DOREFA YAFANYA MKUTANO MKUU WA MWAKA 2022
Friday, December 30, 2022
DOREFA YAFANYA MKUTANO MKUU WA MWAKA
DOREFA YAFANYA MKUTANO MKUU WA MWAKA 2022
Friday, December 23, 2022
RAIS DK SAMIA ATOA VYAKULA VITUO VYA WATOTO
Na John Gagarini Kibaha
Saturday, December 10, 2022
WAJASIRIAMALI WATAKIWA KUWA WANYENYEKEVU
Monday, December 5, 2022
MIPANGO YAANDAA WATAALAMU
WAHITIMU WAANDALIWA KUAJIRIWA NA KUJIAJIRI.
Na Wellu Mtaki, Dodoma
CHUO cha Mipango na Maendeleo Vijijini kimejikita katika utoaji wa Elimu na vitendo katika kuhakikisha wanatoa wahitimu ambao watakaokwenda kujiajiri wenyewe na kuajiriwa.
Bi Omolo amesema kuwa kutokana na Mafunzo yanayotokana katika chuo hiko Wahitimu Watatumia ujuzi huo waliopata katika Kujiajiri wenyewe na kwenda Kuisaidia jamii.
Aliwataka wahitimu na wale wanafunzi watakaoendelea na mafunzo kwa ngazi ya juu kuwa na chachu ya kuendelea kujifunza ili kuongeza maarifa,ujuzi na ubunifu unaohitajika katika kuboresha utendaji wao wa kazi.
Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Mipango Vijijini Prof. Hozen Mayaya ameeleza mafanikio waliyoyapata kwa mwaka 2021/2022 katika miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa Mabweni na Kumbi za mihadhara kwa kutumia fedha za vyanzo vya ndani ya chuo na Ruzuku kutoka Serikalini na kueleza matarajio yao ya 2022/2023 ya kujenga Maktaba kubwa na ya kisasa pamoja na bweni la wanafunzi katika eneo la Kisesa Jijini Mwanza.
Akisoma hotuba kwa niaba ya wanafunzi wenzake muhitimu Gift Kyando ameishukuru Serikali na Wizara ya Fedha na Mipango ambayo ni Wizara Mama ya chuo chao na kuomba Chuo kuendelea kuwasaidia ili waweze kusonga mbele zaidi hasa wanapohitaji kupata Barua za uthibitisho kutoka Chuoni .
Mahafali ya 36 ya Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini ya mwaka 2022 yana jumlaya wanafunzi 6,225 waliohitimu wakiwemo wanaume 2,722 na wanawake 3,502 katika fani mbalimbali za Maendeleo vijijini.
Mwisho.