Thursday, March 13, 2025

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA (THBUB) YATEMBELEA VIWANDA PWANI

TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imefanya ziara kutembelea viwanda kuangalia uzingatiwaji wa haki za binadamu ili zisivunjwe

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Kamishna wa Tume Nyanda Shuli wakati wa ziara ya kutembelea viwanda ili kufanya uchunguzi kujua kama kuna changamoto za uvunjifu wa haki.

Shuli amesema kuwa baadhi ya viwanda vimekuwa vikilalamikiwa kuvunja haki za binadamu kwa unyanyasaji wa wafanyakazi, uchafuzi taka maji na haki mbalimbali.

"Lengo la ziara ni kuangalia hali ya haki za binadamu na uzingatiwaji wa misingi ya utawala bora kuangalia usalama wa mazingira ya kazi na uzingatiaji wa viwango vya ajira,"amesema Shuli.

Amesema kuwa malalamiko waliyoyapokea watayafanyia kazi na kutoa majibu jambo kubwa ni kuona haki inatendeka ili kuondokana na uvunjifu wa haki za binadamu.

Kwa upande wake Bob Cheng ambaye ni Mkurugenzi wa kiwanda cha Keds Tanzania Company Ltd kinachojihusisha na uzalishaji wa sabuni za unga, vipande, pampasi na pedi za akinamama.

Cheng amesema kuwa kiwanda chao kinazingatia masuala ya haki za binadamu na lengo lake ni kukuza uchumi wa wananchi na hata maji ya kiwanda hicho hayana madhara ambapo asilimia 60 ya wafanyakazi wanaishi eneo jirani na kiwanda hivyo kama kungekuwa na changamoto yoyote wangefahamu.

Amesema kuwa wanafanya utafiti ili kuongeza bidhaa na uzalishaji wenye kuzingatia ubora na bei ambayo inaendana na soko.

Aidha kamishna aliambatana na Taasisi za Serikali ambazo ni OSHA, NEMC na Maofisa kutoka Ofisi ya RAS (Ofisa biashara, Ofisa Kazi na Ofisa Maendeleo ya jamii) kwa lengo la kuleta ufanisi katika ziara hiyo.


Wednesday, March 12, 2025

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA (THBUB) INAFANYA ZIARA KWENYE VIWANDA MKOANI PWANI KUANGALIA UZINGATIWAJI WA HAKI ZA BINADAMU

TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imefanya ziara kutembelea viwanda kuangalia uzingatiwaji wa haki za binadamu ili zisivunjwe.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Kamishna wa Tume Nyanda Shuli wakati wa ziara ya kutembelea viwanda ili kufanya uchunguzi kujua kama kuna changamoto za uvunjifu wa haki.

Shuli amesema kuwa baadhi ya viwanda vimekuwa vikilalamikiwa kuvunja haki za binadamu kwa unyanyasaji wa wafanyakazi, uchafuzi taka maji na haki mbalimbali.

"Lengo la ziara ni kuangalia hali ya haki za binadamu na uzingatiwaji wa misingi ya utawala bora kuangalia usalama wa mazingira ya kazi na uzingatiaji wa viwango vya ajira,"amesema Shuli.

Amesema kuwa malalamiko waliyoyapokea watayafanyia kazi na kutoa majibu jambo kubwa ni kuona haki inatendeka ili kuondokana na uvunjifu wa haki za binadamu.

Kwa upande wake Bob Cheng ambaye ni Mkurugenzi wa kiwanda cha Keds Tanzania Company Ltd kinachojihusisha na uzalishaji wa sabuni za unga, vipande, pampasi na pedi za akinamama.

Cheng amesema kuwa kiwanda chao kinazingatia masuala ya haki za binadamu na lengo lake ni kukuza uchumi wa wananchi na hata maji ya kiwanda hicho hayana madhara ambapo asilimia 60 ya wafanyakazi wanaishi eneo jirani na kiwanda.

Amesema kuwa wanafanya utafiti ili kuongeza bidhaa na uzalishaji wenye kuzingatia ubora na bei ambayo inaendana na soko 

Aidha kamishna aliambatana na Taasisi za Serikali ambazo ni OSHA, NEMC na Maofisa kutoka Ofisi ya RAS (Ofisa biashara, Ofisa Kazi na Ofisa Maendeleo ya jamii) kwa lengo la kuleta ufanisi katika ziara hiyo.


Wednesday, March 5, 2025

DOWEICARE YATOA YATOA MSAADA WA FEDHA UJENZI WA DARAJA LULANZI


KIWANDA cha Doweicare cha Kibaha Mkoani Pwani kimetoa fedha kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa daraja la Mtaa wa Lulanzi-Matunda ili kuboresha barabara ya mtaa huo.

Akikabidhi fedha hizo kwa uongozi wa Serikali ya Mtaa wa Lulanzi Mkurugenzi wa Kiwanda hicho Bob Chen amesema kuwa wameamua kutoa fedha hizo ili kukabili changamoto za jamii.

Amesema kuwa Kiwanda chao kimekuwa kikitoa misaada mbalimbali kwenye jamii ikiwa ni sehemu ya kurudisha kwa jamii kama sehemu ya huduma za jamii ambapo fedha hizo ni asilimia 57.5 ya fedha za mradi huo.

"Tunashirikiana na jamii kwenye masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja elimu, afya, barabara na masuala yanayohusu jamii,"amesema Chen.

Naye Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Lulanzi Thobias Shilole amesema kuwa wanakishukuru kiwanda hicho kwa msaada walioutoa utasaidia sana ujenzi wa daraja hilo.

Shilole amesema wananchi wamekuwa wakijitolea fedha kwa ajili ya ujenzi huo hivyo hiyo itakuwa imewaongezea nguvu kwenye kuanza ujenzi wa daraja ili kupunguza changamoto kwa wananchi wanaotumia barabara hiyo.

Amewataka wadau mbalimbali wa maendeleo kuendelea kuchangia ujenzi huo ili upunguze changamoto kwa watu wakiwemo wanafunzi wakati wakienda na kurudi shule.


WATAALAMU UDSM WAKUTANA NA VIONGOZI TBN

Wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), wamekutana na baadhi ya viongozi na wajumbe wa Tanzania Bloggers Network (TBN) kwa mahojiano maalum yenye lengo chanya la kukusanya maoni yao ili kuimarisha masuala ya blogging, nchini.

Hatua hiyo ya kukusanya maoni imekuja kufuatia wataalamu hao kuagizwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambayo ipo katika utafiti maalum kwa nia ya dhati kuboresha Sera na kanuni zake mbalimbali katika eneo hilo la majukwaa ya mtandaoni.

Kikao hicho kimefanyika kwa mafanikio katika ofisi za TBN zilizopo kwa Aziz Ali, Temeke, watafiti hao wamechukua maoni ya TBN Makao Makuu, wakisema pia watafika katika Ofisi za Kanda za TBN.

Akizungumza Katibu Mkuu wa TBN Khadija Kalili amesema TCRA imefanya uamuzi sahihi kukutana na wadau wake kwa kupitia wataalamu hao kwani maoni yao yatawapa picha halisi juu ya tasnia ya habari na blogging kwa ujumla wake.

Amesema kilio kikubwa cha wana TBN ni gharama za usajili na tozo ya leseni kiasi ni kikubwa ambacho kwa uhalisia wengi bado hawamudu kulipia.

Amesema hali hiyo imefanya idadi kubwa ya wana TBN kushindwa kumudu kuendesha mitandao yao kutoka 300+ waliokuwapo kwanza hadi kufikia 100+ tu wanaoweza kulipia na kwa kusuasua.

Ameshauri pia TCRA kuendeleza utamaduni wa kukutana na wadau wake ikiwamo kwa mafunzo ya kuwaimarisha uwezo wao pamoja na kuangazia athari za gharama za bando za mtandao na vifaa.

Amesema ikiwa sekta ya blogging ndani ya tasnia ya habari ikisimamiwa vizuri kwa ushirikiano wa karibu na TCRA ni wazi kwamba Tanzania itanufaika na maudhui bora na yenye viwango ambayo yatasaidia kulinda maadili ya jamii yetu.

TBN yenye wanachama 300 waliopo wanaendesha mitandao kwa kusuasua kutokana na ada na tozo.

Watalaam hao walionesha kushangazwa na kuwapo kwa Chama Cha Bloggers chenye usajili kamili na wanachama zaidi ya 300, na pia wakaelewa bloggers ni tofauti na jumuiya zingine za waandishi wa mitandao ambao hawana blogs.

Wataalamu hao ni pamoja na Prof. Siasa Mzenzi, Dkt. Patrokil Kanje , Dkt. Said Suluo.

Wengine ni Mjata Daffa , Ally Mshana na Viongozi na wajumbe wa TBN, wakiongozwa na Katibu Mtendaji Khadija Kalili , Beda Msimbe na Rahel Pallangyo.



Mwisho

DOWEI CARE YATOA MSAADA WA FEDHA UJENZI WA DARAJA LULANZI

KIWANDA cha Dowei Care cha Kibaha Mkoani Pwani kimetoa fedha kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa daraja la Mtaa wa Lulanzi-Matunda ili kuboresha barabara ya mtaa huo.

Akikabidhi fedha hizo kwa uongozi wa Serikali ya Mtaa wa Lulanzi Mkurugenzi wa Kiwanda hicho Bob Chaing amesema kuwa wameamua kutoa fedha hizo ili kukabili changamoto za jamii.

Amesema kuwa Kiwanda chao kimekuwa kikitoa misaada mbalimbali kwenye jamii ikiwa ni sehemu ya kurudisha kwa jamii kama sehemu ya huduma za jamii ambapo fedha hizo ni zaidi ya asilimia 60 ya fedha za mradi huo.

"Tunashirikiana na jamii kwenye masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja elimu, afya, barabara na masuala yanayohusu jamii,"amesema Chaing.

Naye Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Lulanzi Thobias Shilole amesema kuwa wanakishukuru kiwanda hicho kwa msaada walioutoa utasaidia sana ujenzi wa daraja hilo.

Shilole amesema wananchi wamekuwa wakijitolea fedha kwa ajili ya ujenzi huo hivyo hiyo itakuwa imewaongezea nguvu kwenye kuanza ujenzi wa daraja ili kupunguza changamoto kwa wananchi wanaotumia barabara hiyo.

Amewataka wadau mbalimbali wa maendeleo kuendelea kuchangia ujenzi huo ili upunguze changamoto kwa watu wakiwemo wanafunzi wakati wakienda na kurudi shule.


Monday, March 3, 2025

VYAMA SITA RAFIKI KUSINI MWA AFRIKA VISIYUMBISHWE VISIMAMIE SHABAHA YA KUWALETEA WANANCHI MAENDELEO

VYAMA vya Ukombozi Kusini mwa Afrika vimetakiwa vibadili mbinu za kuongoza na visikubali kuyumbishwa na mabadiliko ya dunia na kuacha shabaha ya kuziongoza nchi zao.

Hayo yalisemwa jana kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Mjini Kibaha na Makamu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Steven Wassira wakati akifungua mafunzo kwa viongozi wa vyama hivyo.

Wassira alisema kuwa baadhi ya nchi duniani havipendi kuona vyama hivyo vinaongoza wao wanaona demokrasia ni kuviondoa vyama hivyo madarakani.

"Mabadikiko ni mengi duniani lakini yasivitoe vyama vyetu kwenye shabaha yake ya msingi ambayo ni maisha bora na mazuri kwa wananchi huu ndiyo msingi wa vyama hivi,"alisema Wassira.

Alisema kuwa hiyo ndiyo misingi iliyowekwa na waasisi wa mataifa hayo ambayo yalipigania Uhuru wa nchi zao na kuacha misingi imara ambayo inapaswa kufuatwa.

Kwa upande wake Katibu wa masuala ya siasa uhusiano wa kimataifa na Halmashauri Kuu ya CCM NEC Rabia Hamidu alisema kuwa nchi hizo zinapaswa kuonyesha umoja wao ili kuzisaidia nchi za Afrika.

Naye Naibu Mkurugenzi wa idara ya masuala ya Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara na idara ya kimataifa ya kamati kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) na mkuu wa ujumbe wa IDPC Zhang Yanhong alisema kuwa ni jambo zuri kwa ushirikiano wa vyama hivyo sita na CPC.

Naye Mkuu wa Shule ya Mwalimu Julius Nyerere Profesa Marcelina Chijoriga alisema wanatoa mafunzo kwa viongozi wa vyama vya siasa, taasisi za umma na serikali pamoja na taasisi za watu binafsi.

SERA YA TAIFA YA MAENDELEO YA VIJANA 2007 YAENDELEA KUNADIWA

Leo tarehe 3.3.2025 Ndugu Omary Abdul Punzi Mwanadiplomasia na Mratibu wa Makongamano ya Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana Mwaka 2007 toleo la Mwaka 2024 katika kamati ya Vijana Wazalendo waliopewa kibali Maalumu na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu 

Kwa ajili ya Kuinadi na kuineza Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana 

Amemtembelea Mheshiwimiwa Godfrey Eliakimu Mzanva Mkuu wa Wilaya ya Moshi kwa ajili ya kumpongeza kwa Kuaminiwa na Mheshiwimiwa Dk Samia Suluhu Hasani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya.

Unakumbuka kuwa Mheshiwimiwa Godfrey Eliakimu Mzanva ni miongoni mwa wakimbiza mwenge mwaka 2024 waliofanya vizuri katika kuendesha Makongamano ya vijana.

Aidha mazungumzo hayo yalitoa mwafaka wa Kuandaa Kongamano la Vijana Kuhusu Umuhimu wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Ambalo litajikita zaidi kuelezea historia ya Tanzania, Itifaki, Maadili na Uzalendo kwa Vijana,Madhara ya matumizi ya madawa ya kulevya, utunzaji wa Mazingira na Fursa zinatopatikana Wilaya ya Moshi Mkoa wa Kilimanjaro