DIWANI Mteule kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Picha ya Ndege Grace Jungulu amerudisha fomu ya udiwani na kuwataka wana CCM kujitokeza kwa wingi kupiga kura Oktoba mwaka huu.
Jungulu amerudisha fomu kwenye ofisi ya Kata ya Picha ya Ndege Manispaa ya Kibaha huku akisindikizwa na wanachama na wananchi wa Kata hiyo.
Amewataka wanaccm na wananchi kwa ujumla kuhakikisha Oktoba wabakipigia kura za kishindo chama ili kiendelee kuongoza serikali.