Thursday, August 14, 2014

johngagariniblog: KAMATI ZA MADIWANI SARAKASI TUPU NA DIWANI CHADEMA...

johngagariniblog: KAMATI ZA MADIWANI SARAKASI TUPU NA DIWANI CHADEMA...:  Baadhi ya madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani wakiwa kwenye kikao cha baraza hilo kilichofanyika leo mjini Kibaha  Na...

DEREVA TEXI ALIYEPOTEA SIKU 8 AKUTWA AMEKUFA

Na John Gagarini, Kibaha
BAADA ya dereva wa Texi Richard Ponera (36) mkazi wa Mwendapole wilayani Kibaha mkoani Pwani kupotea kwa siku nane amepatikana akiwa ameuwawa  na kuporwa gari alilokuwa akiliendesha.
Marehemu ambaye alikuwa akifanyia shughuli zake kwenye kituo kikuu cha Mabasi cha Maili Moja wilayani humo alipotea Agosti 6 Mwaka huu majira ya saa 1 usiku alipokodishwa na watu wawili wasio fahamika waliojifanya kuwa ni wateja.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani humo Mrakibu Msaidizi wa Polisi (SSP) Athuman Mwambalaswa alisema kuwa mwili wake ulitupwa vichakani.
Kamanda Mwambalaswa alisema kuwa mwili wa marehemu ulikutwa huko eneo la Mihande Mashambani Mlandizi wilayani Kibaha ukiwa umeharibika vibaya huku gari  alilokuwa akiendesha lenye namba za usajili T 905 BHT aina ya Corolla nyeupe.
“Chanzo cha mauaji hayo ni katika kuwania mali ambayo ni gari hilo ambalo halijapatikana na hakuna mtu ambaye amekamatwa hadi sasa na bado uchunguzi unaendelea kuwatafuta watu waliohusika na tukio hilo,” alisema Mwambalaswa.
Alisema kuwa jeshi hilo linaendelea kufuatilia juu ya tukio hilo na halitasita kumchukulia hatua kali za kisheria watu waliohusika na tukio hilo la kusikitisha, marehemu alizikwa juzi na ameacha watoto wawili ambao ni Ruben (14) anayesoma kidato cha kwanza St Anne na Kontrada anayesoma darasa la sita shule ya Msingi Jitegemee Jijini Dar es Salaam.

Mwisho. 

Sunday, August 10, 2014

johngagariniblog: DEREVA TEXI APOTEA MAZINGIRA YA KUTATANISHA ALIKOD...

johngagariniblog: DEREVA TEXI APOTEA MAZINGIRA YA KUTATANISHA ALIKOD...: Na John Gagarini, Kibaha DEREVA wa Texi wa Maili Moja Richard Ponera (36) mkazi wa Mwendapole wilayani Kibaha mkoani Pwani amepotea k...

POLISI YAKANUSHA MTU KUCHUNWA NGOZI PWANI


JESHI la Polisi mkoani Pwani limekanusha uvumi ulioenea na kudai kuwa mkazi wa Kijiji cha Dondo wilaya ya Mkuranga Hamis Mahimbwa (20) kuwa amekufa kwa kuchunwa ngozi mwili mzima ila ni kutokana na kuungua na moto.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana mjini Kibaha kaimu kamanda wa Polisi mkoani humo mrakibu Msaidizi wa Polisi (SSP) Athuman Mwambalaswa amesema kuwa hakuna tukio kama hilo mkoani hapo.
Akifafanua juu ya tukio la mtu huyo kufa amesema kuwa mnamo Agosti 6 mwaka huu majira ya saa 2:00 usiku huko katika kijiji cha Dondo Tutani kata ya Kisiju wilayani humo Hamis Mahimbwa (27) alikutwa na wananchi akiwa ameungua moto mwili mzima.
Kamanda Mwambalaswa amesema marehemu alipiga kelele kuomba msaada baada ya kuungua na moto na kumchukua na kumpeleka hospitali kwenye kituo cha afya cha Kalole Kisiju na kuanza kupatiwa matibabu lakini kutokana na kuungua sana na moto alifariki dunia Agosti 7 mwaka huu majira ya saa 11:00 alfajiri.
Amesema kuwa baada ya kifo hicho ilipelekwa taarifa kwenye kituo cha polisi cha Mkuranga na jalada la uchunguzi MKU/IR/1202/2014 lilifunguliwa ili kubaini kifo chake.
Amebainisha kuwa baada ya kufunguliwa jalada hilo Ofisa Mpelelezi Mkuu wa Polisi wa makosa ya Jinai wa wilaya akiwa na timu ya askari wa upelelezi waliungana na maofisa wa usalama waliungana na Daktari wa wilaya ya Mkuranga Kibela kwenda kwenye eneo la tukio na kituo cha afya cha Kisiju kwa uchunguzi zaidi wa tukio hilo.
Aidha amesema kuwa daktari alichukua sampuli ya ngozi ambapo kwenye eneo la tukio ilikutwa suruali, majivu ya tisheti aliyokuwa amevaa, kandambili, kibiriti, chupa ya plastiki ya soda ambayo ilikuwa na mafuta ya petroli na katika eneo hilo hakukuwa na purukushani ya watu wengi ambapo mashahidi waliokwenda kumsaidia alipopiga kelele walimkuta marehemu akiwa anongea na kudai kuwa ameungua kwa moto bila ya kusema aliye muunguza.
Kaimu kamanda wa polisi huyo wa mkoa wa Pwani amesema baba mlezi wa marehemu Athuman Mahimbwa alipohojiwa alisema kuwa mwanae alikuwa akiugua ugonjwa wa Kifafa kwa miaka 17 na alimwambia kuwa anakufa kwa kuungua na moto na kutokana na uchunguzi uliofanywa na polisi pamoja na daktari umebainisha kuwa kifo chake kimesababishwa na moto na si kuchunwa ngozi.



Saturday, August 9, 2014

DEREVA TEXI APOTEA MAZINGIRA YA KUTATANISHA ALIKODISHWA NA WATU



Na John Gagarini, Kibaha
DEREVA wa Texi wa Maili Moja Richard Ponera (36) mkazi wa Mwendapole wilayani Kibaha mkoani Pwani amepotea katika mazingira ya kutatanisha baada ya kukodishwa na watu wasiofahamika.
Ponera alikodishwa na watu wawili ambao hawakufahamika  Agosti 5 mwaka huu majira ya saa 2:30 usiku akiwa anaendesha gari lenye usajili na T 905 BHT aina ya Corolla nyeupe.
Akizungumza na mjini Kibaha kuhusina na tukio hilo katibu wa Umoja wa madereva Texi Kibaha Mjini (KITAGURO) Fadhil Kiroga alisema kuwa dereva huyo tangu alipoondoka siku hiyo hadi leo hakurudi na hakuna taarifa yoyote  iliyopatikana juu yake.
Kiroga alisema kuwa siku ya tukio hilo Ponera alionekana akipatana na watu hao kwa muda kidogo kama dakika 10 hivi kisha akaondoka na watu hao ambao walikuwa wawili.
“Baada ya mapatano licha ya kuwa madereva wengine hawakuweza kujua walichokuwa wakiongea na Ponera waliondoka na alipofika Mlandizi aliwasiliana na mwenzetu ambaye ni Salum Mbawala na kumwambia kuwa kwa sasa yuko Mlandizi,” alisema Kiroga.
Alisema kuwa baada ya hapo simu yake haikuweza kupatikana tena kwani baada ya kuona harudi wenzake walijaribu kumpigia lakini simu yake haikupatikana tena.
“Ponera hapa alikuwa hana muda mrefu tangu aanze kazi na alipata gari hilo ambalo alikuwa amekabidhiwa kama wiki mbili zilizopita na gari lenyewe halikuwa kwenye hali nzuri sana kusema labda ilikuwa ni kishawishi cha watu labda kutaka kuliiba gari hilo, hatujui kilichomtokea mwenzetu,” alisema Kiroga.
Aidha alisema kuwa wamefanya jitihada mbalimbali ambapo walikwenda polisi kutoa taarifa juu ya tukio hilo na kupewa namba KMM/RB/847/2014 pia walitoa taarifa kwenye vituo vya Mlandizi na Tumbi kisha kutembelea maeneo ya Yombo, Miswe na Mzenga bila ya mafanikio.
Kwa uapande wake mke wa dereva huyo Rosemary Urasa (31) alisema kuwa siku ya tukio hilo alikuja naye hadi Maili Moja yeye akenda sokoni kununua vitu vya nyumbani akamwacha stendi kwa ajili ya kuendelea na shughuli zake kama kawaida.
“Nakumbuka majira ya saa 5 asubuhi nilimpigia simu baada ya gari linguine ambalo liko hapa nyumbani lilikuwa linapiga honi lenyewe nikamwambia aje alizime lakini kwa bahati nzuri kuna mtu alifanikiwa kulizima nikamjulisha alikuwa njiani kuja lakini akarudia eneo linaloitwa Picha ya Ndege, toka hapo kila nikipiga simu simpati,” alisema Urasa.
Alibainisha kuwa mumewe ambaye wamezaa naye watoto wawili walihamia Kibaha baada ya kufanikiwa kujenga na kuzaa watoto wawili ambao ni Ruben (14) anayesoma kidato cha kwanza St Anne na Kontrada anayesoma darasa la sita shule ya Msingi Jitegemee.
Aidha alisema kuwa wakati mwingine mumewe hufanya kazi na kukesha hivyo siku hiyo usiku alijua kuwa atakesha lakini ilipofika asubuhi alishangaa kutokumwona kwani endapo anakuwa amekesha asubuhi ni lazima arudi lakini siku hiyo hakumwona ikambidi aje kwenye eneo analopaki lakini alipouliza wakasema tangu alivyoondoka jana hajaonekana tena.
Naye mmiliki wa gari hilo Athuman Kimia alisema kuwa siku hiyo ya tukio aliwasiliana na Ponera ambapo kulikuwa na tatizo la kulipia gari linapokuwa barabarani na kumpa 170,000 kwa ajili ya kulipia.
Kimia alisema kuwa baada ya kama saa moja alimpigia na kumwambia kila kitu kashalipia hivyo mambo mazuri na ndipo alipoendelea na shughuli kama kawaida.
“Tumekubaliana kila baada ya wiki awe ananipa malipo ya kazi lakini nilipigiwa simu kuambiwa kuwa Ponera aonekani na nilipojaribu kumpigia simu yake haipatikani sijui kilichomtokea ninini kwani yeye huwa ananipigia endapo kumetokea tatizo kwani sasa hivi ni wiki ya pili tangu nimkabidhi gari ,” alisema Kimia.
Mwisho.

