Monday, November 25, 2013

WATU MILIONI MOJA NA NUSU HUFARIKI

Na John Gagarini, Kibaha

IMEELEZWA kuwa watu milioni moja na nusu hufariki dunia kila mwaka kutokana na ajali za barabarani zinazotokea hapa nchini.

Hayo yalisemwa mjini Kibaha na kamanda wa kikosi cha usalama barabarani nchini Mohamed Mpinga, wakati wa maadhimisho ya siku ya kukumbuka watu waliokumbwa na majanga ya ajali za barabarani.

Kamanda Mpinga alisema kuwa mbali ya vifo hivyo pia jail hizo zinasababisha majeruhi zaidi ya 20,000 hadi 50,000 huku wengine wakipata ulemavu wa kudumu.

“Ajali ni moja ya vyanzo vya vifo vya watu wengi hapa nchini ambapo zinashika nafasi ya nane kwa kusababisha vifo na ifikapo mwaka 2020 kitakuwa ni chanzo cha tano kwa vifo,” alisema Kamanda Mpinga.

Alisema kuwa hadi mwezi Oktoba mwaka huu jumla ya ajali zaidi ya 19,000 zimetokea na kusababisha vifo zaidi ya 3,000 ukiachilia jail za hivi karibuni iliyoua watu saba mkoani Morogoro na iliyotokea mkoani Dodoma na kuua watu watatu.

“Watu wanaokufa ni nguvu kazi ya Taifa ambapo wengi wao ni vijana wenye umri kati ya miaka (18) hadi (35) hivyo Taifa kupoteza nguvu kazi kubwa ambayo ndiyo inayozalisha mali na kukuza uchumi wa nchi,” alisema Kamanda Mpinga.

Aidha alisema kuwa jeshi la polisi litaendelea kuchukua hatua kali kwa madereva wazembe ambao wamekuwa wakichangia kwa kiasi kikubwa kutokea kwa ajili za barabarani na kuwataka abiria kutoa taarifa kwa madereva wanaoendesha mabasi kwa mwendo wa kasi.

Kwa upande wake mtendaji wa shirika la Global Helmet Vaccine Initiative Bw Alpherio Nchimbi alisema kuwa lengo la maadhimisho hayo ambayo hufanyika kila mwaka ni kuwakumbuka wahanga wote waliopata matatizo kutokana na ajali za barabarani duniani.

Alisema kuwa moja ya wahanga wa ajali ni wanafunzi ambao wamekuwa wakigongwa mara wanapokuwa wakivuka kwenda ama kurudi shuleni.

“Tunawashauri madereva na wale wanaotumia vyombo vya moto kuachana na tabia ya kutumia vilevi ambavyo vimeonekana kuwa ni chanzo kikuu cha ajali za barabarani,” alisema Nchimbi.

Mwisho.

MADEREVA BODABODA WAFA AJALINI

Na John Gagarini, Kibaha

JUMLA ya watu nane wamepoteza maisha katika matukio mawili tofauti yaliyotokea mkoani Pwani likiwemo la madereva bodaboda wa tano kupoteza maisha kwa kugongana na gari la mizigo aina ya Scania uso kwa uso.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha kamanda wa polisi mkoani Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Pwani Ulrich Matei alisema kuwa matukio hayo yalitokea Novemba 21 mwaka huu majira ya saa 2: usiku.

Kamanda Matei alisema kuwa kwenye tukio la kwanza waendesha pikipiki (bodaboda) walipoteza maisha baada ya kugonga uso kwa uso na gari lenye namba za usajili T.602 ACT katika kichwa na tela lenye namba T.493 ABP aina ya Scania  likiendeshwa na Bw Dastan Migunda (35), mkazi wa Kitunda Dar es Salaam majira ya saa 2.00 usiku huko eneo la Ruvu Darajani kata ya Vigwaza barabara ya Dar es Salaam – Morogoro Wilaya ya Bagamoyo.

“Waliopoteza maisha katika tukio hilo ni, Bw Saidi Dosa (17), Bw Severine Luoga (19),  Bw Philemon Job (20), Bw Nassoro Mzalamila (18) na Bw Sadam Mapunda (21)  huku majeruhi wa ajali hiyo ni Bw Peter Maswaga (25) wote hawa ni wakazi wa Picha ya Ndege Wilaya ya Kibaha,” alisema Kamanda Matei.
.
Alisema kuwa kuwa chanzo cha tukio hilo ni mwendo kasi wa waendesha pikipiki watatu pikipiki zao zenye namba T.164 CHF, T.953 CQB na T.426 CJZ zote zikiwa ni aina ya Sanlg ambapo walikuwa wanatokea Picha ya Ndege kwenda Kijiji cha Buyuni kumfuatilia Bw Ramadhani Rajabu (16) dereva wa bodaboda kwa Mathias aliyetuhumiwa kwa wizi wa Pikipiki yenye namba.T.216 CNC aina ya Sanlg.

“Miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Tumbi Kibaha ikisubiri kufanyiwa uchunguzi wa Daktari na Majeruhi anaendelea na matibabu Hospitali ya Tumbi Kibaha,” alisema Matei.

Katika tukio la Pili, Kamanda Matei alithibitisha watu watatu kupoteza maisha huko Kitongoji cha Kibong’wa Kijiji cha Kisarawe Kata ya Kisarawe Tarafa ya Sungwi Wilaya ya Kisarawe  Mkoa wa Pwani majira ya saa 8.50 mchana.

Alisema kuwa watu hao walifikwa na mauti wakati walikuwa wanachimba kokoto kwenye shimo ambao ni Bi Mwazani Salehe (18), Ally Twaha (2), pamoja na Hasnatha Semin mwenye miezi (5) wote wakazi wa Kibong’wa.

Kamanda Matei aliongeza kuwa watu hao walifariki dunia baada ya kuangukiwa na udongo ulioporomoka na kuwafukia wote kwenye machimbo ya kokoto wakiwa wamejipumzisha chini ya shimo.

Aidha alisema tukio hilo mtu mmoja alinusurika kifo ambaye ni Bi Amina Emil (28), mkulima mkazi wa Kibong’wa ambaye alijeruhiwa na amelazwa Hospitali ya Wilaya Kisarawe akiendelea na matibabu, miili ya marehemu imefanyiwa uchunguzi na kukabidhiwa nduguzao kwa mazishi.
Mwisho.

STORY

Na John Gagarini, Bagamoyo

KUFUATIA Baraza la Madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo
MkoaniPwani,kuridhia kupitisha

rasmi kuanza kwa mchakato wa jimbo la Chalinze kuwa Wilaya baadhi ya
wakazi wa mji huo wameunga

mkono hatua hiyo.

Azimio hilo la Chalinze kuwa wilaya liliafikiwa baada ya Mwenyekiti wa
baraza hilo, Bw Shukuru
Mbato kuwataka madiwani hao kupiga kura za ndio ama hapana,katika
kikao cha baraza hilo,ambapo

wote kwa kauli moja walipiga kura ya ndio na hivyo kubariki maamuzi hayo.

Kwa nyakati tofauti baadhi ya wananchi walisema kuwa maamuzi hayo
yametolewa katika muda muafaka

na itasaidia Jimbo hilo kuendelea kukua kwa haraka hatimaye kuongeza
ajira na uchumi wake.

Mmoja wa wananchi hao ,Bi Kibena Mtoro alisema kwa kuanza kwa mchakato
huo ni faraja kwa wakazi

wa Chalinze na Bagamoyo kwajumla.

"Unajua mchakato huu umekuja muda muafaka kwakuwa umeenda sambamba na
ugawaji wa

vijiji,vitongoji vipya na kata mpya,hivyo kutaondoa tatizo la viongozi
kutawala maeneo makubwa

ambayo hushindwa kufikia wananchi kirahisi na utekelezaji kuwa
hafifu," alisema Bi Mtoro.

Kwa upande wake Bw Alex Matonange alisema kuwa mara mji huo
utakapokuwa wilaya itasaidia

kurahisisha upatikanaji wa huduma za kiutendaji ambazo kwa sasa
wanazipata mbali huko wilayani

Bagamoyo

Naye mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo,Bw Samuel
Salianga alisema kuwa ushirikiano

baina ya madiwani hao na viongozi mbalimbali watawezesha kufanikisha
jambo hilo.

Bw Salianga aliongeza kwamba mchakato huo wa jimbo la Chalinze kuwa
wilaya unahitaji uharaka

kabla ya kikao cha baraza la maendeleo la wilaya hiyo (DCC) na cha Mkoa (RCC).

Na John Gagarini, Kibaha

KATIKA kuhakikisha mji wa Kibaha unaongeza fursa za uwekezaji
Halmashauri ya Mji huo Mkoani

Pwani,imetenga hekari zaidi ya 3,000 kwa ajili ya viwanda ili kukuza
uchumi wa mji huo sambamba

na kuongeza ajira kwa vijana.

