Friday, July 21, 2023
WANANCHI WATAKIWA KUJITOKEZA MAADHIMISHO YA MASHUJAA JULAI 25
Thursday, July 20, 2023
*MBOYA MBUZI SODO CUP YAFANA*
KIBAFA INATISHA...ikiwa ni wiki mbili baada ya uongozi mpya wa chama cha soka wilaya ya Kibaha kuingia madarakani imeshuhudiwa viongozi wa chama hicho wakihudhuria mashindano ya soka la ufukweni maarufu kama "Beach soka"
Mashindano hayo yamefanyika Mlandizi yakiwa ni ya Mboya mbuzi SODO cup...
Katika mashindano hayo imeshudiwa viongozi kadhaa wapya wa KIBAFA wakihudhuria ambapo wameongozwa na mwenyekiti wa KIBAFA comrade Robert Munisi...makamu mwenyekiti bwana David Mramba...
Pia alikuwepo katibu msaidizi wa KIBAFA bwana Omary Abdul pamoja na wajumbe wa kamati tendaji ya KIBAFA bila kusahau mwenyekiti wa kamati ya Beach soka bwana Nassoro Shomvi
Katika hali ya kuonesha KIBAFA wapo kazini pia mbunge wa jimbo la Kibaha vijiijini mheshimiwa Michael Mwakamo alihudhuria mashindano hayo hali iliyoibua shangwe na vibe la aina yake kwa wakazi na mashabiki wa Beach soka waliojitokeza kutoka Mlandizi na Kibaha kwa ujumla...
Katika mashindano hayo timu ya Kilangalanga umeibuka mshindi wa fainali hiyo baada ya kuibamiza timu ya Msalabani goli 4-1 na kuifanya timu ya Kilangalanga kupata zawadi ya mbuzi mnyama huku mshindi wa pili na washiriki wengine nao wakijizolea zawadi lukuki....ambapo mshindi wa pili ambaye ni timu ya Msalabani wamepata zawadi ya kuku ndege....mfungaji bora akipata pesa taslimu elfu30,mchezaji bora wa mshindano sambamba na golikipa bora wakipata mche wa sabuni kila mmoja.
Katika nyakati mbalimbali mwenyekiti wa KIBAFA comrade Robert Munisi amekuwa akisikika akisema KIBAFA ya sasa ni kwa ajili ya kuhakikisha soka linachezwa Kibaha na kuhakikisha Kibaha inakuwa wilaya ya mfano kwa Tanzania nzima
Wednesday, July 19, 2023
*WIZARA YA MADINI YADHAMIRIA KUONDOA CHANGAMOTO KWA WACHIMBAJI WA MADINI WAKUBWA NA WA KATI*
*Dkt. Biteko asikiliza mafanikio na kero za wachimbaji wa madini wakubwa na wa kati*
WIZARA ya Madini imedhamiria kuweka mipango thabiti kuhakikisha changamoto zilizopo kwenye Sekta ya Madini zinatatuliwa kwa lengo la kuongeza tija kwenye uzalishaji wa madini nchini.
Hayo yamebainishwa na Waziri wa Madini Dkt. Doto Biteko wakati akifungua kikao cha kujadili maendeleo, changamoto na kero zinazozikabili Kampuni kubwa na za kati zinazojishughulisha na uchimbaji wa madini nchini.
"Leo ni siku ya kuwasikiliza wachimbaji wakubwa wa madini na wa kati kama tunavyo wasikiza Wachimbaji Wadogo kama wanachangamoto gani ili tuweze kuzifanyia kazi lakini pia tunajiandaa na Mkutano wa Mkuu wa Kisekta wa Mwaka unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu," amesema Dkt. Biteko.
Pamoja na mambo mengine, Dkt. Biteko amesema tayari serikali imerahisisha mazingira ya kikodi kwa wachimbaji wa madini ili kuondokana na changamoto mbalimbali zinazoweza kujitokaza katika kutimiza wajibu yao.
Kwa upande wake, Waziri wa Madini Maji, Nishati na Madini kutoka Zanzibar Staibu Hassan ameipongeza Wizara ya Madini kwa hatua kubwa ambapo amesema wizara hiyo imekuwa mwalimu wa mataifa mengi kujifunza usimamizi bora wa shughuli za biashara na uchimbaji madini.
Naye, Mwenyekiti wa Chemba ya Migodi, Mhandisi Philibart Rweyemamu amesema Chama anachokiongoza kipo tayari kushirikiana na serikali ili kuondoa changamoto na kutoa suluhisho la kudumu katika sekta hiyo ili hatimaye kufikia lengo la kuchangia asilimia 10 kwenye Pato la Taifa ifikapo 2025.
"Kikao cha namna hii kitakuwa kinafanyika kila robo mwaka ili kutoa taarifa kwa serikali juu ya maendeleo ya shughuli zetu, kuueleza umma nini kinachofanyika pamoja na kuishauri serikali kitu gani tunafikiri kifanyike ili kurahisisha utendaji wa Sekta ya Madini," amesema Mhandisi Rweyemamu.
Katika kikao hicho Kampuni tano za uchimbaji mkubwa wa madini zimetoa taarifa za utekelezaji wa miradi inayotekelezwa ikiwemo Kampuni ya Nyati Corporation, Sotta Mining, Tembo Nickel Corporation, Twiga Minerals na Faru Graphite Limited.
WATAKIWA WASIDANGANYE MAKAZI
MKUU wa Mkoa wa Dodoma,Mhe.Rosemary Senyamule amewaasa wananchi na wakazi wa Dodoma kuacha kudanganya maeneo ya makazi ili kuepusha migogoro ya ardhi.
Mhe.Senyamule ameyasema hayo wakati akizindua mpango mkakati kwa ajili ya kushughulikia na kutatua migogoro ya ardhi kwa jiji la Dodoma.
Aidha amesema kuwa jiji la Dodoma limekuwa na ongezeko la wananchi hivyo kufuatia ongezeko hilo limepelekea matumizi ya ardhi kuwa ni mengi na mengine kuwa ya kiholela bila mpangilio ambapo kwa kutatua changamoto hii mkoa wa Dodoma kupitia Mkuu wa mkoa wa Dodoma imeandaa timu kwa ajili ya kutatua na kumaliza migogoro.
"Kuna changamoto mbalimbali zinazochangia migogoro hii kushindwa kuisha kutokana na uchache wa vifaa vya tehama, ukosefu wa huduma bora kwa wananchi,eneo la jiji kuwa dogo, lugha mbaya kwa wananchi zinazotolewa na watumishi wa jiji,kipandikizi yaani kupandikiza zaidi ya kiwanja kimoja kupewa watu tofauti pamoja na wananchi kupuuza jumbe za simu" Amesisitiza Senyamule.
Aidha ameongeza kuwa jambo hili litafanyika ndani ya miezi 6 yaani Julai hadi Disemba ambapo kutafanyika uhakiki wa maeneo ambayo yanamalalamiko ambapo wahusika wanavamia maeneo ambayo sio ya kwao pamoja na kurekebisha mifumo kwa kushirikiana na ofisi ya Rais tamisemi.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Dodoma,Mhe. Jabir Shekimweri amesema kuwa mpango huo utaweza kuwasaidia kutambua mapungufu gani ya ndani na madhaifu gani ya nje ili ili kuishi matarajio ya kiongozi wa kitaifa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kuhakikisha jiji la Dodoma linapagwa vizuri ili kuendana na hadhi ya makao makuu ya nchi.
Amesema ni matumaini yake kwamba elimu ya kutosha itatolewa kwa kamati ili kuhakikisha wanakuwa na uelewa huku akisisitiza maeneo ya wazi kupewa watu sahihi ili kuhakikisha wanajenga vitu vyenye manufaa kwa wananchi.
Aidha ametoa rai kwa watumishi wa ardhi kuhudumia wateja vizuri kwa kutoa kauli nzuri kwa wateja pamoja na kuheshimu watu.
TCRA KUENDELEA KUSIMAMIA SEKTA YA MAWASILIANO
MAMLAKA ya mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema inaendelea kusimamia Sekta ya Mawasiliano kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika ngazi ya Kitaifa, Kikanda na Kimataifa ili kuhakikisha Sekta ya Mawasiliano inatoa mchango katika maendeleo ya nchi na kuwa kichocheo cha ukuaji wa uchumi wa kidijiti na uchumi wa buluu.
Hayo ameyasema Mkurugezi Mtendaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Dkt. Jabiri Bakari wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini dodoma kuhusu taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya TCRA 2022/23 na Mpango kazi 2023/24.
Dkt,Jabiri amesema Takwimu zinaonesha kuwa wastani wa bei ya dakika ndani ya Mitandao bila kifurushi zinaendelea kushuka na Mwenendo wa gharama za upigaji wa simu nje ya kifurushi zimeendelea kushuka hivyo kwa gharama za mwingiliano kumepelekea kuwa na tofauti ndogo sana ya gharama za kupiga simu ndani na nje ya mtandao.
Aidha, Dkt Jabiri ametoa rai kwa Vyombo vya utangazaji kuendelea kuzingatia sheria, kanuni na weledi katika kutoa maudhui, vilevile kwa wananchi kutosambaza maudhui ambayo yanakiuka misingi ya sheria, mila na desturi za Taifa la Tanzania.
TCRA ilianzishwa chini ya Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Namba 12 ya mwaka 2003 baada ya kuunganishwa kwa iliyokuwa Tume ya Utangazaji Tanzania (TBC) na Tume ya Mawasiliano Tanzania (TCC). TCRA ilianza kutekeleza majukumu yake tarehe 1 Novemba 2003.
WAZALISHAJI CHUMVI WATAKIWA KUONGEZA UZALISHAJI
WAZIRI wa Madini Dk Dotto Biteko amewatakaka wazalishaji wa chumvi nchini kuongeza uzalishaji chumvi ili kukidhi soko la ndani na la nje kutoka tani 273,000 kwa mwaka hadi tani 303,000.