Thursday, December 15, 2016
Wednesday, December 14, 2016
MSOGA KUJENGA UWANJA WA KISASA
Na John Gagarini, Msoga
MKOA wa Pwani unatarajiwa kuwa na uwanja wa kisasa ambao utasaidia kukuza soka la vijana na kuinua michezo kwenye mkoa huo ambao umepania kuwa moja ya mikoa itakayolea vipaji.
Uwanja huo unatarajiwa kujengwa kwenye Kijiji cha Msoga kata ya Msoga Halmashauri ya Chalinze wilayani Bagamoyo na serikali ya watu wa China lengo likiwa ni kukuza sekta ya michezo kwa vijana kwenye mkoa na nchi kwa ujumla.
Akizungumza katika hafla maalumu iliyoandaliwa kwa ajili ya kwenda kutembelea eneo ambalo litajengwa uwanja huo Dk Kikwete alisema kwamba uwanja huo wa wa mpira wa miguu utajengwa kwa ufadhili wa serikali ya watu wa china na kuongeza kuwa utakuwa ni mkombozi mkubwa katika kukuza na kuinua vipaji kwa vijana wadogo.
“Tumehamasisha wadau wa michezo kujenga uwanja lengo lake kubwa ni kuhakikisha kwamba Tanzania katika siku za usoni inakuwa ni wachezaji wengi wenye vipaji ambao wataweza kuunda timu nzuri ya Taifa ambayo itaweza kufanya vizuri katika mashindano mbali mbali ya Kimataifa,” alisema Dk Kikwete.
“Uwanja huu wa mpira wa miguu pindi utakapokamilika utaweza kuwa ni mkombozi mkubwa wa vijana wadogo hususan wale wa shule, hivyo nimeshazungumza na rafiki zetu wa serikali ya china na wamekubali kutujengea kwa hivyo ni jambo la msingi sana katika kuendeleza sekta ya michezo kwa watoto wetu hawa mbao wataweza kuleta mafanikio makubwa katika siku zijazo,”allisema Kikwete.
Dk Kikwete alisema kuwa anaipongeza serikali ya china kwa kuona umuhimu wa kusaidia kujenga kiwanja hicho, na kuongeza kuwa pindi kitakapokamilika kitakuwa na michezo mingine ambayo itakuwa ikifanyika mbali na mchezo huo wa soka lengo ikiwa ni kuwapa fursa vijana kuweza kuonyesha vipaji walivyonavyo.
Naye Mwakilishi wa balozi wa China nchini Tanzania Yang Tong aliahidi kuendelea kutoa ushirikiano wa dhati katika kukuza sekta ya michezo hususani kwa vijana wadogo ikiwa ni sambamba na kujenga viwanja ili watoto wasiweze kucheza katika viwanja vya vumbi.
Naye Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alisema kwamba lengo lake kubwa ni kuhakikisha anakuza michezo wa vijana wadogo katika jimbo lake hivyo kukamilika kwa ujenzi wa uwanja huo kutaweza kuwasaidia vijana kukuza vipaji vyao.
Nao baadhi ya wadau wa mchezo wa soka katika kijiji hicho cha Msoga akiwemo Michael James pamoja na Mohamed Halfan wamempongeza Rais mstaafu Dk Jakaya Kikwete kwa ubunifu wa ujenzi huo wa uwanja kwa ajili ya vijana wadogo kwani kutaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kuleta mabadiliko chanya katika michezo ukiwemo wa soka.
Mwisho.
CCM WAANZA MCHAKATO WA KUMPATA MGOMBEA UDIWANI MISUGUSUGU
Na John Gagarini, Kibaha
RAMADHAN Bogas ameshinda kura za maoni za kumpata mgombea udiwani kata ya Misugusugu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya kupata kura 43 huku aliyeshinda udiwani kabla ya mahakama kutengua matokeo Addhu Mkomambo akiambulia kura mbili.
Uchaguzi huo ambao ulifanyika Misugusugu ulisimamiwa na Yusuph Mbonde, Selina Wilson na Mohamed Mpaki ambao ni wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya, ulihusisha wagombea saba.
Akizungumza na waandishi wa habari katibu wa CCM Kibaha Mjini Abdala Mdimu alisema kuwa kura zilizopigwa zilikuwa 115 na hakuna kura iliyoharibika.
Mdimu akitaja matokeo alisema kuwa mshindi wa pili alikuwa Eliasi Masenga aliyepata kura 37, Ramadhan Mataula aliyepata kura 15 huku Salumu Mkali akipata kura 14, huku watano akiwa Mkomambo aliyepata kura mbili, Francis Alinamiswe alipata kura mbili na Laurence Likuda naye kura mbili.
Alisema kuwa bado vikao mapendekezo vinaendelea kukaa ambapo jana kilitarajiwa kukaa kikao cha kamati ya siasa ya kata ambapo leo kikao cha kamati ya Usalama na maadili wilaya kinakaa.
“Desemba 16 kamati ya siasa ya wilaya itakaa na baadaye vitaendelea vikao vya mkoa na Desemba 19 Halmashauri Kuu ya mkoa itafanya uteuzi wa mwisho wa mgombea atakayekiwakilisha chama kwenye uchaguzi huo,”alisema Mdimu.
Uchaguzi huo mdogo wa udiwani unarudiwa baada ya mahakama ya mkoa kutengua matokeo kutokana na malalamiko yaliyotolewa na diwani wa Chadema ambapo mgombea wa CCM Addhu Mkomambo alikuwa ameshinda.
Mwisho.
Monday, December 5, 2016
ZAIDI YA 15 WAFAULU DARASA LA SABA PWANI
Na John Gagarini, Kibaha
JUMLA ya wanafunzi 15,528 mkoani Pwani wamefaulu
kwenda shule za sekondari kwa mwaka 2017 baada ya kufanya mtihani wa kumaliza
darasa la saba mwaka huu.
Aidha wanafunzi 9,290 wamefeli sawa na asilimia
37.4 na wanafunzi wote waliofaulu wamechaguliwa kujiunga na elimu ya sekondari
ambapo wamefaulu kwa kupata alama zaidi ya 100 kati yao 288 wamepata daraja la
A.
Hayo yamesemwa mjini Kibaha na Kaimu ofisa elimu
mkoa wa Pwani Modest Tarimo wakati wa uchambuzi wa matokeo ya mtihani wa
kuhitimu eilimu ya msingi mwaka 2016 ya mkoa na kusema kuwa wanafunzi
waliofanya mtihani walikuwa ni 24,818.
Tarimo amesema kuwa wanafunzi 2,636 walipata daraja
B, wanafunzi 12,604 wamepata daraja C na wote waliopata daraja A na C wote
wamechaguliwa kujiunga na sekondari
Amesema kuwa wanafunzi waliokuwa wakitarajiwa
kufanya mtihani walikuwani 24,913 ambapo waliofanya walikuwa ni 24,818 wavulana
wakiwa ni 11,334 na wasichana walikuwa ni 13,484 sawa na asilimia 99.9.
Ameeleza kuwa ufaulu kwa mwaka huu umeshuka kwani
ni asilimia 62.5 ikilinganishwa na mwaka 2015 ambapo ufaulu ulikuwa ni asilimia
63.1 matokeo haya hayaridhishi kwani ufaulu badala ya kupanda lakini umeshuka
kwa asilimia 0.5 na kwa matokeo hayo mkoa umeshika nafasi ya 21 kitaifa.
Amebainisha kuwa watahiniwa 95 hawakufanya mtihani
sawa na asilimia 0.3 kutokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na utoro,
wanafunzi 75, mimba mwanafunzi mmoja, vifo 11, ugonjwa wawili na sababu nyingine
sita ambapo wadau wanapaswa kupiga vita utoro ambao umepungua 204
ikilinganishwa na mwaka jana.
Kaimu ofisa elimu huyo wa mkoa ambaye ni ofisa
taaluma amesema serikali iliweka wastani wa asilimia 80 ya ufaulu kwa shule za
msingi ikiwa ni mkakati wa kufikia mpango wa matokeo makubwa sasa BRN ambapo
wadau wa elimu wanapaswa kukabiliana na changamoto zinaosababisha ufaulu
kushuka.
Naye Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Edward
Mwakipesile amesema kuwa wadau wa elimu wanapaswa kushirikiana na idara ya elimu
ya mkoa ili kuhakikisha matokea ya wanafunzi yanakuwa mazuri ambapo kwa mwaka
huu yanaonekana kushuka.
Mwakipesile amesema kuwa mbali ya changamoto ya
matokeo hayo pia changamoto iliyopo ni vyumba vya madarasa ambavyo ni vichache
na kusababisha madawati kukosa sehemu ya kukaa baada ya zoezi la utengenezaji
madawati kufanikiwa.
Mwisho.
Subscribe to:
Posts (Atom)