha jinsi gani changamoto ya ubovu wa barabara inavyokuwa shida,"amesema Awadhi.

Sunday, January 5, 2025

WAHUKUMIWA MAISHA NA MIAKA 20 KWA UKATILI WA KIJINSIA

WATUHUMIWA wawili Mkoani Pwani waliokuwa wanakabiliwa kwa kesi za ukatili wa kijinsia wamehukimiwa vifungo tofauti ambapo mmoja amefungwa kifungo cha maisha jela na mwingine amefungwa kifungo cha miaka 20 jela.

Aidha jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani lilipeleka Mahakamani kesi 125 za makosa mbalimbali ambapo kati ya kesi hizo 47 zimepata mafanikio kwa watuhumiwa kuhukumiwa vifungo mbalimbali.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani ACP Salim Morcase alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya mafanikio ya jeshi hilo kwa kipindi cha mwezi Disemba 2024.

Morcase amesema kuwa jumla ya kesi za ukatili wa kijinsia kulikuwa na kesi tano za makosa ya kubaka na kulawiti.

"Watuhumiwa hao wawili walipata adhabu hizo ambapo wa kwanza alipatikana na hatia ya kubaka na kulawiti na wa pili alikutwa na hatia ya unyanyasaji wa kingono,"amesema Morcase.

Amesema kuwa watuhumiwa 52 wamehukumiwa vifungo tofauti tofauti kutokana na aina ya makosa yaliyokuwa yakiwakabili.

MADEREVA 11 MKOANI PWANIWAFUNGIWA LESENI

JUMLA ya makosa 17,246 ya usalama barabarani yamekamatwa huku madereva 11 wakifungiwa leseni zao Mkoani Pwani kwa makosa mbalimbali waliyoyafanya wakiwa barabarani.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani ACP Salim Morcase amesema madereva hao wamefungiwa leseni kwa mujibu wa sheria.

Morcase amesema kuwa madereva hao walifungiwa leseni kwa makosa ya kuendesha magari wakiwa wamelewa, kuendesha magari kwa uzembe na kuyapita magari mengine pasipo kuchukua tahadhari.

"Madereva wengine 24 walifikishwa mahakamani kwa makosa ya kupandisha abiria kwenye magari ambayo yanapelekwa nje ya nchi IT na kusababisha ajali za barababani,"amesema Morcase.

Amesema kuwa madereva hao walifikishwa mahakamani kwa mujibu wa kifungu cha 28 (3) (b) cha Sheria ya usalama barabarani sura ya 168 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2022. 

"Tumetoa elimu ya usalama barabarani kwa makundi mbalimbali, bodaboda, madereva wa mabasi makubwa, madereva wa mabasi madogo na madereva wa magari ya shule,"amesema Morcase.

Ameongeza kuwa wametoa elimu madereva wa pikipiki 4,293 katika vijiwe 199 vya pikipiki na abiria wa mabasi makubwa na madogo wapatao 13,094 kwenye maeneo mbalimbali.

"Elimu waliyoipata ni umuhimu wa kufahamu namba za gari unayosafiria, wahudumu wa basi hilo, dereva na kondakta na kufahamu muda wa kuanza safari, umuhimu wa kutoa taarifa kwa mamlaka husika pale abiria anapoona vitendo
vya uvunjifu wa sheria za usalama barabarani ambavyo vitahatarisha usalama,"amesema Morcase.

Amebainisha kuwa pia wamewaelimisha abiria juu ya mwendokasi, kuyapita magari mengine bila ya tahadhari, madhara ya kupakia mizigo ya hatari ndani ya mabasi na kushushwa kwenye basi pale gari linapofika mizani ili lisionekane kama limezidisha uzito.

COREFA KUJENGA OFISI UWANJA WAKE

CHAMA Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) kimepata eneo lenye ukubwa wa hekari tano kwa ajili ya ujenzi wa ofisi na uwanja wake.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Mwenyekiti wa Corefa Robert Munis alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.

