Friday, December 29, 2017

RC NDIKILO AIPIGA TAFU KILUVYA UNITED MILIONI MBILI

 Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo

 Baadhi ya wachezaji wa Kiluvya United inayoshiriki ligi daraja la kwanza wakimskiliza mkuu wa mkoa wa Pwani hayupo pichani walipomtembelea ofisini kwake mjini Kibaha

 Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo akimkabidhi kiongozi wa timu ya Kiluvya United kiasi cha shilingi milioni 2 kwa ajili ya kuihamaisha iweze kushinda michezo yake na kuingia Ligi Kuu ya Voda Com

 Nahodha wa Timu ya Kiluvya United ya mkoani Pwani Ramadhan akishukuru baada ya kukabidhiwa fedha kwa ajili ya hamasa na mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo.






Na John Gagarini, Kibaha
KUELEKEA mchezo wake wa ligi daraja la Kwanza leo dhidi ya Ruvu kuwania kupanda Ligi Kuu unaotarajiwa kuchezwa  kwenye uwanja wa Filbert Bayi wilayani Kibaha mkoa wa Pwani umeipatia timu ya Kiluvya United kiasi cha shilingi milioni mbili kwa ajili ya hamasa ili waweze kushinda mchezo huo.
Akizungumza wakati wa kukabidhi fedha hizo kwa viongozi wa timu hiyo walioambatana na wachezaji ofisini kwake mjini Kibaha mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo alisema kuwa lengo ni kuhakikisha wanashinda mchezo huo. 
Ndikilo alisema kuwa viongozi wa timu hiyo walifika ofisini kwake na kuomba msaada wa kuisaidia timu yao ili iweze kufanya vizuri kwenye michezo yake mitano iliyosalia ya ligi hiyo na endapo watashinda watafanikiwa kupanda Ligi Kuu ya Voda Com.
“Tuko pamoja na timu yetu ambayo inawakilisha mkoa na leo tunawakabidhi fedha ambazo zimetolewa na wadau wa mkoa ili kufanikisha malengo ya kupanda Ligi Kuu kwani uwezekano huo upo,” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa wadau wanachotaka ni timu yao kushinda kwani imeonyesha ina uwezo wa kufanya hivyo kutokana na uwezo inaounyesha wanaamini inaweza kufanya vizuri na kujiweka kwenye nafasi nzuri ya harakati zake za kiutaka kupanda daraja ili kufikia Ligi Kuu ya Voda Com.
“Wadau wa soka wa mkoa wa Pwani wamejitolea fedha hizo kama hamasa ya kufanya vyema kwenye mchezo wa leo ambao utakuwa na ushindani mkubwa kwani timu hizo ziko kwenye nafasi nzuri ya kupanda Ligi Kuu ambapo Ruvu ndiyo kinara wa kundi hilo na United wakiwa kwenye nafasi ya tatu,” alisema Ndikilo.
Aidha alisema kuwa mdau ambaye anataka kuipeleka timu ya Kiluvya United nchi ya Ulaya ya Finland atafurahi kuona timu hiyo inashinda mchezo huo na kutoa zawadi ya mwaka mpya kwa wadau wa mkoa wa Pwani.
Naye nahodha wa timu hiyo Ramadhan Ally alisema kuwa wao wkao tayari kwa pambano hilo na watahakikisha wanapambana kwa nguvu zote ili wapate ushindi na kujiweka vizuri kwenye harakati zao za kupanda daraja.
Ally alisema kuwa kutokana na kupewa fedha hizo zitawasaidia kama morali kwao kwa ajili ya kupata ushindi huo ambao utakuwa muhimu ili kuwapa raha watu wa mkoa wa Pwani.
Mwisho.

MWENYEKITI UVCCM AWASHUKIA WATENDAJI WA SERIKALI NA VIONGOZI WA KUCHAGULIWA

 
 Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Kheri James akisalimiana na mwenyekiti wa UVCCM Kibaha Mjini Azilongwa wakati alipowasili wilayani Kibaha kwenye mkutano wa kumpongeza kuchaguliwa kwenye nafasi hiyo uliofanyika kata ya Kongowe. 

 Moja ya Vijana wa UVCCM Kibaha Mjini akimvalisha skafu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Kheri James alipowasili wilayani Kibaha

 Baadhi ya Vijana wa UVCCM Mkoani Pwani wakishanglia jambo wakati wa mkutano huo

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo akiongea kwenye mkutano huo.
 
 
Na John Gagarini, Kibaha
 
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Kheri James amewataka viongozi wa serikali na wale wa kuchaguliwa nchini kuhakikisha wanashiriki kwenye mikutano ya viongozi wa kitaifa ili waweze kupokea maagizo mbalimbali.

Aliyasema hayo mjini Kibaha wakati wa sherehe za kumpongeza kwa kuchaguliwa kwenye nafasi hiyo zilizoandaliwa na Uvccm Kibaha Mjini na kusema kuwa maagizo yanayotolewa hayawezi kufanyiwa kazi kutokana na wahusika kutokuwepo.

James alisema kuwa viongozi na watendaji wa serikali ambao hawashiriki vikao kama hivyo hawafai waondoke kwani wameshindwa kazi.

"Hapa tunatoa maagizo na wao hawapo kwani maelekezo hayo yanapotolewa watu wa kuyapokea hawapo kuanzia ngazi ya halmashauri za wilaya, wilaya na Mkoa wanapaswa kujirekebisha kama wanaona hawawezi kazi watupishe," alisema James.

Alisema kuwa maelekezo yanayotolewa ni kuzikabili changamoto ambapo atendaji wa serikali wanaposhindwa kutatua kero za wananchi ambazo ni ilani ya chama kuna sababisha chama kuwa na wakati mgumu nyakati za uchaguzi kwa wagombea wa ccm.

"Watendaji wanaohujumu waondoke kwani wao ndiyo watekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa ajili ya wananchi," alisema James.

"Viongozi hawapaswi kulewa madaraka ambayo ni kitu kibaya sana na ni sawa na ulevi na hutafsiriwa baada ya muda wa kuwa madarakani kwisha ambapo watu watakuhukumu kwa matendo yako na kuwa bakora ya kukuchapia," alisema James.

Alisema kuwa hataki uongozi wa mitandao wa fb,insta, WhatsApp anataka viongozi wa kufanya kazi kwani kazi ya kuongoza ni ngumu sana hasa wakati wa kuhakiki mali za jumuiya hiyo watapambana na watu wenye vyeo vikubwa na fedha nyingi hivyo ni vita kubwa.

Aidha aliwata viongozi wa chama kutowatumia tu vijana wakati wa uchaguzi wasiwafanye kama ngazi ya kupandia na kama hawatawashirikisha vijana wampe taarifa na suala la ajira liangaliwe kwani baadhi ya wafanyakazi wanaajiriwa toka nje kwa kazi zinazowezwa kufanywa na watanzania.

"Wamiliki waangalie maslahi ya wafanyakazi vitendea kazi kwani baadhi wanafanya kazi kwenye viwanda ambvyo huzalisha kwa kutumia kemikali ambazo zinaweza kuwa maafa endapo hawatapewa vifaa vya kuwakinga kwani inaweza kusababisha vifo kwani viwanda si kwa ajili ya kusababisha vifo," alisema James.

Aliwataka wabunge wasiwe wa mifukoni wakichaguliwa wanaondoka na kusubiri hadi muda wa uchaguzi kwa sasa hawana nafasi wanajitokeza muda huo na kuanza vurugu wakidai fulani anampinga kumbe hawakuwajibika na kujiweka mbali na wananchi pia viongozi wa chama pamoja madiwani kuhakikisha kuwa asilimia tano ya vijana inakuwa agenda ya kudumu kwenye vikao mbalimbali.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa ccm Mkoa Pwani Ramadhan Maneno alisema kuwa watahikikisha wana hakiki mali za umoja huo wakiwa kama wasimamiaji wa jumuiya zote za chama.

Awali mwenyekiti wa umoja huo Chalangwa Seleman wa mkoa alitaka viongozi kufuata maelekezo ya rais ili kufanya umoja huo kuwa kimbilio na watayatrkeleza yale yote yaliyotolewa na mwenyekiti wao.