 |
Mkuu wa mkoa wa Pwani
mwenye shati jeupe Injinia Evarist Ndikilo akionyeshwa ramani ya majengo ya
mabweni ya shule ya sekondari ya Nasibugani na moja ya wasimamizi wa ujenzi huo
yanayaojengwa na vijana toka Jeshi la Kujenga Taifa JKT Ruvu Mlandizi wilayani
Kibaha, kushoto ni katibu tawala wa mkoa Zuber Samataba |
Na John Gagarini, Mkuranga
MKUU wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo
emelipongeza Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kambi ya Ruvu Mlandizi wilayani
Kibaha kwa kujitolea kujenga mabweni ya shule ya Sekondari ya Nasibugani iliyopo
kata ya Msonga Tarafa ya Kisiju wilayani Mkuranga.
Alitoa pongezi hizo alipotembelea shule hiyo
ili kujionea maenedeleo ya ujenzi huo wa mabweni matano na nyumba tano za
walimu za shule hiyo ambapo wanafunzi wanalala kwenye baadhi ya vyumba vya
madarasa.
Ndikilo alisema kuwa kambi hiyo ilitoa vijana
zaidi ya 100 ambao wanaenedelea na ujenzi huo ambao umefikia hatua ya linta na
kwa sasa wana miezi mitatu.
“Jeshi limeonyesha uzalendo wa hali ya juu kwa
kujitolea kujenga bure mabweni hayo lengo ni kuhakikisha wanafunzi wa shule
hiyo wanaishi kwenye mazingira mazuri kuliko ilivyo sasa,” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa jeshi hilo limeunga mkono serikali
kwa kujitolea kujenga mabweni hayo hivyo kuokoa fedha nyingi endapo wamengepewa
wakandarasi.
“Hadi sasa wametumia fedha kidogo sana kiasi
cha zaidi ya milioni 120 lakini endapo wangewapa wakandarasi fedha ambazo
zingetumika zingekuwa ni nyingi zaidi,” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa watu wanaojitolea wanaisadia
serikali kwa kuiunga mkono kwa mambo mambo ya kimaendeleo inayoyafanya hali
ambayo inapunguza gharama na fedha hizo zinazookolewa zinatumika kwenye mipango
mingine.
“Kwa kuwa ujenzi unaendelea tunawaomba wadau
mbalimbali waendelee kujitokeza kusaidia ujenzi huo ili ukamilike mapema na
wanafunzi waweze kuishi kwenye mazingira mazuri na mnachotakiwa kukifanya kwa
sasa ni kufanya upembuzi kujua mahitaji ya vitu vinavyotakiwa ili kukamilisha
zoezi hili,” alisema Ndikilo.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mkuranga
Gilbert Sanga alisema kuwa anawashukuru wadau mbalimbali ambao wamejitolea
kujenga mabweni hayo na kufikia hatua hiyo.
Sanga alisema kuwa Waziri wa elimu Profesa Joyce
Ndalichako alitoa kiasi cha shilingi milioni 250 ambazo zianaendelea kutumika
katika ujenzi wa mabweni hayo hadi sasa
Alisema kuwa kazi ya kupanua ilianza kwa
wananchi kuchangia zaidi ya milioni nne na kuwataka wanaochangisha wawasilishe
fedha walizochangisha ili zifanye kazi husika
“Halmashauri walisema wametenga fedha kiasi cha
shilingi milioni 32 kwa bweni moja wanafunzi 48 tu tuliungana na kamati ya
ulinzi na usalama nao walikubali kuongeza mabweni zaidi na mkoa nao ukakubali
na kambi ya wazalendo ambao walipiga kambi na walifyetua tofali 45,000 na ni
kazi ambayo haina bajeti,” alisema Sanga.
Kwa upande wake msimamizi wa ujenzi toka kikosi
cha Ruvu JKT Mohamed Boko alimwomba mkuu wa mkoa wa Pwani kufanya jitihada ili
ujenzi huo uweze kukamilika ambapo kazi hiyo ilipangwa kufanyika kwa miezi
miwili lakini imekuwa kubwa na muda kuongezeka.
Mwis