Akizungumzia na waandishi wa habari jinsi mji wa kibaha unavyokua na
changamoto zake,Mwenyekiti

wa Halmashauri ya mji wa kibaha, Bw Addhudad Mkomambo alisema katika
awamu ya kwanza katika eneo

la Zogowale kwenye shamba la zegereni  walipima viwanja 10 ambavyo
vimeshachukuliwa viwanja sita

na vimebaki vinne.

Bw Mkomambo alisema maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya fursa hiyo , ni
eneo la Zogowale lenye

hekari 1,048 kwenye shamba la Zegereni ambalo lilikuwa likimilikiwa na
Serikali na Kitovu  cha

mji huo.

"Maeneo mengine ni Mitamba ambapo wizara ya mifugo imeikabidhi
halmashauri hiyo hekari zaidi ya

2,000 na Miyomboni katika kata ya Misugusugu ambapo pametengwa kwa
ajili ya kuendeleza viwanda

vidogovidogo," alisema Bw Mkomambo.

Alisema kuwa kati ya viwanja vilivyochukuliwa tayari ni kiwanda cha
nondo ambacho kimeshaanza

kazi, kiwanda cha jipsam,kiwanda cha kuchuja mafuta machafu,pamoja na
ujenzi wa kiwanda cha

kiwanda cha biskuti.

"Kwasasa tumetangaza viwanja 20 katika eneo hilo hilo ambapo watu
wameshachukua fomu za viwanja

vyote na bado tutaendelea kutenga maeneo zaidi ili kuhakikisha mji wa
Kibaha unakuwa na viwanda

vingi ili kupanua wigo wa ajira," alisema Bw Mkomambo.

Aliongeza kuwa hata hivyo alibainisha kuwa wanakabiliana na changamoto
ya madalali wanaomiliki

maeneo makubwa bila ya kuyaendeleza kwa muda mrefu hatimaye kuwa pori
lengo likiwa kuyauza kwa

gharama kubwa miaka ya usoni .

"Watu wengine wanashangaza ,wanachukua maeneo makubwa hekari 500 hadi
1,000,pasipo kuyatumia eti

wanayaacha kwa ajili ya kuyauza kwa gharama kubwa baadae,watu wa namna
hiyo hatuwahitaji katika

mji wa kibaha,"alisema Mkomambo.


Mwenyekiti huyo wa halmashauri alisema Kufuatia hali hiyo ,wamejipanga
kupambana na  watu
hao kwa kuhakikisha wanawafuatilia kwa muda uliopangwa na
atakayebainika kuwa ni mbambaishaji

atavunjiwa mkataba wake.

Aliwataka wawekezaji nchini kuwekeza viwanda Kibaha kwani mji wa Dar
es salaam umejaa hivyo

kwasasa wilaya ya kibaha inatoa vipaumbele kwa kuendelea kutenga
maeneo mengi ya viwanda ili

kukuza mji huo na kuongeza ajira.

mwisho.

Na John Gagarini, Kibaha

KATIKA kuhakikisha wanafunzi waishio mazingira magumu taasisi isiyo ya
kiserikali ya Mbonde

Foundation inayoshughulika na watoto wanaoishi katika mazingira magumu
na yatima imetoa vifaa

vya shule kwa wanafunzi zaidi ya 40 wa shule ya msingi Boko
Timiza,wilayani Kibaha mkoani Pwani.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Kibaha Bw Wilson Ezekiel
alisema msaada huo kwa

wanafunzi ambao ni viatu, madaftari na Kalamu ni mwanzo wa usaidizi
kwa watoto hao mpaka

watakapofikia elimu ya sekondari.

Bw Ezekiel alisema watoto hao ambao kila mmoja amepatiwa namba maalum
ya utambulisho na tayari

wameshatengewa bajeti ya mwaka mzima kwa ajili ya mahitaji yao muhimu ya shule.

Mmoja wa wanafunzi ambao wamefaidika na msaada huo Said Ally wa darasa
la tatu ameishukuru

taasisi hiyo kwa kuwapatia msaada huo ambao utawasaidia kufanya vizuri
katika masomo yao na

halikadhalika wamewasaidia wazazi wao kwa kiasi Fulani katika
kuwapunguzia majukumu.

Naye mmoja wa wazazi wa watoto hao Bw Ally Mohamed ameishukuru taasisi
hiyo na kusema kuwa

wameonyesha kuwajali wanafunzi na wamepunguza mzigo kwa wazazi ambao
wengi wana majukumu mengi

huku hali ya maisha ikiwa ngumu.

Bw Mohamed aliwataka kuendelea na usaidizi wao kwa watoto wenye
uhitaji ili kuweza kuongeza kasi

ya mafanikio katika sekta ya elimu ili kuunga mkono hatua ya serikali
kuwataka wadau kujitokeza

kuisaidia.

mwisho.

Na John Gagarini, Kibaha

WAZAZI na wananchi wa wilaya ya Kibaha wametakiwa kuwasaidia wanafunzi
wa shule mbalimbali

mkoani Pwani ili kuwanusuru na ajali za barabarani kwani kati ya
wahanga ni kundi hilo ambalo wanahitaji kusaidiwa.

Hayo yalisemwa mjini Kibaha na kamanda wa kikosi cha usalama
barabarani nchini Mohamed Mpinga, wakati wa maadhimisho ya siku ya
kukumbuka watu waliokumbwa na majanga ya ajali za barabarani.

Kamanda Mpinga alisema kuwa baadhi ya wanafunzi wamepoteza maisha
kutokana na ajali mbalimbali hususani wanapokuwa wakivuka barabara
waendapo shule au wanaporudi nyumbani hivyo lazima wapewe msaada
kuwanusuru na ajali.

Katika hatua nyingine alisema mbali ya vifo hivyo vya wanafunzi pia
ajali hizo zinasababisha majeruhi zaidi ya 20,000 hadi 50,000 huku
wengine wakipata ulemavu wa kudumu.

“Ajali ni moja ya vyanzo vya vifo vya watu wengi hapa nchini ambapo
zinashika nafasi ya nane kwa kusababisha vifo na ifikapo mwaka 2020
kitakuwa ni chanzo cha tano kwa vifo,” alisema Kamanda Mpinga.

Alisema kuwa hadi mwezi Oktoba mwaka huu jumla ya ajali zaidi ya
19,000 zimetokea na kusababisha vifo zaidi ya 3,000 ukiachilia jail za
hivi karibuni iliyoua watu saba mkoani Morogoro na iliyotokea mkoani
Dodoma na kuua watu watatu.

“Watu wanaokufa ni nguvu kazi ya Taifa ambapo wengi wao ni vijana
wenye umri kati ya miaka (18) hadi (35) hivyo Taifa kupoteza nguvu
kazi kubwa ambayo ndiyo inayozalisha mali na kukuza uchumi wa nchi,”
alisema Kamanda Mpinga.

Aidha alisema kuwa jeshi la polisi litaendelea kuchukua hatua kali kwa
madereva wazembe ambao wamekuwa wakichangia kwa kiasi kikubwa kutokea
kwa ajili za barabarani na kuwataka abiria kutoa taarifa kwa madereva
wanaoendesha mabasi kwa mwendo wa kasi.

Kwa upande wake mtendaji wa shirika la Global Helmet Vaccine
Initiative Bw Alpherio Nchimbi alisema kuwa lengo la maadhimisho hayo
ambayo hufanyika kila mwaka ni kuwakumbuka wahanga wote waliopata
matatizo kutokana na ajali za barabarani duniani.

Alisema kuwa moja ya wahanga wa ajali ni wanafunzi ambao wamekuwa
wakigongwa mara wanapokuwa wakivuka kwenda ama kurudi shuleni.

“Tunawashauri madereva na wale wanaotumia vyombo vya moto kuachana na
tabia ya kutumia vilevi ambavyo vimeonekana kuwa ni chanzo kikuu cha
ajali za barabarani,” alisema Nchimbi.

Mwisho.

VIZIWI WAHITAJI MSAADA WA VIFAA VYA MICHEZO

Na John Gagarini, Kibaha

TIMU ya Viziwi mkoani Pwani (PDSC) inatarajia kuingia kambini Desemba
20 mwaka huu kwenye uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha kujiandaa na
mashindano ya maadhimisho ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha katibu
wa timu hiyo Daudi Kulangwa alisema kuwa timu hiyo kwa sasa inaendelea
na mazoezi yake kwenye uwanja wa Kongowe wilayani Kibaha.

