Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani Bonaventura Mushongi akiwaonyesha waandishi wa habari hawapo pichani silaha aina ya SMG no 01304 ikiwa na risasi 30 ya Askari Jackson Shirima wa Saadani National Park ambaye aliporwa na mtuhumiwa Swalehe Mangupili na kufichwa kichakani huko Kijiji cha Gama wilaya ya Bagamoyo
Na John
Gagarini, Kibaha
JUMLA ya
makosa makubwa ya uhalifu 4,208 yameripotiwa kwenye vituo vya polisi mkoani
Pwani kwa mwaka 2016 ambapo kumekuwa na ongezeko la makosa 419 ikilinganishwa
na mwaka 2015 ambao ulikuwa na makosa 3,784.
Aidha makosa
madogo 16,332 yaliripotiwa katika kipindi hicho cha mwaka 2016 ambapo kuna
ongezeko la makosa 2,396 ikilinganishwa na mwaka 2015 ambapo kulikuwa na makosa
13,936.
Hayo yalisemwa
mjini Kibaha na kamanda wa polisi mkoani Pwani Bonaventura Mushongi wakati
akitoa taarifa ya mwaka mmoja uliopita na kusema kuwa watu waliohusika na
matukio hayo walifikishwa mahakamani.
Mushongi alisema
kuwa ongezeko la makosa hayo kumetokana na misako iliyofanywa, doria na
oparesheni kwenye maeneo mbalimbali sambamba na ushirikishwaji wa jamii kwenye
kufichua uhalifu.
“Tunawashukuru
wananachi kwa kuendelea kutupa taarifa mbalimbali ambazo zimesaidia kukabiliana
na uhalifu na tunaomba ubia uendelee kwani uwiano wa askari na raia bado
hautoshi kwani askari mmoja anahudumia raia zaidi 1,000 hivyo ulinzi shirikishi
ni muhimu,” alisema Mushongi.
Alisema kuwa
katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita walifikisha mahakamani makosa 1,439 na
makosa 159 watuhumiwa walikutwa na hatia na kuhukumiwa kifungo wakati makosa 29
watuhumiwa walishindwa kutiwa hatiani na kuachiwa huru na makosa mengine kesi bado zinaendelea
kwenye mahakama mbalimbali.
“Tumejiwekea
mikakati mbalimbali ya kukabiliana na uhalifu kwa kuimarisha vikosi mbalimbali
vilivyopo ndani ya mkoa, kuzuia na kutanzua matukio hayo kabla hayajatokea au
baada ya kutokea, kuimarisha doria za miguu katika maeneo tete kila wilaya kwa
ushirikiano na wananchi,” alisema Mushongi.
Aidha alisema
kuwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni upungufu wa vitendea kazi
ikiwa ni pamoja na uchache wa magari,Jografia ya mkoa kwwenye mipango miji ni
ngumu katika kumpata mhalifu kwa haraka pindi uhalifu unapotokea.
“Mwaingiliano
na mkoa wa Dar es Salaam unafanya wahalifu kuweza kuingia kirahisi na kufanya
makosa,kutokuwa na mpango bora wa matumizi ya ardhi hivyo kusababisha migogoro
ya ardhi katika jamii, uwepo wa ukanda wa mkubwa katika bahari unaosababisha
kuwepo kwa bandari bubu nyingi za kupitisha wahamiaji haramu na biashara za
magendo,” alisema Mushongi.
Alibainisha kuwa
mwaka uliopita kulikuwa na matukio makubwa ambayo yaliyovuta hisia za watu
ikiwa ni pamoja na kupatikana maiti saba wilaya ya Bagamoyo na mauaji ya
viongozi wa serikali za vijiji kwa wilaya za Mkuranga, Rufiji na Kibiti ambapo
katika matukio hayo watu 11 walikamatwa na
kufikishwa mahakamani.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment