Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Kamishna wa Tume Nyanda Shuli wakati wa ziara ya kutembelea viwanda ili kufanya uchunguzi kujua kama kuna changamoto za uvunjifu wa haki.
Shuli amesema kuwa baadhi ya viwanda vimekuwa vikilalamikiwa kuvunja haki za binadamu kwa unyanyasaji wa wafanyakazi, uchafuzi taka maji na haki mbalimbali.
"Lengo la ziara ni kuangalia hali ya haki za binadamu na uzingatiwaji wa misingi ya utawala bora kuangalia usalama wa mazingira ya kazi na uzingatiaji wa viwango vya ajira,"amesema Shuli.
Amesema kuwa malalamiko waliyoyapokea watayafanyia kazi na kutoa majibu jambo kubwa ni kuona haki inatendeka ili kuondokana na uvunjifu wa haki za binadamu.
Kwa upande wake Bob Cheng ambaye ni Mkurugenzi wa kiwanda cha Keds Tanzania Company Ltd kinachojihusisha na uzalishaji wa sabuni za unga, vipande, pampasi na pedi za akinamama.
Cheng amesema kuwa kiwanda chao kinazingatia masuala ya haki za binadamu na lengo lake ni kukuza uchumi wa wananchi na hata maji ya kiwanda hicho hayana madhara ambapo asilimia 60 ya wafanyakazi wanaishi eneo jirani na kiwanda hivyo kama kungekuwa na changamoto yoyote wangefahamu.
Amesema kuwa wanafanya utafiti ili kuongeza bidhaa na uzalishaji wenye kuzingatia ubora na bei ambayo inaendana na soko.
Aidha kamishna aliambatana na Taasisi za Serikali ambazo ni OSHA, NEMC na Maofisa kutoka Ofisi ya RAS (Ofisa biashara, Ofisa Kazi na Ofisa Maendeleo ya jamii) kwa lengo la kuleta ufanisi katika ziara hiyo.