Kulangwa alisema kuwa mashindano hayo yatafanyika Januari 7 hadi 11
mwaka 2014 ambapo wao na Dar es Salaam wamealikwa watachuana na timu
wenyeji ambao ni Unguja na Pemba.

“Tunaendelea na mazoezi lakini changamoto yetu kubwa ni ukosefu wa
vifaa kama vile jezi ambapo tunacheza vifua wazi, hatuna viatu na
kujikuta wakicheza pekupeku na mipira,” alisema Kulangwa.

Alisema kuwa wanawaomba watu mbalimbali wakiwemo wabunge wa mkoa wa
Pwani wajitokeze kuwasaidia ili waweze kufanya vema.

“Maombi yetu tayari tumeyapeleka ofisi ya Mfuko wa Maendeleo ya
Wanawake (WAMA) pamoja na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Pwani ambao
wameonyesha nia ya kutusaidia,” alisema Kulangwa.

Alibainisha kuwa mbali ya changamoto hizo wanaendelea na mazoezi chini
ya walimu wao Zuberi Boka na Philbert Mbwette na kuwataka watu
waitembelee timu yao na kuiunga mkono ili iweze kufanya vizuri kwenye
mashindano hayo.

Mwisho.

NGUMI PWANI KESHO

Na John Gagarini, Kibaha

BONDIA Zumba Kukwe wa Maili Moja wilayani Kibaha mkoani Pwani leo
anatarajiwa kushuka ulingoni kupambana na Baraka Nuhu wa Chalinze
wilayani Bagamoyo kwenye ukumbi wa Ndelema Inn uliopo Chalinze.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jana mjini Kibaha Kukwe
maarufu kama Lazima Ukae au Mzee wa Uganda alisema kuwa amejiandaa
vema na pambano hilo  na anatarajia kuibuka na ushindi kwenye pigano
hilo ambalo ni la kirafiki la uzito wa kati la raundi nane.

Mzee wa Uganda alisema kuwa tangu alivyotoka nchini Uganda Oktoba
kupambana na bondia Badru Lusambya ambapo alitoka sare, amekuwa kwenye
mazoezi makali chini ya mwalimu wake Gaudence Oyaga.

“Nimejiandaa vizuri na ninatarajia kufanya vema kwenye pambano hili
licha ya kwamba mpinzani wangu sijamfahamu vizuri lakini mashabiki
wangu wasiwe na wasiwasi kwani lazima niwakilishe vizuri na naamini
kuwa lazima akae,” alisema Mzee wa Uganda.

Aidha alisema kuwa mchezo alilocheza nchini Uganda umempa uzoefu
mkubwa kwani ameweza kupata mbinu mpya za kupigana na bondia huyo wa
Uganda ambaye anaishi nchini Uingereza, hivyo anaamini kuwa ushindi ni
lazima.

Mbali ya pambano hilo lililoandaliwa na Mama Ndelema Intertainmet na
Shumbili Promotion kutakuwa na mapambano mengine kati ya Mwaite Juma
na Adam Mustapha, Shani Jaribu na Dula Kiroba, Singa Angokile na Juma
Shumbili.

Mapambano mengine ni ati ya Osama Kaongwa na Mustapha Tozo, Alex Kado
na Juma Soja, Issa Mawe na Khalid Hongo, Ismail Tembo na Bodi
Kitongoji, Salehe Mkalekwa na Jumanne Mvuteni, mgeni wa pambano hilo
anatarajiwa kuwa diwani wa Bwiringu Nasir Karama.

Mwisho.

Tuesday, November 5, 2013

WAFA KWA MATUKIO TOFAUTI

Na John Gagarini, Kibaha

Jeshi la Polisi Mkoani Pwani linamshikilia Zaina Selemani umri miaka 14 mkazi wa Kitongoji cha Janga tarafa ya Mlandizi Wilaya ya Kibaha kwa tuhuma za mauaji ya mtoto wake aitwaye Mariam Stamili mwenye miezi tisa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishina Msaidizi Ulrich Matei amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na ameeleza kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo mnamo tarehe 21/10/2013 majira ya saa 00:00 usiku kwa kumnywesha vitu vinavyosadikiwa kuwa ni sumu ya panya huko Kata ya Janga mtoto wake huyo.
Kamanda Matei ameongeza kuwa kifo cha mtoto huyo hapo awali ilidaiwa kuwa kilitokana na kusumbuliwa na maradhi ya degedege hali iliyopelekea familia yake na majirani kuamini hivyo na kupelekea taratibu zingine za mazishi kufanyika.
Kamanda Matei ameongeza kuwa siku ya tukio, baada ya mzazi wa mtoto huyo kununua sumu hiyo alimnyeshwa mtoto wake na baada ya kuona hali yake imebadilika na kuwa mbaya alimpigia simu mume wake Stamili Shabani umri miaka 21 na kumweleza kuwa mtoto wao anasumbuliwa na ugonjwa wa degedege hivyo wampeleke kwa mganga wa kienyeji.
Ameongeza kuwa baada ya mume wake kurejea nyumbani walimchukua motto huyo na kumpeleka kwa mganga huko Kijiji cha Disunyara ambapo marehemu alianza kupatiwa matibabu lakini hata hivyo kutokana na hali yake kuzidi kuwa mbaya walimchukua mtoto huyo na kwenda nae kituo cha afya Mlandizi ambapo alipoteza maisha siku ya tarehe 21/102013 majira ya saa 00:00 usiku.
Baada ya kutokea kwa kifo hicho mwili wa marehemu ulichukuliwa na ndugu zake na kuzikwa majira ya saa 17:00 jioni huko Kijiji cha Kilangalanga, lakini hata hivyo baada ya kumalizika kwa mazishi hayo mtuhumiwa wa mauaji hayo usiku wa kuamkia tarehe 23/10/2013  alianza kulia na kumwambia mume wake huyo kuwa mtoto wao hakufa kwa ugonjwa wa degedege ila alikuwa amemnywesha sumu hivyo kumuomba amsamehe.
Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma dhidi yake mara baada ya upelelezi kukamilika.
Katika tukio jingine mnamo tarehe 03/11/2013, majira ya saa za 6.30 usiku huko Kijiji cha Mindutulieni Kata ya Talawanda Tarafa ya Chalinze (W) Bagamoyo (M) Pwani. Said Mbena miaka 30, mbena, mkulima mkazi wa Kijiji cha Mindutulieni aliuawa kwa kupigwa na fimbo sehemu mbalimbali za mwili na Machocho Matei miaka 35, mmasai, mfugaji, mkazi wa Kijiji cha Mindutulieni baada ya kutokea ugomvi kati yao wakiwa kwenye sherehe za ngoma za kienyeji nyumbani kwa Asha Rashid. Mtuhumiwa baada ya kukamatwa akiwa njiani kupelekwa katika ofisi ya Kijiji cha Mindutulieni kabla ya kufikishwa katika ofisi hiyo aliuawa na wananchi waliojichukulia sheria mkononi. Miili ya marehemu ya marehemu imehifadhiwa katika ofisi ya Kijiji hicho ikisubiri kufanyiwa uchunguzi na Daktari.
Aidha mnamo tarehe 02/11/2013, majira ya saa za 9.00 usiku huko Kitongoji cha Mlandizi Kati Kata ya Mlandizi Tarafa ya Mlandizi Wilaya ya Kibaha (M) Pwani. Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Kingstone umri kati ya miaka 30-35, mkulima mkazi wa Mlandizi aliuawa na mtu / watu wasiofahamika kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali sehemu ya mguu wa kushoto kwenye maungio ya goti, hali iliyosababisha damu nyingi kuvuja na kusababisha kifo chake. Mwili wa marehemu umehifadhiwa chumba cha maiti Hospitali ya Tumbi Kibaha ukisubiri kufanyiwa uchunguzi na Daktari / kutambuliwa na ndugu.
Kadhalika Kamanda Matei ameeleza kuwa mnamo tarehe 02/11/2013, majira ya saa za 4.00 asubuhi huko Kijiji cha Kazimzumbwi Kata ya Kisarawe Tarafa ya Sungwi barabara ya Dar es Salaam - Kisarawe (W) Kisarawe (M) Pwani. Gari Na. T.762 BSB aina ya Noah likiendeshwa na Dereva asiyefahamika akitokea Dar es Salaam kwenda Msanga aligongana uso kwa uso na pikipiki Na. T.219 BUM aina Fekon iliyokuwa ikiendeshwa na Sixbert Ngatunga miaka 36, mkazi wa Kazimzumbwi akitokea Kisanga kwenda Kazimzumbwi. Katika ajali hiyo dereva wa pikipiki alifariki dunia papo hapo. Mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi na Daktari na kukabidhiwa ndugu kwa mazishi. Chanzo cha ajali ni mwendo kasi wa dereva wa Gari Na. T.762 BSB aina ya Noah.