Friday, May 22, 2015

SHULE HATARINI KUANGUKA


WANANCHI wa Kijiji cha Mkoko wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wameiomba Halmashauri kubomoa baadhi ya madarasa ya  shule ya Msingi Mkoko ambayo yananyufa na yako hatarini kuanguka hivyo kufanya wanafunzi kusoma kwa hofu.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo hivi karibuni Muhsin Mkumbi alisema kuwa majengo hayo yako kwenye hali mbaya na wakati wowote yanaweza kuanguka na kuleta madhara.
Mkumbi alisema kuwa madarasa hayo ni mabovu sana na hayastahili kutumika kutokana na ubovu wake hivyo ni vema Halmashauri ikayabomoa na kuyajenga upya ili kuepuka madhara ambayo yanaweza kutokea.
“Madarasa hayo yameharibika sana na yataanguka wakati wowote hivyo tunaiomba halmashauri iyabomoe kwani ni hatari kwa wanafunzi na walimu wanaofundisha shule hiyo, hali ni mbaya sana tunaomba hatua madhubuti zichukuliwe,” alisema Mkumbi.
Alisema kuwa hata baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakiogopa kwenda shule kutokana na hali hiyo ya ubovu wa madarasa hayo ambayo yamewekewa na miti kuyazuia ili yasianguke na tunawasiwasi kwani yakianguka yataleta tatizo.
Kwa upande wake ofisa elimu wa kata ya Msata Rajab Msakam alikiri kuwepo kwa tatizo hilo na kusema kuwa madarasa mengi yana nyufa kutokana na ardhi ya eneo hilo ujenzi wake kuwa mgumu kwani inapasuka na kusababisha nyufa.
Msakamali alisema kuwa talipeleka jambo hilo sehemu husika ili kuangalia namna ya kuikabili hali hiyo ambayo inahatarisha usalama wa wanafunzi pamoja na walimu wanaofundisha madarasa hayo yenye nyufa.
Naye Mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete alisema kuwa tayari suala hilo limepelekwa halmashauri na kinachosubiriwa ni kibali kwa Kijiji kwa ajili ya kuvunja madarasa hayo ambayo yanahatarisha usalama wa wanafunzi na walimu.
Mwisho.

Tuesday, May 19, 2015

RIDHIWANI ATOA MSAADA WA FEDHA NA SARUJI KWENYE ZAHANATI

Na John Gagarini, Chalinze
ADHA ya akinamama wajawazito kujifungua mbele za wanaume kutokana na zahanati ya Kijiji cha Pongwe Kiona wilayani Bagamoyo mkoani Pwani kuwa na chumba kimoja cha matibabu huenda ikaondoka baada ya kuchangiwa kiasi cha shilingi milioni moja na mifuko 70 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya wanawake na wanaume.
Kutokana na zahanati hiyo kuwa na chumba kimoja imesababisha akinamama kujifungua huku kukiwa na wanaume jambo ambalo limesababisha kutokuwa na usiri hivyo utu wa mwanamke kutokuwepo.
Msaada huo umetolewa na Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete ambapo fedha na Saruji  vilikabidhiwa na Katibu wa Mbunge huyo Iddy Swala kwa niaba ya Mbunge.
Akizungumzia changamoto hiyo mwenyekiti wa kijiji hicho Rajab Mgaya alisema kuwa zahanati hiyo ilijengwa mwaka 1964 na ina wodi moja tu.
“Tunamshukuru Mbunge kwani hii ilikuwa changamoto kubwa kwa akinamama wanaojifungua huku kukiwa na akinababa nao wanapata matibabu humo hivyo usiri kutokuwepo kutokana na hali hiyo,” alisema Mgaya.
Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kimange Husein Hadingoka alisema kuwa mbunge huyo ameonyesha upendo wa hali ya juu kwa kutoa vitu hivyo ambavyo vitasaidia ujenzi huo.
Hadingoka alisema kuwa wananchi watafanya ujenzi huo ambapo yeye alitoa 100,000 kwa ajili ya kufanikisha ujenzi huo na kusema atafurahi kuona uujenzi huo unakamilika mapema.
Naye moja ya wakazi wa Kijiji hicho ambaye ni mwanamama Sikudhani Ally alisema kuwa kujifungua huku wanaume wakiwepo ni mtihani mkubwa lakini kwa mpango huo utakuwa umeweka stara ya mwanamke.
Kwa upande wake katibu wa Mbunge Swala alisema kuwa mbunge ametoa msaada huo baada ya kutemebelea hivi karibuni akiwa kwenye ziara zake za kikazi na wananchi kutoa kilio chao juu ya hali hiyo.

Mwisho.

