Na John
Gagarini, Kibaha
WATU
watatu wamefariki dunia huku wengine watatu wakijeruhiwa walipokuwa wakitokea
Bungeni mkoani Dodoma kushuhudia kuapishwa kwa wabunge saba wa Viti Maalumu wa
Chama Cha Wananchi (CUF) baada ya gari walilokuwa wakisafiria kugongana na lori
la mizigo.
Hayo
yalisemwa mjini Kibaha na kamanda wa Polisi mkoani Pwani Jonathan Shana
alipozungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa watu hao walifia papo hapo.
Kamanda
Shana alisema kuwa tukio hilo lilitokea Septemba 6 majira ya saa 8:30 usiku
eneo la Kijiji cha Ubena Zomozi barabara ya Dar es Salaam-Morogoro wilaya ya
Kipolisi Chalinze-Bagamoyo.
“Gari
lililokuwa limetoka Dodoma kwenda Muheza mkoani Tanga ni aina ya Toyota Noah
lenye namba za usajili T 968 CSK likiendeshwa na dereva Uled Sarumaa (32) mkazi
wa Muheza liligongana na gari aina ya Scania lenye namba za usajili T 929 CBK
lenye tela namba T 472 CAX lililokuwa likiendeshwa na Yasin Kanoni (35) mkazi
wa Jijini Dar es Salaam na kusababisha vifo hivyo,”alisema Shana.
Aliwataja
waliokufa kwenye ajali hiyo kuwa ni dereva wa Noah Sarumaa, Mary Komba (40)
mkulima mkazi wa Muheza na mtu aliyetambuliwa kwa jina moja la Isaack
mfanyabiashara anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka (37).
“Majeruhi
wa ajali hiyo kuwa ni Juma Nindi (47) mfanyabiashara wa Muheza, Chausiku Hassan
(47) mkulima wa Muheza na Ester Mafie (67) mkulima mkazi wa Muheza,” alisema
Shana.
Aidha
alisema kuwa miili ya marehemu imehifadhiwa kwenye Hospitali Teule ya Rufaa ya
mkoa wa Pwani Tumbi kusubiri uchunguzi wa daktari na kusubiri ndugu kwa ajili
ya mazishi huku majeruhi wakiwa wamelazwa kituo cha afya cha Chalinze
Alibainisha
kuwa na chanzo cha ajali kinachunguzwa na alipoulizwa juu ya waliokufa kama ni
viongozi wa CUF amesema kuwa bado hajapata taarifa kuhusiana na hilo pia dereva
wa lori Yasin Kanoni alikimbia mara baada ya tukio hilo na kwa sasa anatafutwa.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment