JUMUIYA ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) imejipanga kuhakikisha inakabili kero za wafanyabiashara na kupokea maoni na mapendekezo ya wafanyabiashara wote nchini na kuzifikisha sehemu husika.
Wednesday, July 26, 2023
JUMUIYA YA WAFANYABIASHARA TANZANIA (JWT) KUPAZA SAUTI
Monday, July 24, 2023
URAIA WETU YAZINDULIWA
Sunday, July 23, 2023
RC ATAKA WALIOCHOMA MOTO BONDE MZAKWE WASAKWE
MKUU wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama Mkoani Dodoma kuhakikisha vinawasaka na kuwabaini wote waliohusika na uchomaji moto katika Bonde la Mzakwe.
Senyamule ametoa agizo hilo leo Julai 21, 2023 mara baada ya kufika katika eneo hilo kujionea athari za uharibifu zilizosababishwa na moto ulioanza majira ya saa saba mchana.
Amesema asilimia 70 ya maji katika Jiji la Dodoma yanatoka katika bonde la Mzakwe na ni eneo la hifadhi hivyo ni muhumimu kukakikisha linalindwa na kuhifadhiwa kwa ustawi wa afya na mazingira ya watu wote.
Aidha, amewapongeza vijana wa JKT Makutupora walioshiriki katika zoezi la kuzima moto uliotokea hii leo tarehe katika Bonde la Mzakwe Jijini Dodoma. Senyamule amewapongeza kwa uzalendo walionyesha wa kudhibiti moto huo na kuzuia usilete madhara makubwa, amesema wameonyesha uzalendo mkubwa, uhodari na ushupavu.
"Tumesikitishwa sana na moto huu kwa kuwa si kwamba umeathiri ikolojia ya eneo hili lakini pia umeharibu miundombinu ya Tanesco ikiwa ni pamoja na nguzo, hivyo kwanza nawapongeza vijana wetu kwa jitihada za kufanikisha kuzima moto huu na pili vyombo vyote vinavyohusika na uchunguzi vifanye kazi yake ili kubaini chanzo” Senyamule amesisitiza.
Amemuagiza Meneja wa Bonde la Wami Ruvu kuhakikisha kuwa wanachonga barabara maalum kwa lengo la kukinga moto katika bonde hilo ili athari za moto zisiwe kubwa pindi moto utokeapo.
Awali Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto Mkoa wa Dodoma Julishaeli Mfinanga amesema kuwa walipata taarifa kwa njia ya simu kupitia namba za dharura 114 na kuwahi eneo la tukio kwa haraka. Amesema moto umedhibitiwa na hakuna madhara makubwa na wanaendelea na doria kuhakikisha usalama katika eneo hilo.
Saturday, July 22, 2023
*UJUMBE KUTOKA KENYA WAJIFUNZA USIMAMIZI SEKTA YA MADINI*
Ujumbe kutoka Kenya ukiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Madini wa nchi hiyo Elijah Mwangi umefika nchini kujifunza kuhusu namna bora ya usimamizi wa Sekta ya Madini ambapo Katibu Mkuu Wizara ya Madini Kheri Mahimbali ameupokea ujumbe huo.
Akizungumza katika kikao na ujumbe huo, Mahimbali amesema Tanzania ni sehemu salama ya uwekezaji kutokana na uongozi bora wa Serikali unaosimamiwa na Rais Samia Suluhu Hassan ambapo umepelekea kuifanya sekta hiyo kupata mafanikio makubwa.
Mahimbali amesema Wizara ya Madini ina Taasisi tano ambazo ni Tume ya Madini, Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Taasisi ya Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) pamoja na Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) ambazo hutekeleza majukumu yake kwa ushirikiano.
Naye, Katibu Mkuu Wizara ya Madini kutoka Kenya Elijah Mwangi ameipongeza Wizara ya Madini kwa usimamizi bora wa sekta hiyo na kumuomba Mahimbali kuendelea kushirikiana katika nyanja mbalimbali ikiwemo tafiti na usimamizi wa biashara ya madini.
Katika kikao hicho mada mbalimbali zimewasilishwa ambapo Mtendaji Mkuu wa GST Dkt. Mussa Budeba amewasilisha mada juu ya madini yapatikanayo Tanzania na aina za tafiti zilizokwisha fanyika.
Dkt. Budeba amesema kwa sasa GST imejikita zaidi kwenye tafiti za madini ya kimkakati ambapo mpaka sasa Tanzania imefanyiwa tafiti za Kijiolojia kwa asilimia 96.
Kwa upande wake, Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini Mhandisi Ally Maganga amewasilisha mada juu ya shughuli za Tume ya Madini ikiwemo uwepo wa Masomo na Vituo vya Ununuzi wa Madini, Mfumo wa Leseni pamoja na shughuli za wachimbaji wadogo.
Mhandisi Maganga amesema uwepo wa masoko na vituo vya kuuzia madini umesaidia kuongeza mapato ya Sekta ya Madini ambapo mchango wa sekta hiyo kwenye Pato la Taifa umeendelea kuimarika mwaka hadi mwaka ambapo kwa sasa umefikia asilimia 9.7 ikiwa lengo ni kufikia mchango wa asilimia 10 ifikapo mwaka 2025.
Friday, July 21, 2023
MKE WA MBUNGE AWAPIGA TAFU WASANII.
Mke huyo wa Mbunge huyo alitoa fedha hizo wakati wa uzinduzi wa chama hicho uliofanyika Visiga Madafu wilayani humo.
Akikabidhi cheki ya fedha hizo aliwataka waigizaji hao kuzitumia fedha hizo kwa ajili ya kujiletea maendeleo yao na kukuza tasnia hiyo ya sanaa ambayo imekuwa na kuwa na maslahi mazuri.
Awali Rais wa chama hicho Dk Cynthia Henjewele alisema kuwa wasanii wanapaswa kuungana na kutumia fursa za mikopo kupitia mfuko wa utamaduni ambayo inatolewa kwa wasanii ambazo hazina riba.
MKE WA MBUNGE ACHANGIA MAMILIONI CHAMA CHA WAIGIZAJI KIBAHA
WANANCHI WATAKIWA KULIPA ANKARA ZA MAJI NA KULINDA MAZINGIRA
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya maji Safi na usafi wa Mazingira Bunda BUWSSA Bi Ester Gilyoma ametoa wito kwa wananchi wa Halmashauri ya Bunda iliopo Mkoani Mara kwa wale wanaotumia maji ya BUWSSA kuacha tabia ya wizi wa maji na badala yake wahakikishe wanalipa Ankara za maji, sambamba na utunzaji wa vyanzo na miundombinu ya maji katika Halmashauri hiyo.
Bi Ester ametoa wito huo Jijini Dodoma katika mkutano wake na Wana habari wakati akielezea utekelezaji wa majukumu ya Mamlaka hiyo na mwelekeo wa utekelezaji wa mwaka wa fedha 2023/2024.
Aidha Mkurugenzi Mtendaji huyo amesema kuwa hapo awali kulikuwa na changamoto kwa wakazi wa Bunda kwa kupata maji yasiyo Safi na salama ambapo kwasasa ndani ya uongozi wa Raisi wa awamu ya sita ya Dkt Samia Suluhu Hassan Serikali imefanya uwekezaji mkubwa katika miundombinu ya maji ikiwemo chujuo la kuchuja na kutibu maji hivyo maji machafu Bunda Sasa basi.
Pia amesema wanaendelea na jitihada za kupunguza au kuondoka kabisa changamoto za upotevu wa maji ikiwa ni pamoja kuwepo kwa Mpango wa kubadili mita goigoi kwani kwa mwaka wa Jana upotevu ulikuwa asiliamia 45,lakini mpaka Sasa upotevu umeendelea kupungua mpaka asiliamia 36.