Munis amesema kuwa eneo hilo ambalo liko Mtaa wa Viziwaziwa wamekabidhiwa na Halmashauri ya Mji Kibaha ambapo tayari wamekabidhiwa barua ya kupewa eneo hilo.

"Tumepewa masharti ya kuhakikisha tunajenga ofisi na uwanja ndani ya muda wa mwaka mmoja tunaishukuru Halmashauri kwa kutupatia eneo hilo na tutahakikisha tunalifanyia kazi,"amesema Munis.

Amesema kuwa lengo ni kuhakikisha Corefa inamiliki uwanja wake ambapo kwa sasa hawana uwanja na ofisi waliyonayo wamepangisha hivyo kuwa na ofisi na uwanja itakuwa jambo zuri.

"Kwa kushirikiana na wajumbe wa bodi ya udhamini inayoongozwa na Waziri wa Viwanda na Uwekezaji Dk Suleiman Jafo watahakikisha ofisi na uwanja vinajengwa kwa muda uliopangwa,"amesema Munis.

Aidha amesema kuwa kamati ya utendaji itakaa kuandaa mipango kuhusiana na namna ya kufanikisha namna ya kuanza ujenzi huo.

"Tunataka tuwe na timu zitakazokuwa zinatumia viwanja vizuri na kuhakikisha tunapandisha timu hadi zifike ligi kuu ambapo kwa sasa Mkoa huo hauna timu yoyote iliyoko ligi kuu,"amesema Munis.

Wakati huo huo imempatia kiasi cha shilingi 100,000 mwandishi wa habari za michezo Abdala Zalala kwa kutambua mchango wake wa kuhamasisha mchezo wa soka ndani ya Mkoa huo.

Kwa upande wake Zalala amesema kuwa anakishukuru chama hicho kwa kutambua mchango wake na kumpa zawadi hiyo na kuahidi kuendelea kuhamasisha soka hasa kwa vijana ndani ya  Mkoa huo bila ya kuchoka.

Zalala amewataka waandishi wa habari wenzake nao kujikita kuandika habari za Soka ili kuinua mchezo huo uweze kutia ajira kwa vijana

COREFA KUANDAA VIJANA KWENYE VITUO KILA WILAYA

CHAMA Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) kimesema kitahakikisha kila Wilaya inakuwa na kituo cha kuandaa vijana ili kuzalisha wachezaji watakaokuja kulitumikia Taifa.

Aidha amesema kwa sasa kuna vituo vinne lakini lengo ni kuwa na vituo saba na baadaye kuwe na vituo kila Halmashauri za mkoa huo ambazo ziko 9.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Mwenyekiti wa Corefa Robert Munis amesema kuwa kwa sasa changamoto za viwanja hazipo kwani viwanja vipo vingi.

Munis amesema kuwa kwa sasa wanahamasisha wazazi kuhakikisha wanawawezesha watoto wao ili washiriki kwenye soka ili vijana wa Mkoa huo waweze kutumia vipaji vyao kujiletea maendeleo

"Tunawapongeza wenzetu Chalinze wameanza ligi ya vijana chini ya miaka 15 haya ndiyo tunayoyataka kwani Pwani lazima Mpira Uchezwe ndiyo kauli mbiu yetu,"amesema Munis.

Amesema kuwa mpira ni ajira lakini ili kufikia lengo hilo lazima ushiriki wa wazazi nao uwepo kwa kuwawekea mazingira ili waweze kucheza na wasiwazuie watoto kucheza.

"Tumeanza mpango wa kusajili shule za soka Academy na kuzitambua ili tushirikiane nao ili malengo yetu yatimie kama viwanja vipo kwa nini vijana wasicheze tuhakikishe vijana wetu wanacheza mpira kwani wataliwakilisha vyema Taifa,"amesema Munis.

Ametaja baadhi ya viwanja vilivyopo ndani ya Mkoa wa Pwani kuwa ni Mwanambaya, Bungu, Mabatini, Tumbi, Mwanakalenge, Kiromo, Msoga, Maili Moja Mwendapole, Kwambonde na vingine vingi ambavyo baadhi vinatumika na vingine viko kwenye ujenzi.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa chama hicho ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya mipango na fedha Mohamed Lacha amesema wanawashukuru wadau mbalimbali ambao wamefanikisha kupata ofisi ya kisasa.

Lacha amesema kuwa jambo kubwa ni kuhakikisha Corefa inasonga mbele kwa kushirikiana na kuepukana na migogoro ambayo huwa inarudisha nyuma masuala ya soka.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Soka la Wanawake Mkoa wa Pwani Asha Mbata amesema kuwa wanafarijika kwani kwa mwaka jana Wilaya zote zikichezesha ligi ya wanawake isipokuwa Mafia pekee ambapo ni mafanikio makubwa sana.

Mbata amesema kuwa wanaandaa ziara ya kutembelea Wilaya ili kuhamasisha wanawake na kucheza soka na Wilaya kuandaa ligi  kwa wanawake.






COREFA KUANDAA VIJANA KUPITIA VITUO KILA WILAYA

CHAMA Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) kimesema kitahakikisha kila Wilaya inakuwa na kituo cha kuandaa vijana ili kuzalisha wachezaji watakaokuja kulitumikia Taifa.

Aidha amesema kwa sasa kuna vituo vinne lakini lengo ni kuwa na vituo saba na baadaye kuwe na vituo kila Halmashauri za mkoa huo ambazo ziko 9.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Mwenyekiti wa Corefa Robert Munis amesema kuwa kwa sasa changamoto za viwanja hazipo kwani viwanja vipo vingi.

Munis amesema kuwa kwa sasa wanahamasisha wazazi kuhakikisha wanawawezesha watoto wao ili washiriki kwenye soka ili vijana wa Mkoa huo waweze kutumia vipaji vyao kujiletea maendeleo

"Tunawapongeza wenzetu Chalinze wameanza ligi ya vijana chini ya miaka 15 haya ndiyo tunayoyataka kwani Pwani lazima Mpira Uchezwe ndiyo kauli mbiu yetu,"amesema Munis.

Amesema kuwa mpira ni ajira lakini ili kufikia lengo hilo lazima ushiriki wa wazazi nao uwepo kwa kuwawekea mazingira ili waweze kucheza na wasiwazuie watoto kucheza.

"Tumeanza mpango wa kusajili shule za soka Academy na kuzitambua ili tushirikiane nao ili malengo yetu yatimie kama viwanja vipo kwa nini vijana wasicheze tuhakikishe vijana wetu wanacheza mpira kwani wataliwakilisha vyema Taifa,"amesema Munis.

Ametaja baadhi ya viwanja vilivyopo ndani ya Mkoa wa Pwani kuwa ni Mwanambaya, Bungu, Mabatini, Tumbi, Mwanakalenge, Kiromo, Msoga, Maili Moja Mwendapole, Kwambonde na vingine vingi ambavyo baadhi vinatumika na vingine viko kwenye ujenzi.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa chama hicho ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya mipango na fedha Mohamed Lacha amesema wanawashukuru wadau mbalimbali ambao wamefanikisha kupata ofisi ya kisasa.

Lacha amesema kuwa jambo kubwa ni kuhakikisha Corefa inasonga mbele kwa kushirikiana na kuepukana na migogoro ambayo huwa inarudisha nyuma masuala ya soka.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Soka la Wanawake Mkoa wa Pwani Asha Mbata amesema kuwa wanafarijika kwani kwa mwaka jana Wilaya zote zikichezesha ligi ya wanawake isipokuwa Mafia pekee ambapo ni mafanikio makubwa sana.

Mbata amesema kuwa wanaandaa ziara ya kutembelea Wilaya ili kuhamasisha wanawake na kucheza soka na Wilaya kuandaa ligi  kwa wanawake.