HABARI MOTOMOTO

Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA Cha Wasioona Nchini kimewataka vijana wenye ulemavu huo kuachana na dhana ya kuwa mara wamalizapo elimu mbalimbali ni laziwa waajiriwe badala yake wajiandae kwa kufanya shughuli za kujiajiri wenyewe.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na makamu mwenyekiti wa chama hicho Taifa Robert Bundala wakati wa mafunzo ya sera ya ajira kwa watu wenye ulemavu kwa vijana wanachama wa chama hicho wilayani Kibaha.
Bundala alisema kuwa soko la ajira kwa sasa ni gumu sana hivyo lazima vijana wajiwekee malengo ya kujiajiri wao wenyewe kupitia fursa zilizopo kwenye maeneo yao kuliko kusubiri kuajiriwa serikalini au sekta binafsi.
“Vijana wasioona wanapaswa kuachana na dhana hiyo badala yake wajiajiri kwa kupitia shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na ujasiriamali na si kutegemea kuajiriwa kwani upatikanaji wa ajira kwa sasa ni mgumu,” alisema Bundala.
Alisema kuwa ushindani wa soko la ajira hapa nchini kwa sasa ni mkubwa sana kwani hata watu wasiona na ulemavu wamekuwa wakilalamika hivyo lazima vijana hao watumie mafunzo mbalimbali wanayoyapata ili kujiajiri.
“Kwa sasa ubaguzi umepungua lakini kikubwa kinachoangaliwa ni uwezo wako wa kielimu kwani kwa wale wenye elimu nzuri wamepata ajira lakini lazima wabadili mfumo wa kusubiri ajira badala yake wajiajiri,” alisema Bundala ambaye ni mwalimu wa shule ya msingi.
Naye Mwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye naye ni mlemavu asiyeona Greyson Mlanga alisema kuwa ni vema vijana wakaangalia fursa za ajira zilizopo kwenye maeneo wanayoishi na kuwaondolea fikra kuwa lazima waajiriwe.
Mlanga alisema kuwa kutokana na ugumu wa ajira vijana wasioona wanapaswa kuangalia suala la kujiajiri kwani kutegemea ajira za kuajiriwa itakuwa ni vigumu sana kuweza kufanikiwa kujiletea maendeleo.
 Kwa upande wake moja ya washiriki wa mafunzo hayo Zuhura Omary alisema kuwa changamoto kwao ni nyingi kutokana na hali waliyonayo pia ni kutokana na kutokuwa na elimu ya kutosha hivyo kujikuta wakikosa ajira.
Mafunzo hayo yaliwahusisha vijana wasioona wapatao 60 kutoka kata nne za Misugusugu, Visiga, Kibaha na Kongowe na kufadhiliwa na The Foundation for Civil Society
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WANANCHI wametakiwa kuhakikisha wanazingatia matumizi ya dawa za minyoo kila baada ya miezi mitatu ili kuepukana na athari ikiwa ni pamoja na magonjwa ya Kisukari na Presha.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Ofisa afya Mstaafu Allice Bakari alipozungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa minyoo ni chanzo cha magonjwa hayo makubwa ambayo yanasababisha vifo.
Bakari alisema kuwa kutokana na watu kutotumia kabisa dawa za kuua minyoo kumesababisha watu kupata athari kubwa za kiafya kutokana na ulaji wa vyakula ambao husababisha watu kupata minyoo.
“Minyoo ni chanzo cha magonjwa mengi makubwa yakiwemo moyo kutanuka, kuchanganyikiwa, mba na baadhi ya viuongo vya ndani kuathirika na kushindwa kufanya kazi na hatimaye ni kifo,” alisema Bakari.
Alisema kuwa tatizo la minyoo linazidi kuwa kubwa kutokana na baadhi hata ya wahudumu wa afya kuumwa kutokana na kutotumia dawa za minyoo kutokana na kutotambua ukubwa wa tatizo hilo.
“Hata baadhi ya madaktari wameathiriwa na hali hiyo kutokana na kutoona kuwa minyoo ni tatizo lakini ukweli ni kwamba hili ni tatizo kubwa sana na inabidi wahudumu wa afya kulifuatilia kwa umakini ili kuwanusuru watu,” alisema Bakari.
Ofisa afya huyo ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye hospitali ya Tumbi iliyopo wilayani Kibaha alisema kuwa minyoo inapokuwa imekithiri mwilini hushambulia viungo mbalimbali vya ndani ya mwili na kuleta athari hizo.
“Ushauri ni kwamba madaktari wanapaswa kuwa makini kwa kuwashauri wagonjwa kutumia dawa za kuwaua wadudu hao kwa kujua kuwa endapo walishawahi kutumia dawa kwani watu wanafikiri minyoo ni kwa watoto pekee,” alisema Bakari.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MRADI mkubwa wa Maji wilayani Kibaha mkoani Pwani unatarajiwa kukamilika Agosti mwaka huu na kuondoa tatizo la ukosefu wa maji ambapo baadhi ya vitongoji wananchi wameanza kukimbia bili za maji.
Akizungumza na wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa uzinduzi wa matawi ya chamaa hicho Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema kuwa mara mradi huo utakapokamilika tatizo hilo itakuwa ni historia.
Koka alisema kuwa mradi huo wa maji ambao chanzo chake ni mto Ruvu utapitia kwenye mitaa yote ya Jimbo hilo ambapo kwa kipindi kirefu wananchi wamekuwa wakilalamika upatikanaji wa maji.
“Tunashukuru kuwa kwenye mradi uliotokea wilaya ya Bagamoyo baadhi ya mitaa ikiwemo ya Vikawe, Vikawe shule maji yanapatikana kwa wingi ambapo sasa watu wanakimbia bili kutokanana kushindwa kulipa kwani awali walikuwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa maji,” alisema Koka.
Alisema kwa sasa maji yamesambazwa kwenye mitaa 14 na mara mradi huo utakapokamilika wakazi wa Kibaha hawatanyanganyana maji na Jiji la Dar es Salaam ambao wanategemea chanzo kimoja hivyo maji kuwa ya mgao.
“Nawaomba msiwe na wasiwasi kwani mradi huo unaendelea vizuri ambapo kwa sasa wanatandaza mabomba ambayo kwa sasa yamefika eneo la Kongowe kilometa 10 kutoka hapa mjini hivyo Mungu akipenda wakati huo uliotajwa maji yatapatikana,” alisema Koka.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WANAWAKE wajawazito wilayani Kibaha mkoani Pwani wametakiwa kuacha kutumia dawa za kienyeji za kuongeza uchungu ili kupunguza vifo vya watoto wachanga.
Hayo yalisemwa na ofisa muuguzi wa kituo cha afya cha Mkoani, Prisca Nyambo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea kituo hicho hivi karibuni na kusema kuwa dawa hizo zianasababisha watoto kufia tumboni.
Nyambo alisema kuwa dawa hizo za kuongeza uchungu za kienyeji ni mbaya kwa watoto waliotumboni kwani wengi wamekuwa wakipoteza maisha.
“Tatizo la watoto kufia tumboni kwa sasa ni kubwa kutokana na wajawazito kutumia dawa hizo ili waweze kujifungua endapo muda umefika na hakuna dalili za kufanya hivyo,” alisema Nyambo.
Alisema kuwa wajawazito wanapaswa kwenda hospitali wanapoona muda wa kujifungua umefika lakini hawajifungui kuliko kutumia dawa hizo ambazo zinasabisha vifo vya watoto.
Aidha alisema vifo vya watoto wachanga ni kati ya saba na tisa kwa kila mwezi kutokana na sababu mbalimbali mojawapo ikiwa ni matumizi ya dawa hizo za kienyeji za kuongeza uchungu ambapo wastani wa wanawake wanaojifungua kwa kipindi hicho ni zaidi ya 300.
Alibainisha kuwa akinamama wajawazito wanaokwenda kujifungua hapo ni wengi kwani baadhi yao wanatoka maeneo ya Jiji la Dar es Salaam kama vile Mbezi, Kibamba, Kimara na Ilala kutokana na ukaribu.
Mwisho.




