Sunday, January 5, 2025

WAHUKUMIWA MAISHA NA MIAKA 20 KWA UKATILI WA KIJINSIA

WATUHUMIWA wawili Mkoani Pwani waliokuwa wanakabiliwa kwa kesi za ukatili wa kijinsia wamehukimiwa vifungo tofauti ambapo mmoja amefungwa kifungo cha maisha jela na mwingine amefungwa kifungo cha miaka 20 jela.

Aidha jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani lilipeleka Mahakamani kesi 125 za makosa mbalimbali ambapo kati ya kesi hizo 47 zimepata mafanikio kwa watuhumiwa kuhukumiwa vifungo mbalimbali.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani ACP Salim Morcase alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya mafanikio ya jeshi hilo kwa kipindi cha mwezi Disemba 2024.

Morcase amesema kuwa jumla ya kesi za ukatili wa kijinsia kulikuwa na kesi tano za makosa ya kubaka na kulawiti.

"Watuhumiwa hao wawili walipata adhabu hizo ambapo wa kwanza alipatikana na hatia ya kubaka na kulawiti na wa pili alikutwa na hatia ya unyanyasaji wa kingono,"amesema Morcase.

Amesema kuwa watuhumiwa 52 wamehukumiwa vifungo tofauti tofauti kutokana na aina ya makosa yaliyokuwa yakiwakabili.

MADEREVA 11 MKOANI PWANIWAFUNGIWA LESENI

JUMLA ya makosa 17,246 ya usalama barabarani yamekamatwa huku madereva 11 wakifungiwa leseni zao Mkoani Pwani kwa makosa mbalimbali waliyoyafanya wakiwa barabarani.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani ACP Salim Morcase amesema madereva hao wamefungiwa leseni kwa mujibu wa sheria.

Morcase amesema kuwa madereva hao walifungiwa leseni kwa makosa ya kuendesha magari wakiwa wamelewa, kuendesha magari kwa uzembe na kuyapita magari mengine pasipo kuchukua tahadhari.

"Madereva wengine 24 walifikishwa mahakamani kwa makosa ya kupandisha abiria kwenye magari ambayo yanapelekwa nje ya nchi IT na kusababisha ajali za barababani,"amesema Morcase.

Amesema kuwa madereva hao walifikishwa mahakamani kwa mujibu wa kifungu cha 28 (3) (b) cha Sheria ya usalama barabarani sura ya 168 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2022. 

"Tumetoa elimu ya usalama barabarani kwa makundi mbalimbali, bodaboda, madereva wa mabasi makubwa, madereva wa mabasi madogo na madereva wa magari ya shule,"amesema Morcase.

Ameongeza kuwa wametoa elimu madereva wa pikipiki 4,293 katika vijiwe 199 vya pikipiki na abiria wa mabasi makubwa na madogo wapatao 13,094 kwenye maeneo mbalimbali.

"Elimu waliyoipata ni umuhimu wa kufahamu namba za gari unayosafiria, wahudumu wa basi hilo, dereva na kondakta na kufahamu muda wa kuanza safari, umuhimu wa kutoa taarifa kwa mamlaka husika pale abiria anapoona vitendo
vya uvunjifu wa sheria za usalama barabarani ambavyo vitahatarisha usalama,"amesema Morcase.

Amebainisha kuwa pia wamewaelimisha abiria juu ya mwendokasi, kuyapita magari mengine bila ya tahadhari, madhara ya kupakia mizigo ya hatari ndani ya mabasi na kushushwa kwenye basi pale gari linapofika mizani ili lisionekane kama limezidisha uzito.

COREFA KUJENGA OFISI UWANJA WAKE

CHAMA Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) kimepata eneo lenye ukubwa wa hekari tano kwa ajili ya ujenzi wa ofisi na uwanja wake.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Mwenyekiti wa Corefa Robert Munis alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.

Munis amesema kuwa eneo hilo ambalo liko Mtaa wa Viziwaziwa wamekabidhiwa na Halmashauri ya Mji Kibaha ambapo tayari wamekabidhiwa barua ya kupewa eneo hilo.

"Tumepewa masharti ya kuhakikisha tunajenga ofisi na uwanja ndani ya muda wa mwaka mmoja tunaishukuru Halmashauri kwa kutupatia eneo hilo na tutahakikisha tunalifanyia kazi,"amesema Munis.

Amesema kuwa lengo ni kuhakikisha Corefa inamiliki uwanja wake ambapo kwa sasa hawana uwanja na ofisi waliyonayo wamepangisha hivyo kuwa na ofisi na uwanja itakuwa jambo zuri.

"Kwa kushirikiana na wajumbe wa bodi ya udhamini inayoongozwa na Waziri wa Viwanda na Uwekezaji Dk Suleiman Jafo watahakikisha ofisi na uwanja vinajengwa kwa muda uliopangwa,"amesema Munis.

Aidha amesema kuwa kamati ya utendaji itakaa kuandaa mipango kuhusiana na namna ya kufanikisha namna ya kuanza ujenzi huo.

"Tunataka tuwe na timu zitakazokuwa zinatumia viwanja vizuri na kuhakikisha tunapandisha timu hadi zifike ligi kuu ambapo kwa sasa Mkoa huo hauna timu yoyote iliyoko ligi kuu,"amesema Munis.

Wakati huo huo imempatia kiasi cha shilingi 100,000 mwandishi wa habari za michezo Abdala Zalala kwa kutambua mchango wake wa kuhamasisha mchezo wa soka ndani ya Mkoa huo.

Kwa upande wake Zalala amesema kuwa anakishukuru chama hicho kwa kutambua mchango wake na kumpa zawadi hiyo na kuahidi kuendelea kuhamasisha soka hasa kwa vijana ndani ya  Mkoa huo bila ya kuchoka.

Zalala amewataka waandishi wa habari wenzake nao kujikita kuandika habari za Soka ili kuinua mchezo huo uweze kutia ajira kwa vijana

COREFA KUANDAA VIJANA KWENYE VITUO KILA WILAYA

CHAMA Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) kimesema kitahakikisha kila Wilaya inakuwa na kituo cha kuandaa vijana ili kuzalisha wachezaji watakaokuja kulitumikia Taifa.

Aidha amesema kwa sasa kuna vituo vinne lakini lengo ni kuwa na vituo saba na baadaye kuwe na vituo kila Halmashauri za mkoa huo ambazo ziko 9.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Mwenyekiti wa Corefa Robert Munis amesema kuwa kwa sasa changamoto za viwanja hazipo kwani viwanja vipo vingi.

Munis amesema kuwa kwa sasa wanahamasisha wazazi kuhakikisha wanawawezesha watoto wao ili washiriki kwenye soka ili vijana wa Mkoa huo waweze kutumia vipaji vyao kujiletea maendeleo

"Tunawapongeza wenzetu Chalinze wameanza ligi ya vijana chini ya miaka 15 haya ndiyo tunayoyataka kwani Pwani lazima Mpira Uchezwe ndiyo kauli mbiu yetu,"amesema Munis.

Amesema kuwa mpira ni ajira lakini ili kufikia lengo hilo lazima ushiriki wa wazazi nao uwepo kwa kuwawekea mazingira ili waweze kucheza na wasiwazuie watoto kucheza.

"Tumeanza mpango wa kusajili shule za soka Academy na kuzitambua ili tushirikiane nao ili malengo yetu yatimie kama viwanja vipo kwa nini vijana wasicheze tuhakikishe vijana wetu wanacheza mpira kwani wataliwakilisha vyema Taifa,"amesema Munis.

Ametaja baadhi ya viwanja vilivyopo ndani ya Mkoa wa Pwani kuwa ni Mwanambaya, Bungu, Mabatini, Tumbi, Mwanakalenge, Kiromo, Msoga, Maili Moja Mwendapole, Kwambonde na vingine vingi ambavyo baadhi vinatumika na vingine viko kwenye ujenzi.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa chama hicho ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya mipango na fedha Mohamed Lacha amesema wanawashukuru wadau mbalimbali ambao wamefanikisha kupata ofisi ya kisasa.

Lacha amesema kuwa jambo kubwa ni kuhakikisha Corefa inasonga mbele kwa kushirikiana na kuepukana na migogoro ambayo huwa inarudisha nyuma masuala ya soka.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Soka la Wanawake Mkoa wa Pwani Asha Mbata amesema kuwa wanafarijika kwani kwa mwaka jana Wilaya zote zikichezesha ligi ya wanawake isipokuwa Mafia pekee ambapo ni mafanikio makubwa sana.

Mbata amesema kuwa wanaandaa ziara ya kutembelea Wilaya ili kuhamasisha wanawake na kucheza soka na Wilaya kuandaa ligi  kwa wanawake.






COREFA KUANDAA VIJANA KUPITIA VITUO KILA WILAYA

CHAMA Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) kimesema kitahakikisha kila Wilaya inakuwa na kituo cha kuandaa vijana ili kuzalisha wachezaji watakaokuja kulitumikia Taifa.

Aidha amesema kwa sasa kuna vituo vinne lakini lengo ni kuwa na vituo saba na baadaye kuwe na vituo kila Halmashauri za mkoa huo ambazo ziko 9.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Mwenyekiti wa Corefa Robert Munis amesema kuwa kwa sasa changamoto za viwanja hazipo kwani viwanja vipo vingi.

Munis amesema kuwa kwa sasa wanahamasisha wazazi kuhakikisha wanawawezesha watoto wao ili washiriki kwenye soka ili vijana wa Mkoa huo waweze kutumia vipaji vyao kujiletea maendeleo

"Tunawapongeza wenzetu Chalinze wameanza ligi ya vijana chini ya miaka 15 haya ndiyo tunayoyataka kwani Pwani lazima Mpira Uchezwe ndiyo kauli mbiu yetu,"amesema Munis.

Amesema kuwa mpira ni ajira lakini ili kufikia lengo hilo lazima ushiriki wa wazazi nao uwepo kwa kuwawekea mazingira ili waweze kucheza na wasiwazuie watoto kucheza.

"Tumeanza mpango wa kusajili shule za soka Academy na kuzitambua ili tushirikiane nao ili malengo yetu yatimie kama viwanja vipo kwa nini vijana wasicheze tuhakikishe vijana wetu wanacheza mpira kwani wataliwakilisha vyema Taifa,"amesema Munis.

Ametaja baadhi ya viwanja vilivyopo ndani ya Mkoa wa Pwani kuwa ni Mwanambaya, Bungu, Mabatini, Tumbi, Mwanakalenge, Kiromo, Msoga, Maili Moja Mwendapole, Kwambonde na vingine vingi ambavyo baadhi vinatumika na vingine viko kwenye ujenzi.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa chama hicho ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya mipango na fedha Mohamed Lacha amesema wanawashukuru wadau mbalimbali ambao wamefanikisha kupata ofisi ya kisasa.

Lacha amesema kuwa jambo kubwa ni kuhakikisha Corefa inasonga mbele kwa kushirikiana na kuepukana na migogoro ambayo huwa inarudisha nyuma masuala ya soka.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Soka la Wanawake Mkoa wa Pwani Asha Mbata amesema kuwa wanafarijika kwani kwa mwaka jana Wilaya zote zikichezesha ligi ya wanawake isipokuwa Mafia pekee ambapo ni mafanikio makubwa sana.

Mbata amesema kuwa wanaandaa ziara ya kutembelea Wilaya ili kuhamasisha wanawake na kucheza soka na Wilaya kuandaa ligi  kwa wanawake.






VIONGOZI WA DINI NCHINI JAMHURI YA AFRIKA YA KATI WAISHUKURU JWTZ

 

Umoja wa Viongozi wa madhehebu ya dini nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati wameonesha imani kubwa ya ulinzi wa amani unaotolewa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania nchini humu.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti mara baada ya kutembelewa na Kamanda wa Kikosi cha Nane cha Ulinzi wa Amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati Luteni Kanali Theofili Nguruwe wamesema uwepo wa JWTZ umekuwa na tija sana nchini humo kwani wamekuwa wakifanya kazi zao kwa weledi wa hali ya juu.

Akizungumza kwa niaba ya Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Berberati Mhashamu Koffi Denis, Karibu Mkuu wa Jimbo hilo Padre Jean Ancelimo amesema mbali na Ulinzi wa Amani pia limekuwa likitoa misaada mbalimbali ya hali na mali huku akitolea mfano wa ujenzi wa shule ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ambayo imepewa jina la Serengeti.

Naye Askofu Mkuu wa Kanisa la Evenjeliko (AEC) Mhashamu Lucian Nday amesema uwepo wa JWTZ nchini hapo umewafanya waishi kwa amani na zaidi ya yote limewezesha ukuaji wa lugha adhimu ya kiswahili.

Sheikh Rashid Mohamoud Arouna ni Imam wa Masjid Nuur amesema JWTZ limekuwa mstari wa mbele kwenye kila jambo ambalo wanaombwa kutoa msaada kwa ajili ya kuhakikisha nchi yao inakuwa na amani.

Kwa upande wa Kamanda wa Kikosi cha Nane cha Ulinzi wa Amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati Luteni Kanali Theofili Nguruwe amewashukuru viongozi hao na kuahidi kutekeleza majukumu yake kwa weledi wa hali ya juu.

Saturday, January 4, 2025

JESHI LA POLISI MKOANI PWANI LIMEKAMATA WATU 173 KWA TUHUMA ZA MAKOSA MBALIMBALI



WATUHUMIWA 173 wamekamatwa Mkoani Pwani kutokana na makosa mbalimbali ikiwa ni pamoja na nyaya za Shaba kilogramu 3,687.

Aidha kati yao watu wanne wamekamatwa kwa tuhuma ya kukutwa na meno ya Tembo nane yanayokadiriwa kuwa uzito wa kilogramu 67.

Hayo yamesemwa na Kamanda wa Polisi (ACP) Salim Morcase alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha kuelezea mafanikio ya misako na operesheni. 

Morcase amesema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa katika kipindi cha mwezi Desemba mwaka jana 2024.

"Pia watuhumiwa hao walikamatwa na mafuta ya mafuta ya transfoma lita 80, mafuta ya dizeli lita 3,547, mitungi ya gesi 10, madawati 15 ya Shule ya Msingi Kibadagwe, mafuta ya kula dumu 45 sawa na lita 900,"amesema Morcase.

Amesema kuwa watuhumiwa 54 wamekamatwa kwa tuhuma za kukutwa na bhangi kilogramu 3 na gramu 120.5, mirungi kilogramu 7 na gramu 40, pia watuhumiwa 44 wakikamatwa na pombe ya moshi lita 86 na mtambo wa kupikia pombe hiyo.

"Watuhumiwa wengine walikamatwa na vitu mbalimbali vikiwemo injini ya gari aina ya Corolla, pikipiki 35, simu za mkononi 13, nondo 35 na vipande 12, kompyuta mpakato 1, redio 1, spika 2, vitanda 2 na magodoro yake na mabomba ya chuma 5,"amesema Morcase.

Akizungumzia kuhusu nyara za Serikali amesema watu wanne walikamatwa na nyama ya Swala vipande nane vyenye uzito wa kilogramu 32, vichwa vitano na miguu ya Tohe.

"Pia watu saba wamekamatwa kwa tuhuma za kuiba ngombe sita wenye thamani ya shilingi milioni 8.1 ambapo ngombe hao tumewaokoa,"amesema Morcase.

Amewataka wananchi kuendelea kutoa taarifa zinazohusu uhalifu na wahalifu kwa viongozi wa serikali za mitaa watendaji wa kata au kwa wakaguzi kata waliopo kwenye kata zao.