Saturday, December 14, 2013

JOURNALISM

Other journalism grants

An overview of other organisations, institutions and funds that hand out research grants for investigative journalism.

Arab Reporters for Investigative Journalism – Jordan
In-depth journalism projects for the benefit of the Arab public.
For all journalists who are passionate about telling a story but cannot go ahead with their projects because of budget problems. Funded by Denmark.


The Milena Jesenská Fellowship program offers European journalists time off from their professional duties in order to pursue in-depth research on a topic of their choice. Journalists from Armenia, Azerbaijan, Georgia, and Turkey are also eligible to apply.
The call is directed towards cultural journalists, with the term “cultural” being interpreted in a broad sense to encompass a wide variety of intellectual and artistic fields. However, applicants’ work may also deal with societal issues of European relevance.
 

Thursday, December 12, 2013

WADAKWA NA GONGO LITA 140



Na John Gagarini, Kibaha

JESHI la Polisi Mkoani Pwani linawashikilia watu 11 kwa tuhuma za kukutwa na Pombe ya Moshi lita 140 katika matukio mawili tofauti.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Kibaha , Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Ulrich Matei amethibitisha kushikiliwa kwa watu hao na ameeleza kuwa  katika tukio la kwanza Jeshi la Polisi lilifanikiwa kuwakamata watu saba majira ya saa 10:30 jioni Kijiji cha Oyoyo wilayaya ya Mkuranga.

Kamanda Matei aliwataja watuhumiwa hao kuwa Jubely Lokowano (45), Abdallah Ramadhani (36), Tiago Msuya (35), Halima Khamisi (28), Suzan Moses (25), Zaina Abdallah (40), pamoja na Ramadhani Kinjenge (48) wote wakiwa ni wakazi wa Kijiji cha Oyoyo Wilaya ya Mkuranga ambapo watuhumiwa hao walikutwa wakiwa na lita 40 za Pombe hiyo.

Aliongeza kuwa katika tukio la pili Jeshi la Polisi lilifanikiwa kukama lita 100 za Pombe ya Moshi pamoja na mtambo mmoja wa kutengenezea Pombe hiyo huko Kijiji cha Kisemvule Kata ya Vikindu Wilaya ya Mkuranga majira ya saa 10:00 alasiri. 


Waliokamatwa katika tukio hilo ni Shabani Thomas (22), Francis Felician (21), Mwanjaa Amil (35), pamoja na Lucy Samwel (45).

Watuhumiwa wote wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma dhidi yao mara baada ya uchunguzi wa awali kukamilika.

Mwisho.


11 WADAKWA NA GONGO LITA 140



Na John Gagarini, Kibaha

JESHI la Polisi Mkoani Pwani linawashikilia watu 11 kwa tuhuma za kukutwa na Pombe ya Moshi lita 140 katika matukio mawili tofauti.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Kibaha , Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Ulrich Matei amethibitisha kushikiliwa kwa watu hao na ameeleza kuwa  katika tukio la kwanza Jeshi la Polisi lilifanikiwa kuwakamata watu saba majira ya saa 10:30 jioni Kijiji cha Oyoyo wilayaya ya Mkuranga.

Kamanda Matei aliwataja watuhumiwa hao kuwa Jubely Lokowano (45), Abdallah Ramadhani (36), Tiago Msuya (35), Halima Khamisi (28), Suzan Moses (25), Zaina Abdallah (40), pamoja na Ramadhani Kinjenge (48) wote wakiwa ni wakazi wa Kijiji cha Oyoyo Wilaya ya Mkuranga ambapo watuhumiwa hao walikutwa wakiwa na lita 40 za Pombe hiyo.

Aliongeza kuwa katika tukio la pili Jeshi la Polisi lilifanikiwa kukama lita 100 za Pombe ya Moshi pamoja na mtambo mmoja wa kutengenezea Pombe hiyo huko Kijiji cha Kisemvule Kata ya Vikindu Wilaya ya Mkuranga majira ya saa 10:00 alasiri. 


Waliokamatwa katika tukio hilo ni Shabani Thomas (22), Francis Felician (21), Mwanjaa Amil (35), pamoja na Lucy Samwel (45).

Watuhumiwa wote wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma dhidi yao mara baada ya uchunguzi wa awali kukamilika.

Mwisho.