Monday, August 4, 2014

WASOMI WATUMIE TAALUMA ZAO KULETA MAENDELEO

Na John Gagarini, Chalinze
WASOMI kwenye Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wametakiwa kutumia elimu yao kukabiliana na changamoto za kimaendeleo zilizopo jimboni humo.
Hayo yalisemwa na Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alipokuwa akizindua maktaba ya shule ya sekondari ya Chalinze iliyojengwa na na kampuni ya kutengeneza saruji ya Tanga Simenti huku taasisi ya Read International ikiwa imetoa msaada wa vitabu.
Ridhiwani alisema kuwa jimbo hilo lina changamoto nyingi ambazo nyingine zitatatuliwa na wasomi wanaotoka eneo hilo na wengine kwa lengo la kuleta maendeleo.
“Elimu mnayosoma iwe chachu na ya maana kwa kuleta maendeleo ya jimbo hili kwani wazazi wenu wanajitolea kuwasomesha ili baadaye na nyie muweze kuwa msaada kwa jamii na  elimu ya sasa inaendana na vitendo ambavyo ndiyo tafsiri  kwa vile wanavyokuwa wamejifunza wanafunzi na si kuwa wasomi jina ambao hawana msaada kwa jamii inayowazunguka,” alisema Ridhiwani.
Alibainisha kuwa maktaba ambayo tumeizindua leo iwe chanzo cha nyie kujifunza kwa bidii kwa kujisomea baada ya walimu kuwafundisha kwani Watanzania kwa sasa bila ya elimu ni kazi bure na hataweza kufanya jambo lololote la kimaendeleo.
Kwa upande wake kaimu meneja biashra wa kampuni ya Tanga Simenti Yasin Hussein alisema kuwa wamejenga jengo hilo kwa lengo la kuhakikisha shule hiyo inakabiliana na tatizo la ukosefu wa maktaba ambapo hutoa asilimia moja ya faida ya mapato wanayopata kwa kurudisha kwa jamii kwa kusaidia masuala mbalimbali yakiwemo ya mazingira, elimu na afya.
“Tumetumia kiasi cha shilingi milioni 47 kwa ajili ya ujenzi huu ambapo mpango ni kujenga maktaba kwenye shule za Mingoyo Lindi na Kinyerezi Jijini Dar es Salaam na watatumia zaidi ya shilingi milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa maabara na maktaba kwenye mikoa mbalimbali nchini,” alisema Hussein.
Naye mwalimu mkuu wa shule hiyo Emanuel Kahabi alisema kuwa ufunguzi wa maktaba hiyo utasaidia kukabiliana na changamoto ya maktaba ailiyokuwa inakabili shule yao ambayo ina wanafunzi 879.
Mwisho.

Picha no 1397 Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani akiongea wakati wa ufunguzi wa makataba ya shule ya sekondari ya Chalinze kushoto ni mwenyekiti wa bodi ya shule Mbwana Madeni na kulia ni mkuu wa polisi wilaya ya Chalinze Janeth Magori.

picha no 1389 Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akiweka alama kwenye ukuta kama alama ya kumbukumbu baada ya kuizindua makta ya shule ya sekondari ya Chalinze.

picha no 1369 Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya Chalinze wakimsikiliza Mbunge wa Chalinze Riidhiwani Kikwete maara baada ya kuzindua maktaba ya shule hiyo.

picha no 1391 Mwenyekiti wa bodi ya shule ya sekondari ya Chalinze kushoto Mbwana Madeni akiongea katikakati ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete na katikati mkuu wa polisi kanda maalumu wilaya ya Chalinze Janeth Magori.

picha no 1371 wanafunzi wa shule ya sekondari ya Chalinze wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete wakati wa uzinduzi wa maktaba ya shule.

 

Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani akiongea wakati wa ufunguzi wa makataba ya shule ya sekondari ya Chalinze kushoto ni mwenyekiti wa bodi ya shule Mbwana Madeni na kulia ni mkuu wa polisi wilaya ya Chalinze Janeth Magori.
 


Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akiweka alama kwenye ukuta kama alama ya kumbukumbu baada ya kuizindua makta ya shule ya sekondari ya Chalinze.
 

 

Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya Chalinze wakimsikiliza Mbunge wa Chalinze Riidhiwani Kikwete maara baada ya kuzindua maktaba ya shule hiyo.



Mwenyekiti wa bodi ya shule ya sekondari ya Chalinze kushoto Mbwana Madeni akiongea katikakati ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete na katikati mkuu wa polisi kanda maalumu wilaya ya Chalinze Janeth Magori.
 

 

picha no 1371 wanafunzi wa shule ya sekondari ya Chalinze wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete wakati wa uzinduzi wa maktaba ya shule.