   

    

HABARI MOTOMOTO

Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA Cha Wasioona Nchini kimewataka vijana wenye ulemavu huo kuachana na dhana ya kuwa mara wamalizapo elimu mbalimbali ni laziwa waajiriwe badala yake wajiandae kwa kufanya shughuli za kujiajiri wenyewe.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na makamu mwenyekiti wa chama hicho Taifa Robert Bundala wakati wa mafunzo ya sera ya ajira kwa watu wenye ulemavu kwa vijana wanachama wa chama hicho wilayani Kibaha.
Bundala alisema kuwa soko la ajira kwa sasa ni gumu sana hivyo lazima vijana wajiwekee malengo ya kujiajiri wao wenyewe kupitia fursa zilizopo kwenye maeneo yao kuliko kusubiri kuajiriwa serikalini au sekta binafsi.
“Vijana wasioona wanapaswa kuachana na dhana hiyo badala yake wajiajiri kwa kupitia shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na ujasiriamali na si kutegemea kuajiriwa kwani upatikanaji wa ajira kwa sasa ni mgumu,” alisema Bundala.
Alisema kuwa ushindani wa soko la ajira hapa nchini kwa sasa ni mkubwa sana kwani hata watu wasiona na ulemavu wamekuwa wakilalamika hivyo lazima vijana hao watumie mafunzo mbalimbali wanayoyapata ili kujiajiri.
“Kwa sasa ubaguzi umepungua lakini kikubwa kinachoangaliwa ni uwezo wako wa kielimu kwani kwa wale wenye elimu nzuri wamepata ajira lakini lazima wabadili mfumo wa kusubiri ajira badala yake wajiajiri,” alisema Bundala ambaye ni mwalimu wa shule ya msingi.
Naye Mwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye naye ni mlemavu asiyeona Greyson Mlanga alisema kuwa ni vema vijana wakaangalia fursa za ajira zilizopo kwenye maeneo wanayoishi na kuwaondolea fikra kuwa lazima waajiriwe.
Mlanga alisema kuwa kutokana na ugumu wa ajira vijana wasioona wanapaswa kuangalia suala la kujiajiri kwani kutegemea ajira za kuajiriwa itakuwa ni vigumu sana kuweza kufanikiwa kujiletea maendeleo.
 Kwa upande wake moja ya washiriki wa mafunzo hayo Zuhura Omary alisema kuwa changamoto kwao ni nyingi kutokana na hali waliyonayo pia ni kutokana na kutokuwa na elimu ya kutosha hivyo kujikuta wakikosa ajira.
Mafunzo hayo yaliwahusisha vijana wasioona wapatao 60 kutoka kata nne za Misugusugu, Visiga, Kibaha na Kongowe na kufadhiliwa na The Foundation for Civil Society
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WANANCHI wametakiwa kuhakikisha wanazingatia matumizi ya dawa za minyoo kila baada ya miezi mitatu ili kuepukana na athari ikiwa ni pamoja na magonjwa ya Kisukari na Presha.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Ofisa afya Mstaafu Allice Bakari alipozungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa minyoo ni chanzo cha magonjwa hayo makubwa ambayo yanasababisha vifo.
Bakari alisema kuwa kutokana na watu kutotumia kabisa dawa za kuua minyoo kumesababisha watu kupata athari kubwa za kiafya kutokana na ulaji wa vyakula ambao husababisha watu kupata minyoo.
“Minyoo ni chanzo cha magonjwa mengi makubwa yakiwemo moyo kutanuka, kuchanganyikiwa, mba na baadhi ya viuongo vya ndani kuathirika na kushindwa kufanya kazi na hatimaye ni kifo,” alisema Bakari.
Alisema kuwa tatizo la minyoo linazidi kuwa kubwa kutokana na baadhi hata ya wahudumu wa afya kuumwa kutokana na kutotumia dawa za minyoo kutokana na kutotambua ukubwa wa tatizo hilo.
“Hata baadhi ya madaktari wameathiriwa na hali hiyo kutokana na kutoona kuwa minyoo ni tatizo lakini ukweli ni kwamba hili ni tatizo kubwa sana na inabidi wahudumu wa afya kulifuatilia kwa umakini ili kuwanusuru watu,” alisema Bakari.
Ofisa afya huyo ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye hospitali ya Tumbi iliyopo wilayani Kibaha alisema kuwa minyoo inapokuwa imekithiri mwilini hushambulia viungo mbalimbali vya ndani ya mwili na kuleta athari hizo.
“Ushauri ni kwamba madaktari wanapaswa kuwa makini kwa kuwashauri wagonjwa kutumia dawa za kuwaua wadudu hao kwa kujua kuwa endapo walishawahi kutumia dawa kwani watu wanafikiri minyoo ni kwa watoto pekee,” alisema Bakari.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MRADI mkubwa wa Maji wilayani Kibaha mkoani Pwani unatarajiwa kukamilika Agosti mwaka huu na kuondoa tatizo la ukosefu wa maji ambapo baadhi ya vitongoji wananchi wameanza kukimbia bili za maji.
Akizungumza na wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa uzinduzi wa matawi ya chamaa hicho Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema kuwa mara mradi huo utakapokamilika tatizo hilo itakuwa ni historia.
Koka alisema kuwa mradi huo wa maji ambao chanzo chake ni mto Ruvu utapitia kwenye mitaa yote ya Jimbo hilo ambapo kwa kipindi kirefu wananchi wamekuwa wakilalamika upatikanaji wa maji.
“Tunashukuru kuwa kwenye mradi uliotokea wilaya ya Bagamoyo baadhi ya mitaa ikiwemo ya Vikawe, Vikawe shule maji yanapatikana kwa wingi ambapo sasa watu wanakimbia bili kutokanana kushindwa kulipa kwani awali walikuwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa maji,” alisema Koka.
Alisema kwa sasa maji yamesambazwa kwenye mitaa 14 na mara mradi huo utakapokamilika wakazi wa Kibaha hawatanyanganyana maji na Jiji la Dar es Salaam ambao wanategemea chanzo kimoja hivyo maji kuwa ya mgao.
“Nawaomba msiwe na wasiwasi kwani mradi huo unaendelea vizuri ambapo kwa sasa wanatandaza mabomba ambayo kwa sasa yamefika eneo la Kongowe kilometa 10 kutoka hapa mjini hivyo Mungu akipenda wakati huo uliotajwa maji yatapatikana,” alisema Koka.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WANAWAKE wajawazito wilayani Kibaha mkoani Pwani wametakiwa kuacha kutumia dawa za kienyeji za kuongeza uchungu ili kupunguza vifo vya watoto wachanga.
Hayo yalisemwa na ofisa muuguzi wa kituo cha afya cha Mkoani, Prisca Nyambo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea kituo hicho hivi karibuni na kusema kuwa dawa hizo zianasababisha watoto kufia tumboni.
Nyambo alisema kuwa dawa hizo za kuongeza uchungu za kienyeji ni mbaya kwa watoto waliotumboni kwani wengi wamekuwa wakipoteza maisha.
“Tatizo la watoto kufia tumboni kwa sasa ni kubwa kutokana na wajawazito kutumia dawa hizo ili waweze kujifungua endapo muda umefika na hakuna dalili za kufanya hivyo,” alisema Nyambo.
Alisema kuwa wajawazito wanapaswa kwenda hospitali wanapoona muda wa kujifungua umefika lakini hawajifungui kuliko kutumia dawa hizo ambazo zinasabisha vifo vya watoto.
Aidha alisema vifo vya watoto wachanga ni kati ya saba na tisa kwa kila mwezi kutokana na sababu mbalimbali mojawapo ikiwa ni matumizi ya dawa hizo za kienyeji za kuongeza uchungu ambapo wastani wa wanawake wanaojifungua kwa kipindi hicho ni zaidi ya 300.
Alibainisha kuwa akinamama wajawazito wanaokwenda kujifungua hapo ni wengi kwani baadhi yao wanatoka maeneo ya Jiji la Dar es Salaam kama vile Mbezi, Kibamba, Kimara na Ilala kutokana na ukaribu.
Mwisho.




   

    

HABARI MOTOMOTO

Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA Cha Wasioona Nchini kimewataka vijana wenye ulemavu huo kuachana na dhana ya kuwa mara wamalizapo elimu mbalimbali ni laziwa waajiriwe badala yake wajiandae kwa kufanya shughuli za kujiajiri wenyewe.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na makamu mwenyekiti wa chama hicho Taifa Robert Bundala wakati wa mafunzo ya sera ya ajira kwa watu wenye ulemavu kwa vijana wanachama wa chama hicho wilayani Kibaha.
Bundala alisema kuwa soko la ajira kwa sasa ni gumu sana hivyo lazima vijana wajiwekee malengo ya kujiajiri wao wenyewe kupitia fursa zilizopo kwenye maeneo yao kuliko kusubiri kuajiriwa serikalini au sekta binafsi.
“Vijana wasioona wanapaswa kuachana na dhana hiyo badala yake wajiajiri kwa kupitia shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na ujasiriamali na si kutegemea kuajiriwa kwani upatikanaji wa ajira kwa sasa ni mgumu,” alisema Bundala.
Alisema kuwa ushindani wa soko la ajira hapa nchini kwa sasa ni mkubwa sana kwani hata watu wasiona na ulemavu wamekuwa wakilalamika hivyo lazima vijana hao watumie mafunzo mbalimbali wanayoyapata ili kujiajiri.
“Kwa sasa ubaguzi umepungua lakini kikubwa kinachoangaliwa ni uwezo wako wa kielimu kwani kwa wale wenye elimu nzuri wamepata ajira lakini lazima wabadili mfumo wa kusubiri ajira badala yake wajiajiri,” alisema Bundala ambaye ni mwalimu wa shule ya msingi.
Naye Mwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye naye ni mlemavu asiyeona Greyson Mlanga alisema kuwa ni vema vijana wakaangalia fursa za ajira zilizopo kwenye maeneo wanayoishi na kuwaondolea fikra kuwa lazima waajiriwe.
Mlanga alisema kuwa kutokana na ugumu wa ajira vijana wasioona wanapaswa kuangalia suala la kujiajiri kwani kutegemea ajira za kuajiriwa itakuwa ni vigumu sana kuweza kufanikiwa kujiletea maendeleo.
 Kwa upande wake moja ya washiriki wa mafunzo hayo Zuhura Omary alisema kuwa changamoto kwao ni nyingi kutokana na hali waliyonayo pia ni kutokana na kutokuwa na elimu ya kutosha hivyo kujikuta wakikosa ajira.
Mafunzo hayo yaliwahusisha vijana wasioona wapatao 60 kutoka kata nne za Misugusugu, Visiga, Kibaha na Kongowe na kufadhiliwa na The Foundation for Civil Society
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WANANCHI wametakiwa kuhakikisha wanazingatia matumizi ya dawa za minyoo kila baada ya miezi mitatu ili kuepukana na athari ikiwa ni pamoja na magonjwa ya Kisukari na Presha.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Ofisa afya Mstaafu Allice Bakari alipozungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa minyoo ni chanzo cha magonjwa hayo makubwa ambayo yanasababisha vifo.
Bakari alisema kuwa kutokana na watu kutotumia kabisa dawa za kuua minyoo kumesababisha watu kupata athari kubwa za kiafya kutokana na ulaji wa vyakula ambao husababisha watu kupata minyoo.
“Minyoo ni chanzo cha magonjwa mengi makubwa yakiwemo moyo kutanuka, kuchanganyikiwa, mba na baadhi ya viuongo vya ndani kuathirika na kushindwa kufanya kazi na hatimaye ni kifo,” alisema Bakari.
Alisema kuwa tatizo la minyoo linazidi kuwa kubwa kutokana na baadhi hata ya wahudumu wa afya kuumwa kutokana na kutotumia dawa za minyoo kutokana na kutotambua ukubwa wa tatizo hilo.