Thursday, December 5, 2013

WAOMBA KUCHOTA MAJI KWENYE MSITU

Na John Gagarini, Kibaha

WANANCHI WA Kitongoji cha Mpiji wilayani Kibaha mkoani Pwani wameuomba uongozi wa Wakala wa Misitu (TFS) Kanda ya Mashariki kuwaruhusu kupita kwenye eneo la msituo huo ili waweze kupata huduma ya maji ya kisima.

Akizungumza kwenye mkutano ulioandaliwa na Mradi wa Mama Misitu moja ya wananchi wa Kitongoji hicho Bw Shaban Nyoka alisema kuwa wamekuwa wakichapwa bakora na walinzi wa msitu huo mara wanedapo kuchota maji.

Bw Nyoka alisema kuwa kutokana na ukosefu wa maji kwenye Kitongoji hicho huwapasa kwenda kuchota maji kwenye visima vilivyopo kwenye hifadhi ya msitu huo.

“Tumekuwa tukichapwa bakora mara tunapokwenda kuchota maji kwenye visima hivyo vya maji lakini cha kushangaza mifugo ya moja ya wawekezaji kijijini hapo imekuwa haichukuliwi hatua yoyote, tunaomba waturuhusu tuwe tunachota maji huko,” alisema Bw Nyoka.
Alisema kuwa watu wamekuwa wakienda kuchota maji huko lakini wanapokutwa huko na walinzi wa msitu wamekuwa wakiadhibiwa kama vile wahalifu jambo limekuwa likiwafadhaisha.
“Sisi tunaomba hifadhi ituruhusu tuchote maji kwani hatufanyi uharibifu wowote kwani lengo letu ni kwa ajili ya kupata maji tu na si kingine hivyo ni vema wanegeturuhusu tupite huko kwa ajili ya kupata maji tu na si vingenevyo,” alisema Bw Nyoka.
Kwa upande wake mratibu wa mradi huo Bw Yahaya Mtonda alisema kuwa tatizo kubwa linatokana na uharibifu ambao umekuwa ukifanywa ndani ya msitu ambapo sheria hairuhusu kufanyika kwa shghuli yoyote.
Bw Mtonda alisema kuwa mipaka iliyowekwa imevikuta visima hivyo vikiwa ndani ya hifadhi hiyo hivyo kama wanataka kutumia visima hivyo ni vema wakaandika barua kwa meneja ili waweze kuruhusiwa kuchota maji kwenye msitu huo.
“Kama mnataka kufanya hivyo ni vema mkaandika barua rasmi kwenye wakala wa misitu wao ndiyo wenye uwezo wa kuruhusu nyie kupata huduma hiyo ya maji lakini lengo si kuwasumbua wananchi,” alisema Bw Mtonda.
Aliwataka wananchi kutumi kamati za misitu kudhibiti waharibifu wa misitu kwani uharibifu umekuwa mkubwa hali ambayo ina hatarisha misitu hiyo ya hifadhi ambayo ni chanzo kikuu cha utunzaji wa mazingira.

Mwisho.     

