Thursday, December 12, 2013

11 WADAKWA NA GONGO LITA 140



Na John Gagarini, Kibaha

JESHI la Polisi Mkoani Pwani linawashikilia watu 11 kwa tuhuma za kukutwa na Pombe ya Moshi lita 140 katika matukio mawili tofauti.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Kibaha , Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Ulrich Matei amethibitisha kushikiliwa kwa watu hao na ameeleza kuwa  katika tukio la kwanza Jeshi la Polisi lilifanikiwa kuwakamata watu saba majira ya saa 10:30 jioni Kijiji cha Oyoyo wilayaya ya Mkuranga.

Kamanda Matei aliwataja watuhumiwa hao kuwa Jubely Lokowano (45), Abdallah Ramadhani (36), Tiago Msuya (35), Halima Khamisi (28), Suzan Moses (25), Zaina Abdallah (40), pamoja na Ramadhani Kinjenge (48) wote wakiwa ni wakazi wa Kijiji cha Oyoyo Wilaya ya Mkuranga ambapo watuhumiwa hao walikutwa wakiwa na lita 40 za Pombe hiyo.

Aliongeza kuwa katika tukio la pili Jeshi la Polisi lilifanikiwa kukama lita 100 za Pombe ya Moshi pamoja na mtambo mmoja wa kutengenezea Pombe hiyo huko Kijiji cha Kisemvule Kata ya Vikindu Wilaya ya Mkuranga majira ya saa 10:00 alasiri. 


Waliokamatwa katika tukio hilo ni Shabani Thomas (22), Francis Felician (21), Mwanjaa Amil (35), pamoja na Lucy Samwel (45).

Watuhumiwa wote wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma dhidi yao mara baada ya uchunguzi wa awali kukamilika.

Mwisho.


No comments:

Post a Comment