“Hata baadhi ya madaktari wameathiriwa na hali hiyo kutokana na kutoona kuwa minyoo ni tatizo lakini ukweli ni kwamba hili ni tatizo kubwa sana na inabidi wahudumu wa afya kulifuatilia kwa umakini ili kuwanusuru watu,” alisema Bakari.
Ofisa afya huyo ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye hospitali ya Tumbi iliyopo wilayani Kibaha alisema kuwa minyoo inapokuwa imekithiri mwilini hushambulia viungo mbalimbali vya ndani ya mwili na kuleta athari hizo.
“Ushauri ni kwamba madaktari wanapaswa kuwa makini kwa kuwashauri wagonjwa kutumia dawa za kuwaua wadudu hao kwa kujua kuwa endapo walishawahi kutumia dawa kwani watu wanafikiri minyoo ni kwa watoto pekee,” alisema Bakari.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MRADI mkubwa wa Maji wilayani Kibaha mkoani Pwani unatarajiwa kukamilika Agosti mwaka huu na kuondoa tatizo la ukosefu wa maji ambapo baadhi ya vitongoji wananchi wameanza kukimbia bili za maji.
Akizungumza na wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa uzinduzi wa matawi ya chamaa hicho Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema kuwa mara mradi huo utakapokamilika tatizo hilo itakuwa ni historia.
Koka alisema kuwa mradi huo wa maji ambao chanzo chake ni mto Ruvu utapitia kwenye mitaa yote ya Jimbo hilo ambapo kwa kipindi kirefu wananchi wamekuwa wakilalamika upatikanaji wa maji.
“Tunashukuru kuwa kwenye mradi uliotokea wilaya ya Bagamoyo baadhi ya mitaa ikiwemo ya Vikawe, Vikawe shule maji yanapatikana kwa wingi ambapo sasa watu wanakimbia bili kutokanana kushindwa kulipa kwani awali walikuwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa maji,” alisema Koka.
Alisema kwa sasa maji yamesambazwa kwenye mitaa 14 na mara mradi huo utakapokamilika wakazi wa Kibaha hawatanyanganyana maji na Jiji la Dar es Salaam ambao wanategemea chanzo kimoja hivyo maji kuwa ya mgao.
“Nawaomba msiwe na wasiwasi kwani mradi huo unaendelea vizuri ambapo kwa sasa wanatandaza mabomba ambayo kwa sasa yamefika eneo la Kongowe kilometa 10 kutoka hapa mjini hivyo Mungu akipenda wakati huo uliotajwa maji yatapatikana,” alisema Koka.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WANAWAKE wajawazito wilayani Kibaha mkoani Pwani wametakiwa kuacha kutumia dawa za kienyeji za kuongeza uchungu ili kupunguza vifo vya watoto wachanga.
Hayo yalisemwa na ofisa muuguzi wa kituo cha afya cha Mkoani, Prisca Nyambo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea kituo hicho hivi karibuni na kusema kuwa dawa hizo zianasababisha watoto kufia tumboni.
Nyambo alisema kuwa dawa hizo za kuongeza uchungu za kienyeji ni mbaya kwa watoto waliotumboni kwani wengi wamekuwa wakipoteza maisha.
“Tatizo la watoto kufia tumboni kwa sasa ni kubwa kutokana na wajawazito kutumia dawa hizo ili waweze kujifungua endapo muda umefika na hakuna dalili za kufanya hivyo,” alisema Nyambo.
Alisema kuwa wajawazito wanapaswa kwenda hospitali wanapoona muda wa kujifungua umefika lakini hawajifungui kuliko kutumia dawa hizo ambazo zinasabisha vifo vya watoto.
Aidha alisema vifo vya watoto wachanga ni kati ya saba na tisa kwa kila mwezi kutokana na sababu mbalimbali mojawapo ikiwa ni matumizi ya dawa hizo za kienyeji za kuongeza uchungu ambapo wastani wa wanawake wanaojifungua kwa kipindi hicho ni zaidi ya 300.
Alibainisha kuwa akinamama wajawazito wanaokwenda kujifungua hapo ni wengi kwani baadhi yao wanatoka maeneo ya Jiji la Dar es Salaam kama vile Mbezi, Kibamba, Kimara na Ilala kutokana na ukaribu.
Mwisho.




   

    

Sunday, April 26, 2015

KILUVY UNITED YALILIA UDHAMINI TFF

Na John Gagarini, Kibaha
SHIRIKISHO la Soka Nchini (TFF) limeshauriwa kutafuta wadhamini kwa ajili ya ligi mbalimbali na si ligi kuu pekee ili kuzipunguzia gharama timu za madaraja ya chini.
Ushauri huo ulitolewa na mlezi wa timu ya soka ya Kiluvya United ya mkoa wa Pwani Edward Mgogo wakati wa sherehe za kutambulisha kombe walilochukua la ligi ya mabingwa wa mikoa kwa mkuu wa mkoa huo Evarist Ndikilo na kufanikiwa kupanda daraja la kwanza.
Mgogo alisema kuwa timu za madaraja ya chini zina mzigo mkubwa katika kuziendesha timu zao hivyo ni vema zikasaidiwa kupata ufadhili ili ziweze kushiriki ligi zao vizuri.
“Umefika wakati sasa ligi za chini nazo zikawa na udhamini ndiyo kazi ya TFF kuziwekea mazingira mazuri timu ziweze kushiriki vema kwenye ligi ambapo ligi kuu imekuwa na wadhamini tofauti tofauti,” alisema Mgogo.
Alisema kuwa msingi wa wachezaji wa ligi kuu ni ligi ndogo za chini hivyo ni vema TFF ikatafuta wadhamini ili wadhamini ligi hizo ambazo zinatoa wachezaji ambao wanatamba kwenye ligi ya Voda Com.
“Bila ya udhamini timu zinacheza kwenye mazingira magumu sana ambapo sisi tunatarajia kucheza ligi daraja la kwanza hivyo tunaomba TFF iliangalie hili pamoja na wadau wengine wajitokeze kutusaidia ili tufikie lengo letu la kupanda ligi kuu,” alisema Mgogo.
Kwa upande wake mwakilishi wa mkuu wa mkoa ambaye ni ofisa elimu Yusuph Kipengele alisema kuwa mkoa hauna fungu maalumu kwa ajili ya michezo.
 Kipengele alisema kuwa wao kama mkoa wanachoweza ni kutoa barua kwa ajili ya timu kwenda kuomba misaada sehemu mbalimbali kwa ajili ya kusaidiwa ili kuendeleza michezo.
Mwisho.             

    

HABARI MBALIMBALI ZA PWANI

Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA cha Walimu Tanzania (CWT) mkoa wa Pwani kimechagua viongozi wake kukiongoza chama hicho kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Uchaguzi huo ambao ulifanyika mjini Kibaha mwishoni mwa wiki hii ulimerejesha madarakani mwenyekiti wa zamani John Kirumbi ambaye alijinyakulia jumla ya kura 43 kati ya kura 85 za wajumbe wa uchaguzi huo na kuwashinda wenzake sita.
Kirumbi aliwashinda Hamis Kwangaya aliyejipatia kura 41 na Rajab Chalamila aliyepata kura moja huku wengine wakiambulia patupu huku Stella Kiyabo akipata nafasi ya kuwakilisha mkoa ngazi ya Taifa alijinyakulia kura 58.
Katika nafasi hiyo wagombea Hebert Mgimi aliyepata kura 15 na Mikidadi Mbelwa 12 huku nafasi ya mwaka hazina ikienda kwa Abubakary Alawi aliyepata kura 48, Honesta Mwilenga akipata kura 34 na Neema Wasato akipata kura mbili.
Kwa upande wa mwakilishi wa wanawake Martha Kanyawana alipata kura 55, Happy Mahava alipata kura 29 na Ajenta Mrema alipata kura moja upande wa nafasi ya mwakilishi wa watu wenye ulemavu Mohamed Ngomero alipata kura 48 akifuatiwa na Robert Bundala kura 37.
Nafasi ya uwakilishi wa vijana Judith Mangi alishinda kwa kura 42, David Phares alipata kura 27 na Charles Tesha kura 11, mwakilishi wa wenyeviti ni Mustapha Julius kura 80 huku za hapana zikiwa ni tano.
Kwa upande wa mjumbe kwenda baraza la Wafanyakazi TUCTA ni Rajab Mhambage aliyepata kura 71 kura nane za hapana na moja iliharibika huku wajumbe wawili kwenda TUCTA ni Grace Kalinga kura 54 na  Herbet Ngimi kura 28 huku kura mbili zikiharibika.
Akizungumza mara baada ya uchaguzi huo katibu wa CWT Pwani Joseph Nehemia alisema kuwa uchaguzi huo ulikwenda vizuri licha ya changamoto ndogondogo za hapa na pale.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA cha ACT Wazalendo mkoani Pwani kimeanza kujiimarisha baada ya kuweza kujinyakulia wanachama 1,200 kutoka vyama mbalimbali.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini  Kibaha katibu wa ACT mkoa wa huo Mrisho Halfan alisema kuwa chama hicho kimeweza kupata wanachama wengi kwa muda mfupi kutokana na sera nzuri ilizonazo.
Halfan alisema kuwa sera za chama hicho ni zile alizokuwa akitekeleza Mwalimu Julius Nyerere za uzalendo wan chi yake na si manufaa ya mtu au watu wachache.
“Uzinduzi wa matawi nao umesaidia kuwavutia watu kujiunga na chama chetu ambacho ni chama cha wazalendo na kina mlengo tofauti na vyama vingine na kitaleta mageuzi ya kweli,” alisema Halfan.
Alisema kuwa ACT inakuja kivingine ili kufikia lengo la kuwasaidia wananchi kwani baadhi ya vyama havina sera nzuri zaidi ya kushambuliana majukwaani.
“ACT ni chama cha ukweli sisi hatutaki siasa za kukashifiana kama baadhi ya vyama vinavyofanya ambapo hutumia muda mwingi kushambulia upande fulani lakini vinashindwa kuwajibika kwa wananchi,” alisema Halfan
Aidha alisema kwa sasa watu wanataka maendeleo na si malumbano kwani yamewapotezea muda watu badala ya kutafakari kuleta maendeleo ambayo ndiyo kiu ya kila Mtanzania.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA cha wa wafanyakazi wa hifadhi ya mahoteli na majumbani na huduma za jamii (CHODAWU) kimewaomba waajiri kuchagua wafanyakazi bora na hodari wakati wa sherehe za siku ya wafanyakazi duniani Mei Mosi.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mwenyekiti wa CHODAWU mkoani Pwani Paul Msilu alisema kuwa waajiri wafanye uchaguzi mzuri juu ya wafanyakazi bora.
Msilu alisema kuwa kwa mwaka huu chama chao ndiyo kinachoandaa sherehe za wafanyakazi kupitia shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA) kwenye mkoa huo zitakazofanyika wilayani Mafia.
“Tunawaomba waajiri kuwachagua wafanyakazi bora ili iwe motisha na kuondoa manunguniko juu ya uteuzi wa wafanyakazi wenye sifa za kuwa bora,” alisema Msilu.
Aidha alisema anaomba waajiri kuwapatia zawadi zinazostahili ili kuwafanya wafanyakazi wajitume wawapo kazini kwani motisha ya zawadi nzuri ndizo zitaleta jitihada za uwajibikaji.
“Maandalizi yanaendelea vizuri ambapo baadhi ya vitu vimekamilika na bado tunaendelea kuomba michango kutoka kwa wadau mbalimbali wakiwemo waajiri ili kufanikisha sherehe hizo zinazofanyika kila mwaka,” alisema Msilu.
Alisema sherehe hizo ni muhimu kwa wafanyakazi ambao siku hiyo hukaa kwa pamoja na kubadilishana mawazo pamoja na kujua changamoto na mafanikio yao kwa kipindi cha mwaka mmoja.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WALIMU na wanafunzi wametakiwa kushirikiana ili kuhakikisha Taifa la Tanzania linakuwa na watafiti na wagunduzi wa teknolojia mbalimbali.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka wakati wa sherehe za kuwapongeza wanafunzi waliofanya vizuri kwenye shindano la Insha iliyokuwa inasema utatumiaje rasilimali zlizopo kukiabilina na umaskini lililoandaliwa na mbunge huyo.
Koka alisema kuwa utafiti na ugunduzi ndiyo utakaopelekea nchi kupata mafanikio katika maenedeleo kupitia tafiti na ugunduzi wa masuala mbalimbali.
“Tafiti na ugunduzi ndiyo silaha ya kujiletea maendeleo kwa nchi yoyote ile hivyo lazima tuwajenge wanafunzi wetu kuwa wagunduzi na watafiti wa mambo ya kimaendeleo,” alisema Koka.
Alisema kuwa endapo wanafunzi wataandaliwa katika katika masuala hayo basi watweza kugundua teknolojia ambazo wataziuza kama ilivyo kwa mataifa yaliyoendelea ambayo yananufaika.
“Hayo yote tunaweza kuyafikia kwa kuwa na ushirikiano baina ya pande zote wakiwemo walimu, wazazi na wanafunzi wenyewe na insha kama hizi huwasaidia wanafunzi kujenga ujasiri wa kujieleza na kama maandalizi ya elimu ya juu,” alisema Koka.
Awali kwa upande wake mwenyekiti wa Asasi isiyo ya kiserikali ya Youth Under Umbrella Castro David alisema kuwa lengo la insha hiyo ambayo ilishirikisha shule 14 za sekondari ni kuwajengea wanafunzi ustadi wa uandishi wa kazi za fasihi za ubunifu .
David alisema kuwa pia lengo lingine ni  kuziunganisha shule ili ziwe na ushirikiano wa kitaaluma na kufanya utafiti ambapo mshindi alikuwa ni Sara Malambo kutoka shule ya sekondari ya Tumbi ambaye alijinyakulia 100,000, akifuatiwa na Hija Hega wa Visiga 50,000 na Peter Asenga 30,000 ambazo walikabidhiwa na Mbunge huyo.
Mwisho.