HABARI ZA PWANI

Na John Gagarini, Kibaha
HUKU kiwango cha maambukizi  ya ugonjwa wa UKIWMI wilayani Kibaha Mkoani Pwani kikiwa kimepanda kutoka
asilimia 7 mwaka jana hadi hadi kufikia asilimia 9.7 mwaka huu  wakazi wa kata ya Kikongo imetakiwa kuepukana unyanyapaa ili kupunguza maambukizi mapya.
Taarifa zinaonyesha kuwa idadi ya waliopata ushauri na kupima kwa kipindi
cha mwezi Januari hadi Desemaba mwaka huku waliopima ni
6,850 kati yao waliokutwa na maambukizi ya VVU ni 665 wanaume 214 na
wanawake 451.
Akizungumza na wananchi wa kata hiyo wakati wa mafunzo ya kutoa elimu kwa wananchi juu ya mapambano dhidi ya ugonjwa huo iliyoandaliwa na asasi ya kuwaletea maendeleo vijana ya Mlandizi Kibaha (YEN), diwani wa kata hiyo Bi Fatuma Ngozi alisema kuwa moja ya vitu vinavyochangia maambukizi mapya kuendelea ni kutokana na unyanyapaa ambao unaendelea ndani ya jamii.
Bi Ngozi alisema kuwa unyanyanyapaa unasababisha watu walioathirika kushindwa kujibainisha hivyo kuendelea kueneza ugonjwa huo kutokana na kuwa wasiri.
“Jamii inapaswa kuepukana na unyanayapaa ili kuondoa usiri uliopo kwani endapo wangeweka wazi hali zao ili jamii itambue na kuwasaidia,” alisema Bi Ngozi.
Alisema kuwa takwimu zinaonyesha maambukizi kuongezeka licha ya elimu kutolewa kila wakati lakini bado tatizo hilo linaendelea kuwa sugu.
“Kuna sababu nyingi ambazo zimekuwa chanzo cha maambukizi mapya ya ugonjwa huo lakini mojawapo ni unyanyapaa unaoendelea ndani ya jmii,” alisema Bi Ngozi.
Kwa upande wake mkurugenzi wa Naye mkurugenzi wa mtandao wa kuwapatia uwezo vijana (YEN) wa Mlandizi wilyani Kibaha ambao ndiyo walioandaa tamasha hilo Bw Issa Lukolo alisema kuwa lengo mafunzo hayo ni kuwakumbusha watu kujikinga na UKIMWI na kuepukana na njia zinazochangia maambukizi mapya.
Lukolo alisema kuwa jamii inapaswa kuepukana na vitendo ambavyo vimekuwa chanzo cha maambukizi ya ugonjwa huo ambao umekuwa ukimaliza nguvu kubwa na kusababisha jamii kutumia muda mwingi kuuguza wagonjwa.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WAZAZI nchini wameaswa kuhakikisha wanashirikiana na kusimamia malezi ya watoto wao badala ya kuwaachi wasichana wa kazi hali ambayo inachangia kwa kiwango kikubwa mmmonyoko wa maadili.
Hayo yalisemwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishina Msaidizi Mwandamizi Ulrich Matei katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Mkoa wa Pwani Mrakibu Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SSP) Atumani Mwambalaswa wakati wa mahafali ya sita katika shule ya awali ya Memory Day Care Centre iliyopo Kibaha Mkoa wa Pwani.

Akizungumza na wazazi pamoja na walezi wa wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo, Kamanda Mwambalasa alieleza kuwa ni jukumu la kila familia kuhakikisha kuwa, inajiwekea malengo na mikakati ya kuhakikisha haizalishi wahalifu bali inazalisha watu wema na waadilifu.

“Kila mmoja katika familia yake kukataa kuwa na mhalifu na hivyo iwapo sote tukiunganisha nguvu katika mradi mpya wa Jeshi la Polisi uliozinduliwa hivi karibu na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Said Mwema wa Familia yetu haina Mhalifu basi uhalifu utapungua na jamii yetu kuwa salama,”. Alisema Kamanda Matei

Kwa upande wake Mkuu wa Dawati la Jinsi na watoto Mkoa wa Pwani Mrakibu wa Polisi Yusta Milinga, (SP) aliwaomba wananchi kuendelea kujitokeza kwenye madawati yaliyopo kwenye Mkoa na kuwafichua wale wote ambao wamekuwa wakifanya vitendo hivyo ili sheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao na amewataka wazazi na walezi kutokubali kuyamaliza matukio ya ukatili wa jinsi majumbani mwao.

Naye Mkurugenzi wa Kituo hicho Bi Margareth Njimba alisema kuwa kutokana na kutambua umuhimu wa malezi ya mtoto na usalama wao katika makuzi, shule yao wameamua kuanzisha tawi la kupambana na vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia katika shule hiyo kwa kushirikiana na wazazi wa wanafunzi hao pamoja na dawati linalohusika na maswala ya kupambana na vitendo vya ukatili ndani ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani.
Mahafali hayo ya sita katika shule hiyo yalienda sambamba na uzinduzi wa tawi hilo uliofanywa na Mkuu wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Mkoa wa Pwani ambapo tawi hilo litakalokuwa na jukumu la ulinzi na usalama wa Mtoto ili kumfanya awe na makuzi yaliyona maadili jamii.


Mwisho

SITA WAFA PWANI

Na John Gagarini, Kibaha

WATU sita wamepoteza maisha katika matukio tofauti yaliyotokea Mkoani Pwani.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msiadizi Juma Yusufu Ally alithibitisha kutokea kwa matukio hayo na kueleza kuwa katika tukio la kwanza Bw Ramadhani Lubaya (35) mkulima na mkazi wa kijiji cha Kondo aliuwawa na watu wasiofahamika wakati akichunga mifugo ipatayo 90 porini ikiwa ni mchnganyiko wa ng’ombe na mbuzi mali ya Bw Malick Seif.

Tukio hilo lilitokea majira ya saa 9:00 alasiri Novemba  28 mwaka huu  katika Kijiji cha Kondo kata ya Zinga Wilaya ya Bagamoyo kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali kwenye paji la uso.

Bw Ally alisema kuwa katika tukio la pili huko kijiji cha Gwata Kata ya Mzenga Tarafa ya Mzenga Wilaya ya Kisarawe mfanya biashara Bw Peter Gumbi (28) mkazi wa Ngerengere Mkoa wa Morogoro aliuwawa kwa kupigwa risasi na watu wasiofahamika kisha kuporwa Tsh. 1,300,000/= alizokuwa nazo kwa ajili ya kwenda kununulia ng’ombe majira ya saa 8:00 mchana Novemba tarehe mwaka huu.

Alisema kuwa marehemu alikutwa na mauti wakati akitoka kijiji cha Gwata kwenda Dololo kwenye mnada akiwa amepakiwa kwenye Pikipiki. Dereva wa pikipiki hiyo anshikiliwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo.

Aidha katika tukio la tatu alisema mkazi wa Kitongoji cha Madafu Kata ya Vikindu Wilaya ya Mkuranga Bw Hamadi Juma (46) fundi ujenzi aliuwawa na wananchi waliojichukulia sheria mikononi baada ya kumtuhumu kupora pikipiki ambayo mmiliki wake bado kufahamika majira ya saa 3:30 usiku Novemba 28

“Marehemu alifikwa na mauti baada ya kushambuliwa kwa mawe na vigongo sehemu mbalimbali za mwili, kutokana na tukio hilo Jeshi la Polisi linaendesha msako mkali ili kuweza kuwabaini wale waliohusika katika tukio hilo kwa kisingizio cha hasira kali,” alisema Kamanda Ally.

Alibainisha kuwa katika tukio lingine, mnamo Novemba 30 mwaka huu majira ya saa 08:30 usiku huko Kijiji cha Msata Kata ya Msata Wilaya ya Bagamoyo Bw Ally Abdallah Mlenga (56) mkulima na ambaye pia anajishughulisha na kazi za uganga wa kienyeji alivamiwa nyumbani kwake na watu nane ambao walimshambulia kwa mapanga na kumuua na kisha kumjeruhi mtoto wake aitwaye Bw Abdallah Ally (25) kwa kumkata mapanga kichwani na kifuani.

“Watu hao wanaodhaniwa kuwa ni majambazi walivamia nyumba hiyo na kuvunja mlango kwa kutumia kitu kizito na baada ya kutenda kosa hilo hawakuchukua kitu chochote,” alisema Kamanda Ally.

Aidha katika tukio linguine Bw Hassan Hamadi mkazi wa Kijiji cha Mbebetini  Kata ya Kibiti Wilaya ya Rufiji (25) aliuwawa na watu waliojichukulia sheria mkononi katika tukio lilitokea majira ya Desmba 1 mwaka huu majira ya saa 7:45 usiku baada ya kumtuhumu kuvunja duka la Bw Selapia Stephen (47).

Kamanda Ally, alithibitisha kupoteza maisha kwa Omary Milondomo (17) mkazi wa Kinguila baada ya kugongwa na gari katika barabara kuu ya Dar es Salaam – Kilwa majira ya saa 2:30 usiku wa Novemba  30 mwaka huu huko katika Kijiji cha Mbembetini Kata ya Kibiti Wilaya ya Rufiji.

Alibainisha kuwa marehemu alifikwa na mauti baada ya kugongwa na gari ambayo haikufahamika namba ambayo haikusimama baada ya kutenda kosa hilo. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Rufiji ukisubiri kufanyiwa uchunguzi wa daktari.

Mwisho.


SITA WAFA PWANI

Na John Gagarini, Kibaha

WATU sita wamepoteza maisha katika matukio tofauti yaliyotokea Mkoani Pwani.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msiadizi Juma Yusufu Ally alithibitisha kutokea kwa matukio hayo na kueleza kuwa katika tukio la kwanza Bw Ramadhani Lubaya (35) mkulima na mkazi wa kijiji cha Kondo aliuwawa na watu wasiofahamika wakati akichunga mifugo ipatayo 90 porini ikiwa ni mchnganyiko wa ng’ombe na mbuzi mali ya Bw Malick Seif.

Tukio hilo lilitokea majira ya saa 9:00 alasiri Novemba  28 mwaka huu  katika Kijiji cha Kondo kata ya Zinga Wilaya ya Bagamoyo kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali kwenye paji la uso.

Bw Ally alisema kuwa katika tukio la pili huko kijiji cha Gwata Kata ya Mzenga Tarafa ya Mzenga Wilaya ya Kisarawe mfanya biashara Bw Peter Gumbi (28) mkazi wa Ngerengere Mkoa wa Morogoro aliuwawa kwa kupigwa risasi na watu wasiofahamika kisha kuporwa Tsh. 1,300,000/= alizokuwa nazo kwa ajili ya kwenda kununulia ng’ombe majira ya saa 8:00 mchana Novemba tarehe mwaka huu.

Alisema kuwa marehemu alikutwa na mauti wakati akitoka kijiji cha Gwata kwenda Dololo kwenye mnada akiwa amepakiwa kwenye Pikipiki. Dereva wa pikipiki hiyo anshikiliwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo.

Aidha katika tukio la tatu alisema mkazi wa Kitongoji cha Madafu Kata ya Vikindu Wilaya ya Mkuranga Bw Hamadi Juma (46) fundi ujenzi aliuwawa na wananchi waliojichukulia sheria mikononi baada ya kumtuhumu kupora pikipiki ambayo mmiliki wake bado kufahamika majira ya saa 3:30 usiku Novemba 28

“Marehemu alifikwa na mauti baada ya kushambuliwa kwa mawe na vigongo sehemu mbalimbali za mwili, kutokana na tukio hilo Jeshi la Polisi linaendesha msako mkali ili kuweza kuwabaini wale waliohusika katika tukio hilo kwa kisingizio cha hasira kali,” alisema Kamanda Ally.

Alibainisha kuwa katika tukio lingine, mnamo Novemba 30 mwaka huu majira ya saa 08:30 usiku huko Kijiji cha Msata Kata ya Msata Wilaya ya Bagamoyo Bw Ally Abdallah Mlenga (56) mkulima na ambaye pia anajishughulisha na kazi za uganga wa kienyeji alivamiwa nyumbani kwake na watu nane ambao walimshambulia kwa mapanga na kumuua na kisha kumjeruhi mtoto wake aitwaye Bw Abdallah Ally (25) kwa kumkata mapanga kichwani na kifuani.

“Watu hao wanaodhaniwa kuwa ni majambazi walivamia nyumba hiyo na kuvunja mlango kwa kutumia kitu kizito na baada ya kutenda kosa hilo hawakuchukua kitu chochote,” alisema Kamanda Ally.

Aidha katika tukio linguine Bw Hassan Hamadi mkazi wa Kijiji cha Mbebetini  Kata ya Kibiti Wilaya ya Rufiji (25) aliuwawa na watu waliojichukulia sheria mkononi katika tukio lilitokea majira ya Desmba 1 mwaka huu majira ya saa 7:45 usiku baada ya kumtuhumu kuvunja duka la Bw Selapia Stephen (47).

Kamanda Ally, alithibitisha kupoteza maisha kwa Omary Milondomo (17) mkazi wa Kinguila baada ya kugongwa na gari katika barabara kuu ya Dar es Salaam – Kilwa majira ya saa 2:30 usiku wa Novemba  30 mwaka huu huko katika Kijiji cha Mbembetini Kata ya Kibiti Wilaya ya Rufiji.

Alibainisha kuwa marehemu alifikwa na mauti baada ya kugongwa na gari ambayo haikufahamika namba ambayo haikusimama baada ya kutenda kosa hilo. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Rufiji ukisubiri kufanyiwa uchunguzi wa daktari.

Mwisho.


SITA WAFA PWANI

Na John Gagarini, Kibaha

WATU sita wamepoteza maisha katika matukio tofauti yaliyotokea Mkoani Pwani.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msiadizi Juma Yusufu Ally alithibitisha kutokea kwa matukio hayo na kueleza kuwa katika tukio la kwanza Bw Ramadhani Lubaya (35) mkulima na mkazi wa kijiji cha Kondo aliuwawa na watu wasiofahamika wakati akichunga mifugo ipatayo 90 porini ikiwa ni mchnganyiko wa ng’ombe na mbuzi mali ya Bw Malick Seif.

Tukio hilo lilitokea majira ya saa 9:00 alasiri Novemba  28 mwaka huu  katika Kijiji cha Kondo kata ya Zinga Wilaya ya Bagamoyo kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali kwenye paji la uso.

Bw Ally alisema kuwa katika tukio la pili huko kijiji cha Gwata Kata ya Mzenga Tarafa ya Mzenga Wilaya ya Kisarawe mfanya biashara Bw Peter Gumbi (28) mkazi wa Ngerengere Mkoa wa Morogoro aliuwawa kwa kupigwa risasi na watu wasiofahamika kisha kuporwa Tsh. 1,300,000/= alizokuwa nazo kwa ajili ya kwenda kununulia ng’ombe majira ya saa 8:00 mchana Novemba tarehe mwaka huu.

Alisema kuwa marehemu alikutwa na mauti wakati akitoka kijiji cha Gwata kwenda Dololo kwenye mnada akiwa amepakiwa kwenye Pikipiki. Dereva wa pikipiki hiyo anshikiliwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo.

Aidha katika tukio la tatu alisema mkazi wa Kitongoji cha Madafu Kata ya Vikindu Wilaya ya Mkuranga Bw Hamadi Juma (46) fundi ujenzi aliuwawa na wananchi waliojichukulia sheria mikononi baada ya kumtuhumu kupora pikipiki ambayo mmiliki wake bado kufahamika majira ya saa 3:30 usiku Novemba 28

“Marehemu alifikwa na mauti baada ya kushambuliwa kwa mawe na vigongo sehemu mbalimbali za mwili, kutokana na tukio hilo Jeshi la Polisi linaendesha msako mkali ili kuweza kuwabaini wale waliohusika katika tukio hilo kwa kisingizio cha hasira kali,” alisema Kamanda Ally.

Alibainisha kuwa katika tukio lingine, mnamo Novemba 30 mwaka huu majira ya saa 08:30 usiku huko Kijiji cha Msata Kata ya Msata Wilaya ya Bagamoyo Bw Ally Abdallah Mlenga (56) mkulima na ambaye pia anajishughulisha na kazi za uganga wa kienyeji alivamiwa nyumbani kwake na watu nane ambao walimshambulia kwa mapanga na kumuua na kisha kumjeruhi mtoto wake aitwaye Bw Abdallah Ally (25) kwa kumkata mapanga kichwani na kifuani.

“Watu hao wanaodhaniwa kuwa ni majambazi walivamia nyumba hiyo na kuvunja mlango kwa kutumia kitu kizito na baada ya kutenda kosa hilo hawakuchukua kitu chochote,” alisema Kamanda Ally.

Aidha katika tukio linguine Bw Hassan Hamadi mkazi wa Kijiji cha Mbebetini  Kata ya Kibiti Wilaya ya Rufiji (25) aliuwawa na watu waliojichukulia sheria mkononi katika tukio lilitokea majira ya Desmba 1 mwaka huu majira ya saa 7:45 usiku baada ya kumtuhumu kuvunja duka la Bw Selapia Stephen (47).

Kamanda Ally, alithibitisha kupoteza maisha kwa Omary Milondomo (17) mkazi wa Kinguila baada ya kugongwa na gari katika barabara kuu ya Dar es Salaam – Kilwa majira ya saa 2:30 usiku wa Novemba  30 mwaka huu huko katika Kijiji cha Mbembetini Kata ya Kibiti Wilaya ya Rufiji.

Alibainisha kuwa marehemu alifikwa na mauti baada ya kugongwa na gari ambayo haikufahamika namba ambayo haikusimama baada ya kutenda kosa hilo. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Rufiji ukisubiri kufanyiwa uchunguzi wa daktari.

Mwisho.


SITA WAFA PWANI

Na John Gagarini, Kibaha

WATU sita wamepoteza maisha katika matukio tofauti yaliyotokea Mkoani Pwani.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msiadizi Juma Yusufu Ally alithibitisha kutokea kwa matukio hayo na kueleza kuwa katika tukio la kwanza Bw Ramadhani Lubaya (35) mkulima na mkazi wa kijiji cha Kondo aliuwawa na watu wasiofahamika wakati akichunga mifugo ipatayo 90 porini ikiwa ni mchnganyiko wa ng’ombe na mbuzi mali ya Bw Malick Seif.

Tukio hilo lilitokea majira ya saa 9:00 alasiri Novemba  28 mwaka huu  katika Kijiji cha Kondo kata ya Zinga Wilaya ya Bagamoyo kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali kwenye paji la uso.

Bw Ally alisema kuwa katika tukio la pili huko kijiji cha Gwata Kata ya Mzenga Tarafa ya Mzenga Wilaya ya Kisarawe mfanya biashara Bw Peter Gumbi (28) mkazi wa Ngerengere Mkoa wa Morogoro aliuwawa kwa kupigwa risasi na watu wasiofahamika kisha kuporwa Tsh. 1,300,000/= alizokuwa nazo kwa ajili ya kwenda kununulia ng’ombe majira ya saa 8:00 mchana Novemba tarehe mwaka huu.

Alisema kuwa marehemu alikutwa na mauti wakati akitoka kijiji cha Gwata kwenda Dololo kwenye mnada akiwa amepakiwa kwenye Pikipiki. Dereva wa pikipiki hiyo anshikiliwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo.

Aidha katika tukio la tatu alisema mkazi wa Kitongoji cha Madafu Kata ya Vikindu Wilaya ya Mkuranga Bw Hamadi Juma (46) fundi ujenzi aliuwawa na wananchi waliojichukulia sheria mikononi baada ya kumtuhumu kupora pikipiki ambayo mmiliki wake bado kufahamika majira ya saa 3:30 usiku Novemba 28

“Marehemu alifikwa na mauti baada ya kushambuliwa kwa mawe na vigongo sehemu mbalimbali za mwili, kutokana na tukio hilo Jeshi la Polisi linaendesha msako mkali ili kuweza kuwabaini wale waliohusika katika tukio hilo kwa kisingizio cha hasira kali,” alisema Kamanda Ally.

Alibainisha kuwa katika tukio lingine, mnamo Novemba 30 mwaka huu majira ya saa 08:30 usiku huko Kijiji cha Msata Kata ya Msata Wilaya ya Bagamoyo Bw Ally Abdallah Mlenga (56) mkulima na ambaye pia anajishughulisha na kazi za uganga wa kienyeji alivamiwa nyumbani kwake na watu nane ambao walimshambulia kwa mapanga na kumuua na kisha kumjeruhi mtoto wake aitwaye Bw Abdallah Ally (25) kwa kumkata mapanga kichwani na kifuani.

“Watu hao wanaodhaniwa kuwa ni majambazi walivamia nyumba hiyo na kuvunja mlango kwa kutumia kitu kizito na baada ya kutenda kosa hilo hawakuchukua kitu chochote,” alisema Kamanda Ally.

Aidha katika tukio linguine Bw Hassan Hamadi mkazi wa Kijiji cha Mbebetini  Kata ya Kibiti Wilaya ya Rufiji (25) aliuwawa na watu waliojichukulia sheria mkononi katika tukio lilitokea majira ya Desmba 1 mwaka huu majira ya saa 7:45 usiku baada ya kumtuhumu kuvunja duka la Bw Selapia Stephen (47).

Kamanda Ally, alithibitisha kupoteza maisha kwa Omary Milondomo (17) mkazi wa Kinguila baada ya kugongwa na gari katika barabara kuu ya Dar es Salaam – Kilwa majira ya saa 2:30 usiku wa Novemba  30 mwaka huu huko katika Kijiji cha Mbembetini Kata ya Kibiti Wilaya ya Rufiji.

Alibainisha kuwa marehemu alifikwa na mauti baada ya kugongwa na gari ambayo haikufahamika namba ambayo haikusimama baada ya kutenda kosa hilo. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Rufiji ukisubiri kufanyiwa uchunguzi wa daktari.